Monday, March 18, 2024

UMOJA WANAWAKE VIONGOZI WATOA MSAADA HOSPITALI YA RUFAA DODOMA GENERAL

Na Wellu Mtaki, Dodoma 

Umoja wa Wanawake Viongozi na Viongozi wanaochipukia kutoka Taasisi mbalimbali (ESWLT) umetoa msaada wa vifaa mbalimbali katika 

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma General imepokea msaada wa vifaa mbalimbali kutoka  Umoja wa Wanawake Viongozi na Viongozi wanaochipukia kutoka Taasisi mbalimbali (ESWLT)   ikiwa ni katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa Machi 8 kila mwaka.

Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo Hospitalini hapo na kutembelea katika wodi ya wakinamama Katibu wa Umoja huo Sakina Mwinyimkuu amesema kuwa kitendo cha kutoa vifaa hivyo ni miongoni mwa malengo yao ya kusaidia jamii.

Aidha amesema kuwa Umoja huo una lengo la kusaidia vijana Wanawake hasa mabinti ambao wanatarajia baada ya miaka kadhaa wataingia katika Utumishi katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya kusaidia jamii.

Pia ameongeza kuwa Kwa kupitia umoja huu wanawasaidia na kuwalea ili waweze kuwa wazalendo katika nchi pamoja na kulenga kutumia viongozi waliostaafu kwa kupata mazuri ambayo wamefanya na niwazoefu na kwa kupitia wao watajifunza zaidi katika eneo la uongozi

Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt.Grace Magembe ameushukuru umoja wa Wanawake hao kwa kuchagua eneo hilo kutoa msaada huo kwa sababu eneo walilolichagua ni eneo nyeti

"Kina mama wanaojifungua pamoja na watoto wao wanahitaji Sana mashuka ambayo safi ili kuzuia maambukizi ya magonjwa"Amesema

Aidha amewaahidi Wanawake wa Umoja huo kwa niaba ya Wizara ya Afya kuwa wataendelea kujituma,na Siku nyingine wasisite kwenda kutoa msaada.

No comments:

Post a Comment