Tuesday, April 2, 2024

WAFANYAKAZI OFISI YA RAIS FEDHA MIPANGO ZANZIBAR NA WAFANYAKAZI WIZARA YA FEDHA WASAIDIA WATU MAHITAJI MAALUM




Na Wellu Mtaki, Dodoma

Wafanyakazi Ofisi ya Rais fedha na Mipango Visiwani Zanzibar wakishirikiana na wafanyakazi wa wizara ya fedha wametembelea vituo vinne vya watu wenye mahitaji Maalum.

Vituo hivyo ni kituo cha Safina Street Network, Asmaa Bint Shams, kituo Cha  wasioona watu wazima Buigiri na Shule ya Msingi ya watoto wenye mahitaji maalum Buigiri ikiwa ni muendelezo wa ziara yao kila mwaka kutembelea vituo vya watu wenye maitaji Maalum na kutoa misaada ya chakula na fedha.

Hayo yamesemwa na ofisa Uendeshaji Ofisi ya Rais fedha na mipango Zanzibar Rajab Uweje wakati akizungumza na vyombo vya habari Jijini Dodoma mara baada ya ziara wameweza kutambua  mahitaji mengine ya vituo hivyo na ametoa ahadi awamu zijazo watajitaidi kuhakikisha wanatatua changamoto zao.

"Tumetoa ahadi katika vituo hivi tumechukua changamoto zao tuone awamu ijayo tuje kutatua changamoto tunaondoka hapa tukiwa tunaenda kuongea na viongozi wetu kuwaeleza hali iliyopo huku ili awamu ingine tuje tusaidie kutatua changamoto,"amesema  Uweje.

Pia ametoa wito kwa walezi wa vituo hivyo kuendelea kuwatunza watoto hao  na kuwasimamia  vizuri ili kujenga Taifa  lenye raia wema.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Hazina Sports Club Mugusi Musita amesema kuwa upo muhuhimu wa jamii kutambua kusaidia watu wenye maitaji maalum kutokana ha changamoto zilizopo kwenye jamii zao hivyo anaiomba jamii kiujumla kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele kusaidia watoto kwani watoto ndiyo Taifa la kesho.

"Vituo vinamahitaji mengi na makubwa sana   kama viongozi  watambue watoto hawa wanamaitaji sana tumekuja kuwapa chochote ila naona kama havitoshi pia tutachuka nafasi hii kupeleka taarifa za cha changamoto hizi katika Halmashauri ya Chamwino nao waone namna ya kusaidia," amesema Musita.

Naye Mratibu wa  Shirika la Safina Street Network Dodoma Ebeneza Ayo ameiomba jamii kuacha kutoa hela kwa watoto wa mitaani ndiyo inasababisha watoto hao kuendelea  kukaa mitaani kuombaomba bali jamii iendelee kuwapa msaada kwa kuwasidi kuwapekeka katika vituo vya kulelewa ili waweze kupata msaada pamoja na elimu Ili kusaidia kutengeneza Taifa lenye nguvu kazi.

"Tuwapende hao watoto wanaotoka katika manzingira hatarishi tuwe  tayari kuwasaidia kwa mambo  mbalimbali tunavyokutana nao mitaani tujaribu kuwasaidia  waweze kwenda kwenye vituo au ofisi ustawi wa jamii na sio kuwapa hela kwani ukiwapa hela ndiyo wanazidi kukaa mitaani , lakini pia hata sisi wenye mashirika ya kuwasaidia watoto tunachangamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa maji katika kituo chetu hivyo tunaomba jamii iweze kutusaidia,"amesema Ayo.

Mwenyekiti wa Makazi ya watu wasioona Buigiri  Yaledi Daudi ameiomba serikali kuwasaidia kujenga maeneo yao ya Makazi kutokana na nyumba zao kuwa chakavu ili waweze kuishi maisha bora.

"Kwa upande wa serikali tunamshukuru  sana Rais Samia kwa kazi nzuri anayofanya na natoa wito kwa serikali kuwa nyumba zetu tunazoishi zimekuwa chakavu tunaomba serikali itujengee nyumba ili kuwa na maisha bora,"amesema Daudi

Ikumbukwe kuwa ziara hizi hufanyika kila mwaka ikiwa na lengo la kuwasaidia watu waishio manzingira magumu pamoja na watu wenye uhitaji mbalimbali, ziara hizi ufanyika katika maeneo ya visiwani Zanzibar na Bara kwa awamu tofauti tofauti.

No comments:

Post a Comment