Friday, March 31, 2023

MAHAKIMU NA MAJAJI WAPATIWA MAFUNZO

 

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MAHAKIMU na Majaji wamepatiwa mafunzo ya siku mbili kuhusu wajibu wa Mahakama katika kutunza na kulinda uhuru wa kujieleza pamoja na haki za binadamu nchini.

Mafunzo hayo ya siku mbili yanatolewa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) likiwa Ni kukumbushana masuala mbalimbali katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Mratibu wa Mtadao wa THRDC, Onesmo Olengurumwa akizungumza na waandishi wa habari  jijini dodoma wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa Mahakimu na Majaji nchini amesema lengo ni kukumbushana wajibu katika kutekeleza majukumu ya kila siku.

Aidha amesema kuwa umekuwepo na mabadiliko mengi ya kisheria na masuala mbalimbali yanayohusu haki za binadamu hivyo wao kama watu ambao wanatoa haki kila siku katika Mahakama, wanapaswa kuyafahamu ili kulinda haki za binadamu na uhuru wa kujieleza

Amesema pia mafunzo mengine ambayo yatatolewa ni masuala ya maadili kwa Mahakimu na Majaji katika utekelezaji wa majukumu ya utoaji wa haki katika maeneo yao.

Amesema Suala la maadili ni jambo la muhimu sana katika mahakama zetu nchini hivyo mafunzo haya pia yatasaidia kuwakumbusha Mahakimu na Majaji wajibu wao wa kutenda haki kwa kuzingatia maadili ya kazi zao.

Naye Naibu katibu mkuu wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (JMAT) Mary Kallomo, amesema mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha utendaji wao wa kila siku katika kulinda haki za binadamu na uhuru wa kujieleza.

NAIBU WAZIRI KIKWETE ATEMBELEA WANANCHI WA MKANGE


Kuzungumza na Wananchi na kueleza hatua mbalimbali zilizofikiwa na serikali yetu katika kutatua changamoto zinazotokana na shughuli za maendeleo ikiwemo miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Halmashauri yetu. 

Nimetumia nafasi hiyo kuwakumbusha mabadiliko mbalimbali yanayofanyika katika sekta mbalimbali ikiwemo ya Afya, Elimu, Huduma za Jamii, Miundombinu, Maji, Utumishi wa Umma n.k. Ahadi yetu ni kuendelea kuwatumikia na kutatua changamoto zetu.#TukoPamoja #Chalinze #KaziInaendelea

TANESCO YATAKIWA KUWEKA KITENGO CHA KERO KININSIA

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limetakiwa kuweka kitengo maalumu kitakachoshughulika na kusikiliza kero za kijinsia ili kuweka usawa wa kijinsia katika shirika hilo.

Hayo yamesemwa Jijini hapa na Naibu Waziri wa Nishati,Stephen Byabato katika uzinduzi wa Programu ya Mpango wa Jinsia wa miaka minne(2023-2027)wa TANESCO kwa kusirikiana na Benki ya Dunia kupitia mradi wa umeme wa Tanzania hadi Zambia(Tanzania-Zambia Transmission Interconnector Project-TAZA).

Naibu Waziri Byabato amesema kuwa Shirika hilo limekuwa likishughulikia masuala ya jinsia kwa namna mbalimbali hivyo kwasasa ni wakati muafaka wa kuwa na kitengo kitakachokuwa na bajeti,uongozi wa kitengo chenye uelewa na uweledi wa kusikiliza kero za kijinsia mbalimbali zitakazojitokeza.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO,Maharage Chande amesema kuwa lengo la programu hiyo kuwa ni kutatua changamoto wanazokutana nazo wanafunzi wanawake katika maeneo yao ya kazi kwa lengo la kukuza ajira zao ili kuongeza idadi ya wanawake wanaoajiriwa.

Mkurugenzi Chande ametaja maeneo ya kimkakati yatakayopewa kipaumbele kuwa ni kuiboresha sera ya Shirika na kujenga uwezo ili sera iende sambamba na masuala ya kijinsia,kuwepo na taarifa sahihi zinazohusu masuala ya unyanyasaji wa kijinsia kwenye Taasisi,kuruhusu fursa ya ukuzaji wa taaluma kwa wafanyakazi wanawake hasa wanaofanyakazi kwenye miradi na kuwepo kwa nafasi ya mafunzo kwa vitengo kwa wafanyakazi wanawake waliopo kazini ili kuwajengea uwezo kuelekea kwenye ajira kamili.

Aidha  kuhusu mradi wa kusafirisha umeme wa Tanzania hadi Zambia (TAZA),Chande ameeleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Nishati na TANESCO wanatekeleza ujenzi wa mradi wa upanuzi wa njia ya kusafirisha umeme mkubwa wa kilovoti 400 kutoka katika kituo cha kupokea,Kupoza na kusafirisha umeme mkubwa cha Tagamenda Iringa kwenda kwenye nchi zilizopo kusini mwa Tanzania(Southern African Power Pool)kupitia Kisada Iringa,Iganjo Mbeya na Nkangamo Tunduma Songwe.

Chande amekitaja kituo hicho cha Tagamenda kuwa ni kitovu cha kusafirisha umeme mkubwa wa kilovoti 220 kwenda kwenye mikoa takribani 18 nchini.

Na kwa upande mwingine kituo hiki kimeunganishwa na kituo cha umeme cha zuzu Dodoma ili kusafirisha umeme mkubwa kwenda kwenye nchi zilizopo Mashariki mwa Tanzania ambazo ni Kenya,Uganda na Ethiopia kupitia mradi wa kuunganisha umeme baina ya Kenya na Tanzania(Kenya-Tanzania Power Interconnection Project-KTPIP)

Thursday, March 30, 2023

DK SAMIA ANA LENGO LA KUBORESHA AFYA KISARAWE.

RAIS DR SAMIA ANA LENGO LA KUIFANYA SEKTA YA AFYA  KUWA YA MFANO ZAIDI KISARAWE -DR JAFO

Na Mwandishi Wetu, Kisarawe 

WAZIRI wa nchi ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira (Mb) Jimbo la Kisarawe Mhe Dkt. Selemani Said Jafo amekabidhi vifaa mbalimbali vya afya katika Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe kwa lengo la kuboresha huduma za afya katika wilaya hiyo kwa Vijiji 66 Fedha ikiwa ni kutoka kwa Mhe Rais Samia na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi CCM katika Kutekeleza ilani ya 2020-2025.

Katika makabidhiano ya vifaa hivyo Mhe Dr Jafo amewapongeza watendaji wa Idara ya  afya katika hospitali hiyo kwa kazi kubwa wanayofanya katika kuwahudumia wagongwa na pia ameahidi kuwa nao karibu ili kutatua baadhi ya changamoto wanazokutana nazo katika utoaji wa huduma kwa ujenzi wagonjwa.

Aidha wananchi wameishukuru serikali kwa kuwasaidia upatikanaji wa vifaa hivyo kwani vita saidia kupunguza usumbufu wa upatikanaji wa huduma ya matibabu hospitalini hapo

Aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita Kwa kupendelea zaidi Kisarawe katika Upatikanaji wa Huduma ya Afya Kwa kuipatia Vifaa Tiba na fedha mbalimbali kwa Ajili ya Afya ambayo inaifanya Halmashauri ya Wilaya Kisarawe kuwa Nzuri katika Huduma za Afya.

Wednesday, March 29, 2023

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora ametembelea mradi wa Nyumba Za Watumishi Magomeni

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora  ametembelea mradi wa Nyumba Za Watumishi Magomeni na kuongea na watendaji wa Shirika la Nyumba la Watumishi( WATUMISHI HOUSING INVESTMENT), na kuwakumbusha kuendelea kusimamia msingi wa uwanzishwaji wa shirika hilo pasi kusahau kuendelea kujenga nyumba za Watumishi sehemu zenye uhitaji mkubwa kimkakati. #KaziInaendelea #WHI

Tuesday, March 28, 2023

KIKWETE AKUTANA NA TAASISI YA UONGOZI

NAIBU Waziri Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Ndg. Ridhiwani Kikwete, amezunumza na Watendaji wa Taasisi ya @UONGOZI mapema leo na kuwaasa kuendelea na kazi nzuri wanayoifanya bila kusahau msingi wa kuanzishwa kwa taasisi hiyo. #KaziInaendelea #UongoziBora

Sunday, March 26, 2023

WAZIRI UMMY AFIKA KWENYE VIJIJI UGONJWA WA MARBURG ULIPOANZIA


WAZIRI UMMY AFIKA KWENYE VIJIJI UGONJWA WA MARBURG ULIPOANZIA

Na. WAF - Bukoba, Kagera

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amefanya ziara ya kutembelea vijiji vya Kata ya Maruku na Kanyangele vilivyopo Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera kwa lengo la kujionea hali inavyoendelea baada ya kutangazwa kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa wa Marburg Mkoani humo. 

Katika Ziara hiyo, Waziri Ummy ameambatana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Zabron Yoti pamoja na Mwakilishi wa Shirika la UNICEF Tanzania Bi. Shalini Bahuguna ili nao wajionee hali ya ugonjwa huo inavyoendelea kudhibitiwa nchini Tanzania. 

Aidha, Waziri Ummy amesema kwa sasa hali ni salama na kuwataka Wananchi wa vijiji hivyo, wana Kagera na watanzania kwa ujumla kuondoa hofu na kuendelea na shughuli zao kwa kuwa Serikali inawajali Wananchi wake.

“Niwatoe hofu Watanzania tuendelee kufanya kazi zetu lakini tuzingatie maelekezo ya Serikali ya kujikinga na ugonjwa huu kwa kuepuka kushikana mikono hususan kipindi hiki lakini pia tujitahidi kunawa mikono mara kwa mara na maji tiririka kwa sabuni.” amesema Waziri Ummy

Hata hivyo, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea na juhudi za kuhakikisha ugonjwa huo unamalizika kwa haraka na hautatokea tena katika maeneo hayo. 

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kanyangele Bw. Hamim Hassan ameishukuru Serikali kwa kufanya juhudi kubwa ambapo hadi sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyeongezeka kuwa na ugonjwa huo. 

“Hatua za haraka za Serikali kupitia Wizara ya Afya zilizochukuliwa za kuwaweka sehemu maalumu waliokuwa karibu na wagonjwa imesaidia sana kutoendeleza maambukizi kwengine na hali ni shwari kwa sasa.” amesema Bw. Hassan

WAZIRI UMMY ATEMBELEA WATUMISHI WALIOWEKWA KARANTINI

WAZIRI UMMY ATEMBELEA WATUMISHI WALIOWEKWA KARANTINI

Na. WAF - Bukoba, Kagera

WAZIRI wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewatembelea watumishi wa afya waliowekwa sehemu maalumu ya uangalizi baada ya kuwahudumia wagonjwa wa Marburg walioripotiwa katila Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera.

Ziara hiyo ameifanya leo akiambatana na Wawakilishi kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Zabron Yoti na Shirika la Kuhudumia Watoto Duniani (UNICEF) Bi. Shalini Bahuguna baada ya kutembelea katika Vijiji vya Kata ya Maluku na Kanyangele ambapo ugonjwa huo umeanzia

Waziri Ummy amewatia moyo watumishi hao kwakuwa Serikali ipo pamoja nao na lengo ni kuendelea kuwalinda wao na wanaowazunguka ikiwemo familia zao. 

“Niwatie moyo ndugu zangu huu ugonjwa utaisha kwakuwa Serikali imedhamiria kuendelea kupambana ili kutokomeza kabisa na hali itarudi kama zamani.

Mwisho, Waziri Ummy amewataka watumishi hao wa Afya kuzingatia Kanuni na Taratibu za Udhibiti wa Maambukizi (Infection Prevention and Control) wakati wote wanapowahudumia wagonjwa.


Wednesday, March 22, 2023

CHAVITA YAIPONGEZA eGA KWA HUDUMA ZA SERIKALI MTANDAO JUMUISHI KWA WATU WENYE ULEMAVU

 

MWENYEKITI  wa Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani Suleiman Zalala ameipongeza Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kwa huduma jumuishi za utekelezaji wa jitihada za Serikali Mtandao kwa watu wenye ulemavu.

Zalala ametoa pongezi hizo wakati wa kilele cha kikao kazi cha Serikali Mtandao kilichofanyika hivi karibuni katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa (AICC) Jijini Arusha.

Zalala ameishukuru Mamlaka kwa kuthamini na kuona mchango wa kundi maalumu la watu wenye ulemavu kushiriki katika mafunzo hayo ili kuboresha huduma jumuishi za Serikali Mtandao kwa watu wenye walemavu.

"CHAVITA imekuwa na ushirikiano wa muda mrefu na eGA katika mipango mbalimbali ya mafunzo inayoandaliwa na Mamlaka kwa watu wenye ulemavu na kwamba mafunzo hayo yamekuwa yakiwajengea uwezo na uelewa mkubwa wa utekelezaji wa jitahada za Serikali Mtandao katika utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi,"amesema Zalala.

Amesema kubwa wameweza kujifunza na kupata uelewa juu ya mabadiliko mbalimbali ya teknolojia katika utoaji wa huduma na huduma mbalimbali zinazowezeshwa na eGA kwa wananchi kama vile ununuzi wa Luku, kata za maji n.k

Aidha ameomba mafunzo hayo yawe chachu kwa Taasisi nyingine za Umma kuiga mfano wa kile kilichofanywa na Mamlaka kwa kuwashirikisha makundi maalum kwenye uandaaji wa mafunzo na mipango mbalimbali inayotekelezwa na taasisi zao .

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba amewashukuru wadau wote waliohudhuria kikao kazi hicho na kwa michango yao itakayosaidia kufanikisha na kuimarisha utekelezaji wa jitihada za Serikali Mtandao kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi wa Taasisi za umma, pamoja na utoaji wa huduma kwa umma.

“Naimani kuwa kikao hiki kimewajengea uwezo zaidi washiriki wote kuhusu Serikali Mtandao na kila mdau ametambua namna ambavyo anaweza kufanikisha jitihada za Serikali Mtandao kupitia sekta yake,"amesema Mhandisi Ndomba

Mhandisi Ndomba ameongeza kuwa washiriki zaidi ya 1624 wamehudhuria kikao hicho na mada 22 ziliwasilishwa na wadau kutoka katika taasisi mbalimbali za Umma zilizolenga kutathmini na kuimarisha nguzo kuu Nne (4) za Serikali Mtandao.

Amesema kuwa katika kikao hicho wadau wamepata fursa ya kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano katika kutekeleza jitihada za Serikali Mtandao nchini pamoja na kutafuta ufumbuzi wa changamoto za serikali mtandao zilizopo nchini ili kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii .

Amebainisha kuwa washiriki wametoa maoni mbalimbali ya namna ya kukuza jitihada za Serikali Mtandao ikiwa ni pamoja na kushauri uboreshaji wa Mifumo mbalimbali inayotoa huduma kwa umma pamoja na kupanua wigo wa utoaji wa huduma za Serikali Mtandao katika maeneo mbalimbali nchini.


Mkurugenzi amesema Menejimenti ya Mamlaka imeyapokea maoni na ushauri uliotolewa na kwamba eGA ipo tayari kufanyia kazi maoni hayo yanayolenga kuboresha na kukuza jitihada za Serikali Mtandao nchini.

WACHIMBAJI WADOGO WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI

TAASISI YA KUENDELEZA UCHIMBAJI MDOGO IMETAKIWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

KAMISHNA wa Madini Dkt. Abdulrahman Mwanga ameitaka Taasisi ya Kuendeleza Uchimbaji Mdogo (FADev) kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa majukumu yake ili Serikali na jamii itambue kazi zinazotekelezwa na taasisi hiyo.

Rai hiyo, imetolewa Machi 22, 2023 alipokutana na Uongozi wa taasisi ya FADev ambao umefika kwa lengo la kujitambulisha na kueleza majukumu yanayofanywa na taasisi hiyo Kuendeleza Uchimbaji Mdogo katika kikao kilichofanyika ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma.

Dkt. Mwanga ameitaka FADev ishirikiane na Serikali ili kujenga mahusiano mazuri katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali na kusaidia kuepusha kuingiliana na majukumu hayo mara kwa mara.

Aidha ameitaka FADev kuendelea kuilinda taasisi hiyo kwa kuheshimu taratibu na misingi iliyowekwa na nchi ambayo inalinda utu wa watanzania katika majukumu yao.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa FADev Mhandisi Theonestina Mwasha amesema kuwa inaendelea kutekeleza miradi inayokuza na kuimarisha uzalishaji wa dhahabu katika mikoa ya Geita na Shinyanga.

“Tunafanya mafunzo katika maeneo ya uchimbaji tunatoa elimu shirikishi kwa jamii inayozunguka migodi nakuanzisha mchakato wa kutoa elimu ya kuongeza thamani kwa ushirikiano wa wadau,” amesema Mhandisi Mwasha.

Akizungumzia kuwaendeleza wachimbaji wadogo Mhandisi Mwasha amesema taasisi imetoa vifaa vya uchimbaji migodi kwa vikundi mbalimbali walivyofanya navyo kazi sambamba na kuimarisha vikundi vya wanawake 15 katika mikoa ya Geita na Shinyanga.

Mwasha amesema kuwa hadi sasa taasisi ya FADev imefanikiwa kutoa mbinu za ujasiriamali kwenye maeneo ya uchimbaji madini, mafunzo ya utunzaji wa mahesabu, mafunzo ya ukusanyaji na utunzaji wa taarifa na matumizi sahihi ya kemikali zinazotumika kwenye uchenjuaji.

Pia imefanikiwa kutoa mikopo isiyozidi milioni 15 kwa kila kikundi kwa vikundi vitatu kwa kushirikiana na benki ya NBC.

Kikao hicho, kimehudhuriwa na wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Madini, Tume ya Madini na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST).

KINANA AWATAKA WANAWAKE KUGOMBEA NAFASI

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Komredi Abdulrahman Kinana ameitaka Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) kuhakikisha inahimiza wakinamama wa Chama hicho kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama.

Kinana amesema hayo wakati akifungua mafunzo kwa viongozi na watendaji wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) kuanzia ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convertion Jijini Dodoma.

Amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitawaunga mkono 2025 wakikishe wanagombea nafasi zote za uongozi na vikao vya Chama kitawaunga mkono wale wote watakaoenda kugombea.

Aidha Kinana ameitaka Jumuiya hiyo kuhakikisha inatetea haki za kinamama kila mahali, katika hatua nyingine ameitaka kujenga Utamaduni wa kuambiana ukweli na si kuogopana na watumie vikao kuamua mambo ndani ya Jumuiya na wasitumie makundi kuamua vikao.




