Thursday, January 8, 2015

CHANGAMOTO YA MAJI NA VIONGOZI WAUZA KIJIJI

Na John Gagarini, Chalinze
UONGOZI wa Mradi wa maji wa Wami Chalinze wilayani Bagamoyo umetakiwa kutoa taarifa juu ya ukosefu wa maji ambao kwa sasa umedumu takribani mwezi mzima ambapo baadhi ya wanasiasa wa vyama vya upinzani wapotosha ukweli kuhusu tatizo hilo.
Hayo yalisemwa na diwani wa kata ya Bwilingu Nassa Karama katika viwanja vya Masoko wakati mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alipokwenda kusikiliza kero za wananchi wa kata hiyo.
Karama alisema kuwa maji kwa sasa ni kilio kikubwa kwa wakazi wa mjin huo  huku wao wakiwa hawana utaalamu wa kujua tatizo la ukosefu wa maji linatokana na nini hivyo kushindwa kuwapa majibu sahihi wananchi ambapo hali hiyo imesababishwa ndoo kuuzwa kwa shilingi 700 kutoka shilingi 200.
“Suala la kutotoka kwa maji ni la kitaalamu na wahusika wa mradi wa maji wa Wami Chalinze wanapaswa kutoa taarifa juu ya changamoto zinazosababisha ukosefu wa maji ili majibu yasitolewe na wanasissa ambao wanatumia fursa hiyo kupotosha ukweli wa tatazi hilo,” alisema Karama.
Alisema kuwa wananchi wanapata usumbufu mkubwa kwani kwa sasa wananunua maji kwa baadhi ya watu wenye magari ya kuuza maji ambapo kabla ya tatizo hilo walikuwa walikuwa wakinunua kwa sh.200 na sasa ni sh.700 hali inayosababisha kuwapa wakati mgumu baadhi ya wananchi  ambao baadhi yao kipato chao ni cha chini.
“Baadhi ya wanasiasa hao wanapotosha kwa wananchi kuwa kuna mashine mbalimbali za kukamilisha mradi huo zimeuzwa Nairobi nchini Kenya jambo ambalo linachanganya wananchi na kuleta tafsiri tofauti  kutokana na tatizo hilo,” alisema Karama.
Aliutaka uongozi wa maradi kuo kutoa taarifa juu ya ukosefu wa maji ili kutowapa mwanya wanasiasa  wenye nia ya kutumia jambo hilo kama mtaji wao wa kisiasa.
Naye Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akijibu kuhusiana na maswali hayo alisema anafanya taratibu ya kumpeleka waziri wa maji ili aweze kwenda kutembelea maeneo yenye kero kubwa jimboni humo kujionea hali halisi ya ukosefu wa maji.
Ridhiwani alisema kuwa tatizo kubwa la ukosefu wa maji linatokana na tope linaloingia katika mitambo hali inayosababisha maji kushindwa kutokana ambapo kwa sasa wamenunua chujio kwa ajili ya kuchuja uchafu ambao umekuwa ukiziba na maji kushindwa kutoka.
Aliwataka wanasiasa kuacha kupotosha ukweli kwani si jambo zuri kupotosha wananchi  na kuwataka wataalamu kujenga tabia ya kutoa taarifa ya vikwazo vilivyopo ili wananchi wajue.
Mwisho.
Na John Gagarini, Fukayosi
BAADHI ya  viongozi wa Kijiji cha Kidomole wilayani Bagamoyo mkoani Pwani waliohusika kuuza ardhi ya Kijiji hicho kinyume cha sheria wametakiwa kujiandaa kusimama kwenye vyombo vya sheria kujibu tuhuma hizo.
Viongozi hao kwa wameuza eneo kubwa la Kijiji ambapo wananchi wa maeneo hayo wanatakiwa kuondoka na kumpisha mununzi huyo ambaye amechukua eneo kubwa la kijiji.
Akizungumza na wananchi wa Kijiji hicho Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete, wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua shughuli za maendeleo alisema viongozi hao lazima wachukuliwe hatua za kisheria kwa ukiukaji wa maadili ya uongozi.
“Inashangaza kuona mtu anakuja na risiti na kusema kuwa kanunua eneo lote la Kijiji na wananchi wanatakiwa kuondoka kumpisha eti mwekezaji jambo kama hili haliwezekani kwani taratibu haziruhusu na viongozi waliofanya hivi wajiandae kwa kukimbilia tutapambana nao ili haki ya wananchi ipatikane,” alisema Ridhiwani.

Alisema kuwa hatakuwa tayari kuona wananchi hao wanaondolewa kwani sheria za ardhi haziruhusu kuuza eneo la Kijiji zaidi ya hekari 50 zaidi ya hapo lazima suala hilo lipelekwe kwa kamishana wa ardhi.

“Inashangaza kusikia kiongozi kauza hekari zaidi ya 100 kwa mwekezaji sheria haisemi hivyo hata hizo hekari 50 lazima wanakijiji waridhie kwa kufanya mkutano mkuu ili kumpitisha muombaji lakini siyo watu wawili au watatu wanakaa huko ofisini na kuuuziana eneo kinyemela utaratibu huu haupo kisheria,” alisema Ridhiwani.

Akizungumzia kuhusiana na baadhi ya maeneo ya Kijiji kuwemo kwenye eneo la ranchi ya Taifa (NARCO) alisema kuwa uongozi wa halmashauri unapaswa kuonyesha mipaka kwani wananchi walioko kwenye eneo hilo walianza kuishi kabla ya ranchi hiyo.

Aidha alisema maeneo yote yanayomilikiwa na ranchi ya Taifa yaliwekewa mipaka na inajulikana rasmi kisheria tofauti na hapo ambapo ranchi hiyo ndo inaanza kuonyesha mipaka huku kukiwa hakuna alama yoyote na kuutaka uongozi wa ranchi kushirikiana na wananchi hao ili kuondoa malalamiko kwani wanapaswa kuondolewa kwenye maeneo hayo.
Mwisho.



No comments:

Post a Comment