Hayo yamesemwa na Diwani wa Kata hiyo Karim Mtambo alipokuwa akiwasilisha utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kipindi cha miaka mitano 2020-2025.
Mtambo amesema kuwa anaishukuru serikali kwani imegusa sekta zote za kiamendeleo hivyo kufanya kero nyingi kupungua na wananchi kupata huduma kwa urahisi.
"Mfano hospitali ya Wilaya ya Lulanzi kwa sasa haina changamoto ya maji ikilinganishwa na kipindi cha nyuma na wananchi nao wanapata huduma ya maji kwa asilimia 95, ujenzi wa ofisi ya Kata ambapo iko hatua ya ukamilishaji",amesema Mtambo.
Amesema kuwa huduma za afya nazo zimetengewa fedha nyingi, miundombinu ya barabara nayo imeboreshwa, soko bado lina changamoto na kituo cha polisi nacho bado.
"Sekta ya elimu nayo imepatiwa fedha nyingi ambapo kwenye shule zetu za msingi miundombinu imeboreshwa na ufaulu umeongezeka ikilinganishwa na zamani,"amesema Mtambo.
No comments:
Post a Comment