WATUMISHI WA e-GA WAHIMIZWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA MISINGI MIKUU SITA YA MAMLAKA

MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) Mhandisi Benedict Ndomba amewataka watumishi wa Mamlaka hiyo kufanya kazi kwa kuzingatia misingi mikuu sita ya Taasisi.

Ndomba alisema hayo wakati wa kikao cha Watumishi wa Mamlaka kilichofanyika kwa muda wa siku tatu katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuwajengea uwezo watumishi hao katika masuala mbalimbali yanayohusu utumishi wa umma

Alisema kuwa e-GA inaongozwa na misingi mikuu sita ambayo inaelekeza kuhusu tabia na mwenendo wa watumishi wake kwa ngazi zote na kufafanua utamaduni wa mahali pa kazi ili kuhakikisha watumishi wote na wateja wa Mamlaka wanaouelewa wa pamoja wa jinsi wanavyotakiwa kuhudumiwa na nini kinachotarajiwa kutoka kwao.

"Nawakumbusha watumishi wote wa Mamlaka kuzingatia misingi hiyo ambayo ni uadilifu, ubunifu, kutathmini wateja, ushirikiano, kufanya kazi kwa pamoja na weledi katika utendaji kazi wao wa kila siku,"alisema Ndomba.

Alisema kuwa Mamlaka imekuwa taasisi ya mfano inayofanya shughuli zake za kila siku kwa kasi na ari inayokubalika, kutokana na uadilifu mkubwa wa Menejimenti na watumishi waliodhamiria kuweka juhudi kubwa katika kuboresha utendaji wa Serikali na utoaji huduma bora kwa umma.

“Nawakumbusha watumishi wote kuimarisha uadilifu na kila mtumishi na kutimiza wajibu wake kwa kufanya kazi kwa bidii, nidhamu na kwa weledi kwa kuzingatia misingi hiyo huku Mamlaka ikiendelea na jitihada mbalimbali za kuhakikisha kuwa watumishi wanafanya kazi katika mazingira bora na salama,”alisema Ndomba.

Aidha alisema kuwa katika kikao hicho mada mbalimbali zilizolenga kujenga uelewa na ufahamu kwa watumishi ziliwasilishwa ikiwemo Afya mahali pa kazi, Rushwa mahala pa kazi, Maadili ya utendaji, Haki na Wajibu, HIV/AIDS na magonjwa sugu yasiyoyakuambukiza, mawasiliano mazuri kwa utendaji bora wa kazi, namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo na maisha kazini.

Kikao hicho kilihitimishwa na Bonanza la Michezo lilifanyika katika viwanja vya Gymkana ambapo michezo mbalimbali ikiwemo kukimbiza kuku, kuvuta kamba, kukimbia kwa kutumia magunia, kukimbia na yai kwenye kijiko na mbio fupi.


Sunday, March 19, 2023

RIDHIWANI AWAAGA KIDATO CHA SITA KIKARO

 


MBUNGE wa Chalinze ameshiriki sherehe za kuwaaga wanafunzi wanaomaliza kidato cha 6 katika shule ya sekondari ya Kikaro Miono. Katika sherehe hizo Mh. Mbunge aliwasisitizia wanafunzi hao kuepuka tamaa za dunia na kujali masomo kwanza. #ELIMU #MionoChalinze

RIDHIWANI KIKWETE AFUNGUA VYOO VILIVYOJENGWA NA IFM CHARITY




MBUNGE wa Chalinze ameshiriki sherehe yaMiaka 10 ya Taasisi ya Ifm Charity kwa kufungua Vyoo vilivyojengwa na Taasisi hiyo na kula chakula nao katika kituo cha kulelea Watoto Yatima cha Hope-Miono, Chalinze. Mh. Mbunge amewashukuru wanachuo hao kwa kujali wenye uhitaji #10IFMSO

Saturday, March 18, 2023

KANUNI UASALAMA MIGODINI

WACHIMBAJI WA MADINI WATAKIWA KUZINGATIA KANUNI ZA USALAMA MIGODINI

SERIKALI imewataka Wachimbaji wa Madini kuzingatia Kanuni za Usalama na kufuata Sheria na Taratibu za Uchimbaji ili kuepusha ajali katika maeneo ya uchimbaji.

Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa Machi 17, 2023 alipotembelea na kuzungumza na wachimbaji katika eneo la ajali ya wachimbaji wadogo waliofunikwa na kifusi na kufariki eneo la Igando Kata ya Magenge Tarafa ya Butundwe Mkoani Geita.

Dkt. Kiruswa, ameiagiza Tume ya Madini kutoa elimu ya Sheria ya Madini hususan elimu ya usalama kwa wachimbaji wanaozunguka maeneo ya uchimbaji katika kipindi cha mvua na kuchukua tahadhari.

"Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan inatoa pole kwa wananchi waliopoteza ndugu na marafiki katika ajali hii. Tunawataka wachimbaji mzingatie sheria zilizowekwa na Serikali ili mfanye shughuli zenu kwa tija," amesema Dkt. Kiruswa.

Aidha, amewataka wachimbaji katika eneo hilo kushirikiana na Serikali na mkoa kuchukua hatua kwa wachimbaji wote watakaobainika kukaidi maelekezo ya Serikali kwa wote wanaofanya uchimbaji kwenye maeneo yaliyokatazwa.

Kwa upande wake, Kamishna wa Madini Dkt. Abdulrahman Mwanga amewataka wachimbaji katika maeneo yenye uwekezaji kutoa ushirikiano kwa watu wenye leseni ya madini ili wafanye shughuli zao bila usumbufu. Amewataka pia kuzingatia usalama katika kazi zao.

Naye, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Geita Mhandisi Martin Shija amemuelezea Dkt. Kiruswa kuwa, hatua mbalimbali zilichukuliwa kabla na baada ya ajali. Amesema mmiliki wa leseni na Serikali ya kijiji waliweka walinzi shirikishi kwenye eneo hilo ili kuzuia uchimbaji haramu na kuepusha madhara.

"Baada ya ajali tumeimarisha ulinzi katika eneo hilo, tumeendelea kufanya kaguzi mara kwa mara ili kubaini kama kazi zinaendelea na kuchukua hatua pale dosari inapojitokeza,"amesema Mhandisi Shija.

Naye, mwekezaji wa eneo hilo lenye leseni ya utafiti Abdul Stanslaus amesema katika eneo hilo ameendelea kuwa na mahusiano mazuri na jamii katika eneo hilo. Ameomba Serikali kuendelea kutoa elimu kuhusu Sheria ya Madini ili wachimbaji wanaozunguka maeneo ya uchimbaji kuwa na uelewa mkubwa.

Naibu Waziri amefanya ziara baada ya wachimbaji wadogo 8 kufariki tarehe 10 Machi, 2023 baada ya kutokea ajali ya wachimbaji kukutwa na maji ndani ya mashimo wakiwa wanaendelea na shughuli za uchimbaji.

Thursday, March 16, 2023

KAMATI YA NISHATI NA MADINI YAIPONGEZA SERIKALI KUIPATIA GST MASHINE ZA UTAFITI WA MADINI NCHINI

 

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAIPONGEZA SERIKALI KWA KUIPATIA GST MASHINE ZA KISASA ZA UTAFITI WA MADINI NCHINI

Na Mwandishi Wetu Dodoma

KAMATI ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Serikali Awamu ya Sita kwa kuipatia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) vifaa na mashine za kisasa kwa ajili kuongeza wigo wa  utafiti wa madini nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na makamu  mwenyekiti wa Kamati hiyo Judith Kapinga mbunge wa viti maalum wakati akiongea na vyombo vya habari mapema baada ya kukamilisha ziara hiyo.

Ziara hiyo ya kutembelea maabara za GST kwa ajili ya kujionea utekelezaji wa majukumu ya GST , Mhe.  Mbunge Judith Kapinga aliipongeza serikali kwa kuwekeza mashine za kisasa katika kufanya uchunguzi, utambuzi na unjenjuaji wa madini mbalimbali.

"Kwa kweli niipongeze Serikali ya Awamu ya Sita kwa juhudi inazofanya katika kuiwekeza  taasisi yetu ya GST kwa kuipatia mashine mbalimbali za uchunguzi , utambuzi na uchenjuaji wa madini " alisema Kapinga

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Songwe Philipo Mulugo  ambaye pia ni mjumbe wa Kamati hiyo alishauri  kuwa katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2023/2024  GST iongezewe nguvu zaidi ya kibajeti ili kuweza kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.

Kabla ya ziara hiyo kuanza, Mtendaji Mkuu wa GST Dkt. Mussa Budeba aliwakaribisha wajumbe wa Kamati na kuwashukuru kwa mchango wao mkubwa wanaotoa katika kusimamia GST katika kutekeleza majukumu yake. 

"Ninashukuru sana Kamati hii kwa usimamizi wake nzuri ambao umeendelea kuifanya GST kuboreka zaidi katika  utoaji wa huduma zake,"Alisema Dkt. Budeba.

Mapema baada ya utambulisho huo Dkt. Budeba alimkaribisha Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa kwa ajili ya kuanza ziara hiyo ambapo Dkt. Kiruswa aliishukuru Kamati kwa namna mnavyoendelea kuishauri na kuisimamia Wizara ya Madini kwa ufanisi mkubwa. 

"Sisi tunafarijika sana kwa namna mnavyotusimamia Wizara  na Taasisi zake na tunawakaribisha GST muweze kujione mlichokisoma kwenye taarifa zetu". Aliongeza Dkt. Kiruswa

Katika ziara hiyo wajumbe wa Kamati hiyo walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali juu ya utekelezaji wa majukumu ya GST hasa juu ya  uchunguzi wa sampuli za madini katika maabara ya GST.

Wednesday, March 15, 2023

67 WAKAMATWA NA VITU MBALIMBALI


JESHI la Polisi Mkoani Pwani linawashikilia watu 67 kutokana na makosa mbalimbali ikiwa ni pamoja na tuhuma ya kukutwa na silaha moja aina ya gobore.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani (ACP) Pius Lutumo alisema kuwa watu hao walikamatwa kwenye misako na opereseheni zilizofanywa katika kipindi cha wiki mbili Machi Mosi hadi Machi 14.

Lutumo alisema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa kutokana na tuhuma za makosa mbalimbali ambapo watapelekwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

"Lengo la misako hiyo ni kuzuia uhalifu ambapo tunawashukuru wananchi kwa ushirikiano ili kufanikisha kukabiliana na uhalifu,"alisema Lutumo.

Alitaja baadhi ya vitu vingine vilivyokamatwa ni pamoja na bhangi viroba vitatu, puli 102 na kete 789 na pombe ya moshi lita 143 na mtambo mmoja wa kutengenezea pombe hiyo.

"Vitu vingine ni pikipiki 10 ambazo zina usajili wa aina tofauti isipokuwa pikipiki tatu ambazo hazina usajili na watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara upelelezi utakapokamilika,"alisema Lutumo.

Aidha alisema kuwa Polisi inatoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kuhusiana na taarifa za uhalifu na wahalifu ili kuendelea kuufanya mkoa kuwa shwari.

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria



MAKAMU Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Florent Kyombo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama na Naibu Waziri wake Mhe. Ridhiwani Kikwete wakimkabidhi fedha mlengwa wa TASAF Wilayani Uyui Bi. Amina Abdallah zilizochangwa na Wajumbe wa Kamati hiyo kumuwezesha mlengwa huyo kukamilisha ujenzi wa nyumba aliyoanza kuijenga kutokana na ruzuku ya TASAF anayoipata.

Monday, March 13, 2023

TASAC YAKANUSHA TAARIFA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII

Na Mwandishi Wetu Dodoma

SHIRIKA la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) limekanusha Taarifa zilizokua zikisambaa hivi karibuni kwenye mitandao ya kijamii hususan Twitter na Instagram kuhusu mikataba ya mafunzo ya kazi kwa vijana zaidi ya 400 ilivunjwa bila kufuata utaratibu ikiwa imebaki mwaka mmoja kuisha kwa mikataba hiyo.

Akizungumza na Wandishi wa habari Jijini Dodoma Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Wakala wa Meli Tanzania(TASAC) Kaimu Abdi Mkeyenge amesema taarifa zilizozidi kusambaa ni pamoja na vijana kufanya kazi bila bima ya afya na kwamba ilitoa rushwa kwa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) katika mashauri ya kazi yaliyofunguliwa na vijana hao ili haki isitendeke.

Mkeyenge amesema kuwa mwezi Julai, 2022 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilifanya mabadiliko ya Sheria ya Uwakala wa Meli Tanzania kwa kufuta majukumu ya kipekee ya uwakala wa meli, uhakiki wa mizigo, udhibiti wa nyaraka na kupunguza wigo wa jukumu la kufanya uwakala wa forodha katika bidhaa zilizokuwa zinagombolewa na kuondoshwa na TASAC.

"TASAC ilikuwa ikitekeleza majukumu hayo kupitia vijana waliokuwa wameajiriwa moja kwa moja pamoja na waliokuwa wakifanya mafunzo ya kazi lakini kufuatia mabadiliko hayo Agosti 11 mwaka 2022 TASAC ilivunja mikataba ya mafunzo ya kazi kwa jumla ya vijana 209 waliokuwa wakifanya kazi za uhakiki wa shehena na si zaidi ya 400 kama ilivyoripotiwa katika mitandao ya kijamii,"amesema Mkeyenge.

Amesema kuwa vijana hao waliandikiwa barua kuwa mikataba yao haitahuishwa tena ifikapo tarehe 30 Agosti, 2022 kutokana na merekebisho ya Sheria ambayo yamesababisha baadhi ya majukumu ya TASAC kufutwa na kuhamia sekta binafsi.

 "Kwa mujibu wa masharti ya mikataba, TASAC ilikuwa inawapa mkataba ya miezi mitatu na kuongeza muda kila ilipoonekana inafaa kutokana na utendaji kazi wa mtu,"amesema Mkeyenge. 

Aidha, mikataba ilikuwa imeainisha utaratibu wa namna ya kuvunja mikataba ya mafunzo kazi na ndiyo utaratibu uliotumika kuvunja mikataba hiyo.

"Kwa kuwa vijana wanaolalamika walikuwa kwenye mafunzo kazi na siyo waajiriwa wa moja kwa moja, TASAC kama taasisi nyingine yoyote ya Serikali haina wajibu wa kuwakatia bima ya afya vijana inaowachukua kwa mafunzo kazini kwani stahiki zao zimeainishwa kwenye Muongozo wa Kitaifa wa Mafunzo Kazini uliotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu,"amesema Mkeyenge.

Ameongeza kuwa TASAC ni taasisi ya Serikali inayosimamiwa na Sheria, Kanuni na Miongozo ya Serikali, hivyo basi mashauri yake kisheria yanasimamiwa na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ikiwa ni pamoja na shauri hilo na kuwahakikishia TASAC haijatoa na haiwezi kutoa rushwa yoyote kwa CMA ili kuzuia haki isitendeke kama ilivyoripotiwa katika mitandao ya kijamii.

"Kati ya vijana 209 waliofutiwa mikataba yao, ni vijana 41 tu ambao hawakuridhika na maamuzi hayo na Vijana 32 kati ya vijana 41, shauri lao lilifutwa na CMA kwa kuwa liliwasilishwa nje ya muda, hivyo ni vijana 9 tu ambao shauri lao dhidi ya TASAC lilipokelewa na lipo katika Tume ya Usuluhisi na Uamuzi vijana 168 waliobaki hawakupinga uamuzi wa TASAC wa kuvunja mikataba yao kutokana na mabadiliko ya Sheria ambayo yalikuwa ni nje ya uwezo wa Shirika,"amesema Mkeyenge.

Amebainisha kuwa suala hilo lipo kwenye chombo cha maamuzi kisheria na TASAC haipaswi kulizungumzia shauri hilo lakini ilionekana ni busara kulitolea ufafanuzi wa kilichofanyika kwa upande wa TASAC na kuacha hatua za maamuzi zinazoendelea kuchukua mkondo wake.

"TASAC kama Shirika la Umma linatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo inayotolewa na Serikali, hivyo linatoa wito kwa Umma kuwa na subira wakati Tume inapoyafanyia kazi mashauri hayo,"amesema Mkeyenge.

WCF YALIPA FIDIA KWA WAFANYAKAZI BILIONI 49.4

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umefanikiwa kulipa fidia ya shilingi bilioni 49.4 kwa wafanyakazi wanaoumia kuugua ama kufariki kazini 10,454 tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 2015. 

Takwimu hizo zimetolewa Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo Dkt. John Mduma wakati akielezea utekelezaji wa majukumu ya Mfuko mbele ya Waandishi wa Habari mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari – MAELEZO.

Dkt.Mduma amesema kwamba Serikali kupitia WCF imeleta mageuzi makubwa nchini kwani kabla ya kuanzishwa kwa mfuko malipo ya fidia nchini kwa mwaka mzima yalikuwa chini ya shilingi milioni 200 lakini baada ya kuanzishwa kwa malipo yanaongezeka mwaka hadi mwaka.  

“Hadi kufikia Juni 30 mwaka 2022 WCF imelipa mafao yenye thamani ya shilingi bilioni 44.6 kwa wanufaika mbalimbali ikiwa ni ongezeko kubwa kwa kulinganisha na kipindi cha kabla ya kuanza kwa mfuko kwa hesabu zisizokaguliwa katika kipindi cha Julai 2022 hadi Desemba 2022 WCF ililipa mafao ya jumla ya shilingi bilioni 6.1 kwa wanufaika 1,004 na hivyo kufanya wanufaika wa Mfuko toka kuanzishwa kwake kufikia 10,454 ambao wamelipwa jumla ya shilingi Bilioni 49.4.” alisema Dkt. Mduma.

Amesema kuwa Mfuko huo umekuwa ukilipa malipo endelevu (pensheni) kwa wanufaika ambapo kwa mwezi Juni 2022, wanufaika 1,114 walilipwa kiasi cha shilingi milioni 231.3 kwa mwezi huo.

Akizungumzia kuhusu Kusajili Waajiri Tanzania Bara amesema kuwa kwa taarifa zisizokaguliwa, hadi kufikia mwezi Februari 2023, WCF ilikuwa imesajili jumla ya waajiri 29,978 ambapo amefafanua kuwa ongezeko kubwa la waajiri kujisajili na Mfuko katika kipindi cha awamu ya sita ni kutokana na hatua za makusudi za Serikali kuweka vivutio vya kufanya biashara na kuondoa vikwazo vilivyokuwepo ikiwa ni pamoja na kupunguza viwango vya uchangiaji na kutoa msamaha wa riba.

Aidha katika upande wa uwekezaji hadi kufikia Juni 30 mwaka 2022, Mfuko umekusanya jumla ya shilingi bilioni 241.4 toka kwenye mapato yatokanayo na uwekezaji ambapo kwa takwimu za hivi karibuni, WCF ilitengeneza shilingi bilioni 69.8 katika mwaka wa fedha 2020/2021 na shilingi bilioni 74.2 katika mwaka wa fedha 2021/2022. 

Ameongeza kuwa jumla ya mali za Mfuko hadi Juni 30 mwaka 2022 ni shilingi bilioni 545.1 ambapo asilimia 89.7 ya uwekezaji wa Mfuko upo kwenye Hati fungani za Serikali.


 

Saturday, March 11, 2023

KIKWETE ATAKA BARUA ZA KIUTUMISHI KUJIBIWA KWA WAKATI

MHE. RIDHIWANI AELEKEZA BARUA ZA MASUALA YA KIUTUMISHI KUJIBIWA KWA WAKATI KUEPUKA MALALAMIKO YASIYO YA LAZIMA

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka watumishi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma kujibu kwa wakati barua za masuala ya kiutumishi ili kuepuka malalamiko yasiyo ya lazima ambayo yamekuwa yakielekezwa katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mhe. Kikwete ametoa maelekezo hayo Jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa idara hiyo kilicholenga kufahamu majukumu yanayotekelezwa na kuhimiza uwajibikaji.


Mhe. Kikwete amewasisitiza watumishi wa idara hiyo ya Utawala wa Utumishi wa Umma kutosita kujibu barua za wadau kwa wakati hata kama zina mapungufu, ili wahusika wafahamu mapungufu yaliyopo kwenye masuala yao ya kiutumishi ambayo yamewasilishwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa ajili ya kupata kibali au kutolewa maamuzi.

“Natambua kuna mapungufu ya masuala ya kiutumishi katika barua mnazolalamikiwa kutozijibu kwa wakati, lakini mnapaswa kuzijibu kwani msipofanya hivyo, mnatoa mwanya kwa wahusika kuilalamikia ofisi na hatimaye kuichafua taswira nzuri ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,” Mhe. Kiwete amefafanua.

Aidha, amewataka watumishi wa idara hiyo kuchakata  utoaji wa vibali vya uhamisho wa watumishi wa umma kwa kuzingatia takwimu zinazoainishwa na Mfumo wa Tathmini ya Hali na Mgawanyo wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma ili vibali vya uhamisho vinavyotolewa visiathiri utendaji kazi wa baadhi ya taasisi katika eneo la utoaji huduma bora kwa wananchi.


Kuhusiana na utendaji kazi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma kwa ujumla, Mhe. Kikwete amewapongeza watumishi wa idara hiyo kwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu licha ya kuwa ni mengi na yenye changamoto nyingi.


Mhe. Kikwete ameongeza kuwa, watumishi wa idara hiyo wanatakiwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi ili kutimiza azma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

Friday, March 10, 2023

CHAMA CHA MADEREVA WANAWAKE TANZANIA KUJA NA MRADI WA USAFIRISHAJI

CHAMA Cha Madereva Wanawake Tanzania (CWMT) kinatarajia kuanzisha kampuni ya usafirishaji ili kujiongezea kipato na kutoa ajira kwa wanachama wake.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa chama hicho Naetwe Ihema alisema kuwa lengo ni kumkwamua mwanamke ili ajitegemee na asiwe tegemezi.

Ihema ambaye ni dereva wa mabasi ya Mwendokasi alisema kuwa madereva wanawake kwa sasa ni wengi ambao wanafanya kazi kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye Taasisi za serikali na binafsi lakini walikuwa hawana Umoja wao.

"Tumeanzisha chama hichi ambacho mwanzo ilikuwa ni kikundi tukaona tujiongeza na kuwa chama ambacho kimesajiliwa na moja ya malengo yetu ni kuwa na kampuni ya usafirishaji kwa mabasi ya kwenda mikoani na daladala ambapo wanachama wetu watakuwa ndiyo madereva,"alisema Ihema.

Alisema kuwa wanatarajia kuongea na watu wenye kampuni za mabasi kwa kuanzia mabasi madogo (daladala) ili waingie makubaliano kama ni kuwakopesha au njia yoyote ili waweze kupata mabasi ili waanze kufanya hiyo kazi.

"Tutaanzisha hiyo kampuni ya usafirishaji kwani ajira kwa madereva wanawake ni changamoto ambapo waajiri wanakuwa hawawaamini wanawake lakini ni madereva wazuri na uwezo wao ni mkubwa,"alisema Ihema.

Aidha alisema kuwa madereva wanawake hawasababishi ajali kutokana na kuwa makini na hofu ya kuogopa kupoteza uhai wa watu ndiyo sababu udereva wao ni wa kujihami na siyo kujiamini.

"Mafanikio tuliyoyapata kwa mtu mmoja mmoja ni kuweza kuhudumia familia ambapo kwa wale walioolewa wanauwezo wa kushirikiana na waume zao katika kuendesha maisha na ambao hawajaolewa wanasomesha, wamejenga na wanafanya maendeleo makubwa,"alisema Ihema.

Aliongeza kuwa sifa ya mwanachama awe anaendesha chombo chochote cha moto ambapo baadhi ya wanachama wao ni marubani wa ndege, manahodha wa meli, madereva wa mitambo ya ujenzi, magari ya mizigo, mabasi makubwa, madereva wa treni, madereva wa uba, madereva wa mwendokasi na magari ya watu binafsi. Chama hicho kilianzishwa mwaka 2020 na kina wanachama 120.







CHAMA CHA MADEREVA WANAWAKE TANZANIA CHAJA NA MIKAKATI MIKUBWA

CHAMA Cha Madereva Wanawake Tanzania (CWMT) kinatarajia kuanzisha kampuni ya usafirishaji ili kujiongezea kipato na kutoa ajira kwa wanachama wake.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa chama hicho Naetwe Ihema alisema kuwa lengo ni kumkwamua mwanamke ili ajitegemee na asiwe tegemezi.

Ihema alisema kuwa madereva wanawake kwa sasa ni wengi ambao wanafanya kazi kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye Taasisi za serikali na binafsi lakini walikuwa hawana Umoja wao.

"Tumeanzisha chama hichi ambacho mwanzo ilikuwa ni kikundi tukaona tujiongeza na kuwa chama ambacho kimesajiliwa na moja ya malengo yetu ni kuwa na kampuni ya usafirishaji kwa mabasi ya kwenda mikoani na daladala ambapo wanachama wetu watakuwa ndiyo madereva,"alisema Ihema.

Alisema kuwa wanatarajia kuongea na watu wenye kampuni za mabasi kwa kuanzia mabasi madogo (daladala) ili waingie makubaliano kama ni kuwakopesha au njia yoyote ili waweze kupata mabasi ili waanze kufanya hiyo kazi.

"Tutaanzisha hiyo kampuni ya usafirishaji kwani ajira kwa madereva wanawake ni changamoto ambapo waajiri wanakuwa hawawaamini wanawake lakini ni madereva wazuri na uwezo wao ni mkubwa,"alisema Ihema.

Aidha alisema kuwa madereva wanawake hawasababishi ajali kutokana na kuwa makini na hofu ya kuogopa kupoteza uhai wa watu ndiyo sababu udereva wao ni wa kujihami na siyo kujiamini.

"Mafanikio tuliyoyapata kwa mtu mmoja mmoja ni kuweza kuhudumia familia ambapo kwa wale walioolewa wanauwezo wa kushirikiana na waume zao katika kuendesha maisha na ambao hawajaolewa wanasomesha, wamejenga na wanafanya maendeleo makubwa,"alisema Ihema.

Aliongeza kuwa sifa ya mwanachama awe anaendesha chombo chochote cha moto ambapo baadhi ya wanachama wao ni marubani wa ndege, manahodha wa meli, madereva wa mitambo ya ujenzi, magari ya mizigo, mabasi makubwa, madereva wa treni, madereva wa uba, madereva wa mwendokasi na magari ya watu binafsi. Chama hicho kilianzishwa mwaka 2020 na kina wanachama 120.




WEJISA WASHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI



WANAWAKE WA WEJISA WAJUMUIKA KUSHEHEREKEA SIKU YA WANAWAKE DAR

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Weka Jiji Safi (WEJISA Company Ltd) kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu wake Bi.Nuru Hassan amepongeza juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan katika kuweka mazingira mazuri ya kufanya kazi ikiwemo wafanyakazi wanawake jambo ambalo limeongeza uchapakazi kwa jinsia hiyo.

Nuru amesema hayo kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambayo inafanyika Machi 8 ya Kila mwaka.

"Rais wetu Samia tunamuunga mkono kwa sababu nafasi aliyonayo amesaidia kuongeza mwamko kwa wanawake kufanya kazi na wale ambao walikuwa hawana kazi na kutafuta shughuli zozote ili waweze kujiondoa kwenye utegemezi," alisema Nuru.

Amesema kuwa kampuni ya WEJISA itaendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega na ndiyo maana leo tumekuja hapa kusheherekea pamoja na kujifunza mengi kwa wafanyakazi wetu wanawake,"alisema Nuru Hassan

Aidha amesema kuwa amepata faraja kujumuika na Wanawake hao kwani wamekuwa chachu ya Maendeleo ya Kampuni hiyo.

Wanawake hao wa WEJISA wanatoka vitengo mbalimbali ikiwemo wanaosafisha maeneo ya Jiji, ikiwemo ufagiaji, ukusanyaji wa taka na usafi wa mazingira.

Lengo la tukio hilo ni kupeana moyo kama Wanawake katika kuamua mambo na kufanikisha utendaji bora wa kazi.

Kwa upande wake Patricia Kimelemeta Mwandishi Kinara wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto Mkoa wa Dar es Salaam ambaye alitoa mada ya malezi na makuzi kwa watoto katika tukio hilo la kusheherekea siku ya Wanawake, ambapo alitoa rai Kwa wazazi kuendelea kutoa elimu kwa watoto wao ikiwemo kujenga ukaribu wa kuwachunguza ilikujua changamoto wanazokutana nazo.

Kwa upande wao baadhi ya Wanawake wafanyakazi wa WEJISA waliishukuru kampuni hiyo kwani imekuwa mkombozi kwao na wamekuwa wakifanya kazi moyo.

"Mimi nina familia, nikitoka nyumbani naandaa kabisa chakula kwa wanangu.

Aidha, amewataka Wanawake kuzingatia sheria za Usalama barabarani kwani wamekuwa wakishuhudia matukio mengi, ikiwemo wao kugongwa.' Alisema Bi. Asha Salum.

Kwa upande wake. Bi. Sharifa Magombeka amesema kuwa, anafanya kazi ya kuzoa taka ilikupata kipato chake halali,

"Mwanamke ni kujitambua, nafanya kazi yangu ya kuzoa taka hii kupata kipato kihalali, tunamshukuru Mhe Rais kuendelea kuweka mazingira ya ufanyaji kazi na tumejumuika hapa tumepata elimu, lakini pia tumefurahia pamoja" alisema Sharifa.


Thursday, March 9, 2023

JWTZ WATANGAZA NAFASI KUJIUNGA NA JESHI

Na Mwandishi Wetu Dodoma

JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetangaza nafasi za kujiunga na Jeshi kwa vijana wa Kitanzania wenye elimu ya kuanzia kidato cha nne hadi shahada ya uzamili ambao wamemaliza mkataba wa miaka miwili wa mafunzo ya kujitolea katika Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na kurudishwa majumbani.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiao wa (JWTZ) Luteni Kanali Gaudentius Ilonda wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu nafasi za kujiunga na Jeshi hilo.

Ilonda amesema kuwa nafasi hizo zinawahusu vijana wenye umri kuanzia miaka 18 hadi 26 kwa wenye elimu ya kidato cha 4 na cha sita na umri usiozidi miaka 27 kwa wenye elimu ya juu.

Amesema kuwa nafasi hizo haziwahusu vijana ambao bado wapo katika kambi mbalimbali za JKT kwa sasa bali zinawahusu wale ambao tayari wamemaliza mikataba yao ya mafunzo ya miaka miwili na kurudishwa majumbani na wenye vigezo vilivyotajwa vya kuomba nafasi hizo.

"Maombi yote yaandikwe kwa mkono na yawasilishwe makao makuu ya Jeshi hilo Dodoma kwanzia leo tarehe 9 Machi hadi tarehe 20 Machi 2023 yakiwa na viambatanisho kama vile nakala ya kitambulisho cha Taifa au namba ya Nida, nakala ya cheti cha kuzaliwa, vyeti vya shule na chuo, nakala cheti cha JKT na namba ya simu ya mkononi ya muombaji,"amesema Ilonda.

Aidha amewataka wananchi kuwa makini na matapeli kwani kumekuwa na tabia ya kuibuka matapeli pindi matangazo hayo ya nafasi ya kujiunga na Jeshi hilo zinapotangazwa. 

KIKWETE AOMBA USHIRIKIANO KUTIMIZA LENGO LA RAIS KUWA NA MUUNDO WA UTUMISHI KWA USTAWI WA TAIFA

MHE. RIDHIWANI KIKWETE AOMBA USHIRIKIANO KUTIMIZA LENGO LA MHE. RAIS LA KUWA NA SERA ZA KIUTUMISHI NA MIUNDO YENYE TIJA KWA USTAWI WA TAIFA

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka watumishi wa Idara ya Uendelezaji Sera na Idara ya Uendelezaji Taasisi kumpa ushirikiano wa kutosha kwenye eneo la kusimamia uendelezaji wa sera katika Utumishi wa Umma na miundo ya Taasisi za Umma.

Mhe. Kikwete ametoa rai hiyo Jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa Idara ya Uendelezaji Sera na Idara ya Usimamizi wa Taasisi kwa nyakati tofauti kilicholenga kufahamu majukumu yanayotekelezwa na Idara hizo pamoja na kuhimiza uwajibikaji.

 Amesema kuwa ili aweze kumsaidia vema Waziri mwenye dhamana kufikia lengo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuwa na sera za utumishi wa umma zenye tija na miundo inayotekelezeka kiutendaji kwa ustawi wa taifa.

Mhe. Kikwete amesema ameteuliwa na Mhe. Rais kumsaidia Waziri mwenye dhamana ya kusimamia utumishi wa umma na utawala bora, hivyo hana budi kufahamu kwa kina majukumu yanayotekelezwa na idara hizo ili aweze kuyazungumzia pale yanapohitaji ufafanuzi na uelewa kwa umma.

“Malengo ya kukutana nanyi leo ni kufahamiana na kujua majukumu yenu kwa kina kwa kuwa mimi nina jukumu la kumsaidia Mhe. Waziri kujibu maswali ya kiutumishi na utawala bora yanayoulizwa Bungeni,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Ameongeza kuwa, anatamani kujua kila kitu kinachofanyika katika idara hizo pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo kiutendaji kwani kwa kufanya hivyo atakuwa kwenye nafasi nzuri ya kutekeleza kwa ufanisi lengo la Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aidha Kikwete ameitaka Idara ya Undelezaji Sera kuhuisha sera za kiutumishi ili ziendane na wakati na ziweke mazingira rafiki ya kuzihusisha sekta binafsi kutoa mchango katika kuboresha utumishi wa umma kama Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan alivyoelekeza.

Wednesday, March 8, 2023

KIKWETE ATAKA USHIRIKIANO KUTIMIZA LENGO LA RAIS DK SAMOA SULUHU HASSAN KUWA NA SERA KWA USTAWI WA TAIFA

MHE. RIDHIWANI KIKWETE AOMBA USHIRIKIANO KUTIMIZA LENGO LA MHE. RAIS LA KUWA NA SERA ZA KIUTUMISHI NA MIUNDO YENYE TIJA KWA USTAWI WA TAIFA

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

NAIBU Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewataka watumishi wa Idara ya Uendelezaji Sera na Idara ya Uendelezaji Taasisi kumpa ushirikiano wa kutosha kwenye eneo la kusimamia uendelezaji wa sera katika Utumishi wa Umma na miundo ya Taasisi za Umma.

Mhe. Kikwete ametoa rai hiyo jijini Dodoma wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa Idara ya Uendelezaji Sera na Idara ya Usimamizi wa Taasisi kwa nyakati tofauti kilicholenga kufahamu majukumu yanayotekelezwa na Idara hizo pamoja na kuhimiza uwajibikaji.

 Amesema kuwa ili aweze kumsaidia vema Waziri mwenye dhamana kufikia lengo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuwa na sera za utumishi wa umma zenye tija na miundo inayotekelezeka kiutendaji kwa ustawi wa taifa.

Mhe. Kikwete amesema ameteuliwa na Mhe. Rais kumsaidia Waziri mwenye dhamana ya kusimamia utumishi wa umma na utawala bora, hivyo hana budi kufahamu kwa kina majukumu yanayotekelezwa na idara hizo ili aweze kuyazungumzia pale yanapohitaji ufafanuzi na uelewa kwa umma.

“Malengo ya kukutana nanyi leo ni kufahamiana na kujua majukumu yenu kwa kina kwa kuwa mimi nina jukumu la kumsaidia Mhe. Waziri kujibu maswali ya kiutumishi na utawala bora yanayoulizwa Bungeni,” Mhe. Kikwete amesisitiza.

Ameongeza kuwa, anatamani kujua kila kitu kinachofanyika katika idara hizo pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo kiutendaji kwani kwa kufanya hivyo atakuwa kwenye nafasi nzuri ya kutekeleza kwa ufanisi lengo la Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aidha, Mhe. Kikwete ameitaka Idara ya Undelezaji Sera kuhuisha sera za kiutumishi ili ziendane na wakati na ziweke mazingira rafiki ya kuzihusisha sekta binafsi kutoa mchango katika kuboresha utumishi wa umma kama Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan alivyoelekeza.

TASAC YATOA FURSA SEKTA USAFIRISHAJI MAJINI

Na Mwandishi Wetu Dodoma

SHIRIKA la Wakala wa  Meli Tanzania (TASAC) linatoa fursa katika sekta ya usafiri majini kwa kuazisha utaratibu kwa kusajili meli kwa masharti nafuu ukarabati wa ujenzi wa meli na kuazisha maegesho ya boti ndogo katika ukanda wa Pwani, viwanda vya utengenezaji wa maligafi za ujenzi wa boti za plastiki pamoja na kujenga bandari rasmi za uvuvi.

Hayo yamesemwa na Mkurugezi Mkuu wa Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) Kaim Abdi Mkeyenge wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa majukumu ya shirika. 

Mkeyenge amesema shirika hilo limefanikiwa kuboresha ufanisi wa bandari kwa kupunguza uwezo wa shehena inayoruhusiwa kukaa bandarini kwa wakati mmoja kutoka asilimia 65 hadi asilimia 50 kwa kuweka amri ya Tozo ya Bandari Kavu ambapo wamefungua ofisi 11 za Shirika katika maeneo mbalimbali ili kusogeza huduma karibu na wananchi Shirika lina ofisi katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Mtwara, Tanga, Mwanza, Kagera, Mara, Kigoma, Rukwa, Ukerewe pamoja na Geita.

Amesema TASAC imefanikiwa kukagua meli za kigeni 36 kwa kipindi kuanzia Julai 2022 hadi Desemba 2022 na kuanzia Januari 2023 wamekagua meli za kigeni 37 ambapo shirika linategemea kukagua meli 61 hadi kufikia Juni 2023.

TASAC ilianzishwa chini ya kifungu cha 4 cha Sheria ya Uwakala wa Meli Tanzania, Sura 415 na kuanza rasmi kutekeleza majukumu yake tarehe 23 Februari, 2018. 

Kuundwa kwa TASAC ni hatua ya kisera ya Serikali, kwa upande wa Tanzania Bara, inayokusudia kukuza sekta za usafiri majini, kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma hususan kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Pia kuinua mchango wa usafiri kwa njia ya maji na hii ni kwa sababu Tanzania ina ukanda mkubwa wa Bahari ya Hindi wenye urefu takriban Kilomita 1,424, Maziwa makubwa ya Victoria, Tanganyika na Nyasa

Tuesday, March 7, 2023

OSHA YAPATA MAFANIKIO

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

WAKALA wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) imefanikiwa kuongeza idadi ya maeneo ya kazi yaliyosajiliwa kutoka 4,336 hadi 11,953.

Aidha ongezeko hilo ni sawa na asimilia 276 na  idadi ya kaguzi zilizofanyika zimeongezeka kutoka kaguzi 104,203 hadi kufikia kaguzi 322,241 sawa na asilimia 132.

Hayo yameelezwa na Mtendaji Mkuu wa OSHA  Khadija Mwenda akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali na utekelezaji wa majukumu ya Wakala hiyo Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Mwenda amesema kuwa kumekuwa na ongezeko la upimaji afya za wafanyakazi kwa asilimia 320 upimaji wa afya kutoka wafanyakazi 363,820 hadi kufikia wafanyakazi milioni 1.1 waliopimwa katika kipindi hicho cha miaka miwili kutotokana na kupunguzwa kwa ada mbalimbali.

Amesema kuwa kuboreshwa mifumo ya usimamizi ambayo imewezesha maeneo mengi ya kazi kukaguliwa wafanyakazi wengi kupimwa afya na mafunzo mbalimbali kufanyika ongezeko hilo ni tafsiri kwamba hali ya usalama na afya  katika maeneo ya kazi inazidi kuimarika.

Ameongeza kuwa ongezeko la asilimia 175 ya wafanyakazi waliopata mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kutoka wafanyakazi 32,670 hadi kufikia wafanyakazi 43,318. 

"Katika kusimamia Sheria ya Usalama na Afya kwa lengo la kuzuia ajali magonjwa na vifo vitokanavyo na kazi maeneo ya kazi ambayo hayakuzingatia Sheria na Kanuni za Usalama na Afya yalichukuliwa hatua mbali mbali za kisheria zikiwemo kupewa hati ya maboresho (Improvement Notice) ambapo maeneo ya kazi 1,588 yalipewa hati hizo na maeneo ya kazi mengine 105 yalitozwa faini,"amesema Mwenda. 

Amebainisha kuwa miongoni mwa majukumu ya OSHA ni kuchunguza ajali mbali mbali zinazotokea katika sehemu za kazi kwa lengo la kubaini vyanzo vya ajali hizo ili kushauri namna bora ya kuzuia ajali kutokea tena.

Dhima kuu ya  Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ni kuelimisha na kuhamasisha masuala ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi kwa kuweka mifumo thabiti itakayo zuia ajali, magonjwa na vifo pamoja na uharibifu wa mali ili kupunguza gharama za uendeshaji na kukuza uchumi wa Taifa.


Monday, March 6, 2023

WANAWAKE WATUMIE MITANDAO KUFIKIA USAWA WA KIJINSIA

Na Mwandishi Wetu Dodoma

WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt Doroth Gwajima  amewataka wanawake wahakikishe wanatumia huduma za mitandao ili kufikia usawa wa kijinsia kwenye maendeleo kwa kupata taarifa mbalimbali za kijamii kama Afya, Elimu, Kilimo, biashara na zinginezo.

Gwajima ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yatakayofanyika March 8 mwaka huu.

Amesema kuwa  pengo la wanawake kumiliki simu na kutumia Mtandao linaongezeka zaidi kwa wanawake wenye umri  mkubwa ( wazee) , wanawake wanaoishi vijinini, pamoja na wanawake wenye ulemavu Mwaka 2022 takwimu zinaonesha asilimia 63 ya wanawake duniani walitumia Mtandao ukilinganisha na asilimia 69 ya wanaume.

Aidha amesema kuwa kwa kushirikiana na jamii yenyewe serikali itaendelea kuelimisha na kufanyia kazi kuondoka vikwazo vyote vinavyozuia mwanamke kutumia Teknolojia ya kidigitali.

Pia ametoa wito kwa wanawake na jamii kwa ujumla kujitokeza kuadhimisha sikukuu ya wanawake duniani chini ya uongozi wa waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na ameimiza wanawake kujiunga na majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi yaliyo ngazi zote Hadi vijinini Ili kunufaika na uwezeshaji wa serikali na wadau wake.

Sunday, March 5, 2023

WATATU WAFA AJALINI WAMO ASKARI POLISI WAWILI

WATU watatu wakiwemo askari wawili wa Wilaya ya Kipolisi Chalinze Mkoa wa Pwani wamefariki dunia huku mmoja akijeruhiwa baada ya gari dogo walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani ACP Pius Lutumo alisema kuwa watu hao walifariki papo hapo.

Lutumo alisema kuwa tukio hilo lilitokea mnamo Machi 5 mwaka huu majira ya saa 11:45 alfajiri huko maeneo ya Mavi ya Ng'ombe Kijiji cha Mboga Kata ya Msoga Tarafa ya Chalinze katika Barabara ya Chalinze/Segera.

"Gari lenye namba za usajili T 323 BAL aina ya Toyota Cresta likiendeshwa na mkaguzi msaidizi wa Polisi Ndwanga Dastani (28) askari wa kituo cha Polisi Chalinze akitokea Chalinze kuelekea Lugoba liliacha njia kutoka upande wa kushoto wa barabara na kwenda upande wa kulia na kugonga kalavati kisha kupinduka na kusababisha vifo vya watu watatu na mmoja kujeruhiwa,"alisema Lutumo.

Aliwataja askari waliokufa kuwa ni Mkaguzi msaidizi wa Polisi Ndwanga Dastani (28) aliyekuwa dereva wa gari hilo, Konstebo  Emmiliana Charles (26) wote askari wa kituo cha Polisi Chalinze na Karimu Simba (27) ambaye ni karani wa Mahakama ya Wilaya Lugoba.

"Majeruhi huyo ambaye naye  ni askari wa Kituo cha Polisi Chalinze Konstebo Mwanaidi Shabani (25) ameumia maeneo mbalimbali ya mwili wake na amepelekwa katika Hospital ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi,"alisema Lutumo.

Aidha alisema kuwa uchunguzi wa awali umeweza kubaini kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi na dereva kushindwa kulimudu gari na kupinduka.

"Miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Lugoba kwa ajili ya kusubiri taratibu za mazishi,"alisema Lutumo.

Thursday, March 2, 2023

WATAKA KUHARAKISHWA UJENZI NYUMBA YA MKURUGENZI NA WAKUU WA IDARA

MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha wametaka kuharakishwa ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi na wakuu wa Idara kwani imepita muda mrefu ujenzi huo bado haujaanza.

Wakizungumza kwenye kikao cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo walisema kuwa kwa kuwa tayari azimio la ujenzi huo limeshapitishwa hakuna sababu ya kuchelewesha ujenzi.

Diwani wa Kata ya Mtambani Godfrey Mwafulilwa alisema kuwa kama hakuna changamoto yoyote ni vema kuanza ujenzi ili watumishi hao wawe na makazi ndani ya Halmashauri.

Mwafulilwa alisema kuwa kama eneo hilo halina mgogoro wowote kwanini ujenzi hauanzi ambapo eneo hilo ni jirani na ilipojengwa hospitali ya Wilaya.

"Tunataka kikao kijacho tupate majibu kuwa ujenzi unaanza lini ili tuweze kuufanya kwa wakati kwani hakuna sababu ya kuchelewesha ujenzi,"alisema Mwafulilwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Erasto Makala alisema kuwa baadhi ya Madiwani walikuwa na hofu kuwa eneo hilo lilikuwa na migogoro.

Makala alisema kuwa eneo hilo lilikuwa na migogoro baadhi ya watu waliibuka na kusema ni lao hivyo kama lina changamoto ni vema wakaelezea ili waweze kujua.

Naye Ofisa Ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Brown Nziku alisema kuwa eneo hilo zamani lilikuwa likimilikiwa na Taasisi ya Mkonge na kupewa kampuni ya UFC lakini ilifutiwa hati na Rais ambapo watu walilivamia.

Nziku alisema kuwa baada ya kurudishwa serikalini ilikabidhiwa Halmashauri ambapo walipewa hekari 9.5 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi na wakuu wa Idara.

Alisema kuwa kwa sasa hatua iliyofikiwa ni ya manunuzi na baada ya hapo ujenzi utaanza mara moja.


NANE WAJERUHIWA AJALI YA BASI LA HAPPY NATION

WATU nane wamejeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria la kampuni ya Happy Nation kutoka Bukoba kwenda Dar es Salaam kuacha njia na kupinduka.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa Polisi Mkoani Pwani ACP Pius Lutumo alisema kuwa basi hilo lilipinduka baada ya kujaribu kulipita gari lililokuwa limesimama.

Lutumo alisema kuwa ajali hiyo ilitokea Februari 2 mwaka huu majira ya 8:30 usiku kwenye Kijiji cha Ruvu Kata ya Vigwaza Wilaya ya Kipolisi Chalinze Bagamoyo.

"Basi hilo lenye namba za usajili T 526 DVJ lilikuwa likiendeshwa na Vincent Mbasha (39) mkazi wa Mbezi Jijini Dar es Salaam na chanzo lilikuwa likilikwepa gari la mizigo aina ya Scania lenye namba T 299 BYF na tela namba T 308 BYF lilikuwa limepata hitilafu na kutoweka alama yoyote kuashiria kuwa kuna gari ndipo dereva huyo wa basi akalikwepa na kupinduka,"alisema Lutumo.

Alisema kuwa basi hilo lilikuwa na abiri 47 ambapo majeruhi wako hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi kwa matibabu zaidi ambapo hali zao zinaendelea vizuri. 

Aidha aliwataja majeruhi hao kuwa ni Nuru Mohamed (38), Selimanda Abdala (63), Amina Jumanne (48), Faudhia Ismail (23), Fredina Omary (15) Abtatus Jovin (18), Idat Reman (27) na Aida Suleiman (24).

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ambaye aliwatembelea majeruhi hao alisema kuwa madereva wanapaswa kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zisizo za lazima.

Kunenge alisema kuwa alipata taarifa kuwa dereva huyo alitaka kulipita gari hilo upande wa kulia badala ya kushoto ambapo ni uzembe hivyo ni vema wakazingatia sheria.

Naye Mganga mfawidhi wa Tumbi Amani Malima alisema kuwa waliwapokea majeruhi hao ambapo wameumia maeneo mbalimbali ya miili yao na wanaendelea vizuri na matibabu.

Malima alisema kuwa wagonjwa hao wanaendelea na vipimo mbalimbali vikubwa ilikugundua majeruhi hao wameumia kiasi gani.


Wednesday, March 1, 2023

MAOFISA ELIMU KATA,WALIMU WAJENGEWA UWEZO

HALMASHAURI ya Mji Kibaha imeendesha semina ya kuwajengea uwezo maofisa Elimu kata,walimu walimu wa shule za msingi na sekondari juu ya masuala ya VVU/UKIMWI mahala pa kazi kwa lengo la kuondoa unyanyapaa na ukatili wa kijinsia.

Mratibu wa UKIMWI wa Halmashauri ya Mji Kibaha Siwema Cheru amesema semina hiyo ni mwendelezo wa Mafunzo mengine ambayo yamekuwa yakitolewa kwa wadau mbalimbali ili kuondoa vitendo vya unyanyasaji sehemu za kazi na kwamba sasa wamefikiwa waratibu wa Elimu kata na walimu ambao ni wadau wakubwa kwenye jamii na wanakaa na wanafunzi muda mrefu ambao pia ni wahanga


Dr.Mariam Ngaja ameeleza kuwa walimu wakipata uelewa wa semina hiyo wanawajibu wa kuwafundisha wanafunzi wao kuhusu afya ya uzazi kwa Vijana na maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya ngono na Elimu ya madawa ya kulevya.


Ngaja ameongeza kuwa semina hiyo ambayo ni utekezaji wa Kawaida wa Idara ni utekelezaji wa mkakati wa nne wa Taifa wa kudhibiti UKIMWI Tanzania hasa kwa wasichana balehe na wanawake Vijana .


Mwalimu Augustine Seso aliyeshiriki semina hiyo ameishukuru Halmashauri kwa kuigharamia na kwamba imewafikia muda muafaka na Sasa wanakwenda kwenye jamii kutimiza lengo la kutoe Elimu ili kuondosha unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kwenye jamii.

WATENDAJI KATA WAKABIDHIWA PIKIPIKI

HALMASHAURI ya wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani imewapatia Pikipiki watendaji wa Kata tano ili kuondoa changamoto ya kushindwa kuyafikia maeneo ambayo hayafikiki kirahisi.

Akikabidhi Pikipiki hizo kwa watendaji hao wa Kata katika ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mbunge wa Kibaha Vijijini Michael Mwakamo amewataka watendaji kuzitumia pikipiki hizo kama ilivyokusudiwa na serikali na siyo kwenda kuzifanya boda boda.

Mwakamo amesema kuwa pikipiki hizo ni kutoka Serikali kuu kwa ajili ya kuondoa changamoto ya usafiri kwa watendaji kata ili kuwarahisishia majukumu yao. 

"Niwasihi watendaji waliopewa pikipiki leo mkazitumie kama ilivyokusudiwa na tusizikute zimebeba abiria mtaani maana siyo nia ya kukabidhiwa bali ni kutekeleza majukumu ya kazi zenu,"amesema Mwakamo.

Amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kuhakikisha wanawasaidia kwenye matengenezo na kuwawekea mafuta pikipiki hizo kwani ni vyombo vya kazi na wasivitumie kama vyombo binafsi. 

Awali Mwakamo aliishukuru Serikali ya awamu ya Sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza ahadi ya kutoa vitendea Kazi kwa watendaji wa ngazi zote Ili kurahisisha utendaji kazi kwa watumishi wa Umama.Kata zilizopokea pikipiki ni Soga, Magindu, Kwala, Gwata na Dutumi ambazo ni kata zilizopo pembezoni mwa Halmashauri.

WALIMU KUZAWADIWA VIWANJA



KATIKA kuhakikisha wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne hawapati sifuri Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema itatoa viwanja kwa walimu shule zao zitakazofanya vizuri.

Akizungumza kwenye kikao cha wadau wa elimu kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha kilichofanyika Kibaha alisema kuwa kuna changamoto katika ufuaulu na masomo ya Sayansi.

John alisema kuwa lengo ni kuondoa asilimia 50 ya wanafunzi ambao wanashindwa kuendelea na masomo kutokana na kutofanya vizuri kwenye mitihani yao ya kumaliza kidato cha nne.

"Tutatoa viwanja kwa walimu ambao watafanya vizuri kwa kuongeza ufaulu ambapo tungetamani kusiwe na daraja sifuri na daraja la nne kwani madaraja haya yanawafanya wasiweze kuendelea na masomo tunataka angalau kuanzia daraja la tatu na kupanda juu,"alisema John.

Alisema kuwa mbali ya kutoa viwanja pia kutakuwa na motisha mbalimbali zitatolewa ikiwemo fedha taslimu kwa walimu watakaofanya vyema na mkazo utawekwa kwenye masomo ya Sayansi ambayo matokeo yake siyo mazuri.

"Pia tunataka Mwalimu anapaswa kuhakikisha mwanafunzi katika somo lake apate alama C na kama atashindwa kufikia hapo itabidi aulizwe changamoto ni nini,"alisema John.

Aliwataka wazazi na wadau wa elimu kushirikiana na shule ili kufanikisha kuondoa sifuri kwenye shule za sekondari zilizokwenye Halmashauri ya Mji Kibaha.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Musa Ndomba alisema kuwa uongozi wa shule ukabili changamoto na siyo kulalamika hata kwa mambo yaliyo ndani ya uwezo wao.

Ndomba alisema kuwa watahakikisha mipango na mikakati iliyowekwa wanaitekeleza ili kuondoa matokeo mabaya kwa wanafunzi wanaomaliza elimu ya Sekondari ili kupata wasomi watakaoshiriki kwenye uchumi ikizingatiwa mkoa wa Pwani ni wa viwanda.

Awali ofisa Elimu Halmashauri ya Mji Kibaha Rosemary Msasi alisema kuwa ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha nne kwa kipindi cha miaka mitano 2018 hadi 2022 umeongezeka.

Msasi alisema kuwa ufaulu huo umeongezeka kwa asilimia 7.89 kwa kutoka asilimia 84.4 hadi asilimia 92.2 na ule wa kidato cha sita kutoka asilimia 99.4 hadi asilimia 100.9.

Baadhi ya walimu wakuu ambao shule zao zilifanya vizuri walisema kuwa kikubwa ni ushirikiano uliopo baina ya walimu wazazi na wanafunzi na Halmashauri.

Kikao hicho cha wadau baadhi ya walioshiriki ni pamoja na kamati ya usalama Wilaya, maofisa elimu wa Kata, watendaji wa kata, wakuu wa shule za msingi na sekondari.

Mwisho.