Thursday, January 8, 2015

CHANGAMOTO YA MAJI NA VIONGOZI WAUZA KIJIJI

Na John Gagarini, Chalinze
UONGOZI wa Mradi wa maji wa Wami Chalinze wilayani Bagamoyo umetakiwa kutoa taarifa juu ya ukosefu wa maji ambao kwa sasa umedumu takribani mwezi mzima ambapo baadhi ya wanasiasa wa vyama vya upinzani wapotosha ukweli kuhusu tatizo hilo.
Hayo yalisemwa na diwani wa kata ya Bwilingu Nassa Karama katika viwanja vya Masoko wakati mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alipokwenda kusikiliza kero za wananchi wa kata hiyo.
Karama alisema kuwa maji kwa sasa ni kilio kikubwa kwa wakazi wa mjin huo  huku wao wakiwa hawana utaalamu wa kujua tatizo la ukosefu wa maji linatokana na nini hivyo kushindwa kuwapa majibu sahihi wananchi ambapo hali hiyo imesababishwa ndoo kuuzwa kwa shilingi 700 kutoka shilingi 200.
“Suala la kutotoka kwa maji ni la kitaalamu na wahusika wa mradi wa maji wa Wami Chalinze wanapaswa kutoa taarifa juu ya changamoto zinazosababisha ukosefu wa maji ili majibu yasitolewe na wanasissa ambao wanatumia fursa hiyo kupotosha ukweli wa tatazi hilo,” alisema Karama.
Alisema kuwa wananchi wanapata usumbufu mkubwa kwani kwa sasa wananunua maji kwa baadhi ya watu wenye magari ya kuuza maji ambapo kabla ya tatizo hilo walikuwa walikuwa wakinunua kwa sh.200 na sasa ni sh.700 hali inayosababisha kuwapa wakati mgumu baadhi ya wananchi  ambao baadhi yao kipato chao ni cha chini.
“Baadhi ya wanasiasa hao wanapotosha kwa wananchi kuwa kuna mashine mbalimbali za kukamilisha mradi huo zimeuzwa Nairobi nchini Kenya jambo ambalo linachanganya wananchi na kuleta tafsiri tofauti  kutokana na tatizo hilo,” alisema Karama.
Aliutaka uongozi wa maradi kuo kutoa taarifa juu ya ukosefu wa maji ili kutowapa mwanya wanasiasa  wenye nia ya kutumia jambo hilo kama mtaji wao wa kisiasa.
Naye Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akijibu kuhusiana na maswali hayo alisema anafanya taratibu ya kumpeleka waziri wa maji ili aweze kwenda kutembelea maeneo yenye kero kubwa jimboni humo kujionea hali halisi ya ukosefu wa maji.
Ridhiwani alisema kuwa tatizo kubwa la ukosefu wa maji linatokana na tope linaloingia katika mitambo hali inayosababisha maji kushindwa kutokana ambapo kwa sasa wamenunua chujio kwa ajili ya kuchuja uchafu ambao umekuwa ukiziba na maji kushindwa kutoka.
Aliwataka wanasiasa kuacha kupotosha ukweli kwani si jambo zuri kupotosha wananchi  na kuwataka wataalamu kujenga tabia ya kutoa taarifa ya vikwazo vilivyopo ili wananchi wajue.
Mwisho.
Na John Gagarini, Fukayosi
BAADHI ya  viongozi wa Kijiji cha Kidomole wilayani Bagamoyo mkoani Pwani waliohusika kuuza ardhi ya Kijiji hicho kinyume cha sheria wametakiwa kujiandaa kusimama kwenye vyombo vya sheria kujibu tuhuma hizo.
Viongozi hao kwa wameuza eneo kubwa la Kijiji ambapo wananchi wa maeneo hayo wanatakiwa kuondoka na kumpisha mununzi huyo ambaye amechukua eneo kubwa la kijiji.
Akizungumza na wananchi wa Kijiji hicho Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete, wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua shughuli za maendeleo alisema viongozi hao lazima wachukuliwe hatua za kisheria kwa ukiukaji wa maadili ya uongozi.
“Inashangaza kuona mtu anakuja na risiti na kusema kuwa kanunua eneo lote la Kijiji na wananchi wanatakiwa kuondoka kumpisha eti mwekezaji jambo kama hili haliwezekani kwani taratibu haziruhusu na viongozi waliofanya hivi wajiandae kwa kukimbilia tutapambana nao ili haki ya wananchi ipatikane,” alisema Ridhiwani.

Alisema kuwa hatakuwa tayari kuona wananchi hao wanaondolewa kwani sheria za ardhi haziruhusu kuuza eneo la Kijiji zaidi ya hekari 50 zaidi ya hapo lazima suala hilo lipelekwe kwa kamishana wa ardhi.

“Inashangaza kusikia kiongozi kauza hekari zaidi ya 100 kwa mwekezaji sheria haisemi hivyo hata hizo hekari 50 lazima wanakijiji waridhie kwa kufanya mkutano mkuu ili kumpitisha muombaji lakini siyo watu wawili au watatu wanakaa huko ofisini na kuuuziana eneo kinyemela utaratibu huu haupo kisheria,” alisema Ridhiwani.

Akizungumzia kuhusiana na baadhi ya maeneo ya Kijiji kuwemo kwenye eneo la ranchi ya Taifa (NARCO) alisema kuwa uongozi wa halmashauri unapaswa kuonyesha mipaka kwani wananchi walioko kwenye eneo hilo walianza kuishi kabla ya ranchi hiyo.

Aidha alisema maeneo yote yanayomilikiwa na ranchi ya Taifa yaliwekewa mipaka na inajulikana rasmi kisheria tofauti na hapo ambapo ranchi hiyo ndo inaanza kuonyesha mipaka huku kukiwa hakuna alama yoyote na kuutaka uongozi wa ranchi kushirikiana na wananchi hao ili kuondoa malalamiko kwani wanapaswa kuondolewa kwenye maeneo hayo.
Mwisho.



Wednesday, January 7, 2015

WAKAZI CHALINZE WALALAMIKA UKOSEFU WA DAWA KITUO CHA AFYA

Na John Gagarini, Chalinze
WAKAZI wa Chalinze Mjini wameiomba Wizara ya Afya kuangalia upya mgawanyo wa dawa kwenye kituo cha Afya cha Chalinze kwani dawa zinazopelekwa kituoni hapo hazikidhi mahitaji.
Wagonjwa wengi wanaokwenda kuhudumiwa kituoni hapo licha ya kuandikiwa dawa hazipatikani na hutakiwa kununua kwenye maduka ya dawa.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mbele ya Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ambaye yuko kwenye ziara ya kukagua masuala ya maendeleo, moja ya wakazi wa Chalinze kitongoji cha Bwiringu aliyejitambulisha kwa jina la Athuman Rashid alisema huduma ya dawa hakuna kabisa.
“Kila ukienda kupata huduma kwenye kituo cha afya Chalinze utahudumiwa vizuri lakini dawa ni mtihani kwani utaambiwa dawa hakuna nenda kanunue kwenye maduka ya dawa,” alisema Rashid.
Rashid alisema kuwa mgawanyo wa dawa kwenye kituo hicho ni mdogo licha ya kuwa kituo hicho kinahudumia wagonjwa wengi lakini kinakuwa na upungufu mkubwa wa dawa.
“Ombi letu sisi kwa Wizara ya Afya ni kuangalia namna gani ya kukiwezesha kituo hichi kuwa na mgao mkubwa wa dawa kwani suala la dawa ni tataizo kubwa sana na linatuathiri kwani maduka ya madawa yanauza kwa bei za juu,” alisema Rashid.
Naye Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa ni kweli changamoto hiyo ni kubwa sana kwenye kituo hicho na ni vema kituo hicho kikaangaliwa upya.
“Wagonjwa wamekuwa wakilalamika sana juu ya upatikanaji wa dawa kwani kituo hichi kinapewa dawa sawa na vituo vingine vya afya ambavyo havina wagonjwa wengi,” alisema Ridhiwani.
Ridhiwani alisema tayari wameshaongea na Wizara hiyo na stoo ya madawa MSD juu ya kuomba kuongezewa mgao wa dawa kutokana na ukubwa wa kituo kwani mahitaji ni makubwa sana.

