Na John Gagarini,
Chalinze
WAKAZI wa Chalinze
Mjini wameiomba Wizara ya Afya kuangalia upya mgawanyo wa dawa kwenye kituo cha
Afya cha Chalinze kwani dawa zinazopelekwa kituoni hapo hazikidhi mahitaji.
Wagonjwa wengi
wanaokwenda kuhudumiwa kituoni hapo licha ya kuandikiwa dawa hazipatikani na hutakiwa
kununua kwenye maduka ya dawa.
Akizungumza kwenye
mkutano wa hadhara mbele ya Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ambaye
yuko kwenye ziara ya kukagua masuala ya maendeleo, moja ya wakazi wa Chalinze
kitongoji cha Bwiringu aliyejitambulisha kwa jina la Athuman Rashid alisema
huduma ya dawa hakuna kabisa.
“Kila ukienda kupata
huduma kwenye kituo cha afya Chalinze utahudumiwa vizuri lakini dawa ni mtihani
kwani utaambiwa dawa hakuna nenda kanunue kwenye maduka ya dawa,” alisema
Rashid.
Rashid alisema kuwa
mgawanyo wa dawa kwenye kituo hicho ni mdogo licha ya kuwa kituo hicho
kinahudumia wagonjwa wengi lakini kinakuwa na upungufu mkubwa wa dawa.
“Ombi letu sisi kwa
Wizara ya Afya ni kuangalia namna gani ya kukiwezesha kituo hichi kuwa na mgao
mkubwa wa dawa kwani suala la dawa ni tataizo kubwa sana na linatuathiri kwani
maduka ya madawa yanauza kwa bei za juu,” alisema Rashid.
Naye Mbunge wa
Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa ni kweli changamoto hiyo ni kubwa sana
kwenye kituo hicho na ni vema kituo hicho kikaangaliwa upya.
“Wagonjwa wamekuwa
wakilalamika sana juu ya upatikanaji wa dawa kwani kituo hichi kinapewa dawa
sawa na vituo vingine vya afya ambavyo havina wagonjwa wengi,” alisema
Ridhiwani.
Ridhiwani alisema
tayari wameshaongea na Wizara hiyo na stoo ya madawa MSD juu ya kuomba
kuongezewa mgao wa dawa kutokana na ukubwa wa kituo kwani mahitaji ni makubwa
sana.
Mwisho. w
No comments:
Post a Comment