KAMPUNI ya utengenezaji Marumaru ya GoodWill na ya Vioo ya Sapphire Glass za Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani zimetoa misaada mbalimbali kwa wahanga wa mafuriko Wilayani Rufiji.
Akikabidhi misaada hiyo ofisa rasilimali watu wa GoodWill Jerry Marandu kwa mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Katibu Tawala wa Mkoa huo Rashid Mchatta amesema wameungana ili kusaidia wahanga hao wa mafuriko.
Marandu ambaye pia aliwakilisha kampuni ya Sapphire Glass amesema kuwa misaada hiyo ni unga wa sembe mifuko 70, mchele mifuko 10 na sabuni mifuko 20 ambavyo wameona vitasaidia sehemu ya mahitaji kwa walengwa hao wa mafuriko.
Naye Katibu Tawala Rashid Mchatta amezishukuru kampuni hizo kwa kujitolea kusaidia jamii kwani ni moja ya jukumu lao hivyo kuiunga mkono serikali kusaidia wananchi wake.
Mchatta amewaomba wadau wengine nao kuunga mkono kwa kutoa misaada mbalimbali ya kibinadamu ili kuwapunguzia changamoto wananchi waliokumbwa na mafuriko kwenye Wilaya za Rufiji na Kibiti.
No comments:
Post a Comment