Friday, June 13, 2025

SUBIRA MGALU ATOA GARI KWA (UWT) BAGAMOYO

MBUNGE wa Mkoa wa Pwani Subira Mgalu ameupatia gari uongozi wa Jumuiya ya Wanawake CCM kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Akizungumza wakati wa kukabidhi gari hilo aina ya Noah Mgalu amesema kuwa moja ya nadhiri aliyojiwekea kipindi cha nyuma ilikuwa ni kuhakikisha anainunulia chombo cha usafiri Jumuiya hiyo ili kurahisisha utendaji kazi.

Mgalu amesema kuwa ni vyema gari hilo likatumika kutafuta kura za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan huko kwenye matawi kwa kuwakumbusha wananchi kile kilichofanyika kwenye maeneo yao.

"Gari hili likatumiwe na Jumuiya zote za chama ikiwemo Wazazi na Vijana ili ziweze kufanikisha malengo ya chama chetu,"amesema Mgalu.

Akikabidhi gari hilo kwa Katibu wa  Wilaya ya Bagamoyo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mery Chatanda amempongeza  Mbunge huyo kwa jinsi ambavyo amekuwa akijitoa kwa Jumuiya hiyo.

Chatanda amewataka viongozi wa Bagamoyo kuhakikisha wanaitumia gari hiyo kwa makusudio yaliyokusudiwa ili kurahisisha shughuli za utendaji wa Jumuiya

No comments:

Post a Comment