Sunday, April 21, 2013
WATOTO WACHANAGA KUPATIWA CHANJO
Malulu alisema kuwa hiyo ni awamu ya tatu ya chanjo ambapo watoto hao hawakuipata ilipoanza Januarimwakahuu
Akizungumzia kukamilika kwa maandalizi ya shughuli hiyo mkuu wa wilaya
KIAMA KWA MADEREVA WANYWA VIROBA KIMEFIKA
Na John Gagarini,
Kibaha
HATIMAYE baada ya kilio cha muda mrefu cha abiria juu ya
madereva ambao wamekuwa wakiweka pombe za viroba kwenye chupa za maji na
kujifanya wanakunywa maji, kimesikika baada ya jeshi la polisi mkoani Pwani
kupata vipima ulevi 100.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha kamanda wa
kikosi cha usalama barabarani Nasoro Sisiwaya alisema kuwa vifaa hivyo
vitasaidia kukabiliana na madereva walevi ambao wamekuwa wakisababisha ajali
kutokana na ulevi.
Sisiwaya alisema kuwa kutokana na kero ya ulevi kuwa kubwa
kwa baadhi ya madereva wamekuja na njia hiyo ili kuwadhibiti madereva hao ambao
wamekuwa wakinywa pombe huku safari ikiendelea.
“Vifaa hivi vitatusaidia katika kukabiliana na madereva hao
ambao ni chanzo kikubwa cha ajali kwani hupoteza umakini wakati wa kuendesha na
kusababisha ajali ambazo zingeweza kuepukika,” alisema Sisiwaya.
Aidha alisema kuwa kitengo cha usalama barabarani kinaendelea
kukabiliana na changamoto za ajali kwa kuweka askari mbalimbali wakiwemo ambao
wanakuwa wamevaa kiraia ili kudhibiti madereva ambao wanakiuka sheria za
usalama barabarani.
“Tunamshukuru Mungu kuwa ajali zinaendelea kupungua kutokana
na udhibiti kuwa mkubwa ambapo kwa sasa makosa madogo yameongezeka ambayo
yanaashiria kupungua kwa ajali katika mkoa,” alisema Sisiwaya.
Aliongeza kuwa kwa sasa wanashirikiana na mamlaka ya
kudhibiti usafiri wa majini na nchi kavu (SUMATRA) katika kuwakamata madereva
wanaovunja sheria ambapo mafanikio yameanza kuonekana kwani makosa makubwa ya
barabarani yamepungua kwa asilimia 26.
Aliwataka wananchi na abiria kutoa taarifa mbalimbali
kuhusiana na madereva ambao hawazingatii taratibu za uendeshaji wawapo
barabarani na wataendelea kufanya operesheni za mara kwa mara ili kuwabaini
madereva wazembe.
Mwisho.
Friday, April 19, 2013
MICHEZO PWANI
Na John Gagarini,
Kibaha
BONDIA wa Maili Moja Kibaha mkoani Pwani Nzumba Nkukwe leo
Jumamosi anatarajia kupanda ulingoni kupambana na bondia Yusuph Yusuph wa
Chalinze wilayani Bagamoyo.
Kwa mujibu wa katibu wa katibu wa chama cha ngumi mkoa wa
Pwani Halfan Mrisho “Swagala” alisema kuwa pambano hilo litachezwa kwenye
ukumbi wa Ndelema uliopo Chalinze.
Swagala alisema kuwa pambano hilo litakuwa ni la kirafiki kwa
kuwapima uwezo wao mabondia hao pamoja na kuhamasisha watu kucheza mchezo huo
mkoa Pwani.
“Lengo kuu ni kumwandaa Nkukwe ambaye anatakiwa kucheza
mapambano 12 ili aweze kushiriki kwenye mashindano ya ubingwa hapa nchini,”
alisema Swagala.
Aidha alisema kuwa pambano hilo lililodhaminiwa na Big Right
litakuwa la raundi 12 na linatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa mabondia hao
wa mkoa huu.
“Nawaomba mashabiki waje kwa wingi ili kuwahamasisha mabondia
wa nyumbani na kutakuw ana usafiri kutokea Maili Moja hadi Chalinze hivyo
itakuwa ni nafasi kwa wadau wa ngumi kujionea vipaji vya vijana wao,” alisema
Swagala.
Alitoa shukrani kwa mdhamini wa mapambano Omary Kimbau kwa
jitihada zake za kuhamasisha mchezo huo kwa vijana wa mkoa wa Pwani kwani
amekuwa akiwaandalia mapambano mbalimbali mabondia.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MCHEZO wa nusu fainali kati ya Fire na Lisborn ulishindwa
kutoa mshindi baada ya mwamuzi wa pambano hilo Hamad Mbegu kutimua mbio kuhofia
usalama wake baada ya kumaliza mpira zikiwa zimesalia dakika chache zikiwa
hazijatiamia dakika 90 na kuamuru yapigwe matuta timu hizo zikiwa sare ya 1-1.
Mchezo huo wa nusu fainali ya pili kuwania kombe la Kibaha
Super Cup ulipigwa kwenye uwanja wa Bwawani Maili Moja wilayani Kibaha
ulizikutanisha timu hizo ili kupata mshindi ambaye angeungana na Mwanalugali
kucheza hatua ya fainali.
Chanzo cha mwamuzi huyo kukimbia ni pale alipoashiria mpira
kwisha huku zikiwa bado dakika 5 kutimia dakikia 90 alimaliza pambano na
kuashiria matuta lakini washabaiki wa timu ya Lisborn walimfuata na kumzonga
huku wakimtishia kumpiga.
Kutokana na mzozo huo mwamuzi aliwaita wachezaji wa Lsborn
kwa ajili ya kupiga matuta lakini walionekana kusuasua hali iliyofanya muda
mwingi upotee karibu dakika 10 hivi huku washabiki wakiwa wamezingira eneo la
goli zilipotakiwa kupigwa penati hali iliyomtia hufo mwamuzi huyo na kukimbia.
Mbali ya hali hiyo pambano hilo lilikuwa na mvutano mkubwa
huku timu hizo zikionyesha kandanda safi na walikuwa Lisborn walioandaika bao
la kuongoza kupitia kwa Kulwa Mwanda dakika ya 72 na Fundikira Fundikira wa
Fire alisawazisha kwenye dakika ya 80 ya mchezo, mchezo huu utarudiwa leo
Jumamosi kwenye uwanja huo huo.
Mwisho.
POLISI PWANI YAKUSANYA MAMILIONI
Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani limefanikiwa kukusanya kiasi cha
zaidi ya shilingi milioni 825 kutokana na makosa madogo madogo ya barabarani
kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita.
Hayo yalisemwa jana na kamanda wa polisi mkoani humo Ulrich
Matei alipoongea na waandishi wa habari mjini Kibaha kuzungumzia mafanikio na
changamoto zinazolikabili jeshi hilo.
Matei alisema kuwa katika kipindi hicho jumla ya makosa
yliyokamatwa katika kipindi cha Januari mwaka 2011 hadi Machi 2013 ni 31,663 ambapo
yaliyolipiwa yalikuwa ni 31,235.
“Katika kipindi hicho ajali zilikuwa 942 za vifo zilikuwa 190
waliokufa walikuwa 224, ajali za majeruhi zilikuwa 510 na waliojeruhiwa
walikuwa 1,109 ambapo inaonyesha kupungua kwa asilimia 25 ukilinganisha na
mikoa mingine,” alisema Matei.
Kwa upande wake kamanda wa kikosi cha usalama barabarani
Nasoro Sisiwaya alisema kuwa wanaendelea na mikakati mbalimbali ya kuzuia ajali
ikiwa ni pamoja na kukamata magari mabovu.
Sisiwaya alisema kuwa wameunda vikosi maalumu viwili kwa
ajili ya kukagua magari ambapo kimoja kinafanya ukaguzi kwenye barabara iendayo
mikoa ya Kusini na kingine barabara ya Morogoro.
Aidha alisema kuwa wanakabiliwa na changamoto kubwa kuyaondoa
magari yanayoharibika barabarani kwani hawana gari la kuyaondolea na matokeo
yake hutumia magari mengine kuyaondoa kwa kutumia mnyororo mgumu.
Mwisho.
Tuesday, April 16, 2013
12,500 KUNUFAIKA MIRADI YA MAJI KIBAHA
Na John Gagarini, Kibaha
JUMLA ya watu 12,500 kwenye
vijiji vinne kwenye Halmashauri ya wilaya ya Kibaha mkoani Pwani watanufaika na mradi wa kitaifa wa maji wa Wami – Chalinze
awamu ya pili wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni tatu.
Akizungumza na waandishi wa
habari ofisini kwake mjini Kibaha kuelezea mafanikio ya wilaya kwa kipindi cha
miaka saba iliyopita mkuu wa wilaya Halima Kihemba alisema kuwa mradi huo
utakamilika wakati wowote mwaka huu.
Kihemba alisema kuwa kwa
sasa mradi huo umefikia asilimia 35 ya utekelezaji wake na kuvitaja vijiji hivyo
kuwa ni Magindu, Lukenge, Gwata na Gumba.
“Mbali ya vijiji
vilivyotajwa hapo juu pia tunatarajia jumla ya vijiji 45 vitanufaika na mradi
mwingine ambao utasaidia kukabiliana na changamoto ya maji ambayo ni kubwa
kwenye wilaya,” alisema Kihemba.
Aidha alisema kuwa kwa
upande wa miradi hiyo yenye thamani ya zaidi ya shilingi zaidi ya bilioni mbili
itategemeana na upatikanaji wa fedha kutoka wadau mbalimbali.
Ameitaja miradi hiyo kuwa
ni mradi wa bomba Vikuruti, Boko Mnemela, Dutuni, bwawa la maji Mperamumbi
uchimbaji wa kisima kirefu chenye uwezo wa kutoa lita 36,000 za maji kwa saa.
“Miradi hiyo itakuwa katika
vijiji vya Lupunga, Mwabwito, Kisabi, Madimla, Disunyala na Makazi Mapya,”
alisema Kihemba.
Ameongeza kuwa kwa upande
wa Kibaha Mjini mitaa 15 ambayo ni Sofu, Muheza, Vikawe, Bondeni, Vikawe
Shuleni, Kidenge, Galagaza, Sagale, Mikongeni, Mwanalugali, Saeni, Jonugha, Zogawale
na Viziwaziwa miradi hii itakuwa na thamani ya zaidi ya shilingi bilioni moja.
Alibainisha kuwa changamoto
kubwa ni pamoja na kutegemea vyanzo vya maji vya ya juu ya ardhi, mabwawa, mito
ambayo hukauka wakati wa ukame na kusababisha shida ya maji hivyo kuweka
mikakati ya kuhamasisha jamii kutunza vyanzo vya maji, kuandaa andiko la miradi
ya maji ili kupata wafadhili na kutumia visima virefu kwa kuwa ni vyanzo vya
uhakika zaidi kulinganisha na mabwawa.
Mwisho.
Monday, April 15, 2013
AMWUA MAMA YAKE MZAZI KWA KUMPIGA NA MCHI KICHWANI
JESHI la Polisi
mkoani Pwani linamshikilia aitwaye Francis Siza miaka (26) kwa tuhuma za
kumuuwa mama yake mzazi Naomi Isaka (55) kwa kumpiga na mchi kichwani.
Akizungumza
na waandishi wa habari mjini Kibaha kamanda wa polisi mkoani humo Ulrich Matei alisema
kuwa tukio hilo lilitokea leo majira ya saa 1:30 asubuhi eneo la Kiluvya
A wilaya ya Kisarawe.
Kamanda Matei
alisema kuwa kijana huyo alifanya tukio hilo baada ya kubaki yeye na mama yake
baada ya wadogo zake wawili wa kike ambao ni wanafunzi kwenda shule.
“Alimpiga na
mchi kichwani mara mbili uapande wa kushoto na kulia chanzo kikiwa ni kutaka
kuuza kiwanja cha mama yake ambapo ni siku moja tangu arudi baada ya kusafiri
kusikojulikana,” alisema Kamanda Matei.
Baadhi ya majirani
ambao walishuhudia tukio hil Nolasko Zenobisi alisema wakati alipokuwa
akiendelea na shughuli zake za kulima alisikia kelele zikipigwa ndipo
alipokwenda katika nyumba hiyo na aliweza kukuta tayari mama huyo ameshafariki.
Zenobisi
alisema alipowajulisha majirani na kuanza kumtafuta mtuhumiwa na kwa bahati
nzuri walimpata akiwa amijificha kichakani ndipo walipomfunga kamba na kumpeleka
eneo alilofanyia tukio.
Aidha
alisema kwamba kijana huyo ambaye ndiye wa kwanza kuzaliwa katika familia yao
alifanya tukio hilo la mauaji baada ya mdogo wake wa kike
anaiyeitwa Neema Siza kuondoka nyumbani na kuelekea shule ya sekondari
Makulenge ambapo ndipo anaposoma kidato cha tatu.
Naye
shuhuda mwingine ambaye akutaka jina lake litajwe gazeti alisema kwamba pia nay
eye asubuhi hiyo alikuwa shambani anaalia ndipo aliposikia sauti na mtu anapika
makelele na kufa na alipokwenda alimwona huyo kijana anakimbia mbio ndipo
wananchi wengine walipoamua kumkimbiza na kumkamata.
Hata hivyo
baadhi ya majirani wengine walisema kwamba kijana huyo alifika mnamo April 14
majira ya saa 4:30 usiku na kumgongea mama yake mzazi na alifunguliwa na
kuingia ndani kulala lakini asubuhi akaamua kufanya tukio hilo.
Naye mtoto wa
Marehemu Neema Siza ambaye anasoma shule ya Makurunge alisema kwamba asubuhi
aliondoka na kumwaga mama yake vizuri na kwenda shule na kwamba nyumbani
alimwacha kaka yake huyo wa kwanza pamoja na mama yake.
Kwa upande wake
mtuhumiwa huyo alisema kuwa kwa upande wake yeye hakugombana wala hawakuwa na
ugomvi wowote na mama yake mzazi isipokuwa alifanya hivyo baada ya kumwona mama
yake mzazi anateseka hivyo akaona bora ampige na kumuuwa ili aweze kupumzika.
“Lakini
kutokana na kosa ambalo nimelifanya kwa sasa najuta, lakini ninafahamu kuwa
sheria itachukua mkondo wake, ingawa mimi nimefanya hivyo kwa sabbau tangu siku
nyingi niliona mama yangu anateseka sana, na ukizingatia baba yetu naye
alishafariki dunia kwa hiyo hali halisi ndiyo iliyofanya nifanye hivyo na
hakuna kitu kingine,” alisema Siza.
Saturday, March 30, 2013
WALIMU WA RIADHA KUPEWA MAFUNZO
Na John Gagarini, Kibaha
IDARA ya Elimu na chama cha Riadha mkoa wa Pwani (RP)
vimeandaa mafunzo kwa walimu wa mchezo wa riadha kutoka mikoa 10 kuanzia Aprili
6 hadi 17 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha mkufunzi wa
chama cha Riadha Tanzania (RT) Robert Kalyahe alisema kuwa mafunzo yatakuwa ya
siku 10 na yatafanyika kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha –Tumbi.
Kalyahe alisema kuwa mafunzo hayo ya hatua ya kwanza
yatasimamiwa na RT ambapo vyeti vya wahitimu vitatambuliwa na chama cha Riadha
Duniani (IAAF).
“Washiriki watakuwa kutoka mikoa 10 walengwa zaidi wakiwa ni
walimu wa shule za msingi, sekondari na wadau wengine wa mchezo huo sifa ikiwa
ni elimu ya kidato cha nne na kuendelea,” alisema Kalyahe.
Alisema kuwa RT imeamua kushirikisha walimu zaidi kwani wao
wana nafasi kubwa kuwaandaa wanafunzi shuleni na wakufunzi watakuwa ni Seleman
Nyumbani, Samwel Tupa na yeye mwenyewe.
Kalyahe ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya ufundi ya mkoa wa
Pwani alisema kuwa hadi sasa ni wadau 26 wamejitokeza kushiriki mafunzo hayo na
kuwataka wadau wengi zaidi kujitokeza kupata elimu hiyo ili waweze kuendeleza
mchezo huo.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)