Wednesday, January 21, 2015

MAJAMBAZI YAUA ASKARI WAWILI

Na John Gagarini, Kibaha

ASKARI wawili wa Jeshi la Polisi Kituo cha Ikwiriri wilayani Rufiji mkoani Pwani wamekufa baada ya watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi kuwashambulia kwa silaha baada ya kuvamia kituo hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya simu toka eneo la tukio Ikwiri wilayani Rufiji Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alisema kuwa majambazi hao walitumia silha kuwaua askari hao.

Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 8 kwenye kituo hicho cha Polisi cha Ikwiriri. Aliwataja askari waliokufa kuwa ni usiku Askari waliokufa ni namba E 8732 CPL Edger Milinga na WP 5558 PC Judith Timoth.

Alisema kuwa licha ya kufanya mauaji hayo pia walifanikiwa kupora silaha aina mbalimbali zikiwemo SMG 2, SAR 3, Ant Riot 1, mali ya serikali na S/Gun Protector mali ya kampuni ya Sigara Tanzania.

Aidha alisema kuwa pia watu hao waliharibu kwa kulipiga risasi gari la polisi la kituo  hicho lenye namba za usajili PT 1965.


Mwisho.

No comments:

Post a Comment