Na Mwandishi Wetu, Kibaha
MLINZI
wa kampuni ya ulinzi ya S&M ambaye alikuwa akilinda ofisi ya DAWSCO
wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Juma Hassan (45) ameuwawa na watu wanaodhaniwa
kuwa majambazi baada ya kuvamia ofisi hiyo.
Kamanda
wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alisema kuwa watu hao ambao idadi yao
haikuweza kufahamika mara moja walimteka kasha kumtupa baada ya kumfunga kamba
miguuni na mikononi pia walimziba na plasta mdomoni na puani.
Alisema
kuwa baada ya kumteka waliingia kwenye ofisi hiyo na kuiba kompyuta nne ambazo
thamani yake haikuweza kufahamika mara moja kasha kutoweka.
“Tunaendelea
na upeelelezi kujua ni watu gani waliofanya tukio hilo la kusikitisha na
tunawaomba wananchi kutoa taarifa endapo watasikia juu ya watu walio husika na
tukio hilo.
Alisema
kwenye tukio linguine makazi wa Mkoani Kibaha Amani Aidan au Mgaya (24) amepoteza
maisha baada ya pikipiki aliyokuwa amepanda kugongana na gari.
Kamanda
Matei alisema tukio hilo lilitokea Machi 5 saa 1 usiku eneo la TAMCO barabara
ya Dar es Salaam – Morogoro ambapo pikipiki hiyo ili gongana na gari namba T
787 AWC aina ya Toyota Coaster lililokuwa likiendeshwa na Thadei Makala (58).
Aidha
alisema katika ajali hiyo mtu mmoja aliyetambuliwa kwa jina moja la Amina (22)
mkazi wa Picha ya Ndege Kibaha alikimbizwa hospitali ya Tumbi kwa matibabu
zaidi baada ya kupata majeruha sehemu za kichwani kulia.
Mwisho.
Na
Mwandishi Wetu, Kibaha
JESHI
la Polisi mkoani Pwani linamtafuta Ramadhan Mfaume maarufu kama Ngosha kwa
tuhuma za kukutwa na silaha aina ya Short Gun na fuvu la mnayama aina ya Fungo
na Ngiri.
Akizungmza
na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani hapo Ulrich Matei
alisema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 4 mwaka huu.
Kamanda Matei alisema kuwa vitu hivyo
vilikamatwa nyumbani kwake kwenye eneo la Fitina haina Posho Kijiji cha Mwavi
kata ya Fukayosi wilaya ya Bagamoyo.
Aidha
alisema kuwa mbali ya silaha hiyo ambayo namba zake hazikuweza kufahamika mara
moja pia kulikutwa risasi 29.
Alisema
mtuhumiwa huyo alitoroka na anatafutwa kuhusiana na tukio hilo na kuwataka
wananchi kutomiliki silaha hizo bila ya kibali ili kuepukana na mkono wa sheria.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment