Saturday, April 19, 2025

BALOZI MATINYI AAHIDI KUITANGAZA TANZANIA KIMATAIFA

BALOZI wa Tanzania nchini  Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, amesema kuwa atatumia uzoefu alioupata katika kazi yake ya  uandishi wa habari kutafuta taarifa na kung'amua mbinu za kuvutia watalii wengi kama ilivyo katika nchi hiyo ambayo inavutiwa na kutembelewa na watalii wengi.

"Nitakapofika katika nchi hizo tisa katika eneo langu la uwakilishi nitahakikisha ninatafuta na kujua ni mbinu gani wanazotumia kuvutia watalii kwani watalii wengi duniani huenda kwenye nchi hizo", alisema Mhe. Balozi Matinyi.

Alisema pia kuwa kwa kutumia uzoefu wake katika uandishi wa habari - fani ambayo hujenga tabia ya udadisi na mbinu za kutafuta taarifa za uwekezaji na pia tabia kulikamilisha jukumu la kazi baada ya kulichukua.

Balozi Matinyi alisema hayo  hivi karibuni katika mahojinao maalumu na kituo cha televisheni cha ZBC cha Zanzibar.

Alifafanua kwa kueleza kuwa diplomasia ya uchumi nchini ilianzishwa katika utawala wa awamu ya tatu ambapo ili kuujenga uchumi wetu baada ya kumaliza kuzisaidia nchi zingine za Afrika kupata uhuru.

"Hii ndiyo sababu viongozi wetu wakuu wanatusisitizia kwamba tunapokwenda nje ya nchi tukaifanyie kazi diplomasia ya uchumi," alidokeza Mhe. Balozi Matinyi.

"Nitakapofika katika nchi hizo tisa zilizoendelea kiuchumi, katika sekta ya uvuvi, kilimo katika viwanda vya mbolea na matrekta, utalii ambapo wanapokea watalii kati ya milioni 6 hadi 7 kwa mwaka wakitumia visiwa vingi na bahari kuvutia watalii, jukumu langu litakuwa kuhakikisha tunapata mbinu zao na Watanzania tunasonga mbele kiuchumi" alisema Mhe. Balozi Matinyi.

Aidha, akizungumzia namna atakakavyoiwakilisha  Zanzibar, alisema kuwa tayari ameshapata maelezo mbalimbali kutoka taasisi za uwekezaji, kama za uchumi wa buluu na utalii na hivyo kuwa katika nafasi nzuri ya kujua namna ya kuielezea Zanzibar.

"Tuna nchi tisa katika eneo ninalokwenda wenye tabia ya kutaka kufahamu vyakula vya watu wengine; hivyo, nitawaeleza kwamba Zanzibar kuna viungo vya kipekee vyenye ladha nzuri."

Mhe.  Balozi Matinyi amezitaja nchi ambazo  atakuwa mwakilishi mbali ya Sweden kuwa Denmark, Finland, Norway, Iceland, Estonia, Latvia, Lithuania na Ukrane.

Akijibu swali kuhusu mgogoro wa nchi za Ukraine na Russia, Mhe. Balozi Matinyi alisema kuwa Tanzania inasimamia amani na hivyo inataka nchi zinapokwaruzana zitafute suluhu kwa mazungumzo na si kupigana vita.


Thursday, April 17, 2025

UJENZI WA MRADI WA MAJI PANGANI KIBAHA WAANZA

 

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imemkabidhi mkandarasi  eneo la mradi wa maji wa Pangani Wilayani Kibaha Mkoani Pwani utakaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.9.

Akizungumza na baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Pangani Kaimu Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Ramadhani Mtindasi alisema kuwa mradi huo ni wa miezi 12.

Mtindasi alisema kuwa Mkandarasi anayetekeleza mradi huo ni kampuni ya Shanxi Construction Engineering Corporation and Mineral Company ya China ambapo kutakuwa na hatua tatu za ujenzi wa pampu mbili, tenki la maji na usambazaji wa maji.

Alisema kuwa mradi huo utahusisha ujenzi wa matenki mawili ambapo pampu itakuwa na uwezo wa kuzalisha lita 250,000 kwa saa ambapo yatajengwa eneo la Shirika la Elimu Kibaha (KEC).

"Maji hayo yatatoka kwenye bomba kubwa la maji lililopo jirani na barabara ya Morogoro na yatapelekwa hadi Pangani kwenye tenki hilo litakalokuwa na uwezo wa ujazo wa lita milioni sita kwa mara moja,"alisema Mtindasi.

Aidha alisema kuwa ili kufanikisha ujenzi huo aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa mkandarasi anayetekeleza mradi huo ili asipate changamoto.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala alisema kuwa wanamshukuru Rais kwa kutoa fedha hizo kwa ajili ya kukabili changamoto ya maji kwenye Kata ya Pangani.

Twamala alisema kuwa ujenzi wa miundombinu ya maji itakuwa ni mkombozi kwa wananchi na kuwataka wawe walinzi wa mradi huo ambao ulipaswa kuanza tangu mwaka 2023 lakini ulichelewa.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa anaomba mkandarasi atekeleze mradi huo kwa wakati ili wananchi wapate huduma hiyo muhimu.

Koka alisema kuwa changamoto hiyo ilikuwa ni kubwa sana na wabanchi walikuwa wakilalamika sana na ni kilio kikubwa ambacho sasa kinaenda kutatuliwa ambapo wananchi zaidi ya 83,000 watanufaika na mradi huo.

Diwani wa Kata ya Pangani Agustino Mdachi alisema kuwa wananchi walikuwa wanalia sana lakini sasa wanafutwa machozi kwa mradi huo kuanza.

Mdachi alisema kuwa mradi huo utakuwa mkombozi kwani mbali ya kuhudumia Kata ya Pangani pia Kata za Maili Moja na Picha ya Ndege zitanufaika na mradi huo

Thursday, April 3, 2025

UJENZI KIWANGO CHA LAMI BARABARA YA PICHA YA NDEGE-BOKOMNEMELA UNARIDHISHA-MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ISMAIL USSI

MWENGE wa Uhuru umeridhishwa na mradi wa ujenzi wa barabara ya Picha ya Ndege-Bomotimiza yenye urefu wa mita 550 kiwango cha lami wenye thamani ya shilingi milioni 760.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi akikagua barabara hiyo ambapo fedha hizo nikutoka serikali kuu kutokana na tozo ya mafuta amesema serikali inapenda wananchi wapate miundombinu mizuri.

Ussi amesema kuwa kutokana na mradi huo kuwa na ubora wananchi wanapaswa kuulinda na kuutunza ili ulete manufaa ya muda mrefu na kuufanyia usafi.

Amesema kuwa serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa kutengeneza miundombinu ambapo mradi huo umejengwa kwa viwango vinavyotakiwa kutokana na usimamizi mzuri.

"Rais Dk Samia Suluhu Hassan anapenda kuona miradi kama hii inakuwa na matokeo mazuri kwani ndiyo malengo ya serikali hivyo ulindeni mradi huu ambao una gharama kubwa,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mhandisi Samwel Ndoveni amesema kuwa mradi huo ulianza Oktoba mwaka 2023 na ulitegemewa kukamilika Aprili 2024 lakini muda uliongezwa na kukamilika Julai 2024 kutokana na mvua za elnino.

Ndoveni amesema kuwa mradi huo kwa sasa uko katika kipindi cha matazamio hadi Julai 2025 na kukabidhiwa rasmi na kuwa kiasi kilicholipwa hadi sasa ni shilingi milioni 696.9 sawa na asilimia 91.7.

Naye Mwentekiti wa Halmashauri ambaye ni Diwani wa Kata ya Sofu Mussa Ndomba amesema kuwa baravara hiyo ambayo inaanzia barabara ya Morogoro ina urefu wa kilometa saba ni muhimu sana.

Ndomba amesema kuwa barabara hiyo inapita kwenye maeneo ya Shule, Magereza na Hospitali na inaunganisha Kata tatu za Sofu, Picha ya Ndege na Bokomnemela ambapo zamani ilikuwa ni changamoto kubwa sana kwa wananchi wa maeneo hayo.


MWENGE WAZINDUA MRADI WA KISIMA CHA MAJI HOSPITALI YA TUMBI KUTOA LITA 10,000 KWA SAA

HOSPITALI ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani ya Tumbi imepata mradi wa kisima kirefu kinachohudumia watu 920 kwa siku ambapo kwa siku kina uwezo wa kuzalisha lita 10,000 kwa saa.

Hayo yamesemwa na ofisa uendeshaji na matengenezo Mhandisi Charles Stephen wa Dawasa Kibaha akitoa taarifa ya mradi wa kisima kirefu cha maji kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ismail Ussi amesema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 45.9.

Stephen amesema kuwa mradi huo umefadhiliwa na taasisi ya Direct Aid Society  na lengo la mradi huo ni kupata chanzo mbadala cha maji ili kusaidia kupata huduma ya maji ya uhakika inapotokea changamoto.

"Hospitali inatumia lita 110,000 kwa siku ambapo awali ilikuwa inategemea chanzo kimoja tu cha Dawasa hivyo kwa sasa maji yatakuwa ya uhakika mara inapotokea changamoto Dawasa,"amesema Stephen.

Amesema mradi huo ulianza Julai mwaka 2024 na kukamilika Agosti 2024.

USSI ATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA MIKOPO ASILIMIA 10 YA HALMASHAURI WAJIKWAMUE KIUCHUMI

VIJANA kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha Mkoani Pwani wametakiwa kujiunga kwenye vikundi ili waweze kupata fedha za mikopo asilimia 10 za mapato ya ndani ya Halmashauri ili wajikwamue kiuchumi.

Hayo yamesemwa na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi alipotembelea kikundi cha The Dream kilichopo Mtaa wa Kilimahewa Kata ya Tangini.

Ussi amesema kuwa ili vijana waweze kujitegemea wanapaswa kuwa na shughuli za kufanya za kujiongezea kipato kwa kufanya shughuli za kiuchumi.

"Tuwapongeze vijana hawa kwa kuonyesha mfano mzuri kwa kukopa fedha ambazo matunda yake yanaonekana kwani fedha hizo za Halmashauri zimewanufaisha hivyo vibana wengine waige kikundi hichi,"amesema Ussi.

Akisoma risala mweka hazina wa kikundi hicho kinajishughulisha na utengenezaji wa Clips na Tambi  Neema Shao amesema kuwa walikopa kiasi cha shilingi milioni 15 kutoka Halmashauri Januari mwaka huu.

Shao amesema kuwa kikundi kinauwezo wa kuzalisha pakiti 600 na kwa mwezi pakiti 12,000 zenye thamani ya shilingi milioni 9.6 ambapo uzalishaji hufanyika kwa siku 20 kwa mwezi.

Amesema kuwa wanauwezo wa kupata faida ya shilingi milioni mbili ambapo hadi sasa wamesharejesha kiasi cha shilingi 625,000 na wameweza kununua Toyo ya kusambazia bidhaa zao ambapo zamani walikuwa wakikodisha pikipiki.


KIONGOZI MBIO ZA MWENGE KITAIFA ISMAIL USSI APONGEZA UJENZI ZAHANATI KILIMAHEWA

MKIMBIZA mbio za Mwenge Kitaifa Ismail Ussi ameweka jiwe la msingi kwenye Zahanati ya Kilimahewa ambayo mara itakapokamilika itahudumia wananchi 68,371 wa Kata tatu.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa ujenzi huo ni azma ya Rais anayoitaka ya kuwaondolea adha wananchi ya kupata huduma za afya mbali.

Ussi amesema kuwa anaipongeza Halmashauri na wananchi kwa kufanikisha ujenzi huo ambapo hadi kukamilika kwake unatarajia kutumia kiasi cha shilingi milioni 234.3.

"Tumeambiwa mara itakapokamilika wananchi hawatapata usumbufu kwenda mbali kupata huduma za afya watapata karibu hivyo kupata muda kufanya shughuli za maendeleo,"amesema Ussi

Akisoma taarifa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Catherine Saguti amesema kuwa ujenzi wa Zahanati hiyo kwa sasa umefikia asilimia 61 ya ujenzi na mradi huo unatarajiwa kukamilika mwaka wa fedha wa 2025/2026.

Saguti amesema kuwa manufaa ni kwa Kata tatu za Tangini, Maili Moja na Pangani zenye jumla ya mitaa 16 ambapo wananchi wataondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Aidha amesema kuwa hadi sasa mradi huo umetumia kiasi cha shilingi milioni 108.3 huku wananchi wakichangia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni moja kwa kujaza kifusi.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka amesema anaishukuru serikali kuwapatia eneo hilo ambalo lilikuwa mali ya Wizara ya Mifugo na kupangiwa matumizi ya jamii.

Koka amesema kuwa afya ni kipaumbele kikubwa kwa wananchi kwani wakiwa na afya njema wataweza kujiletea maendeleo.


MWENGE WAWEKA JIWE LA MSINGI MRADI SHULE YA AWALI MSINGI YA MCHEPUO WA KIINGEREZA KATA YA SOFU

HALMASHAURI ya Mji Kibaha imetoa kiasi cha shilingi milioni 458.4 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya awali na msingi ya Nyerere ya muundo wa Kiingereza iliyopo Mtaa wa Sofu na Kata ya Sofu.

Aidha hadi mradi huo utakapokamilika utatumia kiasi cha shilingi milioni 704.6 ikiwa ni mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akisoma taarifa mbele ya kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ismail Ussi, ofisa elimu awali na msingi Theresia Kyara amesema kuwa ujenzi huo uko hatua ta umaliziaji.

Kyara amesema kuwa ujenzi huo umehusisha vyumba tisa vya madarasa, matundu 17 ta vyoo, kichomea taka, jengo la utawala, ununuzi wa samani na madawati.

Amesema kuwa hadi sasa zimetumika kiasi cha shilingi milioni 297.7 kwa awamu ya kwanza huku awamu ya pili ikitumia milioni 157.1 na awamu ya tatu zitatumika kiasi cha shilingi milioni 89 na ujenzi umefikia asilimia 64.5

Kwa upande wake kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa shule za msingi za mchepuo wa Kiingereza za serikali ni nzuri katika kuendeleza elimu kwa watoto.

Ussi amesema kuwa shule hizo ni nzuri kwani gharama zake ni nafuu hivyo mradi huo ni mkombozi kwa wanafnzi walioko kwenye maeneo jirani na shule hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye pia Diwani wa kata ya Sofu Mussa Ndomba amesema kuwa wananchi waliomba mradi huo ambapo na kupelekwa kwenye baraza la madiwani na kupitishwa.

Ndomba amesema hilo lilikuwa hitaji kubwa la wananchi wa Mtaa na Kata hiyo hivyo utakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi kwa watoto wao.

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE ASIFU MRADI WA MAEGESHO YA MALORI YA MIZIGO

MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.

Akikagua na kupata taarifa kwenye mradi huo uliopo Kata ya Misugusugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa hicho ni chanzo kizuri cha mapato kwa Halmashauri hiyo.

Ussi amesema kuwa mradi huo wa maegesho hayo ambayo yatakuwa ya kisasa yataifanya Halmashauri kuongeza mapato yake hivyo kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

"Jambo ambalo ni zuri ni kulipa fidia na maendelezo kiasi kikichotengwa ni bilioni 1.8 kwa watu 23 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kimelipwa kwa watu 21 hii inaonyesha kuwa wananchi wanalipwa haki zao na hakuna mtu atakaye kosa haki yake,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mthamini wa Halmashsuri ya Mji Kibaha Patrick Kibwana amesema kuwa mradi huo utakuwa wa shilingi bilioni 23 ikiwa ni mapato ya ndani.

Amesema kuwa hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 317.8 bado hakijalipwa huku watu wawili wakiendelea na taratibu za kibenki.

Kibwana kuwa mradi utakuwa na nyumba za kulala wageni sehemu ya kuoshea magari kituo cha zimamoto mama lishe hoteli sehemu ya kutengeneza magari mifumo ya miundombinu ya gesi vyoo na mabafu kituo cha mafuta kituo cha polisi fremu za biashara huduma za afya ghala za kuhifadhia mizigo na mizani ya kupimia uzito.

Amesema kuwa mradi amesema kuwa mradi huo utatoa ajira kwa vijana 1,000 ambapo eneo hilo lina ukubwa wa hekari 18 na utaondoa msongamano wa malori kutoka Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema kuwa maegesho hayo yamejengwa jirani na eneo la viwanda la Zegereni hivyo huduma hiyo inahitajika sana.

John amesema kuwa mradi huo utakuwa ni sehemu ya kuzalisha ajira kwa wananchi hususani vijana kwenye Wilaya hiyo na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano.

 



Wednesday, April 2, 2025

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA AFURAHISHWA MRADI MAEGESHO YA HALMASHAURI YA MJI KIBAHA


MBIO za Mwenge zimekagua eneo la mradi wa maegesho ya magari makubwa ambao utakapokamilika utaiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi bilioni 3.3 kwa mwaka.

Akikagua na kupata taarifa kwenye mradi huo uliopo Kata ya Misugusugu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ussi amesema kuwa hicho ni chanzo kizuri cha mapato kwa Halmashauri hiyo.

Ussi amesema kuwa mradi huo wa maegesho hayo ambayo yatakuwa ya kisasa yataifanya Halmashauri kuongeza mapato yake hivyo kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

"Jambo ambalo ni zuri ni kulipa fidia na maendelezo kiasi kikichotengwa ni bilioni 1.8 kwa watu 23 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kimelipwa kwa watu 21 hii inaonyesha kuwa wananchi wanalipwa haki zao na hakuna mtu atakaye kosa haki yake,"amesema Ussi.

Kwa upande wake Mthamini wa Halmashsuri ya Mji Kibaha Patrick Kibwana amesema kuwa mradi huo utakuwa wa shilingi bilioni 23 ikiwa ni mapato ya ndani.

Amesema kuwa hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 317.8 bado hakijalipwa huku watu wawili wakiendelea na taratibu za kibenki.

Kibwana kuwa mradi utakuwa na nyumba za kulala wageni sehemu ya kuoshea magari kituo cha zimamoto mama lishe hoteli sehemu ya kutengeneza magari mifumo ya miundombinu ya gesi vyoo na mabafu kituo cha mafuta kituo cha polisi fremu za biashara huduma za afya ghala za kuhifadhia mizigo na mizani ya kupimia uzito.

Amesema kuwa mradi amesema kuwa mradi huo utatoa ajira kwa vijana 1,000 ambapo eneo hilo lina ukubwa wa hekari 18 na utaondoa msongamano wa malori kutoka Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amesema kuwa maegesho hayo yamejengwa jirani na eneo la viwanda la Zegereni hivyo huduma hiyo inahitajika sana.

John amesema kuwa mradi huo utakuwa ni sehemu ya kuzalisha ajira kwa wananchi hususani vijana kwenye Wilaya hiyo na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano.

 

Tuesday, April 1, 2025

TAASISI YA BEGA KWA BEGA NA TANZANIA PWANI YACHANGIA DAMU CHUPA 19

TAASISI ya Bega kwa Bega na Tanzania Mkoani Pwani imechangia damu chupa 19 kwenye benki ya damu ajili ya wagonjwa wanaohudumiwa kwenye hospitali Wilayani Kibaha. 

Kiasi hicho cha damu kilipatikana wakati wa bonanza la kuhamasisha wananchi kujitokeza kushiriki kwenye uzinduzi wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Mkoani Pwani 2025 lililofanyika kwenye uwanja wa Bwawani Kibaha.

Mratibu wa taasisi hiyo kitaifa Ruth Mateleka bonanza hilo limefanywa ili kuhamasisha wananchi kushiriki uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru zitakazofanyika leo kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha.

"Kazi yetu kubwa ni kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli za kimaendeleo na kutaja kazi zilizofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan na tunashukuru watu kujitolea damu ili kusaidia wagonjwa,"amesema Mateleka.

Kwa upande wake Zuhura Sekelela ambaye ni mratibu wa taasisi hiyo Mkoa wa Pwani alisema kuwa upatikanaji wa damu hiyo kutasaidia benki ya damu kuwa na damu ili kusaidia wagonjwa.

Sekelela alisema kuwa shughuli nyingine ambazo wanazifanya ni kupanda miti, kufanya usafi kwenye taasisi za umma ikiwa ni pamoja na shuleni, hoapitali na maeneo mbalimbali pamoja na kusaidia watoto waishio kwenye mazingira magumu.

Naye Mchungaji Josephine Mwalusama amesema kuwa yeye kama Mchungaji anamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuhimiza wanawake kushika nafasi za uongozi.

Mwalusama amesema kuwa Rais amefanya kazi kubwa na zinaonekana na ameshukuru Mwenge kuwashiwa Mkoani Pwani kwani utautangaza Mkoa na wajasiriamali watanufaika kwa kuwashwa mwenge huo wa uhuru.

Naye Mwenyekiti wa Vijana kutoka taasisi hiyo ya Bega kwa Bega na Tanzania Mkoa wa Pwani Athuman Lusambi  amesema kuwa wanawahamasisha vijana kushiriki kwenye Mwenge ili wawe wazalendo na nchi yao.

Monday, March 31, 2025

NMB KUTUMIA ZAIDI YA BILIONI 6 MIRADI YA MAENDELEO

BENKI ya inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya kuchangia shughuli za maendeleo kwa mwaka wa 2025.

Hayo yalisemwa na Meneja wa benki hiyo Kanda ya Dar es Salaam ambaye aliwakilishwa na meneja wa tawi la Mlandizi Wilayani Kibaha William Marwa wakati wa Kongamano la Vijana juu ya umuhimu wa kushiriki mbio za mwenge mkoa wa Pwani 2025.

Alisema vijana wanapaswa kujua historia ya mbio za mwenge wa uhuru na fursa zilizopo kupitia mwenge ambao ni alama ya mshikamano wa kuleta maendeleo ya nchi.

"Tangu mwenge umeanza mbio zake kwa sasa ni miaka 61 na pia tunakumbuka kifo cha mwasisi wa Taifa letu miaka 26 iliyopita lazima tumjue kwani aliifanyia nchi hii mambo makubwa,"alisema Marwa. 

Akizungumzia benki hiyo ambayo ni kubwa kuliko zote nchini imekuwa ikichangia maendeleo na ni chachu kwa kuchangia kwenye sekta ya afya, elimu na kutoa mkono wa pole kwa wananchi wanaopata majanga.

"Benki imekuwa ikirudisha sehemu ya faida kwa kuchangia suala la maendeleo kupitia sekta mbalimbali kwani wao ni sehemu ya wateja kwani ina matawi wilaya zote nchini,"alisema Marwa.

Alisema kuwa benki hiyo ina matawi 241 Atm 720 mawakala 50,000 na wateja milioni 8.7 kote nchini na bado inaendelea kuboresha huduma zake kimtandao.

Sunday, March 30, 2025

WAZIRI MKUU MAJALIWA AUPIGIA DEBE UWANJA WA SHIRIKA LA ELIMU KIBAHA KUTUMIWA NA TIMU ZA CHAN NA AFCON

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameupigia debe uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha kutumiwa na Timu za Taifa zitakazokuwa zinajiaandaa na michuano ya  CHAN na AFCON kwa ajili ya mazoezi.

Majaliwa aliyasema hayo alipotembelea kuukagua uwanja huo ambao utatumika kwenye usinduzi wa mbio za mwenge 2025.

Majaliwa alisema kuwa jana alifanya ukaguzi wa viwanja vitatu viyakavyotumika kwa ajili hiyo ambavyo ni vichache.

"Tanzania tumepata uenyeji wa mashindano hayo mawili ambayo ni makubwa hivyo lazima tuwe na viwanja vingi kwa ajili ya mazoezi na hichi kikiboreshwa kinaweza kutumika,"alisema Majaliwa.

Alisema kuwa wataangalia uwezekano wa uwanja huo kutumiwa kwa ajili ya mazoezi na tutaongea na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kama watakikubali itabidi kitumike.

"Kiwanja hichi kikiimarishwa vizuri kinaweza kutumika kwa ajili hata ya ligi kuu ni uwanja mzuri unahitaji maboresho kidogo tu kwani hata taa zipo kwa kweli hapa ni pazuri,"alisema Majaliwa.

Aidha alisema hayo ni matunda ya uwekezaji kwenye sekta ya michezo ambapo Rais Dk Samia Suluhu Hassan ameamua kuwekeza kwenye michezo.

"Kwa vijana wa Halaiki msiishie hapa endeleeni na mazoezi hii iwe ni sehemu ya kuanzia kwa wale watakaocheza mpira wa miguu, pete, riadha na michezo mingine ili muendeleze vipaji vyenu isiwe hapa ndiyo mwisho,"alisema Majaliwa.



WAZIRI MKUU MAJALIWA ARIDHISHWA MAANDALIZI UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU PWANI 2025

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea kuangalia maandalizi ya uwanja utakaotumika kuzindua mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 mkoani Pwani.

Majaliwa alitembelea uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha kuangalia maandalizi ya uzinduzi huo na kuridhishwa na maandalizi hayo na kutaka wakamilishe sehemu ambazo bado hazijakamilika.

Alisema kuwa ameridhishwa na maandalizi hayo ambapo pia alitumia muda huo kutembelea watoto wa halaiki na kusema amefurahishwa na jinsi walivyokuwa na hamasa ya uzinduzi huo.

"Nawapongeza kwa maandalizi mnayoendelea nayo nimeridhishwa kamilisheni sehemu zilizosalia ili kukamilisha mapema,"alisema Majaliwa.

Alisema kuwa amefurahishwa kuona viongozi wakiwemo mawaziri na makatibu wakuu wakiwa mstari wa mbele kuhakikisha maandalizi yanakuwa mazuri.

"Alikeni hata mikoa ya jirani Dar es Salaam, Morogoro na Tanga na watu mbalimbali kwani hili ni jambo la kitaifa shirikisheni wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili hamasa iwe kubwa,"alisema Majaliwa 

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Watu Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete maandalizi yako vizuri ila baadhi ya maeneo ikiwemo katikati ya uwanja ndiyo kunahitaji marekebisho kidogo.

Kikwete alisema kuwa mialiko kwa wageni mbalimbali imetolewa ikiwa ni pamoja na wakuu wa mikoa, wakurugenzi na watu wengine ili kushiriki uzinduzi huo.


Friday, March 28, 2025

VIJANA WAFUNDISHWE UMUHIMU WA MBIO ZA MWENGE

TAASISI mbalimbali nchini zimetakiwa kuwajengea uwezo vijana juu ya umuhimu wa mbio za Mwenge wa Uhuru katika kujenga uzalendo na uwajibikaji katika usimamizi wa shughuli za maendeleo na kutambua fursa za kiuchumi.

Hayo yamesemwa na Skauti Mkuu Nchini na Katibu Tawala (RAS) Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta wakati Kongamano la Vijana juu ya umuhimu wa kushiriki Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025.

Mchatta amesema kuwa vijana wanapaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa namna ambavyo mtaelekezwa na viongozi katika maeneo wanayoishi.

"Tukifanya hivyo tutaupata ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa ufasaha ili muweze kushuhudia kwa vitendo yale yote mtakayojifunza katika Kongamano hili,"amesema Mchatta.

Amesema kuwa Serikali inatambua umuhimu wa kundi la vijana katika kuleta mageuzi ya Kijamii na Kiuchumi kutokana na ari, nguvu na ubunifu walionao. 

"Kwa kutambua hilo serikali kwa kushirikiana na wadau imekuwa ikitoa kipaumbele kwa vijana kupata elimu na makuzi bora kuwapa fursa ya kupata mikopo ya asilimia 10 kupitia Halmashauri na Programu ya Jenga Kesho iliyo Bora (Build Better Tomorrow – BBT) 

Amesema kuwa Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 utazinduliwa mkoa wa Pwani kitendo ambacho kinaonesha nia njema ya Dk Samia Suluhu Hassani Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuendeleza na kuenzi kwa vitendo yale yote aliyoturithisha Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Rais wa Kwanza wa Tanzania. 

Kwa upande wake mratibu wa Kongamano hilo Omary Punzi amesema kuwa ili vijana waweze kufikia mafanikio ya kimaendeleo lazima wazingatie falsafa za Mwalimu Nyerere alizotumia wakati wa kuwashwa Mwenge wa Uhuru.

Punzi amesema moja ya falsafa za Mwenge wa Uhuru ni kuwafanya watu wawe na uzalendo kwa kujitoa kwa ajili ya nchi yao na kutokomeza maadui watatu ujinga umaskini na maradhi. 

Mbio za Mwenge wa Uhuru zitazinduliwa katika viwanja vya Shirika  la Elimu Kibaha Mkoani Pwani na Mgeni rasmi atakuwa Dk Philip Isdor Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

mwisho.


Wednesday, March 26, 2025

MAKAMU WA RAIS DK MPANGO KUZINDUA MBIO ZA MWENGE KITAIFA PWANI

MAKAMU wa Rais Dk Philip Isdor Mpango atazindua mbio za Mwenge kitaifa Mkoani Pwani Aprili 2 mwaka huu kwenye uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya juu ya uzinduzi huo amesema kuwa maandalizi ya uzinduzi yanaenda vizuri.

Kikwete amesema kuwa tayari Makamu wa Rais ameshathibitisha kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo wa mbio za  Mwenge kwa mwaka 2025.

"Kwa vitu vilivyobakia niwaombe mhakikishe vinafika kwa wakati ili kila kitu kiwe kwenye sehemu yake na bado tutaendelea kuangalia maandalizi ili siku hiyo mambo yawe mazuri,"amesema Kikwete.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maandalizi yako vizuri ambapo hadi Machi 29 mambo mengi yatakuwa yamekamilika.

Kunenge amesema kuwa huduma zote zitapatikana kuanzia suala la afya, vyoo, maji, taa kubwa, umeme ambapo kutakuwa na jenereta endapo umeme utakatika.

Amewataka wananchi wa Mkoa huo na mikoa jirani na Watanzania kwa ujumla kujitokeza siku hiyo ili kuweka historia ya Pwani kuzindua mbio za Mwenge Kitaifa.

Tuesday, March 25, 2025

JK AWASILISHA UJUMBE MAALUMU KWA RAIS WA SENEGAL KUTOKA KWA RAIS SAMIA

Mhe. Rais Mstaafu  Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewasilisha  ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Senegal, Mhe. Bassirou Diomaye Faye jijini Dakar.

Katika mazungumzo  yao ya kirafiki,  Rais Mstaafu alieleza dhamira ya dhati ya Rais Samia na Serikali anayoiongoza ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kijamii kati ya Tanzania na Senegal.

Pamoja na masuala ya ushirikiano wa kiserikali, Rais Mstaafu pia alisisitiza umuhimu wa kukuza uhusiano baina ya wananchi wa mataifa haya mawili kupitia sekta za elimu, biashara, utalii, na maendeleo ya vijana na wanawake.

Ziara hii ni sehemu ya juhudi endelevu za Tanzania kuimarisha uhusiano wa kimataifa na mataifa ya Afrika Magharibi, huku ikiweka msisitizo kwa diplomasia ya uchumi na ushirikiano wa watu kwa watu.

MAANDALIZI UWASHWAJI MWENGE WA UHURU KITAIFA PWANI MBIONI KUKAMILIKA



MAANDALIZI ya Uzinduzi wa mbio za Mwenge Kitaifa yamefikia asilimia 96 ambapo Mwenge huo utawashwa Wilayani Kibaha Mkoani Pwani Aprili 2 Mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC) Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maandalizi yanaenda vizuri.

Kunenge amesema kuwa kwa sasa zimebaki siku sita ambapo Mwenge utazinduliwa Aprili 2 na utatembelea kwenye Halmashauri tisa za mkoa huo kwa kuanza na Halmashauri ya Mji Kibaha utakapoanzia.

"Uwanja umekamilika yamebaki maeneo machache ambapo hadi leo sehemu kubwa itakuwa imekamilika na kubaki mambo madogo madogo,"amesema Kunenge.

Amesema kuwa majukwaa yamekamilika na matarajio ni kuwa na watu 16,000 ambapo miundombinu ya maji, sehemu ya magari kukaa tayari, taa, mifumo ya majitaka na ulinzi viko tayari.

Thursday, March 20, 2025

TANROADS YATOA UFAFANUZI LORI LILILOZIDISHA UZITO MIZANI YA VIGWAZA.

WAKALA wa Barabara Tanzania (TANROADS) imetoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ya lori la mizigo lililokamatwa kwenye mizani ya Vigwaza kuwa taratibu za kulikamata lori hilo ulifuatwa.

Aidha gari hilo lilipigwa faini hiyo kwa kuzingatia sheria ya udhibiti wa uzito barabarani ya Afrika Mashariki ya mwaka 2016 na kanuni zake za mwaka 2018.

Akizingumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za mizani hiyo ya Vigwaza Mtaalamu wa Kitengo cha Mizani Tanroads Makao Makuu Vicent Tarmo amesema kuwa gari hilo lilizidisha uzito zaidi ya tani moja.

Tarmo amesema kuwa gari hilo lenye namba za usajili T 137 DLR na tela namba T 567 CUR lilikuwa limetokea nchini Congo likiwa limebeba madini ya Shaba ambapo uwezo wake ni kubeba tani 48 lakini lilikutwa likiwa na uzito tani 48.1.

"Kutokana na kuzidisha uzito huo gari hilo lilitakiwa kulipiwa faini ya shilingi 900,000 ikiwa ni adhabu ya kuzidisha uzito halisi lakini dereva huyo alisema kuwa amezidishiwa uzito hivyo kupinga faini hiyo,"amesema Tarmo.

Amesema kuwa sheria inataka magari yote yenye uzito kuanzia tani 3 na nusu lazima yapime uzito ili kuepusha uharibifu wa barabara hivyo kutokana na gari hilo kuzidisha uzito alipaswa kulipa faini hiyo.

"Dereva huyo amesema kuwa amepita mizani mbalimbali uzito haukuzidi hivyo kwa nini hapa uzidi lakini kwa mujibu wa sheria alipaswa kulipa na siyo kukaidi kulipa,"amesema Tarmo.

Amesema kuwa gari hilo lilipita hapo Machi 13 ambapo kwa siku hiyo yalipimwa mwagari 819 ambapo saba yalibainika kuzidisha uzito ambapo mengine yalilipa na kuendelea safari lakini gari hilo dereva wake aligoma kulipa akidai amezidishiwa uzito.

"Mzani huu ni automatiki lakini yeye alitaka uzito  urudiwe kupimwa jambo ambalo ni kinyume cha utaratibu ambapo hupaswa kupunguza na kulipa uliizidi na kupima tena na siyo kupima upya,"amesema Tarmo.

Ameongeza kuwa uzito unaweza kuzidi kutokana na sababu kadhaa ikiwa ni pamoja na kuongeza mafuta, abiria na busta endapo zitakuwa na hitilafu ambapo hata walipofuatilia mizani nchini Zambia uzito ulikuwa na mabadiliko ikionekana kuzidi.

"Dereva baada ya kuona hizo tofauti alipaswa kuangalia mfumo wa gari lake kwani kutokana na baadhi ya changamoto kama hizo uzito unaweza kuongezeka,"amesema Tarmo.

Kwa upande wake Meneja wa Tanroads Mkoa wa Pwani Baraka Mwambage amesema kuwa kama kunatokea changamoto yoyote kuna taratibu za kufuata ili kuweza kupata haki zao na si kutumia mitandao kutoa malalamiko yao.

Mwambage amesema kuwa malalamiko yanaweza kupelekwa ofisini au kama wana wasiwasi wanaweza kupeleka kwenye vyombo vingine ikiwa ni pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) kama sehemu ya kujua ukweli zaidi.

Hivi karibuni zilisambaa habari kupitia mitandao ya kijamii ambapo picha mjongeo ilimuonyesha dereva mmoja akilalamikia mizani ya Vigwaza kuwa imezidisha uzito.

TCRA KUSHIRIKIANA NA TBN KUSADIA KUZALISHA MAUDHUI YENYE TIJA

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeahidi kufanyakazi na Mtandao wa Wana Blogu Tanzania (TBN) pamoja na vyama vingine vya waandishi wa habari ambavyo vinawakilisha mahitaji na matakwa ya wanachama wao.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe  19 Machi 2025 Jijini Dar es Salaam na Meneja wa Huduma za Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, alipokutana na ujumbe wa TBN ofisini kwake, katika kikao cha kujadiliana changamoto mbalimbali zinazowakabili Bloga nchini.

“Sisi huwa tunapenda kufanya kazi na vyama ambavyo vinawakilisha mahitaji na matakwa ya wanachama wao, badala ya kufanyakazi na mwaandishi mmoja mmoja…tunafurahi sana kufanyakazi na waandishi kupitia vyama vyao,” amesema Mhandisi Kisaka.

Mhandisi Kisaka amesema kuwa TCRA imefurahi kukutana na TBN kwa kuwa wanafahamu kuwa Bloga wanasehemu kubwa sana kwenye maudhui ya ndani, na hata kwenye usajili wa TCRA Bloga wanachukua nafasi kubwa sana katika maudhui ya mtandaoni.

“Kwa hiyo TBN mtakuwa silaha moja wapo nzuri sana yakutuwezesha sisi kama Mamlaka ya Mawasiliano nchini, tunao simamia utangazaji pamoja na maudhui ya mtandaoni kuwa karibu na nyinyi na kuhakikisha maudhui ya mtandaoni yanaleta tija na maendeleo kwa wananchi,” amesema Mhandisi Kisaka.

Friday, March 14, 2025

RAIS MSTAAFU DK KIKWETE AFANYA ZIARA NCHINI JAPAN KUIMARISHA USHIRIKIANO KATI YA BODI YA SHIRIKA LA ELIMU LA KIMATAIFA (GPE) NA JAPAN


Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Elimu la Kimataifa (GPE), yupo Tokyo nchini Japan kwa ziara maalum yenye lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya GPE na serikali ya Japan katika kutatua changamoto za elimu ya msingi katika nchi zinazoendelea.

Katika siku yake ya kwanza Tokyo, Dkt. Kikwete amefanya mazungumzo na Waziri wa Fedha wa Japan, Mhe. Shin-ichi Yokohama, pamoja na Naibu wake, Mhe. Atsushi Mimura. 

Mazungumzo hayo yalijikita katika ushirikiano wa kifedha ili kusaidia miradi ya elimu inayosimamiwa na GPE, ikiwemo upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wa nchi zinazoendelea.

Baada ya mazungumzo hayo, Rais Mstaafu Kikwete alikutana na Bw. Akihiko Tanaka, Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA). 

Shirika hili limekuwa na mchango mkubwa katika miradi ya maendeleo barani Afrika, na mazungumzo yalihusu namna JICA inaweza kusaidia jitihada za GPE katika kukuza elimu bora.

Dkt. Kikwete pia alikutana na Bw. Yohei Sasakawa, Mwenyekiti wa Taasisi ya Nippon. Bw. Sasakawa, mwenye umri wa miaka 86, ni mtu mashuhuri wa kusaidia miradi ya kijamii duniani. 

Katika mazungumzo yao, waligusia nafasi ya sekta binafsi katika kusaidia elimu, hasa kupitia taasisi zisizo za kiserikali. Vilevile, Bw. Sasakawa alishangaza dunia baada ya kufanikisha kupanda Mlima Kilimanjaro tarehe 12 Februari 2024, kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 85 ya kuzaliwa kwake – hatua inayothibitisha kuwa umri si kikwazo kwa ndoto kubwa.

Katika siku zinazofuata, Rais Mstaafu Kikwete anatarajiwa kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. T. Miyaji, pamoja na wabunge wa Bunge la Japan, ambapo ajenda kuu itakuwa nafasi ya elimu na teknolojia katika maendeleo ya jamii.

Pia, atashiriki mijadala maalum kuhusu elimu na teknolojia, kufanya mahojiano na vyombo vya habari, pamoja na kukutana na Mhe. Tetsuro Yano, Rais wa Taasisi ya AFRECO, ambayo inahusika na kukuza ushirikiano kati ya Japan na Afrika.

Ziara hii ni sehemu ya juhudi endelevu za Dkt. Kikwete katika kuboresha mifumo ya elimu duniani, hasa katika nchi zinazoendelea. 

Japan ni mshirika muhimu wa maendeleo ya elimu barani Afrika, na ushirikiano huu unaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuhakikisha watoto wengi zaidi wanapata fursa ya elimu bora.

 


Thursday, March 13, 2025

KIWANDA CHA KEDS CHATOA MSAADA KWA WANAWAKE

KIWANDA cha kuzalisha sabuni cha Keds Tanzania Company Ltd cha Kibaha Mkoani Pwani kimetoa misaada ya sabuni kwa wanawake wa Mtaa wa Lulanzi ambao uko jirani na kiwanda hicho ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe ya siku ya wanawake Duniani.

Akizungumza kiwandani hapo mara baada ya kukabidhi msaada hiyo Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bob Cheng amesema kuwa wanaungana na jamii katika kusaidia wanawake ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe hizo.

Cheng amesema kuwa wamewapatia misaada hiyo ikiwa ni sehemu ya kuenzi mchango wa wanawake ambao ni mkubwa katika kuleta maendeleo kwenye jamii.

"Kiwanda kinaungana na wanawake katika maadhimisho haya hivyo tumeona turudishe kwa jamii ikiwa ni katika ushirikiano na wananchi katika kuleta maendeleo,"amesema Cheng.

Amesema kuwa kiwanda kitaendelea kushirikiana na jamii katika masuala mbalimbali ya maendeleo hususani kwa wananchi walio jirani na kiwanda na wananchi wote kwa ujumla.

Akishukuru kwa msaada huo wa sabuni za unga na vipande Jasmini Issa amesema kuwa wanashukuru kwa msaada huo kwani utawasaidia katika matumizi ya kila siku.

Issa amesema kuwa msaada huo umeonyesha jinsi kiwanda hicho kinavyoshirikiana na jamii katika suala zima la maendeleo ambapo wamekuwa wakisaidia miradi mbalimbali inayohusu wananchi.

Naye Meri Mkwizu amesema kuwa sabuni ni muhimu sana kwa familia na ni moja ya vitu muhimu katika mahitaji kwenye familia na hutumika muda wote.

Mkwizu amesema kuwa sabuni ina bajeti kubwa kutokana na matumizi yake ikiwa ni pamoja na kufulia nguo, kuoshea vyombo, kuogea na kufanyia usafi wa aina mbalimbali ambapo jumla ya wanawake 89 walipewa msaada huo.

KEDS KUENDELEA KUZALISHA BIDHAA BORA

KIWANDA cha Keds Tanzania Company Ltd kimesema kitaendelea kuzalisha bidhaa zenye ubora na bei nafuu kulingana na hali ya soko.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa kiwanda hicho Bob Cheng alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Cheng amesema kuwa katika utengenezaji wa bidhaa zao wanazingatia ubora ili kuendelea kuwa na soko kwa kuwapatia wananchi kitu kilicho bora.

"Malengo ya kuanzishwa kiwanda ni kukuza uchumi wa wananchi kwa kutoa ajira kwa watu wengi pia kutengeneza bidhaa bora zinzokubalika,"amesema Cheng.

Amesema kuwa malengo yao ni kutengeneza bidhaa nyingine lakini kwa sasa wanafanya kwanza utafiti ili kujua ni bidhaa gani watakayoizalisha.

"Kiwanda kinajihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama na kinashirikiana na serikali kwa kufuata taratibu zote za kisheria,"amesema Cheng.

Aidha amesema kuwa kiwanda kinashirikiana na jamii kwa kurudisha kwa jamii kwa kusaidia kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kwenye sekta za elimu, afya, barabara na sekta mbalimbali.

"Kuhusu maji yanayotoka kiwandani hayana athari zozote za kiafya na kimazingira ambapo hata wafanyakazi wetu wanaishi jirani na kiwanda ni asilimia 60 hivyo hayana tatizo lolote,"amesema Cheng.

Kiwanda hicho kinauza bidhaa zake kote nchini pamoja na nchi za jirani baadhi zikiwa ni Uganda, Kenya na Malawi.







TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA (THBUB) YATEMBELEA VIWANDA PWANI

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imefanya ziara kutembelea viwanda kuangalia uzingatiwaji wa haki za binadamu ili zisivunjwe

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamishna wa Tume Nyanda Shuli wakati wa ziara ya kutembelea viwanda ili kufanya uchunguzi kujua kama kuna changamoto za uvunjifu wa haki.

Shuli amesema kuwa baadhi ya viwanda vimekuwa vikilalamikiwa kuvunja haki za binadamu kwa unyanyasaji wa wafanyakazi, uchafuzi taka maji na haki mbalimbali.

"Lengo la ziara ni kuangalia hali ya haki za binadamu na uzingatiwaji wa misingi ya utawala bora kuangalia usalama wa mazingira ya kazi na uzingatiaji wa viwango vya ajira,"amesema Shuli.

Amesema kuwa malalamiko waliyoyapokea watayafanyia kazi na kutoa majibu jambo kubwa ni kuona haki inatendeka ili kuondokana na uvunjifu wa haki za binadamu.

Kwa upande wake Bob Cheng ambaye ni Mkurugenzi wa kiwanda cha Keds Tanzania Company Ltd kinachojihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama.

Cheng amesema kuwa kiwanda chao kinazingatia masuala ya haki za binadamu na lengo lake ni kukuza uchumi wa wananchi na hata maji ya kiwanda hicho hayana madhara ambapo asilimia 60 ya wafanyakazi wanaishi eneo jirani na kiwanda hivyo kama kungekuwa na changamoto yoyote wangefahamu.

Amesema kuwa wanafanya utafiti ili kuongeza bidhaa na uzalishaji wenye kuzingatia ubora na bei ambayo inaendana na soko.

Aidha kamishna aliambatana na Taasisi za Serikali ambazo ni OSHA, NEMC na Maofisa kutoka Ofisi ya RAS (Ofisa biashara, Ofisa Kazi na Ofisa Maendeleo ya jamii) kwa lengo la kuleta ufanisi katika ziara hiyo.


Wednesday, March 12, 2025

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA (THBUB) INAFANYA ZIARA KWENYE VIWANDA MKOANI PWANI KUANGALIA UZINGATIWAJI WA HAKI ZA BINADAMU

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imefanya ziara kutembelea viwanda kuangalia uzingatiwaji wa haki za binadamu ili zisivunjwe.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamishna wa Tume Nyanda Shuli wakati wa ziara ya kutembelea viwanda ili kufanya uchunguzi kujua kama kuna changamoto za uvunjifu wa haki.

Shuli amesema kuwa baadhi ya viwanda vimekuwa vikilalamikiwa kuvunja haki za binadamu kwa unyanyasaji wa wafanyakazi, uchafuzi taka maji na haki mbalimbali.

"Lengo la ziara ni kuangalia hali ya haki za binadamu na uzingatiwaji wa misingi ya utawala bora kuangalia usalama wa mazingira ya kazi na uzingatiaji wa viwango vya ajira,"amesema Shuli.

Amesema kuwa malalamiko waliyoyapokea watayafanyia kazi na kutoa majibu jambo kubwa ni kuona haki inatendeka ili kuondokana na uvunjifu wa haki za binadamu.

Kwa upande wake Bob Cheng ambaye ni Mkurugenzi wa kiwanda cha Keds Tanzania Company Ltd kinachojihusisha na uzalishaji wa sabuni za unga, vipande, pampasi na pedi za akinamama.

Cheng amesema kuwa kiwanda chao kinazingatia masuala ya haki za binadamu na lengo lake ni kukuza uchumi wa wananchi na hata maji ya kiwanda hicho hayana madhara ambapo asilimia 60 ya wafanyakazi wanaishi eneo jirani na kiwanda.

Amesema kuwa wanafanya utafiti ili kuongeza bidhaa na uzalishaji wenye kuzingatia ubora na bei ambayo inaendana na soko 

Aidha kamishna aliambatana na Taasisi za Serikali ambazo ni OSHA, NEMC na Maofisa kutoka Ofisi ya RAS (Ofisa biashara, Ofisa Kazi na Ofisa Maendeleo ya jamii) kwa lengo la kuleta ufanisi katika ziara hiyo.


Wednesday, March 5, 2025

DOWEICARE YATOA YATOA MSAADA WA FEDHA UJENZI WA DARAJA LULANZI


KIWANDA cha Doweicare cha Kibaha Mkoani Pwani kimetoa fedha kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa daraja la Mtaa wa Lulanzi-Matunda ili kuboresha barabara ya mtaa huo.

Akikabidhi fedha hizo kwa uongozi wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bob Chen amesema kuwa wameamua kutoa fedha hizo ili kukabili changamoto za jamii.

Amesema kuwa Kiwanda chao kimekuwa kikitoa misaada mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa jamii kama sehemu ya huduma za jamii ambapo fedha hizo ni asilimia 57.5 ya fedha za mradi huo.

"Tunashirikiana na jamii kwenye masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja elimu, afya, barabara na masuala yanayohusu jamii,"amesema Chen.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Thobias Shilole amesema kuwa wanakishukuru kiwanda hicho kwa msaada walioutoa utasaidia sana ujenzi wa daraja hilo.

Shilole amesema wananchi wamekuwa wakijitolea fedha kwa ajili ya ujenzi huo hivyo hiyo itakuwa imewaongezea nguvu kwenye kuanza ujenzi wa daraja ili kupunguza changamoto kwa wananchi wanaotumia barabara hiyo.

Amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo kuendelea kuchangia ujenzi huo ili upunguze changamoto kwa watu wakiwemo wanafunzi wakati wakienda na kurudi shule.


WATAALAMU UDSM WAKUTANA NA VIONGOZI TBN

Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), wamekutana na baadhi ya viongozi na wajumbe wa Tanzania Bloggers Network (TBN) kwa mahojiano maalum yenye lengo chanya la kukusanya maoni yao ili kuimarisha masuala ya blogging, nchini.

Hatua hiyo ya kukusanya maoni imekuja kufuatia wataalamu hao kuagizwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambayo ipo katika utafiti maalum kwa nia ya dhati kuboresha Sera na kanuni zake mbalimbali katika eneo hilo la majukwaa ya mtandaoni.

Kikao hicho kimefanyika kwa mafanikio katika ofisi za TBN zilizopo kwa Aziz Ali, Temeke, watafiti hao wamechukua maoni ya TBN Makao Makuu, wakisema pia watafika katika Ofisi za Kanda za TBN.

Akizungumza Katibu Mkuu wa TBN Khadija Kalili amesema TCRA imefanya uamuzi sahihi kukutana na wadau wake kwa kupitia wataalamu hao kwani maoni yao yatawapa picha halisi juu ya tasnia ya habari na blogging kwa ujumla wake.

Amesema kilio kikubwa cha wana TBN ni gharama za usajili na tozo ya leseni kiasi ni kikubwa ambacho kwa uhalisia wengi bado hawamudu kulipia.

Amesema hali hiyo imefanya idadi kubwa ya wana TBN kushindwa kumudu kuendesha mitandao yao kutoka 300+ waliokuwapo kwanza hadi kufikia 100+ tu wanaoweza kulipia na kwa kusuasua.

Ameshauri pia TCRA kuendeleza utamaduni wa kukutana na wadau wake ikiwamo kwa mafunzo ya kuwaimarisha uwezo wao pamoja na kuangazia athari za gharama za bando za mtandao na vifaa.

Amesema ikiwa sekta ya blogging ndani ya tasnia ya habari ikisimamiwa vizuri kwa ushirikiano wa karibu na TCRA ni wazi kwamba Tanzania itanufaika na maudhui bora na yenye viwango ambayo yatasaidia kulinda maadili ya jamii yetu.

TBN yenye wanachama 300 waliopo wanaendesha mitandao kwa kusuasua kutokana na ada na tozo.

Watalaam hao walionesha kushangazwa na kuwapo kwa Chama Cha Bloggers chenye usajili kamili na wanachama zaidi ya 300, na pia wakaelewa bloggers ni tofauti na jumuiya zingine za waandishi wa mitandao ambao hawana blogs.

Wataalamu hao ni pamoja na Prof. Siasa Mzenzi, Dkt. Patrokil Kanje , Dkt. Said Suluo.

Wengine ni Mjata Daffa , Ally Mshana na Viongozi na wajumbe wa TBN, wakiongozwa na Katibu Mtendaji Khadija Kalili , Beda Msimbe na Rahel Pallangyo.



Mwisho

DOWEI CARE YATOA MSAADA WA FEDHA UJENZI WA DARAJA LULANZI

KIWANDA cha Dowei Care cha Kibaha Mkoani Pwani kimetoa fedha kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa daraja la Mtaa wa Lulanzi-Matunda ili kuboresha barabara ya mtaa huo.

Akikabidhi fedha hizo kwa uongozi wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Mkurugenzi wa Kiwanda hicho Bob Chaing amesema kuwa wameamua kutoa fedha hizo ili kukabili changamoto za jamii.

Amesema kuwa Kiwanda chao kimekuwa kikitoa misaada mbalimbali kwenye jamii ikiwa ni sehemu ya kurudisha kwa jamii kama sehemu ya huduma za jamii ambapo fedha hizo ni zaidi ya asilimia 60 ya fedha za mradi huo.

"Tunashirikiana na jamii kwenye masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja elimu, afya, barabara na masuala yanayohusu jamii,"amesema Chaing.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Lulanzi Thobias Shilole amesema kuwa wanakishukuru kiwanda hicho kwa msaada walioutoa utasaidia sana ujenzi wa daraja hilo.

Shilole amesema wananchi wamekuwa wakijitolea fedha kwa ajili ya ujenzi huo hivyo hiyo itakuwa imewaongezea nguvu kwenye kuanza ujenzi wa daraja ili kupunguza changamoto kwa wananchi wanaotumia barabara hiyo.

Amewataka wadau mbalimbali wa maendeleo kuendelea kuchangia ujenzi huo ili upunguze changamoto kwa watu wakiwemo wanafunzi wakati wakienda na kurudi shule.


Monday, March 3, 2025

VYAMA SITA RAFIKI KUSINI MWA AFRIKA VISIYUMBISHWE VISIMAMIE SHABAHA YA KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO

VYAMA vya Ukombozi Kusini mwa Afrika vimetakiwa vibadili mbinu za kuongoza na visikubali kuyumbishwa na mabadiliko ya dunia na kuacha shabaha ya kuziongoza nchi zao.

Hayo yalisemwa jana kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Mjini Kibaha na Makamu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Steven Wassira wakati akifungua mafunzo kwa viongozi wa vyama hivyo.

Wassira alisema kuwa baadhi ya nchi duniani havipendi kuona vyama hivyo vinaongoza wao wanaona demokrasia ni kuviondoa vyama hivyo madarakani.

"Mabadikiko ni mengi duniani lakini yasivitoe vyama vyetu kwenye shabaha yake ya msingi ambayo ni maisha bora na mazuri kwa wananchi huu ndiyo msingi wa vyama hivi,"alisema Wassira.

Alisema kuwa hiyo ndiyo misingi iliyowekwa na waasisi wa mataifa hayo ambayo yalipigania Uhuru wa nchi zao na kuacha misingi imara ambayo inapaswa kufuatwa.

Kwa upande wake Katibu wa masuala ya siasa uhusiano wa kimataifa na Halmashauri Kuu ya CCM NEC Rabia Hamidu alisema kuwa nchi hizo zinapaswa kuonyesha umoja wao ili kuzisaidia nchi za Afrika.

Naye Naibu Mkurugenzi wa idara ya masuala ya Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na idara ya kimataifa ya kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na mkuu wa ujumbe wa IDPC Zhang Yanhong alisema kuwa ni jambo zuri kwa ushirikiano wa vyama hivyo sita na CPC.

Naye Mkuu wa Shule ya Mwalimu Julius Nyerere Profesa Marcelina Chijoriga alisema wanatoa mafunzo kwa viongozi wa vyama vya siasa, taasisi za umma na serikali pamoja na taasisi za watu binafsi.

SERA YA TAIFA YA MAENDELEO YA VIJANA 2007 YAENDELEA KUNADIWA

Leo tarehe 3.3.2025 Ndugu Omary Abdul Punzi Mwanadiplomasia na Mratibu wa Makongamano ya Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana Mwaka 2007 toleo la Mwaka 2024 katika kamati ya Vijana Wazalendo waliopewa kibali Maalumu na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu 

Kwa ajili ya Kuinadi na kuineza Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana 

Amemtembelea Mheshiwimiwa Godfrey Eliakimu Mzanva Mkuu wa Wilaya ya Moshi kwa ajili ya kumpongeza kwa Kuaminiwa na Mheshiwimiwa Dk Samia Suluhu Hasani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya.

Unakumbuka kuwa Mheshiwimiwa Godfrey Eliakimu Mzanva ni miongoni mwa wakimbiza mwenge mwaka 2024 waliofanya vizuri katika kuendesha Makongamano ya vijana.

Aidha mazungumzo hayo yalitoa mwafaka wa Kuandaa Kongamano la Vijana Kuhusu Umuhimu wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Ambalo litajikita zaidi kuelezea historia ya Tanzania, Itifaki, Maadili na Uzalendo kwa Vijana,Madhara ya matumizi ya madawa ya kulevya, utunzaji wa Mazingira na Fursa zinatopatikana Wilaya ya Moshi Mkoa wa Kilimanjaro

Friday, February 28, 2025

CCM KATA YA MKUZA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 9.4

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya  ya Mkuza Wilayani Kibaha kimefanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya shilingi bilioni 9.4 na kurudhishwa na kiwango cha utekelezaji wa miradi hiyo.

Akizungumza baada ya kukamilisha ziara ya Halmashauri ya Kuu ya Kata kutembelea miradi hiyo Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mkuza Matata Ngolo amesema kuwa huo ni utekelezaji wa ilani ya CCM.

Ngolo amesema kuwa kabla ya kikao waliona ni vema wakatembelea miradi hiyo ya maendeleo ili kujionea uhalisia wa utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano.

Kwa upande wake diwani wa Kata ya Mkuza Fokas Bundala amesema  kuwa moja ya mafanikio makubwa ni ujenzi wa shule za sekondari mbili ambapo kiutaratibu kila kata inapaswa kujenga sekondari moja.

Bundala amesema kuwa changamoto kubwa iliyopo ni madawati na viti na meza lakini kwenye bajeti inayokuja fedha zimetengwa hivyo itapunguza changamoto hiyo.

Amesema kuwa katika kipindi hicho serikali kupitia mapato yake ya asilimia 10 ilitoa kiasi cha shilingi milioni 660 kwa ajili ya mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kwa vikundi.

MWENGE WA UHURU KITAIFA KUWASHWA PWANI APRILI 2,2025

WANANCHI wa Mkoa wa Pwani wametakiwa kutumia fursa za kiuchumi kwa kuwashwa mwenge wa uhuru mkoani humo Aprili 2 mwaka huu.

Hayo yamesemwa jana Mjini Kibaha na Mkuu wa Mkoa huo Abubakar Kunenge alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Amesema kuwa kuwashwa mwenge wa uhuru Mkoani Pwani ni fursa kiuchumi kwa wananchi pia ni chachu ya maendeleo kwani wananchi watafanya biashara za chakula, malazi, usafiri, vinywaji na utalii.

"Wananchi tumieni fursa hiyo ya uzinduzi wa mbio hizo za mwenge wa uhuru kwa kufanyabiashara ambapo kutakuwa na wageni wengi na hata wenyeji ambao watahitaji huduma mbalimbali,"amesema Kunenge.

Amesema kuwa sherehe hizo za uzinduzi zitapambwa na matukio mengi yakiwemo ya halaiki na burudani nyingine za wasanii.

"Baada ya uzinduzi huo mwenge wa uhuru utakimbizwa katika Halmashauri tisa za mkoa huo ambapo utakagua, kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo,"amesema Kunenge.

Aidha amewahamasisha na kuwaomba wananchi wote wa Mkoa wa Pwani na maeneo jirani kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uzinduzi huo.

"Maandalizi yanaendelea vizuri ambapo muda bado unatosha na mwaka huu tumejipanga vyema kuhakikisha tunafanya vizuri,"amesema Kunenge.

mwisho. 


Monday, February 24, 2025

SHULE ZA AWALI NA MSINGI BINAFSI 101 ZANUFAIKA NA MRADI WA OPPORTUNITY INTERNATIONAL-MOSHA

Ofisa Elimu Taaluma wa Mkoa wa Dar es Salaam, Eva Mosha, ametoa rai kwa wamiliki na walimu wa shule binafsi za awali na msingi kuimarisha ufanisi wa ufundishaji na kuboresha ubora wa elimu, ili kuinua taaluma katika shule zao.

Amesisitiza ,shule hizo zinapaswa kuongeza ubunifu na kujiendeleza kwa kupata mafunzo mbalimbali ya namna ya kuendesha shule zao, ili kuepuka changamoto za kushindwa kuendeleza shule au kukosa wanafunzi.

Mosha alitoa rai hiyo katika hafla ya kupongeza walimu na wamiliki wa shule binafsi za awali na msingi, ambazo zinatoa ada nafuu, waliopatiwa mafunzo ndani ya miaka mitatu kupitia mradi wa Opportunity International ,kwenye ukumbi wa Victoria uliopo Kimara Temboni, Dar es Salaam. 

Mratibu wa Mradi wa Opportunity International Tanzania (HES Tanzania), Oliver Kapaya, alieleza kuwa mradi huo ulianza mwaka 2018 na umefanikiwa kuhusisha shule 101 katika kipindi cha miaka mitatu.

Alieleza, shule 74 zilipata mafunzo na kufuzu kwa kipindi cha miaka minne na shule 15 zimefanikiwa kupata tuzo za kutambua ufanisi wao huku, shule nane zimetunukiwa tuzo kwa utendaji bora.

Violet Oketch, mratibu wa Mradi wa Opportunity International Afrika (HES Africa), alieleza mradi huu unatekelezwa katika nchi nane za Afrika, ikiwa ni pamoja na Tanzania, Rwanda, Zambia, Ghana, DRC Congo, Uganda, Kenya, na Nigeria.

Violet Oketch alishukuru serikali ya awamu ya sita kwa ushirikiano wake na wawekezaji na wafadhili mbalimbali katika sekta ya elimu. 

Brayson Ephata Maleko, Ofisa Elimu Vifaa na Takwimu Temeke, alisema mradi huo umehusisha shule za awali na msingi, namna ya kuendesha shule kwa ufanisi, kupanga mipango, na kusimamia rasilimali fedha.

PWANI YAZINDUA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA WA MAMA SAMIA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amewataka watumishi ambao ni wanasheria kwenye Mkoa huo kuwahudumia wananchi kwenye kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia.

Kunenge ameyasema hayo Mjini Kibaha wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo ya siku tisa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Mkoani Pwani.

Amesema kuwa kampeni hiyo ni nzuri na itawasaidia wananchi wanyonge ambao hawana uwezo wa kulipia gharama za kisheria na kumshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kubuni kampeni hiyo.

Kwa upande wa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Jumanne Sagini amesema kuwa kampeni hiyo ni kuwezesha wanyonge wanapata haki zao kwa wakati.

Naye Naibu Waziri wa maendeleo ya jamii jinsia wanawake na makundi maalum Mwanaid Khamis amesema kuwa kumekuwa na changamoto ya ukatili wa kijinsia, matunzo ya watoto, ardhi na ubakaji.

Mwakilishi wa bodi ya ushauri wa msaada wa kisheria Nuru Awadh amesema kuwa siku tisa ni chache kwani changamoto ya masuala ya kisheria ni kubwa sana hivyo ili kuwafikia wananchi wengi hivyo huduma ziendelee kutolewa.

Mkurugenzi wa mashirika yanayotoa msaada wa kisheria (TANLAP) Christina Ruhinda amesema kuwa kila kata ina wasaidizi wa kisheria nchi nzima ambao wanasaidia kutoa elimu na msaada wa kisheria.


Saturday, February 15, 2025

WAANDISHI WA HABARI WAJENGEWA UWEZO JUU YA MALEZI MAKUZI MAENDELEO YA WATOTO

WAANDISHI wa Habari nchini wametakiwa kuleta mabadiliko chanya kwenye masuala ya malezi na makuzi ya watoto ili kuja kupata viongozi bora wa baadaye.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Osifa Programu kutoka Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Victor Maleko ambaye alikuwa mwezeshaji wa mafunzo kuhusu uandishi wa habari zinazohusu Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (MMMAM).

Maleko alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa ukuaji wa watoto ambao wanatakiwa kupata huduma muhimu katika ukuaji wao ili wawe na makuzi mazuri.

WAANDISHI WATAKIWA KUANDIKA HABARI SAHIHI ZA UCHAGUZI

NAIBU Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Hamis Mwinjuma amevitaka vyombo vya habari kuandika habari sahihi kipindi cha uchaguzi ili kudumisha amani.

Ameyasema hayo Mjini Dodoma alipokuwa akifunga Mkutano wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji Nchini.

Mwinjuma amesema kuwa vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kutoa taarifa sahihi ambazo zitawafanya wananchi kuchagua viongozi bora ambao watailetea nchi maendeleo.

"Kazi yenu kubwa ni kutoa taarifa sahihi kwa wananchi ambao wanaviamini vyombo vya habari kupata taarifa za ukweli na siyo za kupotosha ili kupata viongozi bora,"amesema Mwinjuma.

Kwa upande wake Mhandisi Endrew Kisaka ambaye alimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) amesema kuwa vyombo vya habari vinapaswa kuandika habari za vyama vya siasa wakati wa uchaguzi bila ya upendeleo.

Kisaka amesema kuwa waandishi wazingatie kuandika sera na siyo majibizano au udini, ukabila na kutoingilia faragha za watu na kotoegemea upande wowote bali watoe nafasi kwa watu wote.

Naye katibu wa Mtandao wa Bloggers Tanzania (TBN) Khadija Kalili ameishukuru  TCRA na kuiomba kupunguza gharama za usajili ambapo kwa sasa ni shilingi 500,000 ambayo ni kubwa hivyo wengi kushindwa kulipia.

Kalili alisema kuwa TBN ilisajiliwa mwaka 2015 na ilianza na wanachama 100 hadi kufikia 300 ambapo baadhi walijitoa kutokana na kushindwa kusajili.

Mkutano huo wa mwaka ambao uliansaliwa na TCRA ulihusisha washiriki 528 ambao wanajihusisha na masuala ya utangazaji na watoaji maudhui mtandaoni nchini, waandishi wakongwe wa Redio Tanzania.

WAZIRI KABUDI ATAKA WATANGAZAJI KUACHA MBWEMBWE WATUMIE KISWAHILI SANIFU

WAZIRI wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Profesa Kabudi amewataka watangazaji kuacha mbwembwe na kubananga Kiswahili na kutumia Kiswahili Sanifu ili Tanzania iendelee kuwa nchi inayotumia Kiswahili fasaha.

Profesa Kabudi ameyasema hayo Mjini Dodoma wakati akifungua mkutano wa mwaka wa vyombo vya utangazaji nchini.

Amesema kuwa Tanzania ni nchi kinara wa lugha ya Kiswahili lakini endapo hakutakuwa na juhudi za makusudi za kukisimamia Kiswahili hatutakuwa vinara tena wa lugha hiyo.

"Watangazaji wanapaswa kutumia Kiswahili fasaha na sanifu kwani tuna utajiri wa misamiati hivyo tukitumie vizuri ili kuandaa vipindi vyenye tija kwa wasikilizaji,"amesema Kabudi.

Naye Mkurugenzi wa Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dk Jabiri Bakari amesema kuwa wamekuwa wakifanya utafiti juu ya maudhui ya mtandaoni ili kutoa taarifa sahihi na za umahiri.

Bakari amesema kuwa kuna utafiti umefanywa ambapo utakamilika mwezi huu lengo kuu likiwa ni kuboresha utoaji wa maudhui mitandaoni.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui Saida Muki amesema kuwa watangazaji wa maudhui mitandaoni wanapaswa kuweka maslahi ya nchi mbele  na kujiepusha na maudhui yanayokiuka maadili.