WATOTO WACHANAGA KUPATIWA CHANJO
Na John Gagarini, Kibaha
JUMLA ya watoto 2,628 kati ya
watoto 38,356 wenye umri chini ya mwaka mmoja wanatarajiwa kupatiwa chanjo
mbalimbali mkoani Pwani.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Simon
Malulu mratibu wa maandalizi ya uzinduzi wa chanjo kitaifa yatakayofanyika
Aprili 22 hadi 28 shule ya Msingi Mlandizi wilayani Kibaha ambapo mgeni rasmi
atakuwa mke wa Raisi Mama Salama Kikwete.
Malulu alisema kuwa hiyo ni awamu
ya tatu ya chanjo ambapo watoto hao hawakuipata ilipoanza Januarimwakahuu
“Jumla ya vituo kimkoa ni 258 na vinavyotoa
chanjo ni 206 ambayo ni sawa na asilimia 80," alisema Malulu.
Alitaja chanzo zitakazotolewa
kuwa ni homa ya matumbo, homa ya uwati wa mgongo na magonjwa mengine.
“Mkoa umeweza kupiga hatua katika
kiwango cha utoaji chanjo zote na kuwa juu ya lengo la taifa la asilimia 90,”
alisema Malulu.
Malulu ambaye pia ni ofisa afya
wa mkoa alisema kuwa uzinduzi wa Chanjo hiyo inalenga watoto ambao
hawakukamilisha ama hawajawahi kupatiwa chanjo mbalimbali.
Akizungumzia
kukamilika kwa maandalizi ya shughuli hiyo mkuu wa wilaya
ya Kibaha Halima Kihemba alisema anategemea wananchi kukusanyika
kwa wingi ili kupata uelewa wa chanjo mbalimbali zinazoweza kukinga
magonjwa kwa watoto.
mwisho.
No comments:
Post a Comment