DIWANI wa Kata ya Tumbi Halmashauri ya Mji Kibaha Raymond Chokala amesema fedha zilizotolewa na serikali kiasi cha shilingi bilioni 4.2 kwa kipindi cha miaka mitano zimeleta maendeleo makubwa kwenye Kata hiyo.
Akizungumza kwenye Mkutano wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji ilani kwa kipindi cha miaka mitano 2020-2025 kwa wanachama wa CCM na wananchi wa Mitaa ya Mwanalugali A na B Chokala amesema Kata hiyo imepiga hatua kubwa ya kimaendeleo.
Chokala amesema fedha hizo zimetumika vizuri kwenye sekta za elimu, afya, vikundi vya kiuchumi kupitia asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri, barabara, maji, umeme, kilimo na mifugo.
"Tunaishukuru serikali kwa kutupatia fedha hizo ambazo matokeo yake yameonekana kwani huduma zimeboreka licha ya changamoto chache ambazo zimeendelea kutatuliwa kulingana na bajeti inayopatikana,"amesema Chokala.
Amesema mafanikio hayo yametokana ushirikiano mkubwa ulioonyeshwa baina ya Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka, wananchi, viongozi na watendaji wa serikali bila kusahau chama tawala CCM ambao ndiyo wasimamizi wa ilani.
No comments:
Post a Comment