Na John Gagarini, Chalinze
MRADI wa Maji wa Wami Chalinze awamu ya
tatu mara utakapokamilika unaratajia
kuwafikia wananchi 271,000 wa Jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoa wa
Pwani.
Aidha
mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 60 unatarajia kuanza mwezi Machi
mwaka huu utapunguza tatizo la upatikanaji wa maji kwa wakazi wa Chalinze ambao
wanahudumiwa na mradi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari
ofisini kwake
Meneja wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Chalinze (CHALIWASA)
Mhandisi Christer Mchomba alisema katika awamu
hiyo itaongeza mitandao ya maji kwenye vitongoji 210 kutoka kwenye vijiji 47
ambavyo vilifikiwa kwenye utekelezaji wa awamu ya pili iliyoanza mwaka 2008.
“Katika
awamu ya tatu ya mradi huu yatajengwa pia matenki ya kuhifadhia maji kwenye
vijiji 20 vya awamu ya kwanza kikiwamo kijiji cha Bwiringu, Msata, Lugoba, Msoga,
Mandela na vingine ambavyo havikujengewa matenki,” alisema Mhandisi Mchomba.
Mhandisi Mchomba alisema kwa sasa awamu
ya pili ,wizara inakamilisha ujenzi wa nyongeza ya chujio la maji ambalo
litaongeza wingi wa maji yanayosafishwa na kuzalishwa.
Alisema kuwa watajenga tanki kubwa eneo
la Mazizi lenye uwezo wa kuhifadhi maji yenye ujazo wa lita 200,000 pamoja na
vituo vya maji kwenye vijiji na vitongoji vyote kwenye Jimbo hilo.
“Kwa sasa wanazalisha maji kwa asilimia
85 tu kutokana na mashine kushindwa kufanya kazi kikamilifu ambapo kwa siku ni
mita za ujazo 2,000 badala ya 5,000 kwa siku,” alisema Mhandisi Mchomba.
Kwa upande wake ofisa maabara wa mradi
huo Riziki Kacheche alisema kuwa maji
ghafi yanapokuwa machafu zaidi tope huziba na kuzuia maji kuchukuliwa katika
kiwango kinachotakiwa kwenda kusafishwa na hivyo kusabababisha uwezo wa
kuzalisha maji na kuyasafisha kuwa mdogo.
Mwisho
No comments:
Post a Comment