Mwisho.    w

Tuesday, January 6, 2015

MBUNGE WA JIMBO LA CHALINZE RIDHIWANI KIKWETE AENDELEA NA ZIARA JIMBONI

Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo Ridhiwani Kikwete akiwahutubia wakazi wa Kijiji cha Pera kweny kata ya Kibindu wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wakati wa ziara ya kutembela shughuli za maendeleo

 Ridhiwani Kikwete Mbunge wa Jimbo la Chalinze akikabidhi mpira kwa moja ya Wazee kwenye Kijiji cha Pera Kata Kibindu wakati wa zaiara yake kwenye jimbo hilo

 Hili ni darasa la shule ya msingi ya Kibindu ambayo iliezuliwa paa baada ya kutokea mvua kubwa iliyonyesha mwishoni mwa mwaka jana

 Diwani wa Kata ya Kibindu Mawazo Mkufya akiongea na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete mwenye kofia alipotembelea shule hiyo kuangalia uharibifu uliotokana na mvua kubw ailiyonyesha na kuharibu baadhi ya madarasa na ofisi ya mwalimu mkuu wa shule hiyo

 Moja ya Madarasa ya shule ya Msingi Kibindu yaliyoharibiwa na mvua kubw ailiyonyesha mwaishoni mwa mwaka jana 

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kulia akiongea na waandishi wa habari hawapo kushoto ni diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya. 

 Baadhi ya akinamama wa Kijiji cha Kibindu wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete hayupo pichani wakati wa ziara yake kwenye jimbo hilo

 Choo cha shule ya Msingi Maluiwi kikiwa kimebomoka hali ambayo inawafanya wanafunzi wa shule hiyo kujisaidia porini kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

 Hichi ni choo cha nyasi ambacho kinatumiwa na walimu wa shule ya Msingi Maluiwi

 Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete akiongea na wananchi wa Kitongoji cha Mdaula alipotembelea kwenye ziara yake ya kuangalia shughuli za maendeleo kwenye jimbo hilo.

Monday, January 5, 2015

MCHAKATO WA MAMLAKA YA MJI MDOGO CHALINZE CHANGAMOTO KUBWA, MAJAMBAZI WATUMIA MSITU WA MWIDU

Na John Gagarini, Ubena
MCHAKATO wa kuifanya Chalinze kuwa mamlaka ya Mji Mdogo umekumbwa na changamoto kubwa baada ya makundi mawili ya wakulima na wafugaji kupinga mpango huo.
Makundi hayo ambayo ndiyo makubwa katika Jimbo la Chalinze yameonekana kutoupokea mpango huo kwa madai kuwa utawasababisha kushindwa kufanya shughuli za ambazo ndizo zinazowafanya waweze kuishi.
Changamoto za kupinga mchakato huo zimebainika wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete kutembelea shughuli za maendeleo.
Akizungumzia changamoto hizo Ridhiwani alisema Jimbo hilo lilitenga maeneo kwa ajili ya wafugaji na wakulima katika mpango bora wa matumizi ya ardhi ambapo kila kundi linakaa kwenye eneo lake.
“Changamoto hizi zinakuja kutokana na hali halisi kuwa endapo mamlaka hiyo itakubalika ina maana kutakuwa na sheria ya kuzuia ufugaji wa mifugo pamoja na kuzuia kilimo huku makundi hayo yakitegemea shughuli hizo kuendeshea maisha yao,” alisema Ridhiwani.
Ridhiwani alitoa mfano kwenye maeneo ya wafugaji ya Vijiji vya Chamakweza ambao wana mifugo zaidi ya 18,000, Lukenge wana mifugo zaidi ya 10,000 na Matuli mifugo zaidi ya 8,000.
“Wafugaji wamesema kuwa endapo Mamlaka hiyo itapitishwa mifugo yao wataipeleka wapi na wao ufugaji ndiyo maisha yao kwa ajili ya chakula pamoja na uchumi,” alisema Ridhiwani.
Alisema pia kwa wakulima nao hawataruhusiwa kulima je wataishije wakati kilimo ndiyo shughuli yao ya kuendeshea maisha yao ikiwa ni pamoja na uchumi wao na hawana kitu kingine wanachoweza kukifanya.
“Changamoto hizi katika kueleka Mji Mdogo zimekuwa ni kubwa na ukiangalia zina uzito hivyo mchakato huu umesitishwa huku serikali ikiwa inaangalia namna bora ya kufanya ili kutoathiri maisha ya wananchi,” alisema Ridhiwani.
Aliongeza hata hivyo wananchi wanapaswa kujiandaa na mabadiliko kwani kila jambo lina wakati wake ambapo mipango kama hiyo ina lengo la kuwasogezea huduma karibu wananchi.
Mwisho.
Na John Gagarini, Ubena
WANANCHI wa Kata ya Ubena Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani wameuomba uongozi wa Gereza la Ubena kuwaruhusu kulitumia eneo la pori la Mwidu kwenye barabara ya Morogoro Chalinze ambalo limekuwa likitumiwa na majambazi kujificha kwa ajili ya kuteka magari nyakati za usiku.
Ombi hilo lilitolewa na diwani wa kata hiyo Mrisho Choka mbele ya Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ambaye yuko kwenye ziara kutembelea Jimbo hilo kukagua shughuli za maendeleo.
Choka alisema kuwa kuwa pori hilo limekuwa likitumiwa na majambazi ambao hujificha kisha kutega magogo barabarani na kusababisha ajali kisha kufanya uhalifu kwa kutumia silaha mbalimbali.
“Eneo hili limekuwa hatarishi kwa magari hasa nyakati za usiku ambapo kumekuwa na matukio mengi ya utekwaji wa magari ambayo kabla ya kutekwa husababishiwa ajali kwa kuwekewa magogo hivyo tunauomba uongozi wa gereza kuturuhusu tutumie eneo hilo ili kuzuia vitendo hivyo,” alisema Choka.
Alisema kuwa endapo wananchi watalitumia eneo hilo itasaidia kupunguza vitendo hivyo kwani kwa ambapo kwa sasa majambazi hao wanafanya wanavyotaka kutokana na eneo hilo kuwa pori.
Aidha alisema kuwa wiki iliyopita magari manne yalitekwa na katika kukabiliana na uhalifu katika eneo hilo wamekuwa wakifanya doria na askari polisi lakini hata hivyo majambazi hao wamekuwa wakiwategea na kutekeleza uhalifu.
Kwa upande wake Ridhiwani Kikwete alisema kuwa ombi lao atalipeleka kwenye vyombo husika ili lifanyiwe kazi ili kuondokana na vitendo hivyo ambavyo vimekithiri katika eneo hilo.

Mwisho.

Sunday, January 4, 2015

WALILIA WODI YA WAZAZI

Na John Gagarini, Chalinze
WANANCHI wa Kijiji cha Kwaruhombo kwenye Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wametoa kilio cha kujengewa wodi ya wazazi kwenye kituo cha afya cha Kwaruhombo ili wanawake wajawazito wasijifungue kwenye wodi za kawaida.
Akizungumza kijijini hapo wakati wa ziara ya maendeleo ya mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete, Hadija Stambuli alisema kuwa akinamama wamekuwa wakijifungulia kwenye wodi hivyo kutokuwa na usiri.
Stambuli alisema kuwa hiyo imekuwa changamoto kubwa kwa akinamama wanapokwenda kujifungua wamekuwa wanashindwa kusitiriwa wakati wa uzazi.
“Tunakuomba Mbunge wetu utusaidie wakinamama ili tunapokwenda kujifungua kwani hakuna usiri hivyo tungepata jengo maalumu kwa ajili ya kujifungungulia ingekuwa vizuri,” alisema Stambuli
Akijibu malalamiko hayo mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa kujifungua ni jambo jema na linahitaji usiri.
Ridhiwani alisema kuwa kwa kushirikiana na halmashauri ili kuhakikisha kunakuwa na jengo kwa ajili ya kinamama kujifungulia.
“Tutakaa na uongozi wa Halmashauri ili kuhakikisha kunakuwa na jengo maalumu kwa ajili ya kujifungulia ili kuwaondolea fadhaa akinamama wakati wakijifungua,” alisema Ridhiwani.
Aidha alisikitishwa na matumizi mabaya ya mafuta kwa ajili ya gari la wagonjwa wanaopata rufaa na kuutaka uongozi wa kituo hicho kuhakikisha kinadhibiti matumizi hayo.

Mwisho.

WANANCHI WAMLALAMIKIA MWEKEZAJI

Na John Gagarini, Chalinze
WAWEKEZAJI kwenye Kijiji cha Changarikwa wametakiwa kufuata taratibu za kisheria ili kuondoa migogoro baina yao na wananchi.
Hayo yalisemwa na mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete, wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji hicho kwenye ziara yake ya maendeleo jimboni humo.
Ridhiwani alitoa ushauri huo kufuatia wananchi hao kulalamika dhidi ya moja ya wawekezaji kwenye kijiji hicho kuchukua eneo lenye ukubwa wa hekari 500 na kutotimiza ahadi za kuwasaidia kwenye huduma za kijamii.
Moja ya wananchi wa Kijiji hicho Bakary Hatibu alisema kuwa mwekezaji huyo wakati anaomba ardhi hiyo moja ya masharti waliyokubaliana naye ni kuwajengea shule, zahanati na trekta lakini sasa ni miaka 15 hakuna hata kimoja alichotekeleza.
“Tumekuwa tukipata tabu kwani wakati mwingine tnazuiwa kupita kwenye maeneo amabayo yanamilikiwa na mwekezaji,” alisema Hatibu.
Kwa upande wake Mbunge huyo alisema kuwa kumekuwa na malalamiko mengi dhidi ya wawekezaji kujipatia maeneo pasipo kutimiza masharti ya maombi ya ardhi.
“Jambo la kushangaza ni mwekezaji kupewa hekari 500 na kijiji jambo ambalo ni kinyume cha sheria ya ardhi namba 5 ya mwaka 1999 inayosema kuwa kijiji kinauwezo wa kumpa mwekezaji si zaidi ya hekari 50,” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa kama wameona mwekezaji hafai kwani wao ndiyo waliompa ardhi wanauwezo wa kumnyanganya kwa kufuata taratibu za kisheria endapo wataona ameshindwa kutekeleza ahadi wakati anaomba ardhi.
“Mnauwezo wa kumuondolea umiliki endapo atakiuka masharti kwani huo ni mkataba na endapo atakiuka masharti unaweza kuvunjika na ardhi ikarudishwa kwa wanakijiji,” alisema Ridhiwani.
Alisema ni vema wawekezaji wakatekeleza tatatibu ili kuwa na ushirikiano na wananchi ambao wanatoa ardhi yao ili nao wanufaike nayo.
Mwisho.


Saturday, January 3, 2015

SHULE HATARIN I KUWAANGUKIA WANAFUNZI

 Baadhi ya wananchi na wafanyabiashara wa Kijiji cha Kibindu wilayani Bagamoyo wakimsikiliza Mbunge wao wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete alipotembelea Kijiji hicho wakati wa ziara yake ya kushukuru wananchi baada ya kumchagua kuwa mbunge miezi kadhaa iliyopita

 Akinamama wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete hayupo pichani baada ya kutembelea kijiji cha Kibindu kutoa shukrani kwa wananchi kumchagua kwenye nafasi hiyo miezi kadhaa iliyopita.

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kibindu wilayani Bagamoyo mkoani Pwani

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza na waandishi wa Habari mbele ya jengo la shule ya Msingi Kibindu ambalo lilianguka kufuatia mvua kubwa ziulizonyesha mwishoni mwa mwaka jana kushoto ni diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya.


 Moja ya madarasa ya shule ya msingi Kibindu likiwa limebomoka kufuatia mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa mwaka jana.

 Diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya aliyenyanyua mikono juu akitoa maelezo kwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kulia aliyevaa kofia ya kijani kufuatia mvua kubwa kubomoa madarasa ya shule ya Msingi Kibindu

 Moja ya Madarasa ya shule ya Msingi Kibindu likiwa limeezuliwa paa kufuatia mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa mwaka jana na kusababisha madarasa mawili na ofisi ya mwalimu mkuu kuharibika.

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete akikabidhi mpira kwa baadhi ya viongozi wa timu za soka za Kijiji cha Kibindu

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akionge na wananchi wa Kijiji cha Kibindu alipofanya ziara ya kushukuru wananchi wa Jimbo hilo kwa kumchagua kushika nafasi hiyo miezi kadhaa iliyopita.