Na John Gagarini,
Chalinze
WAWEKEZAJI kwenye
Kijiji cha Changarikwa wametakiwa kufuata taratibu za kisheria ili kuondoa
migogoro baina yao na wananchi.
Hayo yalisemwa na
mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete,
wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji hicho kwenye ziara yake ya maendeleo
jimboni humo.
Ridhiwani alitoa
ushauri huo kufuatia wananchi hao kulalamika dhidi ya moja ya wawekezaji kwenye
kijiji hicho kuchukua eneo lenye ukubwa wa hekari 500 na kutotimiza ahadi za
kuwasaidia kwenye huduma za kijamii.
Moja ya wananchi wa
Kijiji hicho Bakary Hatibu alisema kuwa mwekezaji huyo wakati anaomba ardhi
hiyo moja ya masharti waliyokubaliana naye ni kuwajengea shule, zahanati na
trekta lakini sasa ni miaka 15 hakuna hata kimoja alichotekeleza.
“Tumekuwa tukipata
tabu kwani wakati mwingine tnazuiwa kupita kwenye maeneo amabayo yanamilikiwa
na mwekezaji,” alisema Hatibu.
Kwa upande wake Mbunge
huyo alisema kuwa kumekuwa na malalamiko mengi dhidi ya wawekezaji kujipatia
maeneo pasipo kutimiza masharti ya maombi ya ardhi.
“Jambo la kushangaza
ni mwekezaji kupewa hekari 500 na kijiji jambo ambalo ni kinyume cha sheria ya
ardhi namba 5 ya mwaka 1999 inayosema kuwa kijiji kinauwezo wa kumpa mwekezaji
si zaidi ya hekari 50,” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa kama
wameona mwekezaji hafai kwani wao ndiyo waliompa ardhi wanauwezo wa
kumnyanganya kwa kufuata taratibu za kisheria endapo wataona ameshindwa
kutekeleza ahadi wakati anaomba ardhi.
“Mnauwezo wa
kumuondolea umiliki endapo atakiuka masharti kwani huo ni mkataba na endapo
atakiuka masharti unaweza kuvunjika na ardhi ikarudishwa kwa wanakijiji,”
alisema Ridhiwani.
Alisema ni vema
wawekezaji wakatekeleza tatatibu ili kuwa na ushirikiano na wananchi ambao
wanatoa ardhi yao ili nao wanufaike nayo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment