Saturday, January 3, 2015

SHULE HATARIN I KUWAANGUKIA WANAFUNZI

 Baadhi ya wananchi na wafanyabiashara wa Kijiji cha Kibindu wilayani Bagamoyo wakimsikiliza Mbunge wao wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete alipotembelea Kijiji hicho wakati wa ziara yake ya kushukuru wananchi baada ya kumchagua kuwa mbunge miezi kadhaa iliyopita

 Akinamama wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete hayupo pichani baada ya kutembelea kijiji cha Kibindu kutoa shukrani kwa wananchi kumchagua kwenye nafasi hiyo miezi kadhaa iliyopita.

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kibindu wilayani Bagamoyo mkoani Pwani

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza na waandishi wa Habari mbele ya jengo la shule ya Msingi Kibindu ambalo lilianguka kufuatia mvua kubwa ziulizonyesha mwishoni mwa mwaka jana kushoto ni diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya.


 Moja ya madarasa ya shule ya msingi Kibindu likiwa limebomoka kufuatia mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa mwaka jana.

 Diwani wa kata ya Kibindu Mawazo Mkufya aliyenyanyua mikono juu akitoa maelezo kwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kulia aliyevaa kofia ya kijani kufuatia mvua kubwa kubomoa madarasa ya shule ya Msingi Kibindu

 Moja ya Madarasa ya shule ya Msingi Kibindu likiwa limeezuliwa paa kufuatia mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa mwaka jana na kusababisha madarasa mawili na ofisi ya mwalimu mkuu kuharibika.

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete akikabidhi mpira kwa baadhi ya viongozi wa timu za soka za Kijiji cha Kibindu

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akionge na wananchi wa Kijiji cha Kibindu alipofanya ziara ya kushukuru wananchi wa Jimbo hilo kwa kumchagua kushika nafasi hiyo miezi kadhaa iliyopita.

No comments:

Post a Comment