Thursday, March 7, 2013

WAWILI WAFA


Na Mwandishi Wetu, Kibaha
MLINZI wa kampuni ya ulinzi ya S&M ambaye alikuwa akilinda ofisi ya DAWSCO wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Juma Hassan (45) ameuwawa na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi baada ya kuvamia ofisi hiyo.
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alisema kuwa watu hao ambao idadi yao haikuweza kufahamika mara moja walimteka kasha kumtupa baada ya kumfunga kamba miguuni na mikononi pia walimziba na plasta mdomoni na puani.
Alisema kuwa baada ya kumteka waliingia kwenye ofisi hiyo na kuiba kompyuta nne ambazo thamani yake haikuweza kufahamika mara moja kasha kutoweka.
“Tunaendelea na upeelelezi kujua ni watu gani waliofanya tukio hilo la kusikitisha na tunawaomba wananchi kutoa taarifa endapo watasikia juu ya watu walio husika na tukio hilo.
Alisema kwenye tukio linguine makazi wa Mkoani Kibaha Amani Aidan au Mgaya (24) amepoteza maisha baada ya pikipiki aliyokuwa amepanda kugongana na gari.
Kamanda Matei alisema tukio hilo lilitokea Machi 5 saa 1 usiku eneo la TAMCO barabara ya Dar es Salaam – Morogoro ambapo pikipiki hiyo ili gongana na gari namba T 787 AWC aina ya Toyota Coaster lililokuwa likiendeshwa na Thadei Makala (58).
Aidha alisema katika ajali hiyo mtu mmoja aliyetambuliwa kwa jina moja la Amina (22) mkazi wa Picha ya Ndege Kibaha alikimbizwa hospitali ya Tumbi kwa matibabu zaidi baada ya kupata majeruha sehemu za kichwani kulia.
Mwisho.

Na Mwandishi Wetu, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linamtafuta Ramadhan Mfaume maarufu kama Ngosha kwa tuhuma za kukutwa na silaha aina ya Short Gun na fuvu la mnayama aina ya Fungo na Ngiri.
Akizungmza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani hapo Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 4 mwaka huu.
 Kamanda Matei alisema kuwa vitu hivyo vilikamatwa nyumbani kwake kwenye eneo la Fitina haina Posho Kijiji cha Mwavi kata ya Fukayosi wilaya ya Bagamoyo.
 Aidha alisema kuwa mbali ya silaha hiyo ambayo namba zake hazikuweza kufahamika mara moja pia kulikutwa risasi 29.
Alisema mtuhumiwa huyo alitoroka na anatafutwa kuhusiana na tukio hilo na kuwataka wananchi kutomiliki silaha hizo bila ya kibali ili kuepukana na mkono wa sheria.
Mwisho. 


No comments:

Post a Comment