Thursday, September 28, 2023

SHULE BORA YAWAJENGEA UMAHIRI UFUNDISHAJI SOMO LA HