Sunday, March 31, 2024

KANISA LATAKIWA KUWEKEZA KWA WANAWAKE





Na Wellu Mtaki,Dodoma.

Askofu wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Central Tanganyika Dodoma Dr. Dickson Chilongani  amewataka wahumini wa kanisa hilo kuwekeza nguvu kazi kwa wanawake kwani ukiwekeza kwa mwanamke unakuwa umenufaika.

Kauli hiyo ameitoa Leo Tarehe 31 March 2024 Katika kanisa la Dayosisi Central Tanganyika Dodoma wakati akilihubiria kanisa  kuhusu habari za yesu kristo Mleta Mageuzi pamoja na kueleza habari za kuwekeza Mwanamke kuharakisha Maendeleo.

Amesema kuwa lazima mkubali kwamba ukiwekeza kwa mwanamke mwisho wa yote inalipa ila kwa wanaume inaweza isikulipe na ifikiapo wakati unawaitaji wanaweza usiwaone kwenye itaji lako.

"Wekeza kwa wanawake: Harakisha maendeleo.” Kwa kauli mbiu hii wanawake walitaka watambuliwe na waaminiwe zaidi kuwa wanaweza. Na hapa tena siku ya pasaka tunawaona wanawake wakiwa mstari wa mbele. Saa 12 Alfajiri wakati wanaume bado wanachapa usingizi, Mariamu Magdalene, Mariamu mamaye Yakobo na Salome wanakwenda kaburini na manukato ya thamani ili kuupaka mwili wa Yesu. Wanafanya hivi kwavile Yesu aliposulubiwa, sabato ilikuwa inakaribia na kwahiyo mazishi yalikuwa ni ya haraka haraka, hawakuwa na muda wa kuuandaa mwili wake kwa maziko" Amesema Chilongani.

"Kwahiyo saa 9 mchana Yesu anapokata roho, wanaoshuhudia kifo chake ni wanawake. Inapofika jioni, Yesu anapozikwa, wanaoshuhudia kaburi na mazishi yake ni wanawake. Wanaume wameingia mitini" amesema Chilongani

Aidha amehisihi jamii kuwe na usawa ambao utasaidia kumuwesesha mwanamke kujiamini Katika kujikomboa  kimaisha kwani kumekuwa na mageuzi makubwa sana kwa wanawake na hii ndio inahashiria wanawake wanaweza kuongoza .

"Haya ni mageuzi makubwa sana, kwavile wakati huu wa Yesu Israeli ilikuwa ni nchi yenye mfumo dume na ukilitimba uliokithiri kwelikweli dhidi ya wanawake. Mwanamke alikuwa si kitu. Ndio sababu hata katika Yohana 6 tunasoma kwamba Yesu alilisha watu 5000 kwa samaki 2 na mikate 5. Lakini waliohesabiwa walikuwa ni wanaume peke yao, wanawake hawakuhesabiwa. Ni kana kwamba walikuwa si binadamu. " Amesema Chilongani

Pia amesisitiza wahumini wa kanisa hilo watambue kuwa mwanamke ni mtekekezaji mzuri wa majukumu na hanahakikisha anafanya kazi kwa weledi bali wapo watu ambao awana imani naye na hao ndio wanapelekea kushusha uchumi wa mwanamke kiujumla.

"Na hata katika mahakama za Israeli ushahidi wa mwanamke kisheria ulikuwa haukubaliki. Lakini bado Yesu anawafanya wanawake kuwa mashahidi wa kufufuka kwake na anawatuma wawaambie wanafunzi wake waende Galilaya watamkuta" amesema Chilongani.

Aidha amewataka wahumini wamtangulize Mungu Katika maitaji ya maombi Yao na waachane na tabia ya kupanga aina ya maitaji wanayoyataka kwa Mungu Bali wamwache Mungu atatenda mwenyewe.

"Ni lazima tujifunze kumtanguliza Yesu Kristo na siyo kumtangulia. Askofu Mkuu mstaafu marehemu John Ramadhani aliwahi kusema: “Wakristo wengi badala ya kumtanguliza Roho Mtakatifu wanamtangulia”. Mtu badala ya kumwomba Mungu ampe mke mwema, anampa Mungu masharti kwamba anataka mke mweupe tena mwenye mwanya. Huko ni kumtangulia Mungu. Badala ya kuomba gari, anaomba Scania, wakati hata baiskeli yenyewe hana. Huko ni kumtangulia Mungu. Kumtanguliza Mungu ni kumwomba mke au gari na kuacha mapenzi yake mema yatimizwe" amesema Chilongani 

Pia  hamewahimiza wanawake kuwania nafasi mbalimbali za uongozi Katika ngazi ya kanisa na serikali kwa ujumla na kuzingatia usawa wa kijinsia.

"Somo linatutaka tuwaamini wanawake na tuthamini mchango wao katika kanisa na jamii. Katika kanisa mwaka huu Dayosisi yetu ina mkutano mkuu (sinodi), na tumeanza chaguzi mbalimbali katika ngazi zote. Ningeomba sana kuwe na usawa. Zisiwepo nafasi za wanaume peke yao na za wanawake peke yao" amesema Chilongani 

"Katika taifa, chaguzi pia zimeanza kufanyika kuelekea kwenye uchaguzi mkuu. Ni vyema kuwe na usawa, tuwaamini wanawake. Kubwa zaidi, kumekuweko na baadhi ya wanaume wanaomzodoa Rais Samia kana kwamba hawezi lolote kwasababu tu ni mwanamke. Ni kana kwamba hawaoni kazi ambazo Rais wetu amezifanya katika kipindi chake hiki kifupi cha uongozi. Watu wa jinsi hii ni wabinafsi na hawatufai katika jamii" amesema Chilongani 

Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu ni kanisa la Kiuaskofu katika Dayosisi ya Central Tanganyika. Dayosisi ya Central Tanganyika ilianzishwa mwaka 1927. Ilikatwa kutoka Dayosisi ya Mombasa. Kabla ya hapo Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, Burundi na DRC Congoeneo lote hili lilikuwa chini ya umisheni wa CMS Afrika na kujulikana kama Dayosisi ya Eastern Equatorial Africa na Askofu wa kwanza alikuwa James Hannington (1884 – 1885). Huyu alikuwa shahidi wa kwanza baada ya kuuwawa na Kabaka Mwanga katika eneo la Busuga nchini Uganda 29/10/1885.

BONANZA LA WIZARA YA FEDHA BARA NA VISIWANI LAFANA





Na Wellu Mtaki, Dodoma

Bonanza la mpira wa miguu, kuvuta kamba na mpira mikono limefanyika leo Jijini Dodoma likiwashirikisha watumishi mbalimbali wa Wizara ya Fedha kutoka Bara na Visiwani.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala rasilimali watu Wizara ya Fedha Lusius Mwenda amesema kuwa lengo la bonanza hilo ni kudumisha ushirikiano na undugu kati yao.

Na kusema kuwa kuna tija inayopatikana ikiwemo kuimarisha urafiki wa pande zote mbili, kufahamiana na kuimarisha afya za Watumishi.

"Lengo kubwa katika mashindano ni Ushirikiano kati yetu,sisi huku Tanzania  Bara na wenzetu wa Zanzibar".

"Tija kubwa ambayo inapatikana ni pamoja na watumishi kuimarisha afya, kufahamiana  na kuwa na urafiki wa pande zote mbili, kwa mfano kwa sisi kwenda kule Zanzibar na wao kuja huku kama ambavyo tumekuwa tukifanya".

Akizungumza Mwakilishi kutoka Zanzibar Bwana Rajab Uweje ofisa Uendeshaji Ofisi ya Raisi fedha na mipango Zanzibar amesema kuwa  Tamasha hilo ni ishara nzuri tumelikuta na hivyo tuliendeleze.

"Kwanza bonanza hili tunajenga uhusiano baina yetu nichukue nafasi hii kuzishukuru Taasisi zetu mbili kutudhamini katika Tamasha hili na hiki ni kitu chema sana tumekikuta na hivyo kwahiyo tukiendeleze kwa vizazi vyetu".

Mwenyekiti wa Hazina Sports Club Mugusi Musita amezungumzia suala la mikakati ya uboreshaji wa Tamasha hili kwa muda mrefu ikiwemo kuongeza wigo wa timu shiriki katika Tamasha hili ambapo kwa mwaka huu wamefaniki na kuweza kuongeza timu mpaka kufika sita.

"Kawaida huwa tunacheza Hazina ya Tanzania Bara na Zanzibar lakini mwaka huu tumekuwa na timu sita kwa hiyo mikakati tuliyoiweka ni kuboresha kama kuongeza timu umeona kama polisi walikuwepo hapa lakini kujenga mahusiano mazuri na wenzetu sisi kama Wizara za Kimuungano wenzetu wa visiwani tunafanya kazi moja na ndo tunaboresha mahusiano na kuboresha afya".

Tamasha hili la Pasaka limekuwa likifanyika kwa zaidi ya miaka ishirini mpaka sasa.

Saturday, March 30, 2024

VIONGOZI WAASWA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI WAO - RAS MMUYA.


Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Kaspar Mmuya ameendelea na ziara yake ya kikazi ya ukaguzi wa miradi na kuongea na watumishi kwa lengo la kujitambulisha Katika Halmashauri za Mkoa wa Dodoma ambapo Leo Machi 28, 2024 ametembelea Halmashauri ya Wilaya ya Dodoma Mjini.

Kufuatia uzinduzi wa kampeni ya "Kero yako wajibu wangu", Mmuya ameendelea kuwa sisitiza watumishi kuwa na wajibu wa kusikilza na kutatua kero za wananchi kwa nafasi zao. Hayo ameyasema katika Kikao chake na watumishi wa Halmashauri hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Umonga Jijini Dodoma.

“Ni vyema kujua vipaumbele na  wajibu wako wa Kusikiliza Kero za wananchi wanaotuzunguka tukiwa wawakilishi wao na uongozi mliopewa una jukumu la kutatua kero za wananchi katika Mitaa yetu na dhana ya kuwajibika inaenda Sabamba na utaratibu na kuipa ubora kazi yako.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anawajibika ipasavyo kwa kuleta fedha za miradi katika jamii na kama Msimamizi wa hizo fedha unapaswa kuzingatia ubora wa majengo yanayojengwa na kama kiongozi wajibu wako ni kuhakikisha hizo fedha zinatumika vizuri kama ilivyoelekezwa na usiwe chanzo cha kuwa kero kwa wengine," Amesema. Mmuya.

Vilevile, ametilia mkazo suala la kuongeza ufaulu mashuleni, kuondoa utoro kwa wanafunzi, upandaji na utunzaji miti, mahusiano bora mahala pa kazi, uwajibikaji katika kila ngazi aliyonayo mtu.

Aidha, Katibu Tawala Mkoa amekagua mradi wa ujenzi wa Madarasa 08 na matundu 10 ya vyoo kwa ajili ya wanafunzi wa Kidato cha tano katika shule ya Sekondari Mtumba iliyopo kwenye kata ya Mtumba ambayo ilipokea fedha kiasi cha shilingi Milioni 201.

Mradi mwingine ni ujenzi wa vyumba 08 vya madarasa na matundu 10 ya choo katika shule ya Sekondari Zulu iliyopokea kiasi cha shilingi Milioni 201 na ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya iliyopokea shilingi Bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Maabara, jengo la wagonjwa wa nje ( OPD), jengo la mama na mtoto, Jengo la Mionzi, Jengo la Dawa, jengo la kuhifadhia maiti na kichomea taka.

Friday, March 29, 2024

*DKT.SHEMWELEKWA AWAFUNDA WATUMISHI KIBAHA.*

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa siku ya Jumatano 27 Machi,2024 amefanya kikao rasmi na watumishi kwa lengo la kufahamiana, kujitambulisha na kutoa mwelekeo kiutendaji.

Dkt.Shemwelekwa aliyeteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan tarehe 13 Machi,2024 kuwa Mkurugenzi wa Kibaha Mji amesifu mifumo mizuri iliyowekwa na Watangulizi wake akiwemo Bi.Jenifa Omolo ambaye kwa Sasa ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mhandisi Mshamu Munde aliyehamishiwa Halmashauri ya Nanyamba na kwamba kazi yake Sasa ni kutengeneza kemia mpya itakayotumika ili kufikia malengo ya Serikali ya kuwahudumia wananchi 

Dkt.Shemwelekwa amewataka watumishi kutoa huduma Bora kwa wananchi wakiwa na furaha,kuondoa hofu,woga na wasiwasi na kwamba unapokuwa ofisini mwananchi ana matumaini makubwa nawe ya Kusikilizwa na kutatuliwa changamoto zake.

Aidha,Dkt.Shemwelekwa amewaasa watumishi kuwa wanyenyekevu kwa wananchi,kutumia lugha za staha,kuheshimiana,kushirikiana,kupendana na kusaidiana ili kufanya kazi zenye matokeo na zinazoacha alama za kukumbukwa huku akikemea vikali tabia za kufanyakazi kwa mazoea zisizokuwa na tija kwa Taifa letu.

"Watumishi wa Umma tuache kulalamika,tujielekeze kwenye kuondoa malalamiko na kero za wananchi.Tuwasikilize vizuri na kuwahudumia tukiwa na furaha"...amesema Dkt.Shemwelekwa.

Akizungumzia ukusanyaji wa Mapato ametoa rai kwa watumishi wote kushiriki na sio kuwaachi Kitengo cha fedha na Divisheni ya Biashara pekee kama ilivyozoeleka huku akitoa rai ya kuongeza uadilifu,uaminifu na kuziba mianya yote inayovujisha ama kuchepusha Mapato na kwamba atakayefanya hivyo hata mvumilia.

"Ndugu zangu tukakusanye Mapato kwa uaminifu na uadilifu ili yatumike kwa Maslahi mapana ya watu wote,atakaye thubutu kwenda kinyume atakumbana na mkono wa sheria" ameongeza

Dkt.Shemwelekwa amekumbusha watumishi kuwahi Kazini kama sheria,Kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma zinavyoelekeza na kwamba hiyo sio hiari ni takwa la Kisheria linalomtaka mtumishi kufanya kazi kwa saa nane kwa siku

Mary Chimoto na Hassan Ngonyani  wamesifu utaratibu mpya kiutendaji wa Mkurugenzi Dkt.Shemwelekwa na kwamba kilichobaki ni utekelezaji 

Mkuu wa Divisheni na Utumishi na rasilimali watu Dibogo Protas amesema kazi yake kwenda kutafsiri sheria,Kanuni na taratibu kwani watumishi Sasa wamekumbushwa upya wajibu wao.


Dkt.Rogers Shemwelekwa ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutumiza miaka mitatu Madarakani kwa kuendelea kuwekeza kwenye Miradi mikubwa ya Kimkakati nchini ikiwemo Kibaha Mji ambayo imenufaika na Soko kubwa lenye thamani ya Bilioni nane

MWENYEKITI UVCCM WILAYA YA MPWAPWA AFURAHISHWA NA SOKA



Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Wilaya ya Mpwapwa Yohana Malogo ameendelea na ziara yake katika Kata ya Godegode kimagai na vingh'awe katika kijiji cha isingh'u

Akiwa katika kata ya Vingh'awe kijiji cha Ising'u ameshudia mechi Kati ya Miondo Fc dhidi ya Bondeni Fc

Ambapo amesema Mpira ni Mchakato na mwezi wa tano watakuwa na ligi ya Ngo'mbe

"Tumeona tufike hapa tuone mchezo wenu lakini pia tuwasalimie na tufahamiane"Amesema Malogo

"Tuwaombe tushirikiane,karibuni Ofisini kwetu ile Ofisi siyo ya kwangu,wala siyo ya katibu ni Ofisi yenu vijana Wilaya nzima yakuwasilisha changamoto na matatizo na adha zote zinazohusu vijana kwenye idara ya michezo na idara zingine"Amesema

Naye Katibu wa Umoja wa Vijana UVCCM Wilaya hiyo Alhabib Kibamba amesema kuwa kwa sababu ya serikali imesimama vizuri chini ya Chama Cha Mapinduzi ndo maana tuna amani na tunacheza tukiwa na furaha

Kwa Upande wake Diwani wa kata hiyo ya Vingh'awe Mahuwi Dickson amesema kuwa lengo la bonanza ni kuwaweka vijana pamoja,na Kujenga Mahusiano mazuri baina ya vijana

"Mashindano haya ni ya kata ni vijana ambao wanatoka katika eneo langu la kata mwisho wa siku nahitaji vijana hawa nipate timu bora ambayo sasa nitashirikisha na kata ya jirani"amesema

Aidha ameongeza kuwa mei mosi wataanza tena mashindano ya kushindania Ngo'ombe.

Wednesday, March 27, 2024

BMH YAITEMBELEA WIZARA YA AFYA NA HOSPITALI YA LUMUMBA ZANZIBAR

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma inatarajia kuanzisha ushirikiano wa matibabu na Hospitali ya Rufaa ya Mjini Magharibi (Lumumba), Zanzibar katika huduma za kibingwa. 

Ushirikiano huu utalenga kubadilishana uzoefu kati ya Hospitali hizi mbili za umma.

Akiongea, Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mhe.Hassan Khamis Hafidh, amepongeza ujio wa Viongozi wa BMH na kuwa Hospitali ya Lumumba itanufaika kwa kubadilishana uzoefu.

"Nimefika Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma nikajionea utayari wa Madaktari Bingwa na Vifaa vya kisasa mnavyovitumia, nimefika kwenye wodi maalumu ya Uloto nikiri kwamba naona fahari kuja kwenu hapa maana yapo mengi tutakayo chukua kupitia ushirikiano huu," amesema Mhe Naibu Waziri.

Ameyasema hayo wakati uongozi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa ulipomtembelea ofisini kwake.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bi. Prisca Lwangili, akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa BMH, amesema "Hospitali ya Benjamin Mkapa imekuwa kwa kasi na kutoa matibabu ambayo hayapatikani Afrika Mashariki na Kati.

"Hivyo tumeona ni muhimu kusogeza huduma hizi hapa Zanzibar kwa kuwa hapa pia kuna uhitaji wa huduma za Upandikizaji Uloto ili kutibu seli mundu," amesema. 

Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Mafunzo wa BMH, Bi. Monica Kessy, uhusiano huu ni sehemu ya wajibu wa BMH ili kubadilishana uzoefu kati ya hospitali za umma.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji BMH, Dkt. Januarius Hinju, ameeleza utayari kwa Madaktari Bingwa wa BMH katika huduma.

"Madaktari Bingwa wa BMH tupo tayari kushirikiana na wenzetu ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora," ameongeza.

WANAFUNZI WAASWA KUZINGATIA NIDHAMU


Juma la wadau wa Elimu Mkoa wa Dodoma limehitimishwa kwa viongozi mbalimbali  wa Mkoa wa Dodoma kuzungumza na kushiriki chakula cha mchana na wanafunzi wa Shule za kidato cha sita za Mkoa huo.

Kwa nyakati tofauti akiwa katika shule ya Sekondari ya wavulana Kongwa na Shule ya wasichana Kibaigwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amewaasa wanafunzi hao kuendelea kudumisha nidhamu hususani katika kipindi hiki wanachojiandaa na mitihani yao na kuachana na marafiki wasiofaa ambao watawasababishia matokeo yatakayogharimu maisha ya ndoto zao.

"Tunataka alama A zenye hapa kuna wenzenu wamechafua jina la Shule na nyie mliopo hapa tunategemea nyie mtabadilisha sura hii ambayo sio njema kwa Mkoa, acheni tabia ya kufuata mkumbo kwa kushawishiana mambo yasiyofaa kwasababu kila mtu ana ndoto yake na kila moja atarudi nyumbani kwao kivyake na usipokuwa makini utaharibu maisha yako kwa mikono yako mwenyewe kwasababu tuu ya ushawishi usiofaa kutoka kwa marafiki zenu.

"Lazima muamue kuachana na baadhi ya mambo na kufuata miongozo yenu na kufanya bidii ili kujitofautisha na wengine na kuongeza ufaulu wenu na kujenga dhana nzuri ya shule Bora ni lazima muwe na ufaulu bora na Shule hii ambayo nyie ndio waanzilishi itapata sifa nzuri na sisi kama Mkoa tunayo matarajio kutoka kwenu kupitia matokeo mazuri mtakayotuletea," ameasa Senyamule

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon amewataka wanafunzi hao kuendelea  kujitunza vizuri  kwa kujiweka bize na masomo na shughuli za kielimu ili kuepukana na vishawishi mbalimbali vitakavyowafanya kupata ufaulu usiofaa na kujenga picha mbaya ya shule yao.

Kwa upande wake ofisa Elimu Mkoa  Mwl. Vincent Kayombo amesema Mkoa wa Dodoma unaendelea na maandalizi ya kuhakikisha Mkoa unapata matokeo mazuri katika mitihani ya kidato cha sita inayotarajiwa kufanyika kuanzia Mei 6, Mwaka huu.

Aidha Mwl.Kayombo ameweka bayana kuwa Mkoa umefanya maandalizi ya kuhakikisha wanafunzi wa shule zenye kidato cha sita za Mkoa huo wanashiriki chakula cha mchana na viongozi mbalimbali ikiwa ni katika kuwahamasisha, kuwatoa hofu na kuwajengea ujasiri wanafunzi hao katika kuelekea mitihani yao ya kuhitimu ngazi hiyo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon amewataka wanafunzi hao kuendelea  kujitunza vizuri  Kwa kujiweka bize na masomo na shughuli za kielimu ikiwemo michezo ili kuepukana na vishawishi mbalimbali vitakavyowafanya kupata ufaulu usiofaa na kujenga picha mbaya ya shule yao.

KATA YA LUPETA WALILIA MAJI

Wananchi wa Kijiji Cha kata Lupeta wilaya ya Mpwapwa Jijini Dodoma  wameiomba serikali kuwapelekea huduma ya maji ili kukabili changamoto hiyo.

Hayo yamebainishwa tarehe 26 Machi 2024 wakati wa ziara ya Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Mpwapwa Yohana Malogo kukagua uhai wa Jumuiya, kusajili wanachama wapya
 na kuhimiza ulipaji wa ada.

Walisema kuwa kilio cha maji katika Kata yao imekuwa ni changamoto kiasi cha kushindwa kujua tatizo hilo litaisha lini na serikali inampango gani kwao ili kukabili hali hiyo.

Kwa upande wake Fundi Mkuu wa Maji Geogre Francis Theophil amesema kuwa wapo baadhi ya wananchi wanakata mabomba ya maji usiku bila sababu yoyote kiasi Cha kwamba wanakwamisha swala la maji kupatikana Katika Kijiji hicho.

Theophil amesema kuwa kuna changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu kukata mabomba hali inayosababisha maji kumwagika chini.

Naye Diwani ya Kata ya Lupeta Sospeter Moonho amewahakikishia wananchi mradi wa maji tiririka kufika mwezi wa nne utaenda ili kusaidiia kumtua mama ndoo kichwani pamoja na kuwahakikishia wananchi pia wanaenda kuanza ujenzi wa jengo la zahanati.

Moonho amesema kuwa atahakikisha ujenzi wa jengo la zahanati linakamilika na kama hajakamilisha aulizwe.

Kwa upande wake Mwenyekiti umoja wa Vijana wa Chama Cha mapinduzi ( UVCCM) Yohana Malogo amewataka viongozi wa kata hiyo kuhakikisha mifuko iliyokopeshwa irudidishwe na ujenzi uanze na amewaomba kisima kijengwe kwenye kata hiyo.

Malogo amesema kuwa wanaenda kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wahakikishe wanawasaidia wananchi na kiasi cha fedha kilichopo ujenzi uanze kwani hakuna sababu kuweka fedha wakati wote huku wananchi wakitaabika.

Lengo ya ziara hiyo ya mwenyekiti wa UVCCM ni kukagua uhai wa Jumuiya, kukagua madaftari ya wanachama, kusajili wanachama wapya na ulipaji wa ada, kuhamasisha kufanyika semina kwa viongozi wa kata na Mitaa pamoja na kikao cha ndani na wanachama.

Tuesday, March 26, 2024

SERIKALI KUFUATILIA SUALA LA ELIMU NCHINI

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Maofisa Elimu Kata nchini kufuatilia maendeleo ya shule kwa kuwatembelea walimu na kusikiliza kero zao

Aidha amewataka walimu kuhakikisha wanafanya tathmini ya uelewa wa wanafunzi kwa kuwapatia mazoezi mengi.

Majaliwa ameyasema hayo Machi 25, 2024   kwenye ukumbi wa TAG Mipango Jijini Dodoma wakati wa kilele cha Juma la wadau wa Elimu Mkoa.

Amesema maofisa elimu hao wafuatilie masuala ya walimu na kutatua changamoto zao ili wafanye kazi vizuri.

"Walimu nanyi hakikisheni mnafanya tathmini ya uelewa wa wanafunzi kwa kuwapatia mazoezi mengi kadri iiwezekanavyo,"amesema Majaliwa.

Fedha zinazotolewa kwa ajili ya maendeleo ya Elimu, zitumike kwa ajili hiyo,"amesisitiza Majaliwa.

Amebainisha kuwa Kauli mbiu ya mkutano huo inakwenda sambamba na Sera ya Elimu ya nchi inayosisitiza Uwajibikaji, Utoaji wa Elimu Bora ni vipaumbele vya nchi. 

"Serikali yetu inaimarisha mazingira ya utoaji Elimu kwa kuboresha miundombinu na Elimu bila ada kwani mpaka Sasa shilingi Trilioni 1 zimetolewa kufanikisha hili,"amesema Majaliwa.

Waziri Mkuu ameipongeza Dodoma kwa kuandaa Mkutano huo kwani unakwenda sambamba na Sera ya Elimu ya nchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema Serikali ya awamu ya Sita imefanya mambo mengi kwenye sekta ya Elimu.

Senyamule amesema kuwa wanamshukuru Rais kwa kuinua sekta ya Elimu Dodoma kwani wameimarika sana kipindi cha miaka hii mitatu Dodoma imepanda ufaulu wa darasa la saba na kuingia kumi bora kitaifa mwaka 2022 kwa ufaulu kupanda kutoka 83% mwaka 2022 hadi 87%mwaka 2023 na wameanza kuweka mikakati ya Mkoa kuhakikisha kila mwaka ufaulu unaongezeka.

Ametaja mafanikio yaliyopatikana kipindi hiki kuwa ni ujenzi wa miundombinu ya elimu iliyogharimu shilingi bilioni 92.4 , miradi ya BOOST shilingi bilioni 10.6 iliyowezesha ujenzi wa madarasa 196 na matundu ya vyoo 154 fedha nyingine ni kutoka miradi ya SEQUIP, SWASH, TEA , EP4R na mingine mingi ambayo kwa pamoja imeboresha kiwango cha elimu.

Mkutano wa wadau wa Elimu Mkoa wa Dodoma umefuatia matukio kadhaa yaliyofanyika kwa Juma zima ikiwemo kukimbia mchaka mchaka kwa wanafunzi, uzinduzi wa Bonanza la michezo, ugawaji wa mipira 1000 kwa shule za Msingi za Mkoa kutoka Shirikisho la michezo nchini (TFF).

Pia Juma hilo limewezesha uzinduzi wa kwaya ya Mkoa wa Dodoma, midahalo kwa wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari na kufunga mafunzo kwa wahitimu wa skauti Mkoa.

Juma la wadau wa Elimu Mkoa wa Dodoma limefikia kilele chake likiongozwa na kauli mbiu ya "Uwajibikaji wangu ni msingi wa kuinua ubora wa Elimu na ufaulu Dodoma".

Lengo hasa la Mkutano huo ni kujadili namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya Elimu Mkoa wa Dodoma pamoja na kuweka mikakati ya kuinua Taaluma na ufaulu kimkoa pamoja na kuzindua rasmi Mpango Mkakati wa Elimu Mkoa.

Monday, March 25, 2024

VIONGOZI WAPYA WA KANISA WAPEWA NENO

Na Wellu Mtaki, Dodoma 

Viongozi wa kanisa la Dayosisi Central Tanganyika (DCT ) Mtakatifu Paulo Parishi ya Ndachi Dodoma wamewataka viongozi waliosimwikwa katika Kanisa hilo kuwa mfano ili kujenga jamii yenye maadili.

Hayo yamebainishwa na Mchungaji wa Parishi ya Ndachi Msalato Dodoma  Christopher  Njiliho  Leo Machi 24 ,2024 baada ya kumalizika kwa ibada ya kusimikwa kwa viongozi wa idara mbalimbali ndani ya kanisa hilo ambapo wamesema kuwa kanisa lina nafasi nzuri ya kujenga jamii bora.

"Ninawaomba sana viongozi muwe  wa kwanza kuacha dhambi, kuacha vitendo vibaya ili muende kufundisha wengine ukiwa mfano watu watakusikiliza sana na watapokea ujumbe ambao utawapelekea ili kuzuia vitendo viovu,"amesema Njiliho.

Aidha amesema kuwa kanisa linatakiwa kuwa mfano wa kuigwa ili kuhakikisha linajenga Vijana walio imara kwa kuzingatia maadili na taratibu za Taifa la Tanzania.

Kwa upande wake Mlezi wa idara ya kina Mama  Violeth Njiliho amesema kuwa Vijana wengi wamepotea kwa kukosa Maadili hivyo kama kanisa wanapenda kuhamasisha Vijana kushiriki semina mbalimbali ili kubadilisha mwenendo na kuongeza nguvu kazi kwa Taifa na kanisa .

"Vijana ni nguvu kazi ya Taifa pia ni nguvu kazi ya kanisa Vijana wengi wamepotea kwa kukosa maadili kama kanisa tunaenda kuhamasisha  Vijana wetu waweze kupata semina mbalimbali ili waondoke katika hatua waliyonayo ya utandawazi ili warudi kumtegemea Mungu,"amesema Violeth

Naye Mhasibu wa parishi ya Ndachi Amos Mchoro amesema kuwa kanisa linategemea kuanzisha mradi wa Ujenzi wa frem za maduka ambayo yatasaidia kuinua pato la kanisa na muumini mmoja mmoja kwa kutoa na fursa zitokanazo na mradi huo.

"Mpango tulionayo kwa ajili ya Vijana wa mitaani tunategemea kuanzisha mradi wa kufungua frem za biashara kwa ajili ya kukodisha waumini wote na ambao sio waumini,"amesema Mchoro

Pia amesema kuwa kanisa lipo kwenye mchakato wa kutafuta namna ya kukopeshwa mikopo kwa vijana ili kuhakikisha kila kijana ananufaika na mkopo huo ili kuweza kujikwamua kiuchumi.

"Tunakusanya Vijana ambao wapo mtaani ili kuwavuta walijue neno la Mungu pamoja na kutafuta fedha na kuanza kujikopesha kwa watu ambao wanasali katika kanisa hili na wasio wa kanisa hili,"amesema Mchoro.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Vijana Parishi ya Ndachi Msalato Timotheo Hoya amewataka Vijana wamtumikie Mungu na waachane na vitendo rushwa, wizi, ulawiti pamoja na matumizi ya madawa ya kulevya.

"Vijana wa kanisa wamtumikie Mungu kwa kipindi hichi madam Tanzania kwa sasa inakumbana na matatizo mbalimbali kama matatizo ya rushwa, ukatili , wizi,na matumizi ya madawa ya kulevya,"amesema Hoya.

Awali Mwenyekiti wa Idara ya watoto Joyce Jackson amewahimiza wazazi kuhakikisha wanawakuwakumbusha watoto kwenda kanisani ili kuweza kulishika neno na kulitambua ili kuondokana na vitendo viovu vya ulawiti kwa watoto.

"Mtoto akitembea na neno kwa njia ya haki huwezi kumfanyia ulawiti kutokana na mtoto kutambua vitu viovu na anaishi ndani ya maadili pia nawasihi wazazi wawalete watoto wao makanisani nashangaa kuona mzazi anamwacha mtoto chini ya miaka 15 nyumbani bila kumhimiza kufika kanisani," amesema Jackson.

Kanisa la Dayosisi Central Tanganyika (DCT) la Mtakatifu Paulo Parishi ya Ndachi Dodoma limesimika viongozi 70 katika idara mbalimbali huku likiwa linahudumia wazee vijana na watoto.

Friday, March 22, 2024

WALIOKIUKA SHERIA YA MADINI MAOMBI YAO KUFUTWA

 

WAZIRI wa Madini Antony Mavunde amesema wamiliki waliokiuka na kutotekeleza Sheria ya Madini maombi na leseni zao zitafutwa ili kupisha waombaji wengine kupata fursa ya kuomba maeneo hayo.

Ametoa taarifa hiyo Leo Tarehe 22 March 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wamiliki waliomiliki Maeneo ya uchimbaji wa Madini bila kuyafanyia kazi. 

Aidha amesema kuwa  kwa wamiliki wa akaunti za uombaji na usimamizi wa leseni kwa njia ya mtandao ambao wameonesha matumizi mabaya ya mfumo huo kwa kuwasilisha maombi kwa lengo la kuhodhi maeneo bila kuendelea na kuratibu upatikanaji wa leseni akaunti zao zitasitishwa. 

Amesema miongoni mwa makosa ambayo yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara ni pamoja na wamiliki wengi wa leseni kutoanza au kutoendeleza maeneo ya leseni zao na badala yake wanahodhi maeneo, hawalipi ada stahiki za leseni, hawawasilishi nyaraka muhimu kama Mpango wa Ushirikishwaji wa Watanzania

"Kutokana na kosa la kutolipa ada stahiki za leseni, kiasi cha takribani Shilingi bilioni 36 zinadaiwa kutoka kwa wamiliki na waliokuwa wamiliki wa Leseni za Utafutaji wa Madini, Leseni za Uchimbaji Mdogo wa Madini na Leseni za Uchimbaji wa Kati wa Madini,"amesema Mavunde.

Pia amesema kuwa Tume ya Madini imetoa Hati za Makosa kwa jumla ya leseni 59 kwa sababu wamiliki wake hawajatekeleza masharti na matakwa mbalimbali ya umiliki wa leseni husika Hivyo, taratibu za kufuta leseni hizo zinaandaliwa ili kuruhusu waombaji wengine kupata fursa ya kufanya uwekezaji.

"Vilevile katika uchambuzi uliofanya na Tume ya Madini imebainika kuwa, hadi Februari, 2024 kuna uwepo wa maombi 409 ambayo wamiliki wake wamelipa ada za maombi lakini hawajawasilisha nyaraka muhimu zinazoambatana na maombi hayo." Amesema Mavunde.

Katika atua ingine amesema kuwa uchambuzi uliofanywa na Tume ya Madini imebainika kuwa  hadi Februari, 2024 kuna jumla ya maombi 2,180 ambayo hayajalipiwa ada stahiki za maombi pamoja na kubaini kuwa kuna watumiaji watano (5) wa mfumo wa uwasilishaji wa maombi kwa njia ya mtandao ambao wamekuwa wakitumia mfumo vibaya kwa kuwasilisha maombi bila kulipa ada stahiki. 

Pia ametoa rai kwa wawekezaji wote wenye leseni za uwekezaji katika Sekta ya Madini kuzingatia matakwa ya Sheria ya Madini, Sura ya 123. 

Aidha, Wizara ya Madini itaendelea kuwapa ushirikiano wawekezaji wote wa ndani na nje ya nchi wenye nia ya kufanya uwekezaji wenye tija na kukuza uchumi wa taifa letu kutokana na uvunaji wa rasilimali madini.

SERIKALI KUHAKIKISHA UJENZI KIWANDA USAFISHAJI MADINI LINATIMIA

Na Wellu Mtaki Dodoma

Waziri wa Madini Anthony Mavunde amewataka wachimbaji wa madini hasa yaliyokuwa na changamoto ya uchenjuaji na kulazimika kusafirishwa kwa mfumo wa makinikia, kuendelea kushirikiana kikamilifu na Serikali ili kuhakikisha lengo la ujenzi wa kiwanda cha usafishaji madini linatimia na linabaki kuwa alama ya ushindi katika usimamizi wa sekta ya madini.

Waziri Mavunde ameyasema hayo  Machi 21,2024 Jijini Dodoma kwenye hafla ya kukabidhi leseni kubwa ya uchimbaji madini na leseni ya usafishaji madini ambapo ameongeza kuwa zoezi hilo linaenda kuongeza idadi ya leseni na kufikia 20.

“Ujenzi wa kiwanda cha multi metal refinery naamini itakuwa ni utatuzi wa changamoto iliyokuwepo kwa wachimbaji wa madini nchini kulazimika kusafirisha makinikia ya metali kwenda kwenye viwanda vya nje ya nchi kwa ajili ya uchakataji ili kupata zao la mwisho au kuuza madini katika hali ya makinikia kwa bei ya chini,”amesema Mavunde.

Aidha Waziri Mavunde ameongeza kuwa katika kuhakikisha kuwa changamoto zinazojitokeza kwenye sekta ya madini nchini Wizara inaendelea kufanya mazungumzo na wawekezaji wa nyanja mbalimbali ikiwemo utafutaji, uchimbaji na ujenzi wa viwanda vya usafishaji madini ili kuingia ubia na watanzania jambo litakaloongeza wigo wa upatikanaji wa mitaji, utaalam pamoja na uhaulishaji wa teknolojia.

“Nitumie nafasi hii pia kutoa wito kwa wachimbaji na wamiliki wa migodi inayozalisha makinikia nchini kutumia kiwanda hiki pindi kitakapo kamilika ili kukuza fursa za ajira na mapato yatokanayo na rasilimali madini, ameongeza Mavunde.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha amemuahidi Waziri wa Madini Anthony Mavunde kuwa atatoa ushirikiano kwa mamlaka zote katika kuhakikisha Fungani ya Buzwagi inakuwa na mafanikio makubwa kwa wananchi wa Wilaya ya Kahama.

RC Macha ameongeza kuwa wataendelea kuwahimiza wananchi wa Mkoa huo wa Shinyanga kuendelea kuchangamkia fursa zitakazojitokeza kupiti uwekezaji huo.

“Sambamba na uwekezaji mkubwa unaoenda kufanywa kule, na kama ambavyo tayari mmekwisha kunidokeza kuwa kampuni nyingi na kubwa zimekwisha onesha nia ya kuwekeza Mkoani Shinyanga sisi tunawihimiza wananchi wa pale wachangamkie fursa hii,”amesema.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt. Batilda Burian amesema kupitia uwekezaji huo uliofanywa na Serikali utaenda kuleta fursa mbalimbali kwa wananchi wa mkoa huo ikiwemo kujipatia ajira.

Thursday, March 21, 2024

WAANDISHI WAASWA KUHAMASISHA WANAWAKE KUSHIKA NAFASI ZA UONGOZI

WAANDISHI wa Habari nchini wametakiwa  kutumia kalamu zao kuhamasisha wanawake kushika nafasi mbalimbali za  uongozi na kwenye ngazi za maamuzi kwani uwekezaji kwa wanawake ni fursa na msingi wa kujenga jamii jumuishi. 

Hayo yamesemwa leo Machi Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Lilian Liundi wakati akifungua mafunzo kwa waandishi wa habari juu ya uandishi unaozingatia jinsia hasa juu ya kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika uongozi.

Liundi amesema kuwa Tanzania imeweka historia ya kuwa na Rais mwanamke kwa mara ya kwanza Dk Samia Suluhu Hassan ambaye ameonyesha dhamira ya kuongeza usawa wa kijinsia.

"Pia tumesha kuwa na Maspika wa Bunge wawili wanawake ambao ni Anne Makinda na Dk Tulia Ackson na mawaziri wanawake walioshika nafasi katika wizara zinazoaminika kuwa ni za wanaume kama Wizara ya Ulinzi-Stigomena Tax, Wizara ya Mambo ya nje, Liberata Mulamula pia katibu wa Bunge Nenelwa Mhambi pia historia ya kuwa na mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Zuhura Yunus,"amesema Liundi.

Kwa upande wake Ofisa Habari na Mawasiliano TGNP Monica John amesema kuwa wamekuwa wakishirikiana na wadau mbalimbali katika uchechemuzi juu ya sera na bajeti zinazozingatia masuala ya jinsia na shughuli zao zinahusisha tafiti mbalimbali ili kuibadilisha jamii juu ya changamoto na mafanikio kwa kuwa na ushirikiano baina ya wanajamii na viongozi.

Mradi huo unatekelezwa kwenye Halmashauri za Dar es Salaam ni Jiji la Dar es Salaam, Temeke na Kinondoni, Pwani ni Kisarawe, Chalinze na Kibaha Mjini, Lindi ni Ruangwa, Nachingwea na  Mtwara ni Mikindani, Mtwara na Tandahimba na Mafunzo hayo ya siku tatu yanaratibiwa na TGNP kwa kushirikiana na TADIO kwa udhamini wa shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UN Women). 


CCM PWANI YAIBUKA NA USHINDI UDIWANI

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Pwani kimeshinda Kata zote tatu kwenye chaguzi ndogo zilizofanyika baada ya madiwani wa Kata hizo kufariki dunia.

Chaguzi hizo zilizofanyika kwenye kata tatu za Fukayosi Wilaya ya Bagamoyo Kibaha Mjini na Mlanzi Wilaya ya Kibiti ambapo kote imeshinda wapinzani kwa zaidi ya asilimia 90 ya kura zilizopigwa.

Kwenye uchaguzi wa Kata ya Fukayosi Wilaya ya Bagamoyo mgombea wa CCM Mrisho Some amepata kura 5,883 kati ya kura halali 5,960 sawa na asilimia 98.7 huku vyama vingine vikiwa ni CCK, DEMOKRASIA MAKINI, UDP na UMD.

Katika uchaguzi wa Kata ya Msangani Kibaha Mjini Yohana Gunze alishinda kwa kupata kura 5,862 kati ya kura halali 5,909 zilizopigwa sawa na asilimia 99.2 na kuvishinda vyama vya ADA - TADEA, CCK, DEMOKRASIA MAKINI, DP, N.R.A, UMD na UPDP.

Naye mgombea wa CCM Athumani Mketo Kata ya Mlanzi Wilaya ya Kibiti amepata kura 1,592 kati ya kura halali 1,732 sawa na asilimia 91.9 ambapo vyama vingine vikivyoshiriki ni ACT - WAZALENDO, CUF, DEMOKRASIA MAKINI, N.R.A, UDP, UMD na UPDP.

Akizungumzia ushindi huo Katibu wa Siasa Uenezi na Mafunzo CCM Mkoa wa Pwani David Mramba alisema kuwa ushindi wa CCM ni ishara njema kuelekea kwenye chaguzi zijazo kwani wananchi wana imani kubwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Dk Samia Suluhu Hassan.

Mramba alisema kuwa kwenye uchaguzi ujao wa mwakani wa serikali za mitaa na vitongoji watahakikisha wanapata ushindi wa kishindo kwani huu mdogo ni kama mazoezi kwao.


Wednesday, March 20, 2024

MAMLAKA ZA MAJI ZATAKIWA KULIPA MADENI YATOKANAYO NA TOZO

SERIKALI kupitia wizara ya Maji imezitaka Mamlaka za Maji zote  zinazodaiwa kuwasilisha deni la tozo zake ili kuiwezesha EWURA kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi hii nikutokana na deni la tozo kwa Mamlaka za Maji kufikia takribani shilingi bilioni 4.6. 

Akizindua Taarifa ya Utendaji wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira kwa kipindi cha mwaka 2022/23 ambayo ni ya 15 kutolewa na EWURA, Mhandisi Mwajuma Waziri  Katibu Mkuu wa wizara ya Maji  amezitaka mamlaka hizo  zinazodaiwa ankara za maji  zilipe madeni yake mapema ili kuziwezesha kujiendesha na kuweza kutoa huduma kwa ufanisi.

"Kwa Mamlaka za Maji ambazo utendaji wake hauridhishi niseme wazi hatutasita kuzichukulia hatua, nafahamu kuwa baadhi zinashindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za bei ya maji kuwa chini ikilinganishwa na gharama za uendeshaji". Amesema.

Aidha,Katibu mkuu huyo amewasisitiza watendaji wanaohusika katika usimamizi wa miradi ya Maji nchini kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa Sheria.

"Kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi hii, wahakikishe wanaikamilisha kwa wakati'tunafahamu moja ya changamoto zinazoikabili sekta ya maji nchini ni pamoja na kuchelewa kutekelezwa kwa miradi,sitovumilia kuona hili likijitokeza katika miradi hii mikubwa na yenye maslahi makubwa  kwa taifa"Amesisitiza 

Licha ya hayo,ameziagiza Mamlaka za Maji kushirikiana na  Halmashauri zote za Wilaya kuhamasisha uvunaji wa maji ya mvua katika ngazi zote hasa katika kipindi hiki ambapo mvua zinaendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini.

"Tumejionea mvua hizi katika baadhi yua maeneo zimeleta madhara makubwa, hivyo basi,endapo tutavuna maji haya tutapunguza kama siyo kuondoa kabisa athari zake na pia  kutaiwezesha nchi yetu na wananchi kuwa na akiba ya maji ambayo yatatusaidia kipindi cha ukame". Amesema

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa EWURA Dkt. James Andilile amesema taarifa iliyozinduliwa leo ni ya 15 tangu kuanzishwa kwa Mamlaka hiyo miaka 18 iliyopita na inahusisha uchambuzi wa utendaji wa mamlaka za majisafi na usafi wa mazingira 85 zikiwemo; mamlaka 25 za mikoa, saba (7) za miradi ya kitaifa, 47 za wilaya na Sita (6) za miji midogo.

Dkt.Andilile amesema  Utendaji wa mamlaka za maji na usafi wa mazingira umeendelea kuimarika ambapo kwa mwaka 2022/23, Mamlaka za Maji 78 kati ya 85 zilipata alama kuanzia wastani hadi vizuri sana katika utendaji wa ujumla ikilinganishwa na mamlaka 77 kati ya 90 kwa mwaka 2021/22.

Ameyataja Maeneo yaliyoimarika kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na mwaka 2021/22 kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa kiwango cha maji yaliyozalishwa kutoka mita za ujazo milioni 393 hadi 400 sawa na asilimia 1.8 , kuimarika kwa uwiano kati ya watumishi na wateja kutoka 4.2 hadi 3.8 kwa kila wateja 1000 , kuimarika kwa Uwiano wa maunganisho yaliyofungwa dira za maji kufikia asilimia 92 ikilinganishwa na asilimia 90 ,kuongezeka kwa kiwango cha ubora wa maji yanayosambazwa kwa wateja kutoka asilimia 91 hadi 94;

Maeneo mengine ni kuongezeka kwa wateja wa maji wa majisafi kutoka kutoka 1,385,485 hadi 1,532,362 sawa na asilimia 11 na kuongezeka kwa wateja wa mtandao wa uondoaji majitaka kutoka wateja 55,996 hadi wateja 56,899 sawa na asilimia 16.

“Nafahamu kuwa mafanikio hayo hayakuja bure. Naomba nitumie fursa hii kumpongeza na kumshukuru Mh. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wewe Mheshimiwa Waziri kwa usimamizi wako mahiri wa sekta ya maji kwa kufanya uwekezaji mkubwa kwa lengo la kumtua mama ndoo kichwani na kuimarisha ustawi wa watanzania wote, kwani maji ni uhai,” amesema Dkt. Andilile

Uzinduzi huo umekwenda sambamba na utoaji wa tuzo mbalimbali Kwa Mamlaka zilizofanya vizuri huku zikigawanywa katika makundi Matatu tofauti kulingana na idadi ya wateja inayowahudumia ambapo kundi la kwanza ni Mamlaka za maji zenye wateja chini ya 5000, kundi la pili ni mamlaka za maji zenye wateja chini kati ya 5000 na 20,000 na kundi la Tatu ni mamlaka za maji zenye wateja zaidi ya 20,000.


Tuesday, March 19, 2024

WANANCHI MSANGANI WATAKIWA KUMCHAGUA CHONGELA KUWA DIWANI

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani Jackson Kituka amewataka wananchi wa Kata ya Msangani kumchagua mgombea Udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Gunze Chongela kwenye uchaguzi mdogo utakaofanyika kesho Machi 20.

Uchaguzi huo unafanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata ya Msangani Wilaya ya Kibaha Leonard Mlowe kufariki dunia hivi karibuni.

Kituka ameyasema hayo wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo kwenye uwanja wa Juhudi Msangani.

Amesema kuwa wamchague mgombea huyo wa CCM kwani ni mchapakazi mwadilifu na mwaminifu na wasipoteze muda kuchagua wagombea wa vyama vingine.

Mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini Mwajuma Nyamka amesema kuwa mgombea huyo ndiyo chaguo sahihi katika kuleta maendeleo kwa wananchi wa kata hiyo.

Nyamka amesema kuwa diwani aliyefariki aliacha mipango mingi ya maendeleo ambayo lazima iendelezwe na diwani anayetokana na CCM hivyo wasipoteze muda kuchagua mgombea wa chama kingine.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mussa Ndomba amesema kuwa Kata hiyo imetengewa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 900 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Ndomba amesema kuwa fedha hizo zimetengwa kwa ajili ya miradi mbalimbali kwenye sekta mbalimbali za kijamii.

Mkutano huo uliwahusisha madiwani viongozi wa chama wa ngazi mbalimbali na wanachama wa CCM pamoja na mbunge wa viti maalum Dk Allice Kaijage.

Monday, March 18, 2024

SERIKALI KUIWEZESHA SEKTA YA MADINI KUONDOA CHANGAMOTO WACHIMBAJI WADOGO WADOGO


 Na Wellu Mtaki, Dodoma 

Serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuiwezesha sekta ya madini kwa kuchangia asilimia 10 kwenye pato la Taifa ifikapo mwaka 2025 kwa kuondoa changamoto zote zinazowakabili wachimbaji wa madini wadogo wadogo ili kuwezesha shughuli hiyo kuendelea kukua na kukuza uchumi wa nchi ambapo mpaka sasa mchango wa sekta ya madini kwenye pato la nchi umeongezeka kufikia asilimia 9.7

Akizungumza na waandshi wa habari  jijini Dodoma Mkurugenzi wa taasisi ya Tanzanite Fashion na Miss Utalii Eva Raphael amesema madini ya Tanzanite ambayo mauzo yake hufikia mpaka Dola Milioni hamsini kwa mwaka ndiyo upekee  wa kuadhimisha shughuli yetu hi Tanzanite Fashion week.

Aidha amesema kuwa kutakuwa  na  tamasha kubwa la Kitaifa la Tanzanite Fashion week linatarajiwa kufanyika tarehe 4 mwezi 5 Mwaka 2024 jijini Dodoma katika Ukumbi wa Mabeyo Complex. tamasha hilo litaenda kutangaza Utalii wa Madini na Mali asili mbalimbali zilizopo hapa nchini.

"Tunapenda kuwaalika wachimbaji mbalimbali wa Madini, wachimbaji Wanawake na vyama vyao vyote vya Madini, taasisi mbalimbali za kiserikali na binafsi kwenda kushirikiana na sisi katika wiki ya Tanzanite Fashion"Amesema

Aidha amesema kuwa wiki hiyo ni wiki iliyojaa Maudhui mengi,mafundisho pamoja na dhamira nyingi ya kwenda kuigusa jamii na kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Naye Afisa Utamaduni Wizara ya Utamaduni Sana na Michezo Alice John amempongeza Eva kwa ubunifu huo wa kuandaa tamasha hilo na kusema kuwa anaenda kuieleza na kutumia sanaa kama njia bora ya kufikisha ujumbe

"Tunamshukuru dada Eva kwa kuiona sanaa ni njia bora na anakwenda kutumia Sanaa kutangaza Madini"Amesema John

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kanzidata ya madini taasisi ya Jiologia na utafiti wa madini amesema kuwa Madini ya Tanzanite ndo Madini pekee yanayopatikana hapa nchini ndo maana ameyachagua katika wiki ya Tanzanite Fashion week tumeona ni vema kumuunga mkono ili tuweze kuyatangaza madini na Wizara ya Madini imeona  frusa hii ni bora kwa wachimbaji wadogo Wanawake.

UMOJA WANAWAKE VIONGOZI WATOA MSAADA HOSPITALI YA RUFAA DODOMA GENERAL

Na Wellu Mtaki, Dodoma 

Umoja wa Wanawake Viongozi na Viongozi wanaochipukia kutoka Taasisi mbalimbali (ESWLT) umetoa msaada wa vifaa mbalimbali katika 

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma General imepokea msaada wa vifaa mbalimbali kutoka  Umoja wa Wanawake Viongozi na Viongozi wanaochipukia kutoka Taasisi mbalimbali (ESWLT)   ikiwa ni katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa Machi 8 kila mwaka.

Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo Hospitalini hapo na kutembelea katika wodi ya wakinamama Katibu wa Umoja huo Sakina Mwinyimkuu amesema kuwa kitendo cha kutoa vifaa hivyo ni miongoni mwa malengo yao ya kusaidia jamii.

Aidha amesema kuwa Umoja huo una lengo la kusaidia vijana Wanawake hasa mabinti ambao wanatarajia baada ya miaka kadhaa wataingia katika Utumishi katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya kusaidia jamii.

Pia ameongeza kuwa Kwa kupitia umoja huu wanawasaidia na kuwalea ili waweze kuwa wazalendo katika nchi pamoja na kulenga kutumia viongozi waliostaafu kwa kupata mazuri ambayo wamefanya na niwazoefu na kwa kupitia wao watajifunza zaidi katika eneo la uongozi

Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt.Grace Magembe ameushukuru umoja wa Wanawake hao kwa kuchagua eneo hilo kutoa msaada huo kwa sababu eneo walilolichagua ni eneo nyeti

"Kina mama wanaojifungua pamoja na watoto wao wanahitaji Sana mashuka ambayo safi ili kuzuia maambukizi ya magonjwa"Amesema

Aidha amewaahidi Wanawake wa Umoja huo kwa niaba ya Wizara ya Afya kuwa wataendelea kujituma,na Siku nyingine wasisite kwenda kutoa msaada.

Sunday, March 17, 2024

*MAKARANI WAONGOZAJI WA UCHAGUZI WAFUNDWA;KIBAHA*

 


Na Byarugaba Innocent,Kibaha

Ikiwa imesalia siku tatu tu kabla ya Uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Msangani Jimbo la Kibaha Mjini unatarijiwa kufanyika Siku ya Jumatano tarehe 20 Machi,2024.

Mapema Machi 16,2024  Makarani waongozaji wamepata Mafunzo pamoja na kuapa kiapo cha kutunza Siri Chini ya Kanuni ya 16(1) (a) na 50 (4) ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge,2020 na Kanuni ya 14 (1)(a),(2) na 43(4) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Uchaguzi wa Madiwani),2020 Mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi Salum Papen.

Aidha,Mafunzo hayo yametolewa na Maria Israel,Benjamin Mputtu wakisaidiana na Afisa Uchaguzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Optuna Kasanda ambao wamewasisitiza kwenda kufanyakazi kwa kuzingatia Sheria,Kanuni na taratibu za Uchaguzi

Akifungua Mafunzo hayo,Msimamizi wa Uchaguzi,Mwanasheria nguli wa Mahakama kuu na zilizochini yake Salum Papen amesema.." _Tume imewateua ninyi kwa mujibu wa sheria na Kwa kuzingatia uzoefu wenu katika masuala ya Uchaguzi_ "katendeni haki amesisitiza Papen

Papen ametoa rai kwa Makarani waongozaji kujiamini na kujitambua,kufanyakazi kwa kuzingatia Katiba ya Nchi,Sheria za Uchaguzi na Kanuni zake,Maadili ya Uchaguzi na Maelekezo mbambali yanayotolewa na Tume

Katika hatua nyingine Makarani wametia tamko la kujitoa uanachama au kutokuwa na Chama cha Siasa chini ya Kanuni ya 16 (1)(b) na ( 3 ) ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge,2020 na Kanuni 14(1) (b) na (3) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa,(Uchaguzi wa Madiwani),2020 mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi,Mwanasheria Salum Papen

Aidha,Andrea Isamaki Ofisa kutoka Tume ya Taifa ya  Uchaguzi (NEC) ameshiriki kushuhudia Mafunzo,kiapo cha kutunza Siri na tamko la kujitoa uanachama kwa Makarani waongozaji


Nadia Issa na Benson Shawa,Makarani waongozaji wamesema wanakwenda kufanya kazi kwa weledi mkubwa kwa kuzingatia Sheria,Kanuni na taratibu za Uchaguzi 


Uchaguzi mdogo Kata ya Msangani unafanyika kutokana na kifo cha Mhe.Leonard Mlowe kilichotokea tarehe 23 Disemba,2023 ambapo jumla ya vyama nane (8) vya Siasa vinatarajia kushiriki.

Friday, March 15, 2024

BAADHI YA WANAWAKE WAFANYIWA UKATILI NA WENZA WAO

 Na Wellu Mtaki, Dodoma 

Tafiti zilizofanywa nchini Tanzania zinaonesha kuwa asilimia  40 za wanawake waliopo kwenye umri wa miaka 15 hadi 49 wamefanyiwa ukatili wa kijinsia ikiwemo kupigwa, kukatwa viungo  na kuchomwa moto ambapo kati ya wanawake 100 , 40 wameumizwa na wenza wao .

Aidha chimbuko la ukatili huo ni ukosefu wa kutambua usawa  kati ya wanawake na wanaume, ikiwa ni imani na mazoea kwamba ukatili wa kijinsia unakubalika ndani ya jamii

Tafiti hizo zimetolewa na Kaimu Kamishna Wizara ya Maendeleo ya Jamii ,Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Tullo Masanja katika siku ya utepe mweupe ambapo uhadhimishwa kila mwaka ifikapo March 15 .

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Uchechemuzi na Mawasiliano  Save The  Children  Victoria  Marijani amesema kuwa katika kuunga juhudi za Serikali

Wanashirikiana na serikali katika kuhakikisha watoto wanatambua haki zao za msingi pamoja na kutambua  maeneo ya kwenda Kutoa Taarifa endapo watafanyiwa vitendo vya ukatili.

"Lengo ni kumfanya mtoto apate haki ya kuishi,haki ya kulindwa, haki ya kujifunza na kupata lishe iliyo bora ili Taifa liwe na rasilimali watu ambao wenye nguvu na tija". amesema Masanja 

Naye Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya ushauri ya watoto na vijana Save The Children Tanzania Nancy Kasembo amesema kama Bodi ya ushauri anawakilisha vijana katika kutoa maoni chanya na masuala ya ukatili namna gani watoto na vijana kuwa vinara wa kupinga ukatili lakini pia wakatoa Elimu kwa vijana na watoto wakapaza sauti zao katika kuhakikisha wanatengeneza Taifa lililobora na imara.

Kauli mbiu ya  mwaka huu inasema kujenga kizazi kilicho salama kwa kukomesha ukatili wa kijinsia na watoto Tanzania kwa kupitia vijana wa shule.

TUENDELEE KUUNGANA KUKABILIANA NA MAAFA NCHINI” MKURUGENZI MSAIDIZI JANE

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

Mkurugenzi Msaidizi Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bi. Jane Kikunya amesema Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa wadau mbalimnali katika masuala ya uratibu wa maafa nchini ili kuendelea kuwa na stahimilivu na maafa. 

Ameyasema hayo wakati akifungua Warsha ya siku moja iliyowakutanisha wadau kutoka Serikalini, Makampuni ya simu, Taasisi zinazotoa Misaada ya kibinadamu kwa lengo la kujadili fursa na kutoa maoni kuhusu njia sahihi ya ujumuishaji wa teknolojia ya simu katika mifumo ya kutoa tahadhari ya Awali (Early Warning System – EWS) iliyofanyika tarehe 14 Machi, 2024 Jijini Dodoma.

Warsha hiyo ilihudhuriwa na wataalam kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Wizara ya Mifugo, Wizara ya Maji, Wizara ya Afya, Wizara ya Kilimo pamoja na Taasisi ikiwemo TCRA, TMA, REDCROSS, makampuni ya simu pamoja na Airtel, Vodacom, Tigo/Zanztel.

Aidha alitumia fursa hiyo kueleza majukumu ya msingi ya Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo ni kuratibu masuala ya menejimenti ya maafa nchini huku akiwaasa kuendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali katika mzingo wa menejimenti ya maafa ikiwemo wa kuzuia, kujiandaa, kukabili pamoja kurejesha hali pindi maafa yanatokea.

“Tumienie warsha hii kwa matokeo chanya yaliyokusudiwa kwa kuongeza ujuzi na kushirikishana uzoefu katika masuala yanayohusu fursa mbalimbali kuhusu njia sahihi za kutumia teknolojia ya simu katika mifumo na kutoa taarifa za tahadhari za awali ili kuendelea kuwa na utayari katika kukabili maafa,” alieleza Bi. Jane

Aliongezea kuwa nchi ya Tanzania imekuwa ikikumbwa na maafa ya asili na yale yasiyo ya asili ikiwemo ya mafuriko, matetemeko ya ardhi, moto, maporomoko ya tope na mawe, ukame, upepo mkali, magonjwa ya milipuko kwa binadamu na wanyama hivyo warsha hiyo ni muhimu kwa kuzingatia umuhimu wa taarifa za tahadhari za awali ili kuendelea kujiandaa kisha kukabili kwa wakati na kupunguza madhara yanayoweza kutokea wakati wa maafa hayo.

Alifafanua kuwa, taarifa za awali zinaipa jamii uelewa wa hatua za awali za kuchukua kabla ya madhara ya maafa kuwa makubwa hivyo upo umuhimu wa kuendelea kuzijengea uwezo jamii juu ya matumizi sahihi ya taarifa hizo.

Awali aliwakumbusha kuendelea kupiga namba 190 endapo kunatokea majanga, maafa au dharura ili kupata msaada zaidi kupitia Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu.

WATAKIWA KUONDOKA KUEPUKA MAFURIKO MTO RUFIJI

SERIKALI imetoa taadhari kwa wananchi waliopo katika wilaya za Rufiji na Kibiti unakopita Mto Rufiji kuondoka ili kuepuka athari za mafuriko  baada ya milango ya mradi wa uzalishaji wa umeme wa bwana la Mwalimu Nyerere kufunguliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge baadhi ya mashamba ya wananchi yameathirika kwa kuzingirwa na maji.

Kunenge amesema, baada ya maji hayo kufunguliwa, maji hayo yalizingira mashamba na kuharibu baadhi ya mazao ya wananchi na kwamba kwa sasa bado wananchi wanapaswa kuchukua tahadhari kubwa Iki kuthibiti maafa ikiwemo vifo visivyo vya lazima

"Bwawa Mwalimu Nyerere, limefurika kuliko matarajiyo yaliyo kuwepo,ambapo tulipokea taarifa kutoka wizarani na Shirika la umeme Tanzania Tanesco kwamba wanataka kufungua milango ya Bwawa ambapo tulitoa taarifa za tahadhari Kwa wananchi kuondoka maeneo hayo lakin baadhi hawakufanya hivyo hivyo nasisitiza waondoke katika maeneo hayo"amesema

Aidha amesema taarifa za kufunguliwa Kwa Bwawa hilo zitoleea kuanzia Machi Mosi mwaka hadi zoezi Hilo lilipofanyika  Machi 05, majira ya saa 9:00 alasiri ambapo kina cha maji kilichokuwepo ni mita za ujazo 
188.85 na kwamba mpaka sasa kimepungua na kifikia 183.45 baada ya kufunguliwa

Thursday, March 14, 2024

KATA YA TANGINI YAPATA MILIONI 120 KWA AJILI YA ZAHANATI

KATA ya Tangini Wilayani Kibaha imepata kiasi cha shilingi milioni 120 kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ambapo itakapokamilika itahudumia watu 20,146.

Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Kibaha Diwani wa Kata ya Tangini Mfalme Kabuga amesema kuwa tayari fedha hizo zimetokana na mapato ya ndani.

Kabuga amesema kuwa ujenzi wa zahanati hiyo unatarajia kuanza wakati wowote kuanzia sasa na tayari eneo limepatikana eneo la mtaa wa Kilimahewa.

"Wananchi wa Kata hiyo wanapata huduma za kiafya kwenye Hospitali za Tumbi, Mkoani na Pangani ambapo hutumia gharama kubwa zinazofikia kiasi cha shilingi 4,000 hadi 6,000 za pikipiki kufika kwenye huduma za afya,"amesema Kabuga.

