Sunday, April 28, 2013

ATOA MIPIRA KWA VIJANA


Na John Gagarini, Kibaha
MJUMBE wa Baraza Kuu Taifa kupitia Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoani Pwani Mariamu Chaurembo ametoa mipira mitatu ya mpira wa miguu kwa chipukizi wa Kibaha Mjini na Kibaha Vijijini ili washindanie.
Alitoa mipira hiyo juzi mjini Kibaha wakati wa ziara ya mwenyekiti wa chipukizi Taifa Gabriel Amos Makala, alipotembelea mkoa wa Pwani kujua shughuli zinazofanywa na umoja huo.
Chaurembo alisema kuwa lengo la kutoa mipira hiyo ni chipukizi hao waweze kukuza, kuendeleza na kuibua vipaji kwa kufanya mashindano ambapo mshindi wa kwanza hadi watatu ndiyo watakaojinyakulia mipira hiyo.
“Nimetoa mipira hii ili iweze kuwaniwa na vijana kwenye wilaya ya Kibaha kwani mbali ya vipaji pia ni moja ya njia ya kuwajengea uwezo wa kujua wajibu wao katika kukitumikia chama,” alisema Chaurembo.
Alisema njia mojawapo ya kuwapata vijana ni kupitia michezo hivyo aliona kuna haja ya kuwaunganisha vijana kupitia michezo mbalimbali ambapo kwa sasa ameanza na soka.
“Mimi napenda sana michezo hivyo nimeona njia ya kuwaweka vijana pamoja ni michezo hivyo wazazi nao wanapaswa kuwaendeleza vijana wao kupitia michezo,” alisema Chaurembo.
Wakati huo huo katibu wa hamasa wa chipukizi Taifa Omary Moris ameahidi kutoa mipira 10 na jezi seti moja kwa chipukizi kwenye mkoa huo ili kuhamasisha michezo.
Moris alisema kuwa vifaa hivyo atavitoa baada ya wiki mbili kuanzia sasa ili vijana waweze kufanya michezo na kukuza vipaji vyao vya mpira wa soka.
Mwisho.    
  

No comments:

Post a Comment