Wednesday, March 13, 2024

MADALALI WA KUPIGIA DEBE WAGOMBEA WATAKIWA KUACHA MARA MOJA



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Picha ya Ndege Wilayani Kibaha imewataka watu wanaojifanya madalali wa watu wanaotaka kugombea nafasi za uenyekiti wa serikali za mitaa waache kwani muda wa viongozi walio madarakani haujaisha.

Aidha kimewataka watu kuacha kuwasemea vibaya viongozi walioko madarakani kwani nikukiharibia chama kwani wanatokana na chama hicho.

Hayo yamesemwa na Katibu Mwenezi wa Kata ya Picha ya Ndege Said Namamba wakati wa ziara kwa mabalozi wa Kata hiyo.

Namamba amesema kuwa kuna baadhi ya watu wanajifanya wanawapigia debe baadhi ya watu wanaotaka kuwania nafasi za uongozi huku muda wa kuwania nafasi hizo ukiwa bado.

Naye Mjumbe Mkutano Mkuu kutoka Kata  Subira Said amesema kuwa wametumia fursa hiyo kuwafundisha mabalozi hao kujua wajibu na majukumu yao.

Said amesema kuwa pia wamewaelekeza namna ya kutunza kumbukumbu za wanachama na kuhifadhi taarifa mbalimbali za mashina yao na kutoa taarifa juu ya changamoto kwa balozi wanazoziongoza.

Kwa upande wake Katibu wa Hamasa wa Vijana wa Kata Lenatus Mkude amesema kuwa wao wanataka mabalozi wasikubali kupotoshwa na watu wanaotaka kuwatumia kuwapigia debe wakati muda haujafika.

Mkude amesema wao wanataka utaratibu wa chama ufuatwe ili mgombea atakayechaguliwa kupitia kura za maoni apeperushe bendera ya chama na siyo vinginevyo.


No comments:

Post a Comment