Tuesday, March 10, 2026

DED GAIRO APONGEZWA UJENZI WA SHULE YA AMALI

Hawa Wazee wangu ni Wawakilishi wa wana Kijiji cha Kwipipa kata ya Rubeho.

Walituma salam zao kupitia kwa Mhe. Diwani wiki mbili zilizopita kuwa wananiita. Na leo nimekutana nao kuwasilikiza, kumbe walitaka kunipa shukrani kwa ajili ya Mradi wa Shule ya AMALI iliyojengwa kwenye Kijiji cha Kwipipa. Wameshukuru kwa Usimamizi hadi Ukamilishaji wa shule na hatimae watoto wameanza masomo

Wazee wangu hawa tulianza nao wakati tunatafuta eneo na wakatoa eneo lote la Mradi. Wametoa salamu zao kwa Maandishi, kuongea na mwisho wakatoa mbuzi.


No comments:

Post a Comment