SERIKALI imesema kuwa elimu ni nguzo ya kuwalinda watoto na ukatili ndoa na mimba za utotoni na kuwataka wazazi na walezi kuhakikisha wanatimiza haki ya msingi ya mtoto kupata elimu.
Thursday, June 26, 2025
DMI MISSION TANZANIA KUKABILI MIMBA NDOA ZA UTOTONI
SERIKALI imesema kuwa elimu ni nguzo ya kuwalinda watoto na ukatili ndoa na mimba za utotoni na kuwataka wazazi na walezi kuhakikisha wanatimiza haki ya msingi ya mtoto kupata elimu.
Wednesday, June 25, 2025
MATUMLA PROMOTION KUINUA VIPAJI VYA NGUMI KIBAHA
Thursday, June 19, 2025
DIWANI KATA YA MBWAWA JUDITH MLUGE AELEZA MAFANIKIO YA MIAKA 5
Sunday, June 15, 2025
RIDHIWANI KIKWETE AKISHIRIKI MAADHIMISHO UELEWA KUHUSU ALBINO
Shughuli hii iliongozwa na Mh. Kassim Majaliwa Majaliwa , Waziri Mkuu wa JMT , zilizofanyika katika viwanja wa Mwanga Mkoani Kigoma tarehe 13 Juni 2025.
Maadhimisho haya yamekuwa yakifanyika kila mwaka na utumika kukumbushana umuhimu wa kushirikisha wenye Ualbino, Haki zao, umuhimu wa serikali kuendelea kuangalia maslahi na ulinzi wao.
Katika Shughuli ya Mwaka huu mtandao maalum wa kusajiri watu wenye Ulemavu unaowezesha usajiri kwa njia ya Elektronik hata kwenye maeneo yaliyo nje ya mtandao nao ulizinduliwa.
Mfumo huo unawezesha taarifa za watu wenye ulemavu kuchukuliwa na kuchambuliwa ambapo zitaiwezesha serikali kupata taarifa za kina zitakazowezesha kupanga mipango ya maendeleo ikiwemo kuwashirikisha wenye Ulemavu.
Waziri Mkuu wa JMT alitumia nafasi hiyo pia kutoa maagizo mahsusi kwa wakuu wa Mikoa na wadau waliokuwapo kuhusu matumizi sahihi ya mtandao huo na kuwashirikisha watu wenye Ulemavu kwa jumla katika shughuli mbalimbali ikiwemo Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadae Mwezi Oktoba mwaka huu uku akiwahamasisha watu wenye Ualbino nao kujitokeza kushiriki uchaguzi huo.
Friday, June 13, 2025
SUBIRA MGALU ATOA GARI KWA (UWT) BAGAMOYO
Friday, June 6, 2025
CHOKALA AISHUKURU SERIKALI KUTOA BILIONI 4.2 ZA MAENDELEO KATA YA TUMBI
WAKALA WA VIPIMO (WMA) YATAKA VIPIMO VIHAKIKIWE KILA MWAKA
WAKALA wa Vipimo Nchini (WMA) imetaka vipimo vya ujazo urefu na uzito wakati wa kupima bidhaa au kuhudumia wananchi lazima vihakikiwe kila baada ya miezi 12.
Thursday, May 29, 2025
MWANASHERIA MATATANI AKITUHUMIWA KUGHUSHI AKAUNTI YA KIJIJI NA KUJIPATIA FEDHA

Saturday, May 24, 2025
DIWANI MTAMBO AWASILISHA TAARIFA UTEKELEZAJI WA ILANI YA MIAKA 5
GRACE JUNGULU AONGOZA KIKAO UTEKELEZAJI ILANI KATA YA PICHA YA NDEGE
Wednesday, May 21, 2025
ATAKA SIMBA IUNGWE MKONO KUCHUKUA KOMBE LA SHIRIKISHO DHIDI YA BERKANE
WACHEZAJI viongozi na benchi la ufundi la timu ya Simba wametakiwa kupambana kuhakikisha wanatwaa kombe la Shirikisho.
Aidha washabiki na wapenzi wa soka nchini wametakiwa kuwa na mshikamano na kuacha tofauti zao za ushabiki na kuungana ili kuisadia timu ya Simba kwenye mchezo wao wa fainali dhidi ya Berkane mchezo utakaochezwa uwanja wa Amani Zanzibar.
Akizungumza na Brailo Media aliyewahi kuwa mlezi wa Tawi la Simba Tishio Kibaha Fahim Lardhi amesema kuwa Watanzania wanapaswa kuungana kwenye mchezo huo kwani ni wa heshima kwa nchi.
Lardhi amesema kuwa licha ya Simba kufungwa kwenye hatua ya kwanza kwa magoli 2-0 lakini wanaimani kuwa Simba itapindua matokeo na kuwa mabingwa.
"Tuenzi maneno ya Rais Hayati Dk John Magufuli aliyoitoa kwenye uwanja wa Mkapa wa kutaka Simba au timu nyingine ya Tanzania kuleta kombe la Afrika,"amesema Lardhi.
Amesema kuwa itakuwa ni fedhaha kwa Simba kuchukua kombe hilo ambalo litakuwa kwenye ardhi ya Tanzania ambapo mwaka 1993 walifungwa kwenye fainali na Stella Abidjan ya Ivory Coast.
"Mwaka huu kwa uzalendo wetu tuhakikishe tunalipigania Taifa letu kama kila mtu atatimiza wajibu wake kuanzia wachezaji hadi kwa mashabiki,"amesema Lardhi.
Amewaomba Watanzania kuwa na mshikamano kwa wakati wa maandalizi na wakati wa mchezo kwa kuungana na kuacha tofauti kwani hiyo ni mechi ya heshima kwa nchi.
Monday, May 19, 2025
WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA WARIPOTI HABARI ZA UCHAGUZI KWA UMAKINI
VYOMBO vya Habari nchini vimetakiwa kutoa taarifa za vyama vyote vya siasa kwenye kampeni wakati wa uchaguzi wa mwaka huu ili wananchi waweze kujua sera za vyama na kuchagua viongozi bora.
SERIKALI IDHIBITI FEDHA HARAMU
Friday, May 16, 2025
WATAKIWA KUWATIA MOYO VIONGOZI
Tuesday, May 13, 2025
WAFANYABIASHARA SOKO LA LOLIONDO WARIDHIA KUJENGWA UPYA
KUFUATIA mpango wa Halmashauri ya Mji Kibaha kulibomoa na kujenga upya soko la Loliondo liwe a kisasa uongozi wa soko hilo umeridhia lakini umetoa maombi kwa Halmashauri hiyo.
Sunday, May 11, 2025
ALIYE OKOLEWA NA MKUNGU WA NDIZI AJALI YA MV BUKOBA MIAKA 29 ILIYOPITA ASIMULIA MKASA MZIMA
ILIKUWA mwaka 1996 majira ya asubuhi nilisikia wimbo wa Taifa kupitia Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) wakati huo kwa sasa ni TBC Taifa jambo ambalo si la kawaida kwani unapopigwa wimbo huo basi kuna tukio kubwa la kitaifa ambapo Rais wa Awamu ya Tatu Benjamini Mkapa alitangaza kutokea tukio la ajali ya Mv Bukoba iliyotokea Mkoani Mwanza.
Thursday, May 8, 2025
WANACHAMA WA CCM NYANG'WALE WATAKA KUHARAKISHWA UJENZI WA OFISI.
WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita wametaka ujenzi wa ofisi ya chama ufanyike kwani tayari baadhi ya wadau wamechangia fedha za ujenzi huo.
Wamesema moja ya wadau waliochangia fedha kwa ajili ya ujenzi huo ni Naibu Waziri Mkuu Dotto Biteko ambaye alichangia kiasi cha shilingi milioni 50.
Wamesema kuwa fedha hizo zilikabidhiwa kwa Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Hussein Amar hivyo kutaka fedha hizo zifanye ujenzi huo ili kupata ofisi kwa kazi za chama.
"Tunataka ujenzi ufanyike kwani kama ni fedha zipo hakuna sababu ya kuchelewesha ujenzi huo wa ofisi ya chama ambapo endapo itajengwa itakuwa ya kisasa,"wamesema wanachama hao.
Waliongeza kuwa wanataka fedha hizo zijenge na kukamilisha ofisi ya chama na kwamba wao wanachotaka ni kuona CCM Wilaya ya Nyang'hwale inaendelea kama Wilaya nyingine zilivyoendelea.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Hussein Amar akizungumza kwa njia ya simu ameeleza kusitikishwa na malalamiko ya wananchama hao huku akisema jambo hilo halina usiri wowote.
Amar amesema kuwa yeye ndiye iliyemuomba awasaidie na sio mara moja amekuwa akisaidia na bahati nzuri alipokuja yeye mwenyewe alimkumbushia ombi hilo na akakubali kusaidia lakini hakutamka kiwango.
Aidha amesema kuwa fedha hizo zilivyoingia alimpa taarifa Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti wa Chama, Mwenezi, kamati ya Siasa na kamati ya ujenzi na yeye ndiye aliyetafuta fundi na kuwashauri kuwa kuna fundi kwa hiyo ni vyema akatumika kwakuwa yupo vizuri.
Mbunge huyo ameongeza kuwa yeye binafsi amekuwa na mchango mkubwa sana katika ujenzi wa ofisi hiyo ya Chama maana alishawai kutoa mashine zake na magari yake (Tipa) kufanyakazi katika ujenzi huo.
"Fedha zipo mikono salama na Mei 3 niliongea na Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi kumweleza juu ya fedha kwani zinatakiwa kufanyakazi iliyokusudiwa kwa kuwa mimi sitaki kukaa nazo nipeni akaunti niwahamishie lakini alinijibu kuwa watakaa na kamati yake ya ujenzi na akasema wakati huu aendelee kukaa nazo na wakihitaji kununua vifaa watamjulisha ili atoe hizo fedha",amesema Amar.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyang'hwale Adam Mtore amesema kuwa kama kuna malalamiko ndani ya Chama kuuna utaratibu wake na mara nyingi huanzia ngazi ya chini ya tawi lakini kwakuwa suala hilo linagusa ngazi ya Wilaya ilitakiwa wapeleke malalamiko yao kwa Katibu wa Chama Wilaya.
Saturday, May 3, 2025
KECA YAUNGA MKONO SERIKALI UHIFADHI MAZINGIRA NA UFUGAJI NYUKI
Thursday, May 1, 2025
MKUU WA MKOA WA PWANI ABUBAKARI KUNENGE ATOA WIKI MOJA KWA WAAJIRI WANAOKIUKA HAKI ZA WAFANYAKAZI
Wednesday, April 30, 2025
MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KIBAHA MJINI YATAKIWA KUSHIRIKIANA
Saturday, April 19, 2025
BALOZI MATINYI AAHIDI KUITANGAZA TANZANIA KIMATAIFA
BALOZI wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, amesema kuwa atatumia uzoefu alioupata katika kazi yake ya uandishi wa habari kutafuta taarifa na kung'amua mbinu za kuvutia watalii wengi kama ilivyo katika nchi hiyo ambayo inavutiwa na kutembelewa na watalii wengi.
"Nitakapofika katika nchi hizo tisa katika eneo langu la uwakilishi nitahakikisha ninatafuta na kujua ni mbinu gani wanazotumia kuvutia watalii kwani watalii wengi duniani huenda kwenye nchi hizo", alisema Mhe. Balozi Matinyi.
Alisema pia kuwa kwa kutumia uzoefu wake katika uandishi wa habari - fani ambayo hujenga tabia ya udadisi na mbinu za kutafuta taarifa za uwekezaji na pia tabia kulikamilisha jukumu la kazi baada ya kulichukua.
