Thursday, June 26, 2025

DMI MISSION TANZANIA KUKABILI MIMBA NDOA ZA UTOTONI









SERIKALI imesema kuwa elimu ni nguzo ya kuwalinda watoto na ukatili ndoa na mimba za utotoni na kuwataka wazazi na walezi kuhakikisha wanatimiza haki ya msingi ya mtoto kupata elimu.

Hayo yamesemwa na Madina Mussa ambaye alimwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha wakati wa kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika iliyoandaliwa na DMI Mission Tanzania.

Mussa amesema kuwa ili kutekeleza mazingira rafiki kwa watoto waweze kupata haki hiyo ya msingi imejenga miundombinu mizuri ya watoto kujisomea.

"Katika kukabiliana na ukatili na ndoa za utotoni wazazi na walezi lazima washirikiane na serikali kuhakikisha haki za msingi za mtoto zinalindwa ikiwa ni pamoja na elimu, kumlinda na ukatili na kuishi katika mazingira mazuri kwani haki za mtoto zinaanzia nyumbani,"amesema Madina.

Awali Mkurugenzi wa DMI Mission Tanzania Sister Fathima Jacintha Ran amesema kuwa dhima ya siku hiyo ni Kupanga bajeti na kuweka bajeti kwa haki za watoto.

Ran amesema kuwa lengo ni kuhakikisha ustawi, elimu, na hatma njema za watoto ikiwa ni kukumbusha wajibu wa pamoja kuhakikisha watoto wa Afrika wanapata haki za msingi za elimu bora, huduma za afya, ulinzi na fursa ya kukua.

Naye Ofisa Maendeleo ya Jamii kitengo cha watoto Halmashauri ya Mji Kibaha Hanifa Mruma amesema kuwa mradi ulioanzishwa na shirika hilo wa kupambana na mimba za utotoni ni mzuri na utasaidia kukabiliana na changamoto hiyo.

Kwa upande wake moja ya wanufaika kwenye mradi huo wa Klabu za Wanawake Vijana Chiku Hamis amesema kuwa wanalishukuru shirika hilo kwa kuwapatia vifaa kwa ajili ya kutengeneza batiki na sabuni kwa ajili ya mafunzo ya utengenezaji vitu hivyo. 

Mradi huo wa kupunguza mimba za utotoni unatekelezwa kwenye Kata tatu za Pangani, Tumbi na Kongowe.

Wednesday, June 25, 2025

MATUMLA PROMOTION KUINUA VIPAJI VYA NGUMI KIBAHA

MATUMLA Promotion ya Kibaha imeandaa pambano la ngumi kati ya Abdully Said au Dully Bwengo na Rashid Hassan au Makali litakalopigwa kwenye baa ya UEFA Kongowe Kibaha Juni 28 mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na pambano hilo ambalo litasindikizwa na mapambano mengine matano Mkurugenzi wa Matumla Promotion Abuu Matumla amesema kuwa maandalizi ya awali yamekamilika.

Matumla amesema kuwa maandalizi yakiwemo ya kuwalipa fedha za awali yameshafanyika na mabondia hao watakamilishiwa fedha zao baada ya pambano hilo kukamilika.

"Taratibu za awali zimekamilika ikiwa ni pamoja na malipo ya awali kwa mabondia, vibali na ulinzi vyote viko tayari kinachosubiriwa ni siku ya pambano hilo,"amesema Matumla.

Alisema kuwa malengo ya kuandaa mapambano hayo ni kuhamasisha mchezo huo kwa vijana wa Kibaha kwani mchezo huo ni ajira na kujenga afya bora na kuwaondoa vijana kwenye vitendo hatarishi.

"Tunataka tuinue mchezo wa ngumi Kibaha ambapo pia kutakuwa na pambano la wanawake ikiwa ni sehemu ya kuwahamasisha wanawake nao washiriki mchezo huo kwani hata wao wanauwezo wa kushiriki mchezo huo,"amesema Matumla.

Aidha alisema kuwa mbali ya mapambano hayo pia kutakuwa na burudani za muziki zikiongozwa na mkali wa Singeli Yuda Msaliti na waimbaji wengine wakali wa miondoko hiyo ya singeli.

"Nawaomba wapenzi wa mchezo wa ngumi kujitokeza kwa wingi kushuhudia vipaji vya vijana wao ili kuwapa hamasa wapende mchezo huo ambao umekuwa ukipendwa na wengi,"amesema Matumla.

Thursday, June 19, 2025

DIWANI KATA YA MBWAWA JUDITH MLUGE AELEZA MAFANIKIO YA MIAKA 5

KATA ya Mbwawa Halmashauri ya Mji Kibaha Mkoani Pwani imeweza kufungua barabara 35 kwenye kata kupitia fedha za mapato ya ndani kiasi cha shilingi milioni 10 zilizotolewa kwenye kila kata.

Akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mafanikio kwa kipindi cha miaka mitano Diwani aliyemaliza muda wake wa Kata hiyo Judith Mluge amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano maendeleo makubwa yamepatikana.

Mluge amesema kuwa mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na upatikanaji wa huduma ya maji ambayo haikuwepo ikiwa ni asilimia 80, umeme unapatikana kwa asilimia 80 hadi 100.

"Kuhusu suala la afya kwenye zahanati za Kata hiyo kwa sasa dawa zinapatikana kwa asilimia 90 na ukarabati wa jengo la mama wajawazito liko mbioni kukamilika,"amesema Mluge.

Aidha amesema kuwa katika kukabiliana na changamoto za mimba kwa wasichana wanaendelea na ujenzi wa bweni kwenye shule ya sekondari ya Mbwawa.

"Katika kipindi hicho tumefanikiwa kujenga ofisi ya kata pia nimekinunulia chama kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa ofisi na Mungu akipenda ujenzi utaanza mwakani,"amesema Mluge.

Amesema kuwa kwa upande wa mikopo asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri fedha zilitolewa lakini baadhi wameshindwa kurejesha mikopo kiasi cha shilingi milioni 88.

"Changamoto tuliyoipata ni baadhi ya wakazi wanaokaa ngambo ya mto Ruvu ambapo tulitaka kujenga daraja lakini Mto huo umekuwa ukibadili mwelekeo,"amesema Mluge.

Ameongeza kuwa wanaishukuru serikali kwa kuwapatia fedha kiasi cha shilingi bilioni 1 kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa kipindi cha miaka mitano.

Sunday, June 15, 2025

RIDHIWANI KIKWETE AKISHIRIKI MAADHIMISHO UELEWA KUHUSU ALBINO

Nimeshiriki shughuli za kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelewa Kuhusu Albino.

Shughuli hii iliongozwa na Mh. Kassim Majaliwa Majaliwa , Waziri Mkuu wa JMT , zilizofanyika katika viwanja wa Mwanga Mkoani Kigoma tarehe 13 Juni 2025.

Maadhimisho haya yamekuwa yakifanyika kila mwaka na utumika kukumbushana umuhimu wa kushirikisha wenye Ualbino, Haki zao, umuhimu wa serikali kuendelea kuangalia maslahi na ulinzi wao.  

Katika Shughuli ya Mwaka huu mtandao maalum wa kusajiri watu wenye Ulemavu unaowezesha usajiri kwa njia ya Elektronik hata kwenye maeneo yaliyo nje ya mtandao nao ulizinduliwa. 

Mfumo huo unawezesha taarifa za watu wenye ulemavu kuchukuliwa na kuchambuliwa ambapo zitaiwezesha serikali kupata taarifa za kina zitakazowezesha kupanga mipango ya maendeleo ikiwemo kuwashirikisha wenye Ulemavu.  


Waziri Mkuu wa JMT alitumia nafasi hiyo pia kutoa maagizo mahsusi kwa wakuu wa Mikoa na wadau waliokuwapo kuhusu matumizi sahihi ya mtandao huo na kuwashirikisha watu wenye Ulemavu kwa jumla katika shughuli mbalimbali ikiwemo Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadae Mwezi Oktoba mwaka huu uku akiwahamasisha watu wenye Ualbino nao kujitokeza kushiriki uchaguzi huo.

Friday, June 13, 2025

SUBIRA MGALU ATOA GARI KWA (UWT) BAGAMOYO

MBUNGE wa Mkoa wa Pwani Subira Mgalu ameupatia gari uongozi wa Jumuiya ya Wanawake CCM kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Akizungumza wakati wa kukabidhi gari hilo aina ya Noah Mgalu amesema kuwa moja ya nadhiri aliyojiwekea kipindi cha nyuma ilikuwa ni kuhakikisha anainunulia chombo cha usafiri Jumuiya hiyo ili kurahisisha utendaji kazi.

Mgalu amesema kuwa ni vyema gari hilo likatumika kutafuta kura za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan huko kwenye matawi kwa kuwakumbusha wananchi kile kilichofanyika kwenye maeneo yao.

"Gari hili likatumiwe na Jumuiya zote za chama ikiwemo Wazazi na Vijana ili ziweze kufanikisha malengo ya chama chetu,"amesema Mgalu.

Akikabidhi gari hilo kwa Katibu wa  Wilaya ya Bagamoyo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mery Chatanda amempongeza  Mbunge huyo kwa jinsi ambavyo amekuwa akijitoa kwa Jumuiya hiyo.

Chatanda amewataka viongozi wa Bagamoyo kuhakikisha wanaitumia gari hiyo kwa makusudio yaliyokusudiwa ili kurahisisha shughuli za utendaji wa Jumuiya

Friday, June 6, 2025

CHOKALA AISHUKURU SERIKALI KUTOA BILIONI 4.2 ZA MAENDELEO KATA YA TUMBI

DIWANI wa Kata ya Tumbi Halmashauri ya Mji Kibaha Raymond Chokala amesema fedha zilizotolewa na serikali kiasi cha shilingi bilioni 4.2 kwa kipindi cha miaka mitano zimeleta maendeleo makubwa kwenye Kata hiyo.

Akizungumza kwenye Mkutano wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji ilani kwa kipindi cha miaka mitano 2020-2025 kwa wanachama wa CCM na wananchi wa Mitaa ya Mwanalugali A na B Chokala amesema Kata hiyo imepiga hatua kubwa ya kimaendeleo.

Chokala amesema fedha hizo zimetumika vizuri kwenye sekta za elimu, afya, vikundi vya kiuchumi kupitia asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri, barabara, maji, umeme, kilimo na mifugo.

"Tunaishukuru serikali kwa kutupatia fedha hizo ambazo matokeo yake yameonekana kwani huduma zimeboreka licha ya changamoto chache ambazo zimeendelea kutatuliwa kulingana na bajeti inayopatikana,"amesema Chokala.

Amesema mafanikio hayo yametokana ushirikiano mkubwa ulioonyeshwa baina ya Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka, wananchi, viongozi na watendaji wa serikali bila kusahau chama tawala CCM ambao ndiyo wasimamizi wa ilani.

WAKALA WA VIPIMO (WMA) YATAKA VIPIMO VIHAKIKIWE KILA MWAKA






WAKALA wa Vipimo Nchini (WMA) imetaka vipimo vya ujazo urefu na uzito wakati wa kupima bidhaa au kuhudumia wananchi lazima vihakikiwe kila baada ya miezi 12.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Kituo cha (WMA) kilichopo Misugusugu Wilayani Kibaha Mkoani Pwani Charles Mavunde alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Mavunde amesema kuwa uhakiki huo ni takwa la kisheria ya vipimo sura 340 namba 19 ya mwaka 2002 inataka vipimo vinavyotumika kupima katika biashara au huduma nyingine za kijamii lazima vihakikiwe ndani ya muda huo.

Amesema kuwa sheria inatoa adhabu kwa mtu ambaye hata hakiki vifaa vinavyotumika katika kubebea au kupimia ambapo faini ni kati ya shilingi 100,000 hadi milioni 20 au kifungo jela miaka miwili.

"Kipimo chochote  kinachopima kuhudumia wananchi kinatakiwa  kufanyiwa uhakiki kila baada ya miezi 12 pia tunawapongeza wananchi kwa kuwa  na mwamko   kwenye uhakiki wa dira za maji kwani ni mkubwa," amesema Mavunde.

Amesema wanatarajia kuhakiki mita za maji  zaidi ya 87,000 kufikia mwishoni wa mwezi Juni 2025 ili kutambua usahihi wake kabla ya kwenda kufungwa kwa wateja na wamefanya zoezi la  uhakiki wa mita za umeme zaidi ya 5,500 za umeme mkubwa wa viwanda vya Mkoa wa Dar  es Salaam na mikoa mingine ili kuona kama zipo sahihi kulingana na matumizi viwandani. 

"Kwa upande wa dira za maji katika kipindi cha Julai  hadi Mei mwaka huu tayari wamehakiki dira  57,997 huku wakiwa na uwezo wa kuhakiki dira 100,000 kwa mwaka

Naye Ofisa  Vipimo  Mkuu Gaudence Gaspery amesema kuwa hivi sasa wanahakiki dira za  maji kwa kutumia mtambo wa kisasa wenye uwezo wa kuhakiki dira 10 kwa wakati mmoja.

Gaspery amesema kuwa baada ya kuhakikiwa na kuonekana zinafaa kwa matumizi huwekewa rakili yenye rangi ya chungwa  na ambazo zitagundulika zinahitaji kufanyiwa marekebisho hurekebishwa huku zile ambazo zitagundulika kwamba hazifai huteketezwa.

 

Thursday, May 29, 2025

MWANASHERIA MATATANI AKITUHUMIWA KUGHUSHI AKAUNTI YA KIJIJI NA KUJIPATIA FEDHA

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imefanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi zaidi ya milioni 385 fedha za mauzo ya ardhi ambazo ziliwekwa kwenye akaunti ya kughushi ya mtu binafsi badala ya akaunti ya Kijiji cha Msufini Kidete Wilaya ya Mkuranga.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Domina Mukama akitoa taarifa ya Januari hadi Machi alisema kuwa fedha hizo zilikuwa ni asilimia 10 ya malipo baada ya Kijiji kuuza ardhi.

Mukama alisema kuwa mtu anayetuhumiwa kughushi akaunti hiyo ya Kijiji na kuingia kwenye akaunti yake binafsi ni mwanasheria wa kampuni ya Briliant Sanitary Ware Company Limited ambayo ilinunua eneo hilo.

"Fedha hizo ni asilimia 10 ya mapato kwa ajili ya Kijiji baada ya mauzo ambapo zilipoingia mtu huyo alizitumia kwa matumizi binafsi lakini Takukuru walifanikiwa kuzirejesha fedha hizo ambapo kwa sasa kesi yake iko hatua ya uchunguzi,"alisema Mukama.

Aidha alisema kuwa fedha hizo baada ya kuzirejesha fedha hizo kwenye akaunti ya Kijiji hicho zimepangiwa matumizi ya kujenga madarasa mawili ya Shule ya Sekondari Mbezi Gogoni na madarasa mawili Shule ya Msingi Msufini.

"Katika hatua nyingine Takukuru imefuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo 338 yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 18 na utekelezaji wake unaridhisha,"alisema Mukama.

Alibainisha kuwa wamewafikia wananchi wa makundi mbalimbali ili waweze kuiunga Serikali mkono katika kuzuia vitendo ya rushwa kwa kupitia semina 67, mikutano ya hadhara 72, vipindi vya redio 5, uimarishaji klabu za wapinga rushwa 130.

"Tumejipanga Kuzuia na Kupambana na vitendo vya Rushwa katika uchaguzi Mkuu kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya rushwa katika uchaguzi kwa kuwafikia wadau wote,"alisema Mukama.

Aliongeza kuwa wanatoa elimu kwa wadau ambao ni vyama vya siasa, wasimamizi wa uchaguzi, wanahabari, wananchi na jamii nzima kwa ujumla ambapo anawaasa wananchi kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa ili kuwa salama na kuepuka migogoro yenye kuleta viashiria vyenye rushwa.

"Katika kipindi tajwa Ofisi ilifanya chambuzi za mifumo 14 ikiwa ni pamoja na eneo la makadirio ya ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri ya
Mji Kibaha, Mafia, kituo cha Utalii Kazimzumbwi katika chambuzi wa mfumo wa usambazaji maji uliofanyika kuna mapungufu yalibainika na hatua zilichukuliwa.

Saturday, May 24, 2025

DIWANI MTAMBO AWASILISHA TAARIFA UTEKELEZAJI WA ILANI YA MIAKA 5

KATA ya Picha ya Ndege Halmashauri ya Mji Kibaha umeishukuru serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye kata hiyo.

Hayo yamesemwa na Diwani wa Kata hiyo Karim Mtambo alipokuwa akiwasilisha utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kipindi cha miaka mitano 2020-2025.

Mtambo amesema kuwa anaishukuru serikali kwani imegusa sekta zote za kiamendeleo hivyo kufanya kero nyingi kupungua na wananchi kupata huduma kwa urahisi.

"Mfano hospitali ya Wilaya ya Lulanzi kwa sasa haina changamoto ya maji ikilinganishwa na kipindi cha nyuma na wananchi nao wanapata huduma ya maji kwa asilimia 95, ujenzi wa ofisi ya Kata ambapo iko hatua ya ukamilishaji",amesema Mtambo.

Amesema kuwa huduma za afya nazo zimetengewa fedha nyingi, miundombinu ya barabara nayo imeboreshwa, soko bado lina changamoto na kituo cha polisi nacho bado.

"Sekta ya elimu nayo imepatiwa fedha nyingi ambapo kwenye shule zetu za msingi miundombinu imeboreshwa na ufaulu umeongezeka ikilinganishwa na zamani,"amesema Mtambo.

 

GRACE JUNGULU AONGOZA KIKAO UTEKELEZAJI ILANI KATA YA PICHA YA NDEGE

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Grace Jungulu amewataka viongozi wanaotokana na chama kutoa majibu ya changamoto za wananchi baada ya vikao vya chama na siyo kubaki nayo ndani kwani wao ndiyo wanayoisimamia serikali.

Jungulu ameyasema hayo wakati akiongoza kikao cha uwasilishwaji wa utekelezaji wa ilani ya CCM ya miaka mitano iliyowasilishwa na diwani wa kata hiyo Karim Mtambo.

Amesema kuwa viongozi wamekuwa wakitoa majibu juu ya changamoto mbalimbali kwenye vikao vya chama hivyo kajibu hayo wayapatie na wananchi. 

"Twendeni na kwa wananchi kupitia mikutano ya kila baada ya miezi mitatu tuwajibu wananchi maswali yao kwa kupokea kero zao na kuzitafutia ufumbuzi,"amesema Jungulu.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Picha ya Ndege Karim Mtambo amesema kuwa anaishukuru serikali kwa kutoa fedha ambazo zimetekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mtambo amesema sekta zote zimeguswa na miradi hiyo na kufanya changamoto za wananchi kupungua huku serikali ikiendelea kutatua kero zilizopo.
 

Wednesday, May 21, 2025

ATAKA SIMBA IUNGWE MKONO KUCHUKUA KOMBE LA SHIRIKISHO DHIDI YA BERKANE

 

WACHEZAJI viongozi na benchi la ufundi la timu ya Simba wametakiwa kupambana kuhakikisha wanatwaa kombe la Shirikisho.

Aidha washabiki na wapenzi wa soka nchini wametakiwa kuwa na mshikamano na kuacha tofauti zao za ushabiki na kuungana ili kuisadia timu ya Simba kwenye mchezo wao wa fainali dhidi ya Berkane mchezo utakaochezwa uwanja wa Amani Zanzibar.

Akizungumza na Brailo Media aliyewahi kuwa mlezi wa Tawi la Simba Tishio Kibaha Fahim Lardhi amesema kuwa Watanzania wanapaswa kuungana kwenye mchezo huo kwani ni wa heshima kwa nchi.

Lardhi amesema kuwa licha ya Simba kufungwa kwenye hatua ya kwanza kwa magoli 2-0 lakini wanaimani kuwa Simba itapindua matokeo na kuwa mabingwa.

"Tuenzi maneno ya Rais Hayati Dk John Magufuli aliyoitoa kwenye uwanja wa Mkapa wa kutaka Simba au timu nyingine ya Tanzania kuleta kombe la Afrika,"amesema Lardhi.

Amesema kuwa itakuwa ni fedhaha kwa Simba kuchukua kombe hilo ambalo litakuwa kwenye ardhi ya Tanzania ambapo mwaka 1993 walifungwa kwenye fainali na Stella Abidjan ya Ivory Coast.

"Mwaka huu kwa uzalendo wetu tuhakikishe tunalipigania Taifa letu kama kila mtu atatimiza wajibu wake kuanzia wachezaji hadi kwa mashabiki,"amesema Lardhi.

Amewaomba Watanzania kuwa na mshikamano kwa wakati wa maandalizi na wakati wa mchezo kwa kuungana na kuacha tofauti kwani hiyo ni mechi ya heshima kwa nchi.


Monday, May 19, 2025

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA WARIPOTI HABARI ZA UCHAGUZI KWA UMAKINI

 VYOMBO vya Habari nchini vimetakiwa kutoa taarifa za vyama vyote vya siasa kwenye kampeni wakati wa uchaguzi wa mwaka huu ili wananchi waweze kujua sera za vyama na kuchagua viongozi bora.

Hayo yalisemwa Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Asasi ya Maendeleo ya Vijana (YPC) Israel Ilunde alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi.

Ilunde alisema kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kutoa elimu ambayo itasaidia kujua sera za vyama vyote bila ya kupendelea baadhi ya vyama.

"Vyombo vya habari vitoe taarifa za vyama vyote kwa usawa bila ya upendeleo hata kwa vyama vidogo navyo vipate nafasi ili vieleze sera zao na wananchi wachague wagombea ambao wataona wanawafaa,"alisema Ilunde.

Alisema kuwa wananchi wakisikia sera za vyama vyote watakuwa na maamuzi mazuri ya kuchagua viongozi ambao wataona wana sera nzuri na watakuwa wamechagua wakiwa na uhakika wa wanao wachagua wana sera nzuri.

"Pia vyama vya siasa nchini vinatakiwa vitoe kauli za kulinda amani iliyopo na kuachana na kauli za chuki na uchochezi ambazo zinaweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Aidha alisema kuwa amani ni tunu ya Taifa ambayo inabidi ilindwe ambapo kauli zisizo nzuri husababisha amani kutoweka na wananchi kutoelewana.

"Nayo Tume Huru ya Uchaguzi (INEC) ihakikishe inakutana na wadau wa siasa mara kwa mara ili kuweka mazingira mazuri ya uchaguzi ambapo itasaidia kuondoa malalamiko wakati wa uchaguzi,"alisema Ilunde.

Aliongeza kuwa wananchi kwa maeneo zoezi la uhakiki wapiga kura linafanyika wajitokeze kuangalia taarifa zao na ikifika muda wa kupiga kura wajitokeze kwa wingi kwa wale wenye sifa.

"Kwa makundi ya vijana wanawake na watu wenye ulemavu wanaotaka kuwania nafasi za uongozi wajitokeze kuwania nafasi hizo kupitia  vyama vyao na vyama vitoe nafasi,"alisema Ilunde.

SERIKALI IDHIBITI FEDHA HARAMU

SERIKALI imeshauriwa kutumia sheria zilizopo kudhibiti utoroshwaji wa fedha haramu kwenda nje ya nchi ambapo husababisha kushindwa kuanzisha miradi mipya ya maendeleo na inayoendelea kukwama.

Hayo yalisemwa Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Maendeleo ya Vijana (YPC) Israel Ilunde alipokuwa akizungumza na Mwandishi wa habari hizi.

Ilunde ambaye pia ni Mwentekiti wa Policy Forum alisema kuwa mbali ya miradi kushindwa kufanyika hata ajira kwa vijana hukosekana na hali hiyo huathiri bajeti ya nchi ambapo fedha nyingi hupotea.

"Watu wanaotorosha fedha haramu au utakatishaji wa fedha hufanya udanganyifu kwenye baadhi ya maeneo kwa wafanyabiashara hutumia hati za kibiashara kuweka gharama kubwa, kusafirisha bidhaa kutoka au kwenda nje ya nchi na kudanganya gharama za uendeshaji wa kampuni,"alisema Ilunde.

Alisema kuwa endapo sheria zitawabana watu hao itasaidia kulipa kodi halali kwani kupitia udanganyifu huo hawalipi kodi stahiki hivyo kuitia nchi hasara kubwa.

"Tungeomba sheria ziboreshwe ili kudhibiti watu hao kwa kuwa na mifumo ambayo itadhibiti utoroshwaji wa fedha haramu na watachukuliwa hatua kali za kisheria,"alisema Ilunde.

Aidha aliiomba serikali kuongeza bajeti kwa Wizara ya Habari Sanaa Utamaduni na Michezo ili waandishi waweze kupata mafunzo yatakayoweza kuwafichua watu hao wanaotumia fedha haramu na watu kulipa kodi kwa haki na wasifanye udanganyifu.

"Serikali mashirika yasiyokuwa ya kiserikali taasisi za elimu zitenfeneze vijana kuwa wazalendo watakaochukia udanganyifu ili fedha zinazotokana na kodi zilete maendeleo na itasaidia vijana kuwa na ajira,"alisema Ilunde.

Aliongeza kuwa athari zinazotokana na fedha haramu ni kuathiri sekta muhimu za kimaendeleo kama vile elimu, afya, kilimo na miundombinu na sekta nyingine.

"Vyanzo vinavyosababisha hali hiyo ya utoroshwaji wa fedha haramu ni pamoja na rushwa, hati za kibiashara, usafirishaji wa binadamu, usafirishaji wa madini na utakatishaji wa fedha,"alisema Ilunde. 

Friday, May 16, 2025

WATAKIWA KUWATIA MOYO VIONGOZI

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Kibaha Mkoani Pwani wametakiwa wasiwakatishe tamaa viongozi wanaotokana na CCM bali wawatie moyo.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini Mwajuma Nyamka wakati wa Mkutano Maalum wa Kata ya Maili Moja wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya miaka mitano.

Nyamka amesema kuwa kuna baadhi ya wanachana wa CCM wamekuwa wakibeza mambo yaliyofanywa na viongozi hali ambayo inawakatisha tamaa.

"Ilani inayotekelezwa ni ya CCM hivyo kuwabeza viongozi wake ni kuonyesha mnakataa yaliyofanyika kwani maendeleo ni suala la mchakato ambao ni wa muda mrefu,"amesema Nyamka.

Amesema kuwa chama kiliingia mkataba wa maendeleo na wananchi na kama kuna changamoto ni vema zikawasilishwa kwenye vikao maalumu kuliko kuwatolea maneno mabaya viongozi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi amesema kuwa anawashukuru wajumbe kwa kupitisha ilani ya kata hiyo licha ya tawi la Msufini kuwa na changamoto za miundombinu na afya.

Lutambi amesema kuwa changamoto hizo watazifanyia kazi kwa kushirikiana na wananchi na wataalamu mbalimbali wa Halmashauri ili kukabili changamoto za tawi hilo lililopo kwenye Mtaa wa Muheza

Kwa upande wake katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Method Mselewa amesema kuwa Kata hiyo imeandaa taarifa nzuri ambayo imeonyesha jinsi ilani ilivyotekelezwa.

Mselewa amesema kuwa chama kimefanya kazi kubwa na maendeleo hayawezi kupatikana kwa mara moja ni hatua ambapo kwa vile ambavyo havijakamilika vitafanyiwa kazi.

Naye Mke wa Mbunge huyo Selina Koka amesema kuwa wataendelea kushirikiana na wananchi katika suala la maendeleo ili kuhakikisha wananchi wanakuwa na ustawi.

Koka amesema kuwa kwa upande wa wanawake watahakikisha wanazifikia fursa mbalimbali ikiwemo za mikopo ya wanawake ili waweze kufanya shughuli za ujasiriamali ili wajikwamue kiuchumi.

Tuesday, May 13, 2025

WAFANYABIASHARA SOKO LA LOLIONDO WARIDHIA KUJENGWA UPYA

KUFUATIA mpango wa Halmashauri ya Mji Kibaha kulibomoa na kujenga upya soko la Loliondo liwe a kisasa uongozi wa soko hilo umeridhia lakini umetoa maombi kwa Halmashauri hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mwenyekiti wa soko hilo lililopo Kata ya Tangini Mohamed Mnembwe alisema kuwa wamekubali kubomolewa soko hilo ikiwa ni sehemu ya kuleta maendeleo.

Mnembwe alisema kuwa wametoa maombi yao kwa Halmashauri ya kuongezewa muda wa notisi kutoka miezi mitatu hadi sita, bei ya gharama za kodi kwa mita za mraba zibaki zile zile mara soko litakapokamilika.

"Kuwe na mkataba kati ya Halmashauri na soko juu ya wao kupewa kipaumbele cha kurudi kufanya biashara sokoni hapo bila ya masharti, ukubwa wa fremu ubaki uleule na waongezewe muda wa malipo nafuu hadi mwaka 2042 kwani fremu zitazobomolewa walijenga wao wenyewe kwa gharama zao,"alisema Mnembwe.

Alisema kuwa wanaomba makubaliano waliyoingia juu ya uboreshaji wa soko hilo yasibadilike kwani wao wanachotaka ni maendeleo na kuboresha mazingira ya biashara.

"Tunaunga mkono jitihada za serikali hivyo yale tuliyokubaliana na Halmashauri yawe ni yale yale na kutoa kipaumbele kwa wafanyabiashara waliopo na nafasi zikabaki wapewe wafanyabiashara wapya,"alisema Mnembwe.

Aidha alisema kuwa ujenzi huo utakuwa ni wa miezi 15 ambapo kwa kipindi hicho watahamishia biashara zao kwenye eneo jirani panapotumika kuuza mitumba na watajenga mabanda ya muda.

Soko hilo lina fremu 338 kati ya hizo zinazofanya kazi ni 155, mapaa sita na vibanda 155 ambapo kuna wafanyabiashara zaidi 800 wakiwa wanauza bidhaa za aina tofauti tofauti.

Sunday, May 11, 2025

ALIYE OKOLEWA NA MKUNGU WA NDIZI AJALI YA MV BUKOBA MIAKA 29 ILIYOPITA ASIMULIA MKASA MZIMA

ILIKUWA mwaka 1996 majira ya asubuhi nilisikia wimbo wa Taifa kupitia Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) wakati huo kwa sasa ni TBC Taifa jambo ambalo si la kawaida kwani unapopigwa wimbo huo basi kuna tukio kubwa la kitaifa ambapo Rais wa Awamu ya Tatu Benjamini Mkapa alitangaza kutokea tukio la ajali ya Mv Bukoba iliyotokea Mkoani Mwanza.

Wakati taarifa hiyo inatangazwa nilikuwa nikielekea shule ambapo nilikuwa nasoma Sekondari ambapo imepita miaka 29 tangu kutokea ajali hiyo mbaya ambayo iliacha simanzi kwa Watanzania na hata baadhi ya raia wa nchi mbalimbali.

Meli hiyo ya Mv Bukoba wakati ikisafiri ilibeba watu wa aina mbalimbali kuanzia wafanyabiashara, wataalamu, watu wa dini, rangi tofauti tofauti na rika tofauti ambao walikuwa wakitokea Bukoba Mkoani Kagera kwenda Mkoani Mwanza kwa shughuli zao za kawaida.

Ni takribani miaka 10 imepita tangu nimfahamu moja ya watu walionusurika kwenye ajali hiyo nikijaribu kumshawishi ili anisimulie mkasa huo bila ya mafanikio kwani alishindwa kutokana na huzuni kubwa aliyokuwanayo kutokana na tukio hilo ambalo hataweza kulisahau maishani mwake.

Baada ya kumshawishi kwa muda mrefu hatimaye alikubali na kunisimulia juu ya mkasa huo ambapo alifahamika kutokana na ajali hiyo kwa kunusurika kwa kupitia Mkungu wa ndizi ambao ndiyo uliookoa maisha yake kwa kuushikilia kwa zaidi ya masaa mawili.

Huyo si mwingine bali ni Happy Leopard ambaye kwa wakati ule alikuwa ni mtoto mdogo mwenye umri wa miaka (17) wakati ajali hiyo inatokea akiwa na dada yake ambaye kwa bahati mbaya alifariki dunia katika ajali hiyo.

Akielezea juu ya kilichotokea wakati wa ajali hiyo alisema kuwa yeye na dada yake Emiliana walikuwa wakiishi Singida ambapo dada yake alikuwa ni mtumishi wa Shirika la Bima Tanzania (NIC) walikwenda Bukoba ambapo ndiyo nyumbani kwao kwa ajili ya mazishi ya mama yao mzazi.

Leopard alisema kuwa baada ya mazishi ilibidi waondoke kwenda Mwanza kwa ajili ya kupeleka msiba Moshi ambako ni nyumbani kwa mama yao alikozaliwa.

"Nilipanda kwenye meli majira ya saa 1 jioni ambapo saa 3 safari ndipo ilipoanza nilipanda lakini sikuwa na furaha tulikata tiketi ya meli ya Mv Victoria lakini meli hiyo ilikuwa kwenye matengenezo na tukapanda meli ya Mv Bukoba,"alisema Leopard.

Alisema kuwa yeye na dada yake walikata siti za VIP na abiria walikuwa wengi ambapo baadhi ya abiria walikosa nafasi na kupanda magari kwenda kupanda kituo cha mbele cha Kemondo na kupanda na wengine waliachwa ambapo ndi ilikuwa nusura yao.

"Mimi na dada tulikuwa ndani lakini nilishindwa kulala kila wakati alikuwa akija na kuniangalia akashangaa kwanini silali ambapo dada alilala lakini sikulala ikabidi nitoke nje ambapo pembeni kulikuwa na kwaya ilikuwa ikiimba pia alikuja kuniangalia na kunipa khanga ili nijifunike kwani kulikuwa na baridi,"alisema Leopard.

Alisema kuwa ilipofika majira ya saa 10 alfajiri walipokuwa wakikaribia kufika Mwanza walipofika eneo linaloitwa Kisiwa cha Juma yalitokea mawimbi makubwa na sehemu hiyo ni muingiliano wa maji na kuna mawimbi makali ambapo inasemekana huwa ajali za meli hutokea mara kwa mara ambapo manahodha wazoefu huwa hawapiti hapo na kukwepa eneo hilo.

"Baada ya muda meli ilianza kuyumba na vyombo jikoni vilianza kuanguka askari walikuwa wakisafirisha fedha walianza kuwaambia abiria kaeni upande huu mmeelemea sehemu moja nendeni huku wakati huo tulianza kuona taa za Bugando kwa mbali kidogo meli ilianza kuyumba sasa watu wakawa wanakimbia hawajui la kufanya,"alisema Leopard.

"Tulianguka kama vile mtu anamwaga kitu dada alibaki kule kwenye chumba, nikifanikiwa kushika boya lakini kuna mtu alininyanganya nikazama chini nilipoibuka nikakutana na Mkungu wa ndizi ambao niliungangania hivyo nikawa naelea licha ya mawimbi ya maji kutupiga na niliona watu wengine hao wakiwa na maboya huku wakiomba msaada,"alisema Leopard.

Alisema kuwa kwa mbali aliona baadhi ya watu wakiwa kwenye ubavu wa meli wakiwa wamejishikilia huku kwenye maji kukiwa na maiti nyingi zikiwa zinapelekwa na maji na vitu mbalimbali ikiwa ni pamoja na maburungutu ya fedha na vifaa mbalimbali.

"Tukiwa ndani ya maji nilikuwa nauomba Mungu atusaidie ili tuweze kupona na niliamini dada yangu ni moja ya watu waliokuwa kwenye ubavu wa meli naye atapona lakini kumbe haikuwa hivyo kumbe yeye alibaki kule chumbani na hakuweza kutoka na alikuja kupatikana baada ya kuvunjwa vile vyumba tena siku chache kabla zoezi la kutafuta maiti kusitishwa,"alisema Leopard.

"Ilikuja boti ya wavuvi wakauliza mna hela ili tuwaokoe kama hamna hela basi wakaanza kuchukua fedha na vitu mbalimbali vya abiria wakaweka kwenye boti yao wakaondoka lakini jambo la kushukuru wakatokea wavuvi wengine wakiwa na mtumbwi wakatuokoa na kisha kutupeleka kwenye meli nyingine ambayo ilitokea Uganda wakatuchukua baadhi ya watu walikufa baada ya kuchoka kushikilia maboya kwani walikaa majini muda mrefu sana,"alisema Leopard.

Alisema kuwa meli hiyo ilivuja mafuta ambayo yaliingia kwenye maji na kutupiga hivyo yalituumiza machoni, puani na masikioni na tulipokuwa kwenye ile boti tuliookolewa watu watano, maji yalikuwa yanaingia ikabidi awe anayachota na kuyamwaga nje huku wale wenzake wakiwa wamelala hoi yeye akiwa kidogo ana nguvu.

Alisema kuwa anamshukuru Mungu na siku hiyo alivaa rozari ambayo alipewa na babu yake ambaye alikuwa padri na anaamini Mungu ndiye aliyemwokoa katika ajali hiyo mbaya ya majini kutokea nchini.

"Tangu tunatoka Singida kwenda Bukoba moyo wangu haukutaka kabisa kusafiri nilimkatalia dada hiyo safari hadi majirani zetu walinishawishi kusafiri ambapo aliogopa kupanda meli na majirani waliniambia kuwa kwani umeshawahi kusikia ajali ya meli walinibembeleza ikabidi niende,"alisema Leopard.

"Cha ajabu ile sehemu niliyookolewa alitokea nyoka mkubwa mweusi watu wakanionyesha baada ya kuokolewa wakasema huyo ndiye alikuwa mzimu wake ambapo kama angemuona angemuokoa niliwaambia nikiwa majini niliogopa zaidi mtu na siyo kitu kingine kwani yule aliyeninganganya boya alinifanya nione adui ni binadamu na siyo mnyama au kitu kingine,"alisema Leopard.

Alisema kuwa miaka zaidi ya 10 bila ya kupanda meli baada ya tukio hilo licha ya siku alipopatikana dada yake ilibidi apande kwenda kuzika na walimbembeleza sana apande alikubali lakini aliogopa sana meli akikumbuka tukio hilo na fedha zote za pole alizopewa alizipeleka kanisani kama sadaka kwani hakuona thamani ya kitu chochote kwa wakati huo na ndoto zake zote zikitoweka.

"Dada alikuwa na mipango ya kwenda Uingereza ambapo aliniahidi tungeenda naye na aliahidi angenisomesha kwani mimi nilikuwa mtoto wa mwisho na dada yangu alikuwa akinipenda tulipendana sana nilitamani angepona ili tuje tusimulie kuwa sisi ni mashujaa lakini haikuwa hivyo tukio hilo limeniumiza sana sitaweza kulisahau maishani mwangu,"alisema Leopard.




Thursday, May 8, 2025

WANACHAMA WA CCM NYANG'WALE WATAKA KUHARAKISHWA UJENZI WA OFISI.

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita wametaka  ujenzi wa ofisi ya chama ufanyike kwani tayari baadhi ya wadau wamechangia fedha za ujenzi huo.

Wamesema moja ya wadau waliochangia fedha kwa ajili ya ujenzi huo ni Naibu Waziri Mkuu Dotto Biteko ambaye alichangia kiasi cha shilingi milioni 50.

Wamesema kuwa fedha hizo zilikabidhiwa kwa Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Hussein Amar hivyo kutaka fedha hizo zifanye ujenzi huo ili kupata ofisi kwa kazi za chama.

"Tunataka ujenzi ufanyike kwani kama ni fedha zipo hakuna sababu ya kuchelewesha ujenzi huo wa ofisi ya chama ambapo endapo itajengwa itakuwa ya kisasa,"wamesema wanachama hao.

Waliongeza kuwa wanataka fedha hizo zijenge na kukamilisha ofisi ya chama na kwamba wao wanachotaka ni kuona CCM Wilaya ya Nyang'hwale inaendelea kama Wilaya nyingine zilivyoendelea.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Hussein Amar akizungumza kwa njia ya simu ameeleza kusitikishwa na malalamiko ya wananchama hao huku akisema jambo hilo halina usiri wowote.

Amar amesema kuwa yeye ndiye iliyemuomba  awasaidie na sio mara moja amekuwa akisaidia na bahati nzuri alipokuja yeye mwenyewe  alimkumbushia ombi hilo na akakubali kusaidia lakini hakutamka kiwango.

Aidha amesema kuwa fedha hizo zilivyoingia alimpa taarifa Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti wa Chama, Mwenezi, kamati ya Siasa na kamati ya ujenzi na yeye ndiye aliyetafuta fundi na kuwashauri kuwa kuna fundi kwa hiyo ni vyema akatumika kwakuwa yupo vizuri.

Mbunge huyo ameongeza kuwa yeye binafsi amekuwa na mchango mkubwa sana katika ujenzi wa ofisi hiyo ya Chama maana alishawai kutoa mashine zake na magari yake (Tipa) kufanyakazi katika ujenzi huo.

"Fedha zipo mikono salama na Mei 3 niliongea na Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi kumweleza juu ya fedha kwani zinatakiwa kufanyakazi iliyokusudiwa kwa kuwa mimi sitaki kukaa nazo nipeni akaunti niwahamishie lakini alinijibu kuwa watakaa na kamati yake ya ujenzi na akasema wakati huu aendelee kukaa nazo na wakihitaji kununua vifaa watamjulisha ili atoe hizo fedha",amesema Amar.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyang'hwale Adam Mtore amesema kuwa kama kuna malalamiko ndani ya Chama kuuna utaratibu wake na mara nyingi huanzia ngazi ya chini ya tawi lakini kwakuwa suala hilo linagusa ngazi ya Wilaya ilitakiwa wapeleke malalamiko yao kwa Katibu wa Chama Wilaya.



Saturday, May 3, 2025

KECA YAUNGA MKONO SERIKALI UHIFADHI MAZINGIRA NA UFUGAJI NYUKI

SHIRIKA lisilo la kiserikali la Kibaha Environmental Conservation Action (KECA) limedhamiria kuunga mkono jitihada za serikali kwa uhifadhi wa mazingira na kukuza uchumi kupitia ufugaji wa nyuki.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa (KECA) ambalo linajihusisha na utoaji elimu ya ufugaji nyuki na utunzaji wa mazingira Ibrahim Mkwiru wakati wa uzinduzi wa jengo la ofisi yao.

Mkwiru alisema kuwa nia yao ni kuunga mkono juhudi za Serikali katika uhifadhi wa mazingira na kukuza uchumi wa wananchi kupitia ufugaji wa nyuki ili kuongeza kipato kwa wananchi.

"Tunaiomba Serikali kutupa kibali cha kupanda miti ya mianzi katika maeneo ya wazi karibu na chanzo cha Mto Ruvu ili kusaidia kuhifadhi mazingira na kuchochea maendeleo ya kijamii kupitia njia ya uhifadhi wa mazingira,"alisema Mkwiru.

Kwa upande wake Ofisa Tarafa ya Kibaha Catherine Njau alisema kuwa Serikali inaendelea na dhamira yake ya dhati ya kuunga mkono juhudi za wawekezaji katika sekta ya ufugaji nyuki ili kuhakikisha wafugaji wadogo waliopo vijijini wananufaika kiuchumi na kielimu. 

Njau alosema kuwa kwa muda mrefu wafugaji wa nyuki wanaoishi pembezoni mwa miji wamekuwa wakikosa elimu sahihi ya ufugaji wa kisasa na pia kukosa masoko ya uhakika kwa bidhaa zao.

Alilipongeza shirika la KECA kuwa kama daraja muhimu kwa wafugaji wa nyuki kupata elimu ya kitaalamu na fursa za kibiashara kwa wafugaji ili waweze kupata masoko makubwa.

"Nawasisitiza umuhimu wa kufanya tathmini ya kitaalamu kabla ya kupanda mianzi kwenye maeneo ya vyanzo vya maji,huku akisema baadhi ya miti ina uwezo wa kutumia maji mengi na hivyo inaweza kuhatarisha uhai wa vyanzo vya maji kama mito,"alisema Njau.

Naye Mjumbe wa Bodi ya KECA Edwin Shunda aliwahimiza wananchi na wadau wa mazingira kujitokeza kwa wingi kujifunza mbinu za ujasiriamali na ufugaji wa nyuki wa kisasa.

Thursday, May 1, 2025

MKUU WA MKOA WA PWANI ABUBAKARI KUNENGE ATOA WIKI MOJA KWA WAAJIRI WANAOKIUKA HAKI ZA WAFANYAKAZI

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ametaka utatuzi wa changamoto za wafanyakazi kufanyiwa kazi atoa wiki moja kwa taasisi zinazokiuka taratibu kufuata sheria za kazi.

Kunenge ameyasema hayo jana Mjini Kibaha wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani Mkoa wa Pwani yaliyofanyika kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha.

Amesema kuwa waajiri wanapaswa kutekeleza matakwa ya kisheria ya juu ya haki za wafanyakazi ili waweze kufanya kazi vizuri bila ya malalamiko.

"Katika risala yenu kuna baadhi ya waajiri wanakiuka taratibu ikiwa ni pamoja na kutotoa mikataba ya kazi na stahiki nyingine jambo ambalo ni kinyume cha sheria,"amesema Kunenge.

Awali mratibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Mkoa wa Pwani Susan Shesha amesema kuwa wanaishukuru serikali kuvutia wawekezaji ambapo imewezesha vijana wengi kupata ajira.

Shesha amesema kuwa changamoto iliyopo ni baadhi ya waajiri kutotoa mikataba ya ajira, fedha za matibabu, kutothibitishwa kazini, mapunjo ya mishahara, kuzuia uwepo wa vyama vya wafanyakazi sehemu za kazi, likizo na fedha za matibabu, vitisho.

Wednesday, April 30, 2025

MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KIBAHA MJINI YATAKIWA KUSHIRIKIANA

MASHIRIKA yasiyokuwa ya Kiserikali yanayofanya shughuli zao Halmashauri ya Mji Kibaha yamesisitizwa kufanya kazi kwa ushirikiano na kujiunga  na mitandao ya kitaifa na kimataifa.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa Mtandao wa NGOs za Kibaha Mji (Kibaha Town Alliance of NGOs -KiTAN) Israel Ilunde wakati wa kikao cha wakurugenzi wa mashirika hayo na Msajili Msaidizi wa mashirika yasiyo ya kiserikali Halmashauri ya Mji Kibaha Elia Kabora.

Ilunde amesema kuwa kuna umuhimu wa mashirika hayo kufanya kazi kwa mujibu wa Sheria ikiwemo kutoa taatifa za kila robo mwaka na ripoti za mwaka bila kusahau kulipa ada ya kila mwaka.

Idara ya Maendeleo ja jamii waliwaelimisha wana AZAKI juu ya umuhimu wa malezi ya watoto ili kuwaepusha na ukatili ili waweze kutimiza ndoto zao.

Saturday, April 19, 2025

BALOZI MATINYI AAHIDI KUITANGAZA TANZANIA KIMATAIFA

BALOZI wa Tanzania nchini  Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, amesema kuwa atatumia uzoefu alioupata katika kazi yake ya  uandishi wa habari kutafuta taarifa na kung'amua mbinu za kuvutia watalii wengi kama ilivyo katika nchi hiyo ambayo inavutiwa na kutembelewa na watalii wengi.

"Nitakapofika katika nchi hizo tisa katika eneo langu la uwakilishi nitahakikisha ninatafuta na kujua ni mbinu gani wanazotumia kuvutia watalii kwani watalii wengi duniani huenda kwenye nchi hizo", alisema Mhe. Balozi Matinyi.

Alisema pia kuwa kwa kutumia uzoefu wake katika uandishi wa habari - fani ambayo hujenga tabia ya udadisi na mbinu za kutafuta taarifa za uwekezaji na pia tabia kulikamilisha jukumu la kazi baada ya kulichukua.

Balozi Matinyi alisema hayo  hivi karibuni katika mahojinao maalumu na kituo cha televisheni cha ZBC cha Zanzibar.

Alifafanua kwa kueleza kuwa diplomasia ya uchumi nchini ilianzishwa katika utawala wa awamu ya tatu ambapo ili kuujenga uchumi wetu baada ya kumaliza kuzisaidia nchi zingine za Afrika kupata uhuru.

"Hii ndiyo sababu viongozi wetu wakuu wanatusisitizia kwamba tunapokwenda nje ya nchi tukaifanyie kazi diplomasia ya uchumi," alidokeza Mhe. Balozi Matinyi.

"Nitakapofika katika nchi hizo tisa zilizoendelea kiuchumi, katika sekta ya uvuvi, kilimo katika viwanda vya mbolea na matrekta, utalii ambapo wanapokea watalii kati ya milioni 6 hadi 7 kwa mwaka wakitumia visiwa vingi na bahari kuvutia watalii, jukumu langu litakuwa kuhakikisha tunapata mbinu zao na Watanzania tunasonga mbele kiuchumi" alisema Mhe. Balozi Matinyi.

Aidha, akizungumzia namna atakakavyoiwakilisha  Zanzibar, alisema kuwa tayari ameshapata maelezo mbalimbali kutoka taasisi za uwekezaji, kama za uchumi wa buluu na utalii na hivyo kuwa katika nafasi nzuri ya kujua namna ya kuielezea Zanzibar.

"Tuna nchi tisa katika eneo ninalokwenda wenye tabia ya kutaka kufahamu vyakula vya watu wengine; hivyo, nitawaeleza kwamba Zanzibar kuna viungo vya kipekee vyenye ladha nzuri."

Mhe.  Balozi Matinyi amezitaja nchi ambazo  atakuwa mwakilishi mbali ya Sweden kuwa Denmark, Finland, Norway, Iceland, Estonia, Latvia, Lithuania na Ukrane.

Akijibu swali kuhusu mgogoro wa nchi za Ukraine na Russia, Mhe. Balozi Matinyi alisema kuwa Tanzania inasimamia amani na hivyo inataka nchi zinapokwaruzana zitafute suluhu kwa mazungumzo na si kupigana vita.


Thursday, April 17, 2025

UJENZI WA MRADI WA MAJI PANGANI KIBAHA WAANZA

 

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imemkabidhi mkandarasi  eneo la mradi wa maji wa Pangani Wilayani Kibaha Mkoani Pwani utakaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.9.

Akizungumza na baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Pangani Kaimu Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Ramadhani Mtindasi alisema kuwa mradi huo ni wa miezi 12.

Mtindasi alisema kuwa Mkandarasi anayetekeleza mradi huo ni kampuni ya Shanxi Construction Engineering Corporation and Mineral Company ya China ambapo kutakuwa na hatua tatu za ujenzi wa pampu mbili, tenki la maji na usambazaji wa maji.

Alisema kuwa mradi huo utahusisha ujenzi wa matenki mawili ambapo pampu itakuwa na uwezo wa kuzalisha lita 250,000 kwa saa ambapo yatajengwa eneo la Shirika la Elimu Kibaha (KEC).

"Maji hayo yatatoka kwenye bomba kubwa la maji lililopo jirani na barabara ya Morogoro na yatapelekwa hadi Pangani kwenye tenki hilo litakalokuwa na uwezo wa ujazo wa lita milioni sita kwa mara moja,"alisema Mtindasi.

Aidha alisema kuwa ili kufanikisha ujenzi huo aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa mkandarasi anayetekeleza mradi huo ili asipate changamoto.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala alisema kuwa wanamshukuru Rais kwa kutoa fedha hizo kwa ajili ya kukabili changamoto ya maji kwenye Kata ya Pangani.

Twamala alisema kuwa ujenzi wa miundombinu ya maji itakuwa ni mkombozi kwa wananchi na kuwataka wawe walinzi wa mradi huo ambao ulipaswa kuanza tangu mwaka 2023 lakini ulichelewa.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa anaomba mkandarasi atekeleze mradi huo kwa wakati ili wananchi wapate huduma hiyo muhimu.

Koka alisema kuwa changamoto hiyo ilikuwa ni kubwa sana na wabanchi walikuwa wakilalamika sana na ni kilio kikubwa ambacho sasa kinaenda kutatuliwa ambapo wananchi zaidi ya 83,000 watanufaika na mradi huo.

Diwani wa Kata ya Pangani Agustino Mdachi alisema kuwa wananchi walikuwa wanalia sana lakini sasa wanafutwa machozi kwa mradi huo kuanza.

Mdachi alisema kuwa mradi huo utakuwa mkombozi kwani mbali ya kuhudumia Kata ya Pangani pia Kata za Maili Moja na Picha ya Ndege zitanufaika na mradi huo

Thursday, April 3, 2025

UJENZI KIWANGO CHA LAMI BARABARA YA PICHA YA NDEGE-BOKOMNEMELA UNARIDHISHA-MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ISMAIL USSI

MWENGE wa Uhuru umeridhishwa na mradi wa ujenzi wa barabara ya Picha ya Ndege-Bomotimiza yenye urefu wa mita 550 kiwango cha lami wenye thamani ya shilingi milioni 760.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi akikagua barabara hiyo ambapo fedha hizo nikutoka serikali kuu kutokana na tozo ya mafuta amesema serikali inapenda wananchi wapate miundombinu mizuri.

Ussi amesema kuwa kutokana na mradi huo kuwa na ubora wananchi wanapaswa kuulinda na kuutunza ili ulete manufaa ya muda mrefu na kuufanyia usafi.

Amesema kuwa serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa kutengeneza miundombinu ambapo mradi huo umejengwa kwa viwango vinavyotakiwa kutokana na usimamizi mzuri.

"Rais Dk Samia Suluhu Hassan anapenda kuona miradi kama hii inakuwa na matokeo mazuri kwani ndiyo malengo ya serikali hivyo ulindeni mradi huu ambao una gharama kubwa,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mhandisi Samwel Ndoveni amesema kuwa mradi huo ulianza Oktoba mwaka 2023 na ulitegemewa kukamilika Aprili 2024 lakini muda uliongezwa na kukamilika Julai 2024 kutokana na mvua za elnino.

Ndoveni amesema kuwa mradi huo kwa sasa uko katika kipindi cha matazamio hadi Julai 2025 na kukabidhiwa rasmi na kuwa kiasi kilicholipwa hadi sasa ni shilingi milioni 696.9 sawa na asilimia 91.7.

Naye Mwentekiti wa Halmashauri ambaye ni Diwani wa Kata ya Sofu Mussa Ndomba amesema kuwa baravara hiyo ambayo inaanzia barabara ya Morogoro ina urefu wa kilometa saba ni muhimu sana.

Ndomba amesema kuwa barabara hiyo inapita kwenye maeneo ya Shule, Magereza na Hospitali na inaunganisha Kata tatu za Sofu, Picha ya Ndege na Bokomnemela ambapo zamani ilikuwa ni changamoto kubwa sana kwa wananchi wa maeneo hayo.


MWENGE WAZINDUA MRADI WA KISIMA CHA MAJI HOSPITALI YA TUMBI KUTOA LITA 10,000 KWA SAA

HOSPITALI ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani ya Tumbi imepata mradi wa kisima kirefu kinachohudumia watu 920 kwa siku ambapo kwa siku kina uwezo wa kuzalisha lita 10,000 kwa saa.

Hayo yamesemwa na ofisa uendeshaji na matengenezo Mhandisi Charles Stephen wa Dawasa Kibaha akitoa taarifa ya mradi wa kisima kirefu cha maji kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ismail Ussi amesema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 45.9.

Stephen amesema kuwa mradi huo umefadhiliwa na taasisi ya Direct Aid Society  na lengo la mradi huo ni kupata chanzo mbadala cha maji ili kusaidia kupata huduma ya maji ya uhakika inapotokea changamoto.

"Hospitali inatumia lita 110,000 kwa siku ambapo awali ilikuwa inategemea chanzo kimoja tu cha Dawasa hivyo kwa sasa maji yatakuwa ya uhakika mara inapotokea changamoto Dawasa,"amesema Stephen.

Amesema mradi huo ulianza Julai mwaka 2024 na kukamilika Agosti 2024.

USSI ATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA MIKOPO ASILIMIA 10 YA HALMASHAURI WAJIKWAMUE KIUCHUMI

VIJANA kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha Mkoani Pwani wametakiwa kujiunga kwenye vikundi ili waweze kupata fedha za mikopo asilimia 10 za mapato ya ndani ya Halmashauri ili wajikwamue kiuchumi.

Hayo yamesemwa na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi alipotembelea kikundi cha The Dream kilichopo Mtaa wa Kilimahewa Kata ya Tangini.

Ussi amesema kuwa ili vijana waweze kujitegemea wanapaswa kuwa na shughuli za kufanya za kujiongezea kipato kwa kufanya shughuli za kiuchumi.

"Tuwapongeze vijana hawa kwa kuonyesha mfano mzuri kwa kukopa fedha ambazo matunda yake yanaonekana kwani fedha hizo za Halmashauri zimewanufaisha hivyo vibana wengine waige kikundi hichi,"amesema Ussi.

Akisoma risala mweka hazina wa kikundi hicho kinajishughulisha na utengenezaji wa Clips na Tambi  Neema Shao amesema kuwa walikopa kiasi cha shilingi milioni 15 kutoka Halmashauri Januari mwaka huu.

Shao amesema kuwa kikundi kinauwezo wa kuzalisha pakiti 600 na kwa mwezi pakiti 12,000 zenye thamani ya shilingi milioni 9.6 ambapo uzalishaji hufanyika kwa siku 20 kwa mwezi.

Amesema kuwa wanauwezo wa kupata faida ya shilingi milioni mbili ambapo hadi sasa wamesharejesha kiasi cha shilingi 625,000 na wameweza kununua Toyo ya kusambazia bidhaa zao ambapo zamani walikuwa wakikodisha pikipiki.


KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ISMAIL USSI APONGEZA UJENZI ZAHANATI KILIMAHEWA

MKIMBIZA mbio za Mwenge Kitaifa Ismail Ussi ameweka jiwe la msingi kwenye Zahanati ya Kilimahewa ambayo mara itakapokamilika itahudumia wananchi 68,371 wa Kata tatu.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa ujenzi huo ni azma ya Rais anayoitaka ya kuwaondolea adha wananchi ya kupata huduma za afya mbali.

Ussi amesema kuwa anaipongeza Halmashauri na wananchi kwa kufanikisha ujenzi huo ambapo hadi kukamilika kwake unatarajia kutumia kiasi cha shilingi milioni 234.3.

"Tumeambiwa mara itakapokamilika wananchi hawatapata usumbufu kwenda mbali kupata huduma za afya watapata karibu hivyo kupata muda kufanya shughuli za maendeleo,"amesema Ussi

Akisoma taarifa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Catherine Saguti amesema kuwa ujenzi wa Zahanati hiyo kwa sasa umefikia asilimia 61 ya ujenzi na mradi huo unatarajiwa kukamilika mwaka wa fedha wa 2025/2026.

Saguti amesema kuwa manufaa ni kwa Kata tatu za Tangini, Maili Moja na Pangani zenye jumla ya mitaa 16 ambapo wananchi wataondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Aidha amesema kuwa hadi sasa mradi huo umetumia kiasi cha shilingi milioni 108.3 huku wananchi wakichangia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni moja kwa kujaza kifusi.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka amesema anaishukuru serikali kuwapatia eneo hilo ambalo lilikuwa mali ya Wizara ya Mifugo na kupangiwa matumizi ya jamii.

Koka amesema kuwa afya ni kipaumbele kikubwa kwa wananchi kwani wakiwa na afya njema wataweza kujiletea maendeleo.


MWENGE WAWEKA JIWE LA MSINGI MRADI SHULE YA AWALI MSINGI YA MCHEPUO WA KIINGEREZA KATA YA SOFU

HALMASHAURI ya Mji Kibaha imetoa kiasi cha shilingi milioni 458.4 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya awali na msingi ya Nyerere ya muundo wa Kiingereza iliyopo Mtaa wa Sofu na Kata ya Sofu.

Aidha hadi mradi huo utakapokamilika utatumia kiasi cha shilingi milioni 704.6 ikiwa ni mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akisoma taarifa mbele ya kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ussi, ofisa elimu awali na msingi Theresia Kyara amesema kuwa ujenzi huo uko hatua ta umaliziaji.

Kyara amesema kuwa ujenzi huo umehusisha vyumba tisa vya madarasa, matundu 17 ta vyoo, kichomea taka, jengo la utawala, ununuzi wa samani na madawati.

Amesema kuwa hadi sasa zimetumika kiasi cha shilingi milioni 297.7 kwa awamu ya kwanza huku awamu ya pili ikitumia milioni 157.1 na awamu ya tatu zitatumika kiasi cha shilingi milioni 89 na ujenzi umefikia asilimia 64.5

Kwa upande wake kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa shule za msingi za mchepuo wa Kiingereza za serikali ni nzuri katika kuendeleza elimu kwa watoto.

Ussi amesema kuwa shule hizo ni nzuri kwani gharama zake ni nafuu hivyo mradi huo ni mkombozi kwa wanafnzi walioko kwenye maeneo jirani na shule hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye pia Diwani wa kata ya Sofu Mussa Ndomba amesema kuwa wananchi waliomba mradi huo ambapo na kupelekwa kwenye baraza la madiwani na kupitishwa.

Ndomba amesema hilo lilikuwa hitaji kubwa la wananchi wa Mtaa na Kata hiyo hivyo utakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi kwa watoto wao.

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE ASIFU MRADI WA MAEGESHO YA MALORI YA MIZIGO

MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.

Akikagua na kupata taarifa kwenye mradi huo uliopo Kata ya Misugusugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa hicho ni chanzo kizuri cha mapato kwa Halmashauri hiyo.

Ussi amesema kuwa mradi huo wa maegesho hayo ambayo yatakuwa ya kisasa yataifanya Halmashauri kuongeza mapato yake hivyo kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

"Jambo ambalo ni zuri ni kulipa fidia na maendelezo kiasi kikichotengwa ni bilioni 1.8 kwa watu 23 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kimelipwa kwa watu 21 hii inaonyesha kuwa wananchi wanalipwa haki zao na hakuna mtu atakaye kosa haki yake,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mthamini wa Halmashsuri ya Mji Kibaha Patrick Kibwana amesema kuwa mradi huo utakuwa wa shilingi bilioni 23 ikiwa ni mapato ya ndani.

Amesema kuwa hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 317.8 bado hakijalipwa huku watu wawili wakiendelea na taratibu za kibenki.

Kibwana kuwa mradi utakuwa na nyumba za kulala wageni sehemu ya kuoshea magari kituo cha zimamoto mama lishe hoteli sehemu ya kutengeneza magari mifumo ya miundombinu ya gesi vyoo na mabafu kituo cha mafuta kituo cha polisi fremu za biashara huduma za afya ghala za kuhifadhia mizigo na mizani ya kupimia uzito.

Amesema kuwa mradi amesema kuwa mradi huo utatoa ajira kwa vijana 1,000 ambapo eneo hilo lina ukubwa wa hekari 18 na utaondoa msongamano wa malori kutoka Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema kuwa maegesho hayo yamejengwa jirani na eneo la viwanda la Zegereni hivyo huduma hiyo inahitajika sana.

John amesema kuwa mradi huo utakuwa ni sehemu ya kuzalisha ajira kwa wananchi hususani vijana kwenye Wilaya hiyo na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano.

 



Wednesday, April 2, 2025

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA AFURAHISHWA MRADI MAEGESHO YA HALMASHAURI YA MJI KIBAHA


MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.

Akikagua na kupata taarifa kwenye mradi huo uliopo Kata ya Misugusugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa hicho ni chanzo kizuri cha mapato kwa Halmashauri hiyo.

Ussi amesema kuwa mradi huo wa maegesho hayo ambayo yatakuwa ya kisasa yataifanya Halmashauri kuongeza mapato yake hivyo kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

"Jambo ambalo ni zuri ni kulipa fidia na maendelezo kiasi kikichotengwa ni bilioni 1.8 kwa watu 23 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kimelipwa kwa watu 21 hii inaonyesha kuwa wananchi wanalipwa haki zao na hakuna mtu atakaye kosa haki yake,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mthamini wa Halmashsuri ya Mji Kibaha Patrick Kibwana amesema kuwa mradi huo utakuwa wa shilingi bilioni 23 ikiwa ni mapato ya ndani.

Amesema kuwa hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 317.8 bado hakijalipwa huku watu wawili wakiendelea na taratibu za kibenki.

Kibwana kuwa mradi utakuwa na nyumba za kulala wageni sehemu ya kuoshea magari kituo cha zimamoto mama lishe hoteli sehemu ya kutengeneza magari mifumo ya miundombinu ya gesi vyoo na mabafu kituo cha mafuta kituo cha polisi fremu za biashara huduma za afya ghala za kuhifadhia mizigo na mizani ya kupimia uzito.

Amesema kuwa mradi amesema kuwa mradi huo utatoa ajira kwa vijana 1,000 ambapo eneo hilo lina ukubwa wa hekari 18 na utaondoa msongamano wa malori kutoka Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema kuwa maegesho hayo yamejengwa jirani na eneo la viwanda la Zegereni hivyo huduma hiyo inahitajika sana.

John amesema kuwa mradi huo utakuwa ni sehemu ya kuzalisha ajira kwa wananchi hususani vijana kwenye Wilaya hiyo na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano.