Friday, March 15, 2024

WATAKIWA KUONDOKA KUEPUKA MAFURIKO MTO RUFIJI

SERIKALI imetoa taadhari kwa wananchi waliopo katika wilaya za Rufiji na Kibiti unakopita Mto Rufiji kuondoka ili kuepuka athari za mafuriko  baada ya milango ya mradi wa uzalishaji wa umeme wa bwana la Mwalimu Nyerere kufunguliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge baadhi ya mashamba ya wananchi yameathirika kwa kuzingirwa na maji.

Kunenge amesema, baada ya maji hayo kufunguliwa, maji hayo yalizingira mashamba na kuharibu baadhi ya mazao ya wananchi na kwamba kwa sasa bado wananchi wanapaswa kuchukua tahadhari kubwa Iki kuthibiti maafa ikiwemo vifo visivyo vya lazima

"Bwawa Mwalimu Nyerere, limefurika kuliko matarajiyo yaliyo kuwepo,ambapo tulipokea taarifa kutoka wizarani na Shirika la umeme Tanzania Tanesco kwamba wanataka kufungua milango ya Bwawa ambapo tulitoa taarifa za tahadhari Kwa wananchi kuondoka maeneo hayo lakin baadhi hawakufanya hivyo hivyo nasisitiza waondoke katika maeneo hayo"amesema

Aidha amesema taarifa za kufunguliwa Kwa Bwawa hilo zitoleea kuanzia Machi Mosi mwaka hadi zoezi Hilo lilipofanyika  Machi 05, majira ya saa 9:00 alasiri ambapo kina cha maji kilichokuwepo ni mita za ujazo 
188.85 na kwamba mpaka sasa kimepungua na kifikia 183.45 baada ya kufunguliwa

No comments:

Post a Comment