Na John Gagarini, Kibaha
IDARA ya Elimu na chama cha Riadha mkoa wa Pwani (RP)
vimeandaa mafunzo kwa walimu wa mchezo wa riadha kutoka mikoa 10 kuanzia Aprili
6 hadi 17 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha mkufunzi wa
chama cha Riadha Tanzania (RT) Robert Kalyahe alisema kuwa mafunzo yatakuwa ya
siku 10 na yatafanyika kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha –Tumbi.
Kalyahe alisema kuwa mafunzo hayo ya hatua ya kwanza
yatasimamiwa na RT ambapo vyeti vya wahitimu vitatambuliwa na chama cha Riadha
Duniani (IAAF).
“Washiriki watakuwa kutoka mikoa 10 walengwa zaidi wakiwa ni
walimu wa shule za msingi, sekondari na wadau wengine wa mchezo huo sifa ikiwa
ni elimu ya kidato cha nne na kuendelea,” alisema Kalyahe.
Alisema kuwa RT imeamua kushirikisha walimu zaidi kwani wao
wana nafasi kubwa kuwaandaa wanafunzi shuleni na wakufunzi watakuwa ni Seleman
Nyumbani, Samwel Tupa na yeye mwenyewe.
Kalyahe ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya ufundi ya mkoa wa
Pwani alisema kuwa hadi sasa ni wadau 26 wamejitokeza kushiriki mafunzo hayo na
kuwataka wadau wengi zaidi kujitokeza kupata elimu hiyo ili waweze kuendeleza
mchezo huo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment