Uchaguzi huo unafanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata ya Msangani Wilaya ya Kibaha Leonard Mlowe kufariki dunia hivi karibuni.
Kituka ameyasema hayo wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo kwenye uwanja wa Juhudi Msangani.
Amesema kuwa wamchague mgombea huyo wa CCM kwani ni mchapakazi mwadilifu na mwaminifu na wasipoteze muda kuchagua wagombea wa vyama vingine.
Mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini Mwajuma Nyamka amesema kuwa mgombea huyo ndiyo chaguo sahihi katika kuleta maendeleo kwa wananchi wa kata hiyo.
Nyamka amesema kuwa diwani aliyefariki aliacha mipango mingi ya maendeleo ambayo lazima iendelezwe na diwani anayetokana na CCM hivyo wasipoteze muda kuchagua mgombea wa chama kingine.
Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mussa Ndomba amesema kuwa Kata hiyo imetengewa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 900 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Ndomba amesema kuwa fedha hizo zimetengwa kwa ajili ya miradi mbalimbali kwenye sekta mbalimbali za kijamii.
Mkutano huo uliwahusisha madiwani viongozi wa chama wa ngazi mbalimbali na wanachama wa CCM pamoja na mbunge wa viti maalum Dk Allice Kaijage.
No comments:
Post a Comment