Na John Gagarini, Chalinze
WANANCHI wa Kijiji cha
Kwaruhombo kwenye Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wametoa
kilio cha kujengewa wodi ya wazazi kwenye kituo cha afya cha Kwaruhombo ili
wanawake wajawazito wasijifungue kwenye wodi za kawaida.
Akizungumza kijijini
hapo wakati wa ziara ya maendeleo ya mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete,
Hadija Stambuli alisema kuwa akinamama wamekuwa wakijifungulia kwenye wodi
hivyo kutokuwa na usiri.
Stambuli alisema kuwa
hiyo imekuwa changamoto kubwa kwa akinamama wanapokwenda kujifungua wamekuwa
wanashindwa kusitiriwa wakati wa uzazi.
“Tunakuomba Mbunge
wetu utusaidie wakinamama ili tunapokwenda kujifungua kwani hakuna usiri hivyo
tungepata jengo maalumu kwa ajili ya kujifungungulia ingekuwa vizuri,” alisema
Stambuli
Akijibu malalamiko
hayo mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alisema kuwa kujifungua ni
jambo jema na linahitaji usiri.
Ridhiwani alisema kuwa
kwa kushirikiana na halmashauri ili kuhakikisha kunakuwa na jengo kwa ajili ya
kinamama kujifungulia.
“Tutakaa na uongozi wa
Halmashauri ili kuhakikisha kunakuwa na jengo maalumu kwa ajili ya kujifungulia
ili kuwaondolea fadhaa akinamama wakati wakijifungua,” alisema Ridhiwani.
Aidha alisikitishwa na
matumizi mabaya ya mafuta kwa ajili ya gari la wagonjwa wanaopata rufaa na
kuutaka uongozi wa kituo hicho kuhakikisha kinadhibiti matumizi hayo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment