Friday, March 29, 2024

MWENYEKITI UVCCM WILAYA YA MPWAPWA AFURAHISHWA NA SOKA



Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Wilaya ya Mpwapwa Yohana Malogo ameendelea na ziara yake katika Kata ya Godegode kimagai na vingh'awe katika kijiji cha isingh'u

Akiwa katika kata ya Vingh'awe kijiji cha Ising'u ameshudia mechi Kati ya Miondo Fc dhidi ya Bondeni Fc

Ambapo amesema Mpira ni Mchakato na mwezi wa tano watakuwa na ligi ya Ngo'mbe

"Tumeona tufike hapa tuone mchezo wenu lakini pia tuwasalimie na tufahamiane"Amesema Malogo

"Tuwaombe tushirikiane,karibuni Ofisini kwetu ile Ofisi siyo ya kwangu,wala siyo ya katibu ni Ofisi yenu vijana Wilaya nzima yakuwasilisha changamoto na matatizo na adha zote zinazohusu vijana kwenye idara ya michezo na idara zingine"Amesema

Naye Katibu wa Umoja wa Vijana UVCCM Wilaya hiyo Alhabib Kibamba amesema kuwa kwa sababu ya serikali imesimama vizuri chini ya Chama Cha Mapinduzi ndo maana tuna amani na tunacheza tukiwa na furaha

Kwa Upande wake Diwani wa kata hiyo ya Vingh'awe Mahuwi Dickson amesema kuwa lengo la bonanza ni kuwaweka vijana pamoja,na Kujenga Mahusiano mazuri baina ya vijana

"Mashindano haya ni ya kata ni vijana ambao wanatoka katika eneo langu la kata mwisho wa siku nahitaji vijana hawa nipate timu bora ambayo sasa nitashirikisha na kata ya jirani"amesema

Aidha ameongeza kuwa mei mosi wataanza tena mashindano ya kushindania Ngo'ombe.

No comments:

Post a Comment