Na John Gagarini,
Kibaha
ASKARI wawili wa Jeshi
la Polisi Kituo cha Ikwiriri wilayani Rufiji mkoani Pwani wamekufa baada ya
watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kuwashambulia kwa silaha baada ya kuvamia
kituo hicho.
Akizungumza na
waandishi wa habari kwa njia ya simu toka eneo la tukio Ikwiri wilayani Rufiji
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alisema kuwa majambazi hao
walitumia silha kuwaua askari hao.
Kamanda Matei alisema
kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 8 kwenye kituo hicho cha Polisi cha
Ikwiriri. Aliwataja askari waliokufa kuwa ni usiku Askari waliokufa ni namba E
8732 CPL Edger Milinga na WP 5558 PC Judith Timoth.
Alisema kuwa licha ya
kufanya mauaji hayo pia walifanikiwa kupora silaha aina mbalimbali zikiwemo SMG
2, SAR 3, Ant Riot 1, mali ya serikali na S/Gun Protector mali ya kampuni ya
Sigara Tanzania.
Aidha alisema kuwa pia
watu hao waliharibu kwa kulipiga risasi gari la polisi la kituo hicho lenye namba za usajili PT 1965.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment