Na John Gagarini, Kibaha
WAKAZI wa Kijiji cha Gama wilayani Bagamoyo mkoani Pwani
wameitaka kampuni ya EcoEnergy ya Sweden inayotaka kuwekeza kilimo cha miwa
kukaa pamoja ili kuingia makubaliano nao juu ya kuitumia ardhi yao badala ya kuwatumia madalali wanaojifanya
wanahusika na eneo hilo.
Wakizungumza Kijijini hapo jana kwenye mkutano wa hadhara
uliaondaliwa na uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bagamoyo.
Moja ya wakazi wa Kijiji hicho Ramadhan Alawi alisema kuwa
wao wanachokitaka ni kukaa meza moja na wao na si kuwatumia watu wa kati ambao
hawahusiki na kuwasemea kwani ardhi hiyo ni vema kukawa na maelewano ya namna
nao watakavyonufaika.
“Sisi hatukatai wawekezaji lakini tunachokitaka wawekezaji
hao waje tukae meza moja na kukubaliana namna ya jinsi na sisi tutakavyoshiriki
katika uwekezaji huo na hutataki watu wa kutusemea kwani sisi wenyewe tupo,”
alisema Alawi.
Kwa upande wake Salum Yusuph alisema kuwa tatizo kubwa hapa
ni wananchi kutoshirikishwa katika suala zima la uwekezaji huo kwa wakazi wa
Kijiji chao na hawajui wao watanufaika vipi kwani waliambiwa waondoke kwenye
eneo hilo.
“Hapa tunataka sisi na EcoEnergy tukae pamoja tukubaliane
hasa ikizingatiwa kuwa hapa hatuna shule, zahanati wala huduma za kijamii na
tungependa tuwe kama mashamba mengine ya Mtibwa na Kagera tukae tulime miwa wao
waje kununua kwetu na si kutuondoa,” alisema Yusuph.
Akizungumzia suala hilo msimamizi wa wakulima wadogo wadogo
wa kampuni hiyo Ian Sherry alisema kuwa wao wana lengo la kuwekeza katika
kijiji hicho kwa manufaa ya wananchi na hawana lengo baya kwani kwenye vijiji
walivyowekeza kupitia mradi huo wamenufaika na kuboresha huduma za kijamii.
“Wakazi wa eneo hili wasiwe na wasiwasi kwani taratibu
zinafuatwa na kama kuna matatizo mambo yote yatawekwa sawa ili kuhakikisha
manufaa ya mradi huo ambao utakuwa na uwekezaji mkubwa unaofikia zaidi ya
bilioni saba,” alisema Sherry.
Naye mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bagamoyo Shaibu Mtawa alisema
kuwa kutokana na changamoto ya madai ya wananchi wataandaa mkutano baina ya
pande zote hizo ili kuondoa tofauti zilizojitokeza.
Mtawa alisema kuwa hapa inaonekana wananchi hawajashirikishwa
kikamilifu juu ya uwekezaji huo hivyo chama kitahakikisha mgogoro uliopo
unamalizwa na kesi iliyo mahakamani inaondolewa ili kuleta mwafaka.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment