Friday, March 8, 2024

WANAWAKE WATAKIWA KUWA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

 

Na Wellu Mtaki, Dodoma

WANAWAKE nchini wametakiwa kutambua suala la matumizi sahihi ya fedha ili kuweza kujiongezea kipato zaidi na kujikwamua kiuchumi.

Hayo yameelezwa na  Mkurugezi Msaidizi sehemu ya usimamizi Rasilimali watu Wizara ya fedha Bi, Faudhia Nombo wakati akimwakilisha katibu mkuu wizara ya fedha katika  maonesho ya banda la wizara hiyo  leo Machi 7  siku ya ufunguzi  wa maonyesho ya wanawake  kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani.

Nombo amesema wizara inaendelea kutoa Elimu kwa wanawake kujiandaa wakati wa kustafu kazi katika kipindi cha uzee pamoja na suala la kutunza fedha 

"Wizara haitokaa kimya ila itahakikisha inaendelea kutoa Elimu kwa wanawake ili pindi wanapostafu kazi wapate fedha za kujikimu kipindi chote cha uzee , wapo wanawake wanatumia fedha katika majukumu ambayo si sahihi na mwisho wa siku fedha hupotea na kuelekea mwisho mbaya uzeeni," amesema Nombo.

Aidha amesema kuwa wanawake wengi wanatamani kuingia katika vikoba ili kuweza kujikimu kiuchumi ila wanashidwa kutambua namna ya utunzaji wa fedha hivyo wizara imeona watoe mafunzo ya namna ya kutunza fedha katika maonesho ya siku ya wanawake Dunia.

Pia ametoa wito kwa wanawake wa Dodoma kutambua fursa zilizopo katika wizara hiyo na kutumia kiusahihi ili kufanikisha shughuli zao za kiuchumi.

No comments:

Post a Comment