MBUNGE Mteule wa Jimbo la Kibaha Mjinj kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Silvestry Koka amewataka wale waliowania nafasi hiyo na kura hazikutosha washirikiane ili chama kipate ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.
Koka aliyasema hayo mjini Kibaha wakati akichukua fomu kuwania nafasi hiyo kupitia CCM na kuwa ni wakati wa kuungana ili kuleta ushindi wa chama.
Alisema kuwa kama kulitokea kutofautiana kwa namna moja au nyingine ni kusameheana na kuungana wakati wa kutafuta kura za chama.
"Huu ni wakati wa kuungana na kuondoa tofauti ambazo zilijitokeza wakati wa ndani ya chama ambapo kila mmoja alikuwa akitafuta namna ya kushinda,"alisema Koka.
Alisema kuwa kilichoshinda ni hivyo kusiwe na kuona kuwa fulani kashinda wote ni wana ccm hawapaswi kutofautiana wote wanakipambania chama.
"Tuungane ili kuhakikisha tunakipatia ushindi chama kuanzia Urais, Ubunge na Udiwani tunataka ushindi uwe mkubwa na wakishindo na kuweka historia,"alisema Koka.
Aidha alisema kuwa wanaccm wahakikishe ushindi wa asilimia 100 kama ilivyokuwa kuwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na kwenye kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.
Kwa upande wake Alhaji Mussa Mansour ambaye alikuwa moja ya wagombea wa nafasi hiyo alisema kuwa uchaguzi ndani ya chama umekwisha kinachofuata ni kuzitafuta kura za CCM.
Naye mgombea wa nafasi hiyo Abubakar Allawi alisema kuwa baada ya uchaguzi ndani ya chama kwisha watashirikiana na mgombea huyo kuhakikisha anashinda na nafasi nyingine za Urais na Udiwani ili chama kiendelee kushika dola.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani Hawa Mchafu alisema kuwa anawapongeza wawania nafasi ya ubunge hao kwa kuonyesha ushirikiano na kukipa urahisi chama kupata ushindi itakapofika Oktoba.
mwisho.
No comments:
Post a Comment