Friday, April 19, 2013

MICHEZO PWANI


Na  John Gagarini, Kibaha
BONDIA wa Maili Moja Kibaha mkoani Pwani Nzumba Nkukwe leo Jumamosi anatarajia kupanda ulingoni kupambana na bondia Yusuph Yusuph wa Chalinze wilayani Bagamoyo.
Kwa mujibu wa katibu wa katibu wa chama cha ngumi mkoa wa Pwani Halfan Mrisho “Swagala” alisema kuwa pambano hilo litachezwa kwenye ukumbi wa Ndelema uliopo Chalinze.
Swagala alisema kuwa pambano hilo litakuwa ni la kirafiki kwa kuwapima uwezo wao mabondia hao pamoja na kuhamasisha watu kucheza mchezo huo mkoa Pwani.
“Lengo kuu ni kumwandaa Nkukwe ambaye anatakiwa kucheza mapambano 12 ili aweze kushiriki kwenye mashindano ya ubingwa hapa nchini,” alisema Swagala.
Aidha alisema kuwa pambano hilo lililodhaminiwa na Big Right litakuwa la raundi 12 na linatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa mabondia hao wa mkoa huu.
“Nawaomba mashabiki waje kwa wingi ili kuwahamasisha mabondia wa nyumbani na kutakuw ana usafiri kutokea Maili Moja hadi Chalinze hivyo itakuwa ni nafasi kwa wadau wa ngumi kujionea vipaji vya vijana wao,” alisema Swagala.
Alitoa shukrani kwa mdhamini wa mapambano Omary Kimbau kwa jitihada zake za kuhamasisha mchezo huo kwa vijana wa mkoa wa Pwani kwani amekuwa akiwaandalia mapambano mbalimbali mabondia.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MCHEZO wa nusu fainali kati ya Fire na Lisborn ulishindwa kutoa mshindi baada ya mwamuzi wa pambano hilo Hamad Mbegu kutimua mbio kuhofia usalama wake baada ya kumaliza mpira zikiwa zimesalia dakika chache zikiwa hazijatiamia dakika 90 na kuamuru yapigwe matuta timu hizo zikiwa sare ya 1-1.
Mchezo huo wa nusu fainali ya pili kuwania kombe la Kibaha Super Cup ulipigwa kwenye uwanja wa Bwawani Maili Moja wilayani Kibaha ulizikutanisha timu hizo ili kupata mshindi ambaye angeungana na Mwanalugali kucheza hatua ya fainali.
Chanzo cha mwamuzi huyo kukimbia ni pale alipoashiria mpira kwisha huku zikiwa bado dakika 5 kutimia dakikia 90 alimaliza pambano na kuashiria matuta lakini washabaiki wa timu ya Lisborn walimfuata na kumzonga huku wakimtishia kumpiga.
Kutokana na mzozo huo mwamuzi aliwaita wachezaji wa Lsborn kwa ajili ya kupiga matuta lakini walionekana kusuasua hali iliyofanya muda mwingi upotee karibu dakika 10 hivi huku washabiki wakiwa wamezingira eneo la goli zilipotakiwa kupigwa penati hali iliyomtia hufo mwamuzi huyo na kukimbia.
Mbali ya hali hiyo pambano hilo lilikuwa na mvutano mkubwa huku timu hizo zikionyesha kandanda safi na walikuwa Lisborn walioandaika bao la kuongoza kupitia kwa Kulwa Mwanda dakika ya 72 na Fundikira Fundikira wa Fire alisawazisha kwenye dakika ya 80 ya mchezo, mchezo huu utarudiwa leo Jumamosi kwenye uwanja huo huo.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment