Tuesday, March 12, 2013

UTENDAJI KAZI MAZOEA UNAANGAMIZA TAIFA

Na John Gagarini, Kibaha

IMEELEZWA kuwa utendaji kazi wa mazoea umesababisha Taifa kushindwa kusonga mbele katika kuwaletea maendeleo wananchi kutokana na utendaji wa mazoea wa baadhi ya viongozi na wafanyakazi.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Alafayo Kidata naibu katibu mkuu Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa (TAMISEMI), alipokuwa akizungumza na viongozi wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC) baada ya ziara aliyoifanya kulitembelea Shirika hilo la Umma.

Kidata alisema kuwa baadhi ya watendaji kazi hasa kwenye mashirika na taasisi za serikali wamekuwa hawafanyi kazi ipasavyo na kufanya kazi kwa mazoea hali ambayo imekuwa haileti tija kwa maendeleo ya nchi.

"Tunapaswa kubadilika kama kweli tunataka kuleta mabadiliko ndani ya nchi yetu hatuwezi kufanya kazi kwa mazoea tu lazima kuwe na uwajibikaji vinginevyo tutazidi kulididimiza Taifa," alisema Kidata.

Alisema kuwa kwa upande wa mashirika ya Umma uzalishaji wake umekuwa ukishuka siku hadi siku kutokana na kutowajibika ipasavyo tofauti na mashirika binafsi ambayo yako makini katika utendaji kazi wake.

"Mashirika na taasisi binafsi zimekuwa zikifanikiw akutokana na kuwa makini katika utendaji kazi lakini kwa mashirika na taasisi za serikali hali imekuwa kinyume hii yote ni kutokana na watu kutowajibika ipasavyo," alisema Kidata.

Aidha alisema kwenye taasisi za Umma mfanyakazi anaweza kukaa mwezi mzima hajafanya kazi lakini mshahara unaingia kupitia ATM lakini hakuna mtu anayehoji je uwajibikaji hapo utakuwepo.

"Lazima wafanyakazi wa wajibike ipasavyo na kufanya kazi kama anavyoweza kuwajibika kwenye shughuli yake binafsi na uzalishaji wa kiwango kikubwa ndiyo utakaowaondoa kwenye matatizo mliyonayo hasa ya madeni," alisema Kidata.

Naye mkurugenzi wa KEC Dkt Cyprian Mpemba alisema kuwa changamoto kubw ailiyopo kwenye shirika hilo ni ukosefu wa fedha na madeni makubwa ya watumishi na watoa huduma katika shirika hilo ambalo lilianzishwa miaka ya 70.

mwisho.


  

 





No comments:

Post a Comment