Tuesday, January 13, 2015

VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA NA VIJIJI WAASWA NA WANANCHI WAHAKIKISHIWA KUPATA UMEME


 Na John Gagarini, Bagamoyo
VIONGOZI wa serikali za mitaa na vijiji wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani waliochaguliwa hivi karibuni wametakiwa kusoma mapato na matumizi ili kuepuka kuenguliwa kwenye nafasi zao kama baadhi yao waliopita kukataliwa na wananchi.
Moja ya changamoto zilizosababisha viongozi hao waliopita baadhi yao walienguliwa na wananchi huku wengine wakishindwa kurudishwa kwenye kura za kuteuliwa kuwani uongozi kwenye uchaguzi uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
Hayo yalisemwa Bagamoyo na katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kombo Kamoto alipozungumza na wananchi wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo Ridhiwani Kikwete kwenye  vijiji vya kata za Kibindu, Mbwewe, Mdaula, Bwiringu, Fukayosi, Miono na Kiwangwa.
Kamote alisema kuwa viongozi hao waliochaguliwa na wananchi hasa wale wanaotoka chama hicho kwani hawana budi kuwatumikia wananchi ipasavyo kwa lengo la kuwatatulia changamoto ambazo zinawakabili katika nyanja mbalimbali kwenye huduma za kijamii.
“Mmechaguliwa na wananchi kwa heshima ya chama chetu, hususani kusoma mapato na matumizi hivyo niwasihi mchape kazi kama sheria na taratibu zinavyowaongoza, sitopenda kusikia wananchi wakilalamikia kuhusu utendaji wenu, mtambue mwaka huu mmeapishwa na mahakimu tofauti na miaka yote, hivyo yeyote atayekiuka kiapo hicho ataondolewa kwenye nafasi yake,” alisema Kamote.
Alisema kuwa viongozi hao watatakiwa kuitisha mikutano na kusoma mapato na matumizi kwa wananchi ili waweze kujua yanayofanyika kwenye maeneo yao.
Viongozi hao pia waliaswa kutokuwa madalali wa kuuza ardhi kiholela na kuwakandamiza wananchi ambao wakati mwingine hawajui haki zao za msingi.
“Baadhi waliondolewa kutokana na kushindwa kuitisha mikutano ikiwa ni pamoja na kushindwa kusoma mapato na matumizi hali iliyowafanya waondolewa madarakani au kushindwa kwenye uteuzi wa kuwania nafasi hizo, alisema Kamote.
Aidha alisema kuwa inashangaza kuona baadhi ya viongozi wanakuwa vinara wa kuuza maeneo na kama yupo kiongozi aliyekuwa anafanya hivyo wanapaswa kuacha na kuwa waadilifu ili kulinda nafasi walizopata.
“Viongozi huu si muda wa kuanza majigambo ama kujivunia nafasi mlizoshika  bali mnatakiwa kutimiza wajibu wenu kwa kusimamia ilani ya chama cha mapinduzi ili kuleta maendeleo kwa wananchi,” alisema Kamote.
Kwa upande wake Ridhiwani Kikwete aliwaomba viongozi hao kufanya kazi kwa bidii ili chama kiendelee kuaminika na kushika dola .
“Fanyeni kazi bila kubagua watu ,watumikieni pasipo kujali itikadi za kisiasa na hiyo ndio sifa pekee ya kiongozi wa sasa asiyejali udini,ukabila wala chama alichopo,”alisema Ridhiwani.
Ridhiwani alisema kuwa yeye akiwa mbunge ataendelea kuwatumika ipasavyo katika kuwaondolea changamoto zinazowakabili.
mwisho.
Na John Gagarini,Chalinze
KILIO cha baadhi ya wananchi wa Jimbo la Chalinze kukosa umeme huenda kikaisha baada ya kuhakikishiwa kuwa watapata huduma hiyo kuanzia m,waka huu kupitia miradi ya umeme vijijini kupitia wakala wa umeme Vijijini (REA).
Changamoto hiyo itapungua kwenye maeneo mbalimbali ya Jimbo hilo katika vijiji ambavyo vipo kwenye awamu ya awamu ya tatu inayotarajiwa kuanza mwezi Juni mwaka huu kupitia miradi hiyo ya REA.
Akiwahutubia wananchi wa vijiji vya Kibindu, Mbwewe, Mdaula, Bwilingu, Fukayosi, Kiwangwa na Chalinze mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa serikali ya CCM imejipanga kuikabilia changamoto hiyo.
“Kila maeneo niliyopita nimekutana na malalamiko  kutoka kwa wananchi juu ya kukosa umeme wakati vijiji vingine vya kata hizo vikiwa vimepata umeme na kuhoji huku wao wakiona kwa macho umeme umepita juu na kwenda maeneo jirani,” alisema Ridhiwani.
Ridhiwani alise kuwa anatambua umuhimu wa umeme hivyo amekuwa akifanya jitihada za kufuatilia na ndio maana amelazimika kufuatana na meneja wa miradi ya umemem mkoani Pwani Leo Mwakatobe ambaye anatolea ufafanuzi suala hilo.
“Mfano eneo la Kiwangwa halikuwepo katika umeme unaosambazwa na REA lakini baada ya kufanya juhudi hizo fedha zimepatikana hivyo utakuwa wa REA ambapo tanesco imetoa sh.milioni 420 na REA sh.milioni 800,” alisema Ridhiwani.
Aidha alisema kuwa fedha hizo tayari ziko na kazi ya kuanza kusambaza umeme itaanza wakati wowote, kwani anajua umuhimu wa umeme lakini wananchi na kuwaomba wananchi wafahamu juhudi za serikali.
Kwa upande wake  mhandisi wa Tanesco mkoa wa Pwani, Mhandisi Leo Mwakatobe, alisema wanaendelea kumalizia utekelezaji wa awamu ya pili wa mradi wa REA na kazi iliyobaki ni mkandarasi kuanza kazi wakati wowote kuanzia mwezi huu.
Mwakatobe fedha kwa ajili ya mradi wa kusambaza umeme zimepatikana, hivyo wananchi wenye kuhitaji waanze kuchukua fomu.kinachotakiwa wawe na picha mbili na kitambulisho cha aina yoyote.
Mwisho




No comments:

Post a Comment