Na John Gagarini, Kibaha
WADAU wa soka mkoani Pwani wameipongeza timu ya Taifa kwa
kuifunga Moroco kwa magoli 3-1 kwenye mchezo wa kufuzu kushiriki kombe la
Dunuia nchini Brazil 2014 uliofanyika juzi kwenye uwanja wa Taifa Jijini Dar es
Salaam.
Akizungumza na gazeti hili mjinin Kibaha moja ya wadau wa
soka mkoani Pwani ambaye ni Mjumbe wa halmashauri Kuu ya Taifa Kibaha Mjini,
Rugemalila Rutatina alisema kuwa timu hiyo imeonyesha kiwango kizuri kwa kuweza
kukiangusha kigogo cha soka Barani Afrika.
Rutatina alisema kuwa Stars walionyesha mchezo mzuri ambao
uliwavutia watu waliokwenda kuutazama na kusema sasa matumaini yameanza
kuonekana kwenye soka la Tanzania.
“Tunawapongeza Vijana kwa kuonyesha kuwa wanaweza kwani
waitoa Tanzania kimasomaso kwa kuwapa raha Watanzania kwa kuifunga Moroco ambao
miaka ya nyuma walikuwa ni moja ya timu vigogo barani Afrika kutokana na uwezo
wake kisoka,” alisema Rutatina.
Alisema kuwa miaka ya nyuma Watanzania walikuwa
wakisikitishwa na matokeo yaliyokuwa yakitokea uwanjani kutokana na timu
kufungwa mbele ya mashabiki wake lakini sasa wameweza kuibuka kidedea.
“Kwa kweli vijana wameitoa nchi kimasomaso na hichi ndicho
Watanzania walichokuwa wakikitaka kwa miaka mingi tunawaomba wasibweteke na
ushindi huu bali waongeze jitihada kwa kujituma zaidi kwenye michezo ijayo ili
kwa mara ya kwanza Tanzania iweze kuingia kwenye ramani ya soka kwa kuingia
kwenye kombe la dunia,” alisema Rutatina.
Aidha alisema kuwa jukumu lililobaki kwa shirikisho la soka
nchini (TFF) ni kuitafutia Stars michezo mingi ya kirafiki hasa nje ya nchi ili
kuwpaa uzoefu wachezaji hasa wale ambao bado hawajawa na uzoefu kwa michuano ya
kimataifa.
“Stars itakuwa na michezo mingine ya nje hivyo lazima
wachezaji wapate uzoefu mkubwa kama tunavyojua michezo ya ugenini huwa ni
migumu kutokana na timu husika kutumia mazingira ya nyumbani kushinda,” alisema
Rutatina.
Aliwataka wachezaji wa Stars kulinda viwnago vyao ili
visishuke na kusababisha timu kufanya vibaya kwani bado kuna michezo migumu
mbele yao ili kufuzu kucheza kombe la dunia.
Mwisho.
Na John Gagarini,
Kibaha
BONDIA chipukizi Zumba Kukwe kutoka wilayani Kibaha mkoani
Pwani anatarajiwa kupanda ulingoni dhidi ya Joseph Mbowe wa Jijini Dar es
Salaam Aprili 7 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini kibaha bondia huyo
maarufu kama Chenchidola alisema kuwa pambano hilo litafanyika kwenye ukumbi wa
CCM Mwinjuma Mwananyamala Jijini Dar es Salaam.
Chenchidola alisema kuwa pambano lao hilo litakuwa ni la
utangulizi kabla ya pambano la kugombea ubingwa kati ya Shaban Madilu na Issa
Omary.
“Mchezo huo utakuwa ni wa kujiweka sawa kwani malengo ni kucheza
kwenye mashindano mbalimbali lakini kwa sasa nafanya mapambano ya kujipima
nguvu ili kujiimarisha kabla ya kukutana kuwania ubingwa,” alisema Chenchidola.
Alisema kuwa kwa sasa yuko imara kupambana na bondia yoyote
hapa nchini lakini kabla ya kufikia kupambana na mabingwa lazima ajiweke sawa.
“Natarajia kumpiga kwenye raundi ya pili au ya tatu na si
zaidi ya hapo hivyo akae sawa kwani nimejiandaa vilivyo katika mchezo huo na
endapo atanipiga basi itabidi niombe pambano la marudiano,” alisema
Chenchidola.
Aidha alisema kuwa lengo lake ni kupigana kwenye mapambano ya
ubingwa ambapo kwa sasa anatarajia kupambana na bondia mkubwa hapa nchini ili
awaonyeshe Watanzania kuwa anaweza.
Aliwataka mapromota kujitokeza kuwasaidia chipukizi ili nao
waweze kufikia kwenye viwango vya juu kwani wengi wako hasa mikoani lakini
hawapati nafasi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment