Monday, December 22, 2025

KIDULI YAJISAFISHIA NJIA NUSU FAINALI DARAJA LA TATU MKOA WA PWANI

TIMU ya Kiduli imejihakikishia kuingia hatua ya nusu fainali ya ligi daraja la tatu Mkoa wa Pwani kutoka kundi A baada ya kuifunga Anga kwa magoli 3-2.

Katika mchezo huo ambao ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Kibaha Kiduli ilifunga goli la kuongoza kwa bao lililofungwa na Amrani Mkumbo dakika ya 53 ya mchezo.

Kiduli waliongeza goli la pili lililofungwa na Jonathan Martin dakika ya 63 hata hivyo Anga walirudisha magoli yote ambayo yalifungwa na Elia Nduligu dakika ya 76 na Hussein Haruna alisawazisha dakika ya 85.

Huku kila mtazamaji akiamini kuwa mchezo huo utamalizika kwa sare ya magoli 2-2 Benjamin alipigilia msumari wa mwisho dakika ya 90+5 na kuamsha shangwe kwa mashabiki wa Kiduli.

Kwa matokeo hayo Kiduli inaongoza kundi hilo ikiwa imejikusanyia alama 6 huku ikiwa na mchezo mmoja mkononi na kesho itakuwa ni mchezo kati ya Bagamoyo Sugar na Nyika kutoka kundi B mchezo utakaokuwa na ushindani mkali.

Kundi A lina timu za Kiduli, Anga South Academy na Kampala huku kundi B likiwa na timu za Bagamoyo Sugar, Nyika na Kibaha Mji.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) Nasoro Shomvi "Mbilinyi amesema kuwa hatua ya nusu fainali itachezwa Desemba 30 na 31


No comments:

Post a Comment