Na John
Gagarini, Kibaha
MBUNGE wa
Jimbo la Kibaha Mjini mkoani Pwani Silvestry Koka amelazimika kuwalipa fedha kiasi
cha shilingi 275,000 wanawake watatu wanaouza samaki baada ya mgambo wa kata ya
Maili Moja kumwaga samaki wao kwa madai ya kukiuka kanuni za afya.
Koka ilibidi
alipe fedha hizo kwa wafanyabiashara hao baada ya kuangua kilio mbele ya mbunge
huyo wakati wa mkutano na wananchi wa Kibaha.
Alisema hayo
yalikuwa makosa ya kibinaadamu yaliyofanywa na mgambo hao wakati wakitekeleza
zoezi la usafi kwenye maeneo mbalimbali ya mji wa Kibaha.
“Suala la afya
ni muhimu na mgambo hawa waliteleza na kujikuta wakiharibu mali za
wafanyabiashara ambao wanajitafutia riziki zao huku wengine wakiwa wamekopa
fedha kwa ajili ya kufanyia biashara hiyo,” alisema Koka.
Mbunge huyo
alisema kuwa kuanzia sasa wafanyabiashara na mgambo hao kwa kushirikiana na
ofisi ya afya ya kata kila upande kufuata kanuni na sheria ili kufanikisha
suala la afya.
Kwa upande
wao wakinamama hao mmoja wao aliyejitambulisha kwa jina la Riziki Said alisema
kuwa mgambo hao walifika kwenye biashara yake na kusema kuwa kwakuwa hakupima
afya yake na kuwamwaga samaki wake wenye thamani ya shilingi 65,000.
Naye mfanyabiashara
mwingine Nuru Msangi alisema kuwa mgambo hao walichukua samaki wake wenye
thamani ya shilingi 75,000 na kuzimwaga kwa madai kuwa naye hakupima afya yake.
Alisema kuwa
wafanyabiashara wengi wanashindwa kupima afya zao kutokana na gharama kubwa ya
kupima ya shilingi 5,000 na pia walisema wao kama wanshinikizwa kupima je kwa
wateja wanaokwenda kununua mbona hawabanwi.
Mbunge huyo
alizitaka pande mbili hizo kati ya idara ya afya ya kata hiyo na wafanyabiashara
kuanza mahusiano mazuri upya ili kuondoa ugomvi unaojitokeza mara kwa mara pia
halmashauri itoe elimu juu malipo hayo ya kupima afya ya shilingi 5,000.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment