Jungulu ameyasema hayo wakati akiongoza kikao cha uwasilishwaji wa utekelezaji wa ilani ya CCM ya miaka mitano iliyowasilishwa na diwani wa kata hiyo Karim Mtambo.
Amesema kuwa viongozi wamekuwa wakitoa majibu juu ya changamoto mbalimbali kwenye vikao vya chama hivyo kajibu hayo wayapatie na wananchi.
"Twendeni na kwa wananchi kupitia mikutano ya kila baada ya miezi mitatu tuwajibu wananchi maswali yao kwa kupokea kero zao na kuzitafutia ufumbuzi,"amesema Jungulu.
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Picha ya Ndege Karim Mtambo amesema kuwa anaishukuru serikali kwa kutoa fedha ambazo zimetekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mtambo amesema sekta zote zimeguswa na miradi hiyo na kufanya changamoto za wananchi kupungua huku serikali ikiendelea kutatua kero zilizopo.
No comments:
Post a Comment