Na
John Gagarini, Kibaha
HALMASHAURI
ya Mji wa Kibaha inatarajia kuanza mradi mkubwa wa ujenzi wa Soko la kisasa
pamoja na Stendi utakaogharimu kiasi zaidi ya shilingi bilioni 20 kuanzia
Februari mwaka huu.
Hayo
yalisemwa mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Adhu
Mkomambo alipozungumza na mwandishi wa habari hizi na kusema kuwa taratibu za
mwisho zinakamilika kuanza ujenzi huo.
Mkomambo
alisema kuwa ujenzi huo wa soko na setndi vitakuwa mkombozi kwa wananchi wa
Kibaha na mkoa mzima wa Pwani kutokana na kukosa vitu hivyo kwa muda mrefu.
“Pale
kuna soko na stendi lakini havina hadhi ya Mji hivyo kupitia benki ya uwekezaji
(TIB) tutajenga vitu hivi kwa lengo la kuboresha mji na kuleta maendeleo kwa
wananchi wa wilaya ya Kibaha,” alisema Mkomambo.
Aidha
alisema kuwa vitu hivyo ni moja ya vyanzo vya mapato ya Halmashauri hivyo
ujenzi wake utazingatia ubora na viwango ili kuwa na hadhi kwani soko lililopo
halina ubora kulingana na mji wa Kibaha
“Mbali
ya miradi hiyo ambayo itaanza kwa pamoja pia Halmashauri itaendelea na miradi
yake ya ujenzi wa barabara na uboreshaji wa sekta mbalimbali za jamii ili
huduma ziweze kuwa bora,” alisema Mkomambo.
Alibainisha
kuwa wataendeleza ushirikiano kati ya Halmashauri yake wananchi pamoja na wadau
mbalimbali wa maendeleo ili kuendelea kuuboresha mji huo unaoelekea kuwa
Manispaa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment