Sunday, April 21, 2013

WATOTO WACHANAGA KUPATIWA CHANJO

Na John Gagarini, Kibaha

JUMLA ya watoto 2,628 kati ya watoto 38,356 wenye umri chini ya mwaka mmoja wanatarajiwa kupatiwa chanjo mbalimbali mkoani Pwani.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Simon Malulu mratibu wa maandalizi ya uzinduzi wa chanjo kitaifa yatakayofanyika Aprili 22 hadi 28 shule ya Msingi Mlandizi wilayani Kibaha ambapo mgeni rasmi atakuwa mke wa Raisi Mama Salama Kikwete.

Malulu alisema kuwa hiyo ni awamu ya tatu ya chanjo ambapo watoto hao hawakuipata ilipoanza Januarimwakahuu    

“Jumla ya vituo kimkoa ni 258 na vinavyotoa chanjo ni 206 ambayo ni sawa na asilimia 80," alisema Malulu.

Alitaja chanzo zitakazotolewa kuwa ni homa ya matumbo, homa ya uwati wa mgongo na magonjwa mengine.

“Mkoa umeweza kupiga hatua katika kiwango cha utoaji chanjo zote na kuwa juu ya lengo la taifa la asilimia 90,” alisema Malulu.

Malulu ambaye pia ni ofisa afya wa mkoa alisema kuwa uzinduzi wa Chanjo hiyo inalenga watoto ambao hawakukamilisha ama hawajawahi kupatiwa chanjo mbalimbali.

Akizungumzia kukamilika kwa maandalizi ya shughuli hiyo mkuu wa wilaya
ya Kibaha  Halima Kihemba alisema anategemea wananchi kukusanyika
kwa wingi ili kupata uelewa wa chanjo mbalimbali zinazoweza kukinga
magonjwa kwa watoto.

mwisho.

No comments:

Post a Comment