Monday, March 18, 2024

SERIKALI KUIWEZESHA SEKTA YA MADINI KUONDOA CHANGAMOTO WACHIMBAJI WADOGO WADOGO


 Na Wellu Mtaki, Dodoma 

Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuiwezesha sekta ya madini kwa kuchangia asilimia 10 kwenye pato la Taifa ifikapo mwaka 2025 kwa kuondoa changamoto zote zinazowakabili wachimbaji wa madini wadogo wadogo ili kuwezesha shughuli hiyo kuendelea kukua na kukuza uchumi wa nchi ambapo mpaka sasa mchango wa sekta ya madini kwenye pato la nchi umeongezeka kufikia asilimia 9.7

Akizungumza na waandshi wa habari  jijini Dodoma Mkurugenzi wa taasisi ya Tanzanite Fashion na Miss Utalii Eva Raphael amesema madini ya Tanzanite ambayo mauzo yake hufikia mpaka Dola Milioni hamsini kwa mwaka ndiyo upekee  wa kuadhimisha shughuli yetu hi Tanzanite Fashion week.

Aidha amesema kuwa kutakuwa  na  tamasha kubwa la Kitaifa la Tanzanite Fashion week linatarajiwa kufanyika tarehe 4 mwezi 5 Mwaka 2024 jijini Dodoma katika Ukumbi wa Mabeyo Complex. tamasha hilo litaenda kutangaza Utalii wa Madini na Mali asili mbalimbali zilizopo hapa nchini.

"Tunapenda kuwaalika wachimbaji mbalimbali wa Madini, wachimbaji Wanawake na vyama vyao vyote vya Madini, taasisi mbalimbali za kiserikali na binafsi kwenda kushirikiana na sisi katika wiki ya Tanzanite Fashion"Amesema

Aidha amesema kuwa wiki hiyo ni wiki iliyojaa Maudhui mengi,mafundisho pamoja na dhamira nyingi ya kwenda kuigusa jamii na kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Naye Afisa Utamaduni Wizara ya Utamaduni Sana na Michezo Alice John amempongeza Eva kwa ubunifu huo wa kuandaa tamasha hilo na kusema kuwa anaenda kuieleza na kutumia sanaa kama njia bora ya kufikisha ujumbe

"Tunamshukuru dada Eva kwa kuiona sanaa ni njia bora na anakwenda kutumia Sanaa kutangaza Madini"Amesema John

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kanzidata ya madini taasisi ya Jiologia na utafiti wa madini amesema kuwa Madini ya Tanzanite ndo Madini pekee yanayopatikana hapa nchini ndo maana ameyachagua katika wiki ya Tanzanite Fashion week tumeona ni vema kumuunga mkono ili tuweze kuyatangaza madini na Wizara ya Madini imeona  frusa hii ni bora kwa wachimbaji wadogo Wanawake.

No comments:

Post a Comment