Friday, April 5, 2024

TAASISI YA KUMUOMBEA RAIS NA WASAIDIZI WAKE YAFANYA MAOMBI KUIOMBEA SERIKALI

 

Na Wellu Mtaki, Dodoma

Taasisi ya kumuombea Rais  na wasaidizi wake imefanya maombi ya kuombea viongozi wa serikali akiwemo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Spika wa Wabunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Tulia Akson pamoja na Mawaziri na Wabunge. 

Katibu Mkuu wa taasisi hiyo Angelina Malembeka akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya maombi hayo amesema lengo ni kuwaombea ili waongoze kwa hekima.

Malembeka amesema kuwa anaamini taasisi hiyo itaweza kusaidia mambo mengi yasiyofaa yasipate nafasi na malengo ya taasisi ni kumuombea Rais  na wasaidizi wake pamoja na wataalamu mbalimbali wanaofanya shughuli za jamiii ndani ya nchi.

"Katika utekelezaji wa miradi mbalimbali na utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mambo yanaenda vinzuri ila wao wanafanya kazi ya kuombea Ili kuhakikisha utekelezaji unaenda vizuri zaidi,"amesema Malembeka.

Alisema wanaona mambo yanaenda vizuri katika miradi mbalimbali na utekelezaji wa ilani ya CCM na kazi yao ni kuombea viongozi wawe na ujasiri, nguvu na kuwapa matumaini na ikumbukwe kuwa suala hili la kuombea Rais na wasaidizi wake ni suala la muendelezo na kazi yake ni kujenga Taifa lenye hofu ya Mungu.

Aidha amesema kuwa idadi ya wanachama ni zaidi ya wanachama 600 lakini walioshiriki maombi hayo walikuwa ni 208 ambapo wengine hawakuhudhuria kutokana na sababu mbalimbali.


 

No comments:

Post a Comment