Tuesday, January 6, 2015

MBUNGE WA JIMBO LA CHALINZE RIDHIWANI KIKWETE AENDELEA NA ZIARA JIMBONI

Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo Ridhiwani Kikwete akiwahutubia wakazi wa Kijiji cha Pera kweny kata ya Kibindu wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wakati wa ziara ya kutembela shughuli za maendeleo

 Ridhiwani Kikwete Mbunge wa Jimbo la Chalinze akikabidhi mpira kwa moja ya Wazee kwenye Kijiji cha Pera Kata Kibindu wakati wa zaiara yake kwenye jimbo hilo

 Hili ni darasa la shule ya msingi ya Kibindu ambayo iliezuliwa paa baada ya kutokea mvua kubwa iliyonyesha mwishoni mwa mwaka jana

 Diwani wa Kata ya Kibindu Mawazo Mkufya akiongea na Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete mwenye kofia alipotembelea shule hiyo kuangalia uharibifu uliotokana na mvua kubw ailiyonyesha na kuharibu baadhi ya madarasa na ofisi ya mwalimu mkuu wa shule hiyo

 Moja ya Madarasa ya shule ya Msingi Kibindu yaliyoharibiwa na mvua kubw ailiyonyesha mwaishoni mwa mwaka jana 

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kulia akiongea na waandishi wa habari hawapo kushoto ni diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya. 

 Baadhi ya akinamama wa Kijiji cha Kibindu wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete hayupo pichani wakati wa ziara yake kwenye jimbo hilo

 Choo cha shule ya Msingi Maluiwi kikiwa kimebomoka hali ambayo inawafanya wanafunzi wa shule hiyo kujisaidia porini kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

 Hichi ni choo cha nyasi ambacho kinatumiwa na walimu wa shule ya Msingi Maluiwi

 Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete akiongea na wananchi wa Kitongoji cha Mdaula alipotembelea kwenye ziara yake ya kuangalia shughuli za maendeleo kwenye jimbo hilo.

No comments:

Post a Comment