Balozi Matinyi alisema hayo hivi karibuni katika mahojinao maalumu na kituo cha televisheni cha ZBC cha Zanzibar.
Alifafanua kwa kueleza kuwa diplomasia ya uchumi nchini ilianzishwa katika utawala wa awamu ya tatu ambapo ili kuujenga uchumi wetu baada ya kumaliza kuzisaidia nchi zingine za Afrika kupata uhuru.
"Hii ndiyo sababu viongozi wetu wakuu wanatusisitizia kwamba tunapokwenda nje ya nchi tukaifanyie kazi diplomasia ya uchumi," alidokeza Mhe. Balozi Matinyi.
"Nitakapofika katika nchi hizo tisa zilizoendelea kiuchumi, katika sekta ya uvuvi, kilimo katika viwanda vya mbolea na matrekta, utalii ambapo wanapokea watalii kati ya milioni 6 hadi 7 kwa mwaka wakitumia visiwa vingi na bahari kuvutia watalii, jukumu langu litakuwa kuhakikisha tunapata mbinu zao na Watanzania tunasonga mbele kiuchumi" alisema Mhe. Balozi Matinyi.
Aidha, akizungumzia namna atakakavyoiwakilisha Zanzibar, alisema kuwa tayari ameshapata maelezo mbalimbali kutoka taasisi za uwekezaji, kama za uchumi wa buluu na utalii na hivyo kuwa katika nafasi nzuri ya kujua namna ya kuielezea Zanzibar.
"Tuna nchi tisa katika eneo ninalokwenda wenye tabia ya kutaka kufahamu vyakula vya watu wengine; hivyo, nitawaeleza kwamba Zanzibar kuna viungo vya kipekee vyenye ladha nzuri."
Mhe. Balozi Matinyi amezitaja nchi ambazo atakuwa mwakilishi mbali ya Sweden kuwa Denmark, Finland, Norway, Iceland, Estonia, Latvia, Lithuania na Ukrane.
Akijibu swali kuhusu mgogoro wa nchi za Ukraine na Russia, Mhe. Balozi Matinyi alisema kuwa Tanzania inasimamia amani na hivyo inataka nchi zinapokwaruzana zitafute suluhu kwa mazungumzo na si kupigana vita.
Thursday, April 17, 2025
UJENZI WA MRADI WA MAJI PANGANI KIBAHA WAANZA
MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imemkabidhi mkandarasi eneo la mradi wa maji wa Pangani Wilayani Kibaha Mkoani Pwani utakaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.9.
Thursday, April 3, 2025
UJENZI KIWANGO CHA LAMI BARABARA YA PICHA YA NDEGE-BOKOMNEMELA UNARIDHISHA-MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ISMAIL USSI
MWENGE wa Uhuru umeridhishwa na mradi wa ujenzi wa barabara ya Picha ya Ndege-Bomotimiza yenye urefu wa mita 550 kiwango cha lami wenye thamani ya shilingi milioni 760.
MWENGE WAZINDUA MRADI WA KISIMA CHA MAJI HOSPITALI YA TUMBI KUTOA LITA 10,000 KWA SAA
USSI ATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA MIKOPO ASILIMIA 10 YA HALMASHAURI WAJIKWAMUE KIUCHUMI
VIJANA kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha Mkoani Pwani wametakiwa kujiunga kwenye vikundi ili waweze kupata fedha za mikopo asilimia 10 za mapato ya ndani ya Halmashauri ili wajikwamue kiuchumi.
KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ISMAIL USSI APONGEZA UJENZI ZAHANATI KILIMAHEWA

MWENGE WAWEKA JIWE LA MSINGI MRADI SHULE YA AWALI MSINGI YA MCHEPUO WA KIINGEREZA KATA YA SOFU
KIONGOZI MBIO ZA MWENGE ASIFU MRADI WA MAEGESHO YA MALORI YA MIZIGO
MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.