Friday, March 1, 2013

MTOTO AUNGUZWA NA MAJI YA MOTO




Na John Gagarini, Kibaha
MKAZI wa Mtaa wa Kwa Mfipa wilayani Kibaha Nuru Rashid amewashangaza wakazi wa mtaa huo kwa kushindwa kumpeleka hospitali mwanae mwenye umri wa miaka miwili na nusu baada ya kuungua na maji ya moto.
Akizungumza na baba mzazi Ally Said alisema mwanae ambaye ni wa jinsi ya kiume ameungua kifuani na kusababisha kidonda kikubwa hadi kwenye mkono wake wa kushoto hakumpatia matibabu yoyote hadi siku iliyofuata.
Said alisema kuwa tukio hilo lilitokea Februari 27 mtaani hapo nyumbani kwa mama yake mazazi ambaye walitengana naye zaidi ya mwaka mmoja uliopita ambapo aliolewa na mume mwingine.
“Mimi baada ya kupata habari juu ya mwanangu kuunguzwa na maji siku iliyofuata nilikwenda nyumbani kwake kutaka kumchukua mwanangu ili nimpeleke hospitali lakini alikataa na kusema hadi baba yake wa kambo aje jambo ambalo alilikataa na kumchukua kwa nguvu,” alisema Said.
Alisema kuwa mkewe amekuwa akimficha juu ya matatizo hasa pale anapoumwa na mbaya ni pale alipomficha mwanae baada ya kuungua na kushangaa ni kwanini hataki kumpeleka hospitalini.
Jitihada za kumpata mama huyo yazikuweza kuzaa matunda licha ya mwandishi kufika nyumbani kwake na kuambiwa kaenda dukani na hata aliposubiriwa hakuweza kutokea.
Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa huo Hai Hai alikiri kupata tukio hilo na kusema kuwa ukweli halisi alikuwa nao mama huyo ambaye ndiye aliyekuwa akiishi na mtoto huyo ambaye alikuwa akilia kutokana na maumivu makali aliyoyapata.
Hai alisema kuwa hatua aliyoichukua ni kuandika barua ambayo ilibidi ipelekwe polisi kwa ajili ya taratibu za kisheria na kupatiwa matibabu kwa mtoto huyo na kusema hicho ni kitendo cha unyanyasaji na kuwanyima haki watoto wadogo.
Mwisho.     
 Mtoto aliyeunguzwa na maji ya moto akiwa amepumzika huku nyumbani kwao huko Kwa Mfipa wilayani Kibaha mkoani Pwani (Picha na John Gagarini)






No comments:

Post a Comment