Hayo yalisemwa Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Maendeleo ya Vijana (YPC) Israel Ilunde alipokuwa akizungumza na Mwandishi wa habari hizi.
Ilunde ambaye pia ni Mwentekiti wa Policy Forum alisema kuwa mbali ya miradi kushindwa kufanyika hata ajira kwa vijana hukosekana na hali hiyo huathiri bajeti ya nchi ambapo fedha nyingi hupotea.
"Watu wanaotorosha fedha haramu au utakatishaji wa fedha hufanya udanganyifu kwenye baadhi ya maeneo kwa wafanyabiashara hutumia hati za kibiashara kuweka gharama kubwa, kusafirisha bidhaa kutoka au kwenda nje ya nchi na kudanganya gharama za uendeshaji wa kampuni,"alisema Ilunde.
Alisema kuwa endapo sheria zitawabana watu hao itasaidia kulipa kodi halali kwani kupitia udanganyifu huo hawalipi kodi stahiki hivyo kuitia nchi hasara kubwa.
"Tungeomba sheria ziboreshwe ili kudhibiti watu hao kwa kuwa na mifumo ambayo itadhibiti utoroshwaji wa fedha haramu na watachukuliwa hatua kali za kisheria,"alisema Ilunde.
Aidha aliiomba serikali kuongeza bajeti kwa Wizara ya Habari Sanaa Utamaduni na Michezo ili waandishi waweze kupata mafunzo yatakayoweza kuwafichua watu hao wanaotumia fedha haramu na watu kulipa kodi kwa haki na wasifanye udanganyifu.
"Serikali mashirika yasiyokuwa ya kiserikali taasisi za elimu zitenfeneze vijana kuwa wazalendo watakaochukia udanganyifu ili fedha zinazotokana na kodi zilete maendeleo na itasaidia vijana kuwa na ajira,"alisema Ilunde.
Aliongeza kuwa athari zinazotokana na fedha haramu ni kuathiri sekta muhimu za kimaendeleo kama vile elimu, afya, kilimo na miundombinu na sekta nyingine.
"Vyanzo vinavyosababisha hali hiyo ya utoroshwaji wa fedha haramu ni pamoja na rushwa, hati za kibiashara, usafirishaji wa binadamu, usafirishaji wa madini na utakatishaji wa fedha,"alisema Ilunde.
No comments:
Post a Comment