Amesema kuwa Zahanati hiyo itajengwa na serikali hadi kukamilika na itakapokamilika itawapunguzia gharama za usafiri na pia kuepuka kwenda moja kwa moja kwenye Hospitali kubwa ambapo gharama zinakuwa ni kubwa endapo hawajaanzia ngazi ya chini.

"Tunaishukuru serikali ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan na Mbunge wetu Silvestry Koka na Madiwani wa Halmashauri ya Mji Kibaha ambao wametufanyia mambo makubwa katika kukabili changamoto za wananchi,"amesema Kabuga.

Ametaja mitaa itakayonufaika na zahanati hiyo kuwa ni Maili Moja B, Tangini, Kilimahewa, Machinjioni na Mtakuja na mtaa jirani wa Muheza toka Kata ya Maiili Moja.

ZINGATIENI MTINDO BORA WA MAISHA ILI KULINDA FIGO ZENU


Wakati Tanzania inaungana na mataifa mengine ulimwenguni kuadhimisha Siku ya Figo Duniani leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), Dkt. Alphonce Chandika, amewashauri wananchi kuzingatia mtindo bora wa maisha ili kulinda figo zao.

Dkt. Chandika, ametoa wito huo jijini Dodoma, akisema wananchi wanapaswa wafanye mazoezi kuzingatia mlo usioathiri moyo ili kuzilinda figo.

"Mtindo bora wa maisha unaozingatia milo isiyoathiri moyo utaisaidia kuzilinda figo," amesema Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali.

Siku ya Figo Duniani mwaka huu inaadhimishwa ikiwa na kauli mbiu, 'Afya ya Figo kwa Wote pamoja na Upatikanaji Bora wa Matibabu.'

Dkt Chandika amesema wagonjwa 50 wenye tatizo la figo husafisha damu kwa siku katika Kitengo cha Kusafisha Damu katika Idara ya Magonjwa ya Figo katika BMH.

"Watu wenye tatizo la figo wanasafisha damu mara tatu (3) kwa wiki," ameongeza.

Dkt Chandika amesema mpaka sasa, BMH imeishafanya oparesheni za upandikizaji figo kwa watu 36 toka huduma hii ianze miaka sita (6) iliyopita.

Mwaka 2019, BMH ilikuwa Hospitali ya pili nchini kuanzisha huduma ya upandikizaji figo, lakini ndiyo Hospitali pekee kutoa huduma hiyo bila usaidizi wa Hospitali za nje.

CCWT YATANGAZA MUDA WA KUCHUKUA FOMU ZA UCHAGUZI


Na Wellu Mtaki, Dodoma.

Chama Cha Wafugaji Tanzania (CCWT) kimetangaza muda wa kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi kwa wanachama wake wanaotaka kugombea huku wakibainisha kuwa malipo ya uchukuaji wa fomu hizo yanapaswa kufanyika kupitia akaunti ya tume ya uchaguzi na sio kwenye akaunti ya chama hicho.

Hayo yameelezwa leo Machi 12, 2024 Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya CCWT Bw. Charles Lyuba alipokutana na waandishi wa habari katika ofisi ya chama hicho ambapo amesema kuwa lisiti za malipo zinapaswa kuambatanishwa katika fomu wakati wa kuzirejesha.

“Tangu mwaka jana tumeanza mchakato wa uchaguzi na hadi sasa tunaendelea na chaguzi za ngazi mbalimbali ikiwemo za wilaya, nawatangazia wafugaji na wanachama wote kuwa fomu za kugombea uongozi ndani ya chama chetu ngazi ya kanda na taifa zitaanza kutolewa Machi 13 - 25,2024 na mwanachama yeyote mwenye nia ya kugombea nafasi yeyote ya kanda anapaswa kuzingatia ratiba na kalenda nzima inayotolewa na tume,”amesema.

Amesema wanachama wao ni muhimu kuwa na taarifa sahihi zinazohusu uchaguzi ili kuepuka mikanganyiko na hasa wanapotoa ratiba isije kuonekana kuna watu wana ratiba zao binafsi.

“Hii ndio ratiba ya tume ya uchaguzi na sisi tunasema hiyo tarehe 13 kwa yaani kesho hadi tarehe hadi tarehe 25, Machi tunaanza kutoa hizo fomu za kanda sambamba na fomu za ngazi ya taifa,” amesema.

Aidha Bw. Lyuba amewasisitiza wagombea wote kufuata ratiba ya tume ipasavyo na kuchukua fomu kwa wakati kwa ngazi ya taifa uchaguzi utaanza Aprili 8,2024 utakao wahusisha viongozi wote wa wilaya na walaya ambayo haitakuwa imefanya uchaguzi wa ngazi haitaruhusiwa kufanya uchaguzi wa ngazi ya kanda pamoja na taifa kwasababu watakuwa hawajatimiza takwa la katiba ya wanachama hicho.

Kwa upande wake mjumbe wa tume ya uchaguzi George Kifuliko amewasisitiza wagombea na wanachama wote kuzingatia ratiba ili kuepusha vikwazo vitakavyojitokeza.

Wednesday, March 13, 2024

MADALALI WA KUPIGIA DEBE WAGOMBEA WATAKIWA KUACHA MARA MOJA



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Picha ya Ndege Wilayani Kibaha imewataka watu wanaojifanya madalali wa watu wanaotaka kugombea nafasi za uenyekiti wa serikali za mitaa waache kwani muda wa viongozi walio madarakani haujaisha.

Aidha kimewataka watu kuacha kuwasemea vibaya viongozi walioko madarakani kwani nikukiharibia chama kwani wanatokana na chama hicho.

Hayo yamesemwa na Katibu Mwenezi wa Kata ya Picha ya Ndege Said Namamba wakati wa ziara kwa mabalozi wa Kata hiyo.

Namamba amesema kuwa kuna baadhi ya watu wanajifanya wanawapigia debe baadhi ya watu wanaotaka kuwania nafasi za uongozi huku muda wa kuwania nafasi hizo ukiwa bado.

Naye Mjumbe Mkutano Mkuu kutoka Kata  Subira Said amesema kuwa wametumia fursa hiyo kuwafundisha mabalozi hao kujua wajibu na majukumu yao.

Said amesema kuwa pia wamewaelekeza namna ya kutunza kumbukumbu za wanachama na kuhifadhi taarifa mbalimbali za mashina yao na kutoa taarifa juu ya changamoto kwa balozi wanazoziongoza.

Kwa upande wake Katibu wa Hamasa wa Vijana wa Kata Lenatus Mkude amesema kuwa wao wanataka mabalozi wasikubali kupotoshwa na watu wanaotaka kuwatumia kuwapigia debe wakati muda haujafika.

Mkude amesema wao wanataka utaratibu wa chama ufuatwe ili mgombea atakayechaguliwa kupitia kura za maoni apeperushe bendera ya chama na siyo vinginevyo.


Tuesday, March 12, 2024

WAFANYABIASHARA WA DODOMA WAIOMBA SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BIASHARA





Na Anna Misungwi, Dodoma 

WAFANYABIASHARA wa Mkoa wa Dodoma waiomba serikali kurekebisha miundombinu ya soko la Machinga Complex pamoja  soko la Mavunde  lililopo Kata ya Chang'ombe ambapo kipindi cha mvua maji huingia na biashara kuharibika.

Hayo yamesemwa na wafanyabiashara wa masoko hayo Tarehe 11 Machi 2024 wakati wa ziara ya mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Hamis Livembe, kwenye ziara iliyolenga kupokea changamoto, kero na maoni ya wafanyabiashara.

Mmoja wa wafanyabiashara Abdalla Ramadhan amesema kuwa kumekuwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na miundombinu ya soko kwani maji yanaingia na hivyo kusababisha bidhaa kuharibika.

Ramadhan amesema kuwa pia wanaomba kushushwa kwa ushuru kutoka 1,000 na kuwa 500 kwenye kizimba kwenye soko la Machinga Complex ambapo kizimba kimoja kinaweka wafanyabiashara wawili kwani ushuru wanaolipa unasababisha kushuka kwa biashara zao.

"Wafanyabiashara kipato chetu kinashuka tunaimomba serikali itusaidie kwani kizimba kimoja tunakaa watu wawili na kila mtu kwenye kizimba analipa shilling 1,000 ambapo watu wawili ni shilling 2,000 tunaomba tupunguziwe tulipe shilling 500 kwa kila mtu,"amesema Ramadhan.

Amesema wanaiomba serikali kuacha kuwafungia vizimba kutokana na hali ya wafanyabiashara kudaiwa kulipia ushuru kwani kizimba kikifungwa husababisha kukosa mapato kwa wafanyabiashara na serikali kwa ujumla.

"Tunafungiwa vizimba sababu ya mtu kama hajalipa ushuru siku moja au mbili kitendo ambacho wengi wanashidwa kuja kugomboa maana unapofungiwa lazima uje utoe fedha ndo ufunguliwe tunaomba serikali itusaidie,"wamesema wafanyabiashara hao.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe amesema kuwa lengo la kuja ni kupokea changamoto, kero na maoni na changamoto ambazo zinaweza kutolewa majibu zinatolewa ufafanuzi na ambazo majibu hawana watazipeleka sehemu husika ili kuzitafutia ufumbuzi.

Livembe ametoa wito kwa wafanyabiashara kuhakikisha wanakuwa wamoja katika kushughulikia matatizo kwa umoja.