Saturday, December 27, 2025

VIJANA WATAKIWA KULINDA NA KUTUNZA AMANI YA NCHI

MWANADIPLOMASIA Omary Punzi amewataka Vijana kulinda na kutunza amani umoja uzalendo na mshikamano katika nyakati zote ili kuleta Maendeleo ya Taifa.

Punzi ameyasema hayo katika Bonanza la Michezo kwa Vijana liliratibiwa na Kamati ya Vijana Wazalendo Bonanza lililofanyika kwenye viwanja Soko la Ndizi vya Mabibo (Las Vegas) Jijini Dar es Salaam

Punzi ambaye pia ratibu wa Makongamano amesema kuwa lengo la Bonanza hilo ni kuhimiza amani na utulivu nchini. 

Kwa upande wake Mgeni rasmi katika Bonanza hilo Mwenyekiti wa Mtaa wa Jitegemee  Abdallah Kilema aliwaomba vijana wapende michezo na kuwakumbusha michezo ni Ajira Upendo na Afya hivyo wanamichezo wanawajibu wa kutunza amani ya Taifa.

Naye mratibu kutoka mtandao wa YAS Neema aliwaomba vijana wajitokeze kwa wingi katika fursa mbalimbali za kimaendeleo na wao kama Taasisi wataendelea kudhamini mashindano mbalimbali.

Aidha Gervas Pai alishukuru kwa maandalizi mazuri na vijana kuwa na uwezo mkubwa na kuomba walinde Amani, Umoja na Mshikamano wa Taifa na wajitokeze kwa wingi kushiriki michezo.

Kocha wa Timu ya 7 lite Zayd Rashid aliwaomba wadau wa michezo waendelee kuongeza nguvu katika kuwatafutia vijana vifaa vya michezo ambavyo ni kero kubwa na kumshukuru muaandaji wa Bonanza hilo. 

Naye mchezaji Isack Rashid mchezaji bora wa mashindano hayo anesema kuwa ndoto yake ni kuwa mchezaji mkubwa hapa Tanzania ili kuweza kusaidia nchi yake 

Kwenye Bonanza hilo michezo ya vijana chini ya miaka15 kati ya Las Vegas na 7 lite mshindi ni 7 lite 4-0 mchezo wa pili ilikuwa kati ya Las Vegas na 7 lite ambapo Las Vegas imeshinda magoli 3-2

Mshindi wa kwanza alipatiwa mipira 5 na mshindi wa pili mipira 2 kwa upande wa mchezaji bora na goli kipabora kila mmoja aliibuka na shilingi 5,000.Bonanza hilo likishirikisha timu nne za Las Vegas na 7 lite miaka 15 na Las Vegas na 7 lite chini ya miaka 20.

No comments:

Post a Comment