Hayo yamebainishwa tarehe 26 Machi 2024 wakati wa ziara ya Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Mpwapwa Yohana Malogo kukagua uhai wa Jumuiya, kusajili wanachama wapya
na kuhimiza ulipaji wa ada.
Walisema kuwa kilio cha maji katika Kata yao imekuwa ni changamoto kiasi cha kushindwa kujua tatizo hilo litaisha lini na serikali inampango gani kwao ili kukabili hali hiyo.
Kwa upande wake Fundi Mkuu wa Maji Geogre Francis Theophil amesema kuwa wapo baadhi ya wananchi wanakata mabomba ya maji usiku bila sababu yoyote kiasi Cha kwamba wanakwamisha swala la maji kupatikana Katika Kijiji hicho.
Theophil amesema kuwa kuna changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu kukata mabomba hali inayosababisha maji kumwagika chini.
Naye Diwani ya Kata ya Lupeta Sospeter Moonho amewahakikishia wananchi mradi wa maji tiririka kufika mwezi wa nne utaenda ili kusaidiia kumtua mama ndoo kichwani pamoja na kuwahakikishia wananchi pia wanaenda kuanza ujenzi wa jengo la zahanati.
Moonho amesema kuwa atahakikisha ujenzi wa jengo la zahanati linakamilika na kama hajakamilisha aulizwe.
Kwa upande wake Mwenyekiti umoja wa Vijana wa Chama Cha mapinduzi ( UVCCM) Yohana Malogo amewataka viongozi wa kata hiyo kuhakikisha mifuko iliyokopeshwa irudidishwe na ujenzi uanze na amewaomba kisima kijengwe kwenye kata hiyo.
Malogo amesema kuwa wanaenda kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wahakikishe wanawasaidia wananchi na kiasi cha fedha kilichopo ujenzi uanze kwani hakuna sababu kuweka fedha wakati wote huku wananchi wakitaabika.
Lengo ya ziara hiyo ya mwenyekiti wa UVCCM ni kukagua uhai wa Jumuiya, kukagua madaftari ya wanachama, kusajili wanachama wapya na ulipaji wa ada, kuhamasisha kufanyika semina kwa viongozi wa kata na Mitaa pamoja na kikao cha ndani na wanachama.
No comments:
Post a Comment