Akizungumza wakati wa sherehe za Siku ya Wanawake Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani Hawa Mchafu amesema uwepo wa mazingira hayo unaondoa ukatili wa kijinsia.
Mchafu amesema kuwa uwepo wa usawa na kulinda kulinda haki za wanawake kuna mchango mkubwa katika suala la maendeleo.
"Usawa wezeshi hiyo ni nyenzo muhimu ili kuketa utandaji wa pamoja wa kufikia malengo ya dira ya maendeleo na kuongeza ushiriki wanawake kwenye masuala muhimu yakiwemo ya uongozi,"amesema Mchafu.
Amesema kuwa dhumuni la kuwarudisha wasichana waliopata mimba wakiwa shuleni ni kutimiza ndoto zao kwani siyo wote waliopata ujauzito kwa kupenda au tamaa bali ni kutokana na mazingira wanayoishi na wengine wamepewa na ndugu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa aesma kuwa asilimia 70 ya watumishi ni wanawake menejimenti idara tano zinaongozwa na wanawake ambapo wanafanya kazi nzuri ikiwemo kwenye zoezi la ukusanyaji mapato.
Shemwelekwa amesema kuwa wamewawezesha wanawake wenye biashara ndogo ndogo kuunda vikundi ambapo walikuwa hawakopesheki lakini sasa wamekopeshwa bilioni 2 na wanarejesha vizuri.
Naye Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Leah Lwanji amesema kuwa vikundi 275 vya wanawake vimekopeshwa zaidi ya bilioni 1 ikiwa ni asilimia 94.
Lwanji amesema kuwa majukwaa yamehamasishwa kuanzishwa miradi ya kiuchumi ili waweze kujikwamua na mpaka sasa zimekopeshwa milioni 70 kwa akinamama wa majukwaa.
Moja ya kikundi ambacho ni cha mfano cha Lulu ya Wajane mwaka jana kilipata mkopo wa shilingi milioni 46 ambapo walipaswa kurejesha mkopo huo kwa miaka mitatu lakini kimeweza kurejesha ndani ya miezi 11.
Kiongozi wa kikundi hicho Kanyenda Mweri amesema kuwa fedha hizo za mikopo isiyokuwa na riba zimewasaidia kuwakwamua kiuchumi na kuweza kutoa ajira kwa wanawake wenzao.

No comments:
Post a Comment