Monday, April 15, 2013

AMWUA MAMA YAKE MZAZI KWA KUMPIGA NA MCHI KICHWANI


JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia aitwaye Francis Siza  miaka (26) kwa tuhuma za kumuuwa mama yake mzazi Naomi Isaka (55)  kwa kumpiga na mchi kichwani.
 Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha kamanda wa polisi mkoani humo Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea leo  majira ya saa 1:30 asubuhi eneo la Kiluvya A wilaya ya Kisarawe.
Kamanda Matei alisema kuwa kijana huyo alifanya tukio hilo baada ya kubaki yeye na mama yake baada ya wadogo zake wawili wa kike ambao ni wanafunzi kwenda shule.
“Alimpiga na mchi kichwani mara mbili uapande wa kushoto na kulia chanzo kikiwa ni kutaka kuuza kiwanja cha mama yake ambapo ni siku moja tangu arudi baada ya kusafiri kusikojulikana,” alisema Kamanda Matei.
Baadhi ya majirani ambao walishuhudia tukio hil Nolasko Zenobisi alisema wakati alipokuwa akiendelea na shughuli zake za kulima alisikia kelele zikipigwa ndipo alipokwenda katika nyumba hiyo na aliweza kukuta tayari mama huyo ameshafariki.
 Zenobisi alisema alipowajulisha majirani na kuanza kumtafuta mtuhumiwa na kwa bahati nzuri walimpata akiwa amijificha kichakani ndipo walipomfunga kamba na kumpeleka eneo alilofanyia tukio.
 Aidha alisema kwamba kijana huyo ambaye ndiye wa kwanza kuzaliwa katika familia yao alifanya tukio hilo la mauaji  baada ya   mdogo wake wa kike anaiyeitwa Neema Siza kuondoka nyumbani na kuelekea shule ya sekondari Makulenge ambapo ndipo anaposoma kidato cha tatu.
 Naye shuhuda mwingine ambaye akutaka jina lake litajwe gazeti alisema kwamba pia nay eye asubuhi hiyo alikuwa shambani anaalia ndipo aliposikia sauti na mtu anapika makelele na kufa na alipokwenda alimwona huyo kijana anakimbia mbio ndipo wananchi wengine walipoamua kumkimbiza na kumkamata.
 Hata hivyo baadhi ya majirani wengine walisema kwamba kijana huyo alifika mnamo April 14 majira ya saa 4:30 usiku na kumgongea mama yake mzazi na alifunguliwa na kuingia ndani kulala lakini asubuhi akaamua kufanya tukio hilo.
Naye mtoto wa Marehemu Neema Siza ambaye anasoma shule ya Makurunge alisema kwamba asubuhi aliondoka na kumwaga mama yake vizuri na  kwenda shule na kwamba nyumbani alimwacha kaka  yake huyo wa kwanza pamoja na  mama yake.
Kwa upande wake mtuhumiwa huyo alisema kuwa kwa upande wake yeye hakugombana wala hawakuwa na ugomvi wowote na mama yake mzazi isipokuwa alifanya hivyo baada ya kumwona mama yake mzazi anateseka hivyo akaona bora ampige na kumuuwa ili aweze kupumzika.
 “Lakini kutokana na kosa ambalo nimelifanya kwa sasa najuta, lakini ninafahamu kuwa sheria itachukua mkondo wake, ingawa mimi nimefanya hivyo kwa sabbau tangu siku nyingi niliona mama yangu anateseka sana, na ukizingatia baba yetu naye alishafariki dunia  kwa hiyo hali halisi ndiyo iliyofanya nifanye hivyo na hakuna kitu kingine,” alisema Siza.

No comments:

Post a Comment