Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini Mwajuma Nyamka wakati wa Mkutano Maalum wa Kata ya Maili Moja wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya miaka mitano.
Nyamka amesema kuwa kuna baadhi ya wanachana wa CCM wamekuwa wakibeza mambo yaliyofanywa na viongozi hali ambayo inawakatisha tamaa.
"Ilani inayotekelezwa ni ya CCM hivyo kuwabeza viongozi wake ni kuonyesha mnakataa yaliyofanyika kwani maendeleo ni suala la mchakato ambao ni wa muda mrefu,"amesema Nyamka.
Amesema kuwa chama kiliingia mkataba wa maendeleo na wananchi na kama kuna changamoto ni vema zikawasilishwa kwenye vikao maalumu kuliko kuwatolea maneno mabaya viongozi.
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi amesema kuwa anawashukuru wajumbe kwa kupitisha ilani ya kata hiyo licha ya tawi la Msufini kuwa na changamoto za miundombinu na afya.
Lutambi amesema kuwa changamoto hizo watazifanyia kazi kwa kushirikiana na wananchi na wataalamu mbalimbali wa Halmashauri ili kukabili changamoto za tawi hilo lililopo kwenye Mtaa wa Muheza
Kwa upande wake katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Method Mselewa amesema kuwa Kata hiyo imeandaa taarifa nzuri ambayo imeonyesha jinsi ilani ilivyotekelezwa.
Mselewa amesema kuwa chama kimefanya kazi kubwa na maendeleo hayawezi kupatikana kwa mara moja ni hatua ambapo kwa vile ambavyo havijakamilika vitafanyiwa kazi.
Naye Mke wa Mbunge huyo Selina Koka amesema kuwa wataendelea kushirikiana na wananchi katika suala la maendeleo ili kuhakikisha wananchi wanakuwa na ustawi.
Koka amesema kuwa kwa upande wa wanawake watahakikisha wanazifikia fursa mbalimbali ikiwemo za mikopo ya wanawake ili waweze kufanya shughuli za ujasiriamali ili wajikwamue kiuchumi.
No comments:
Post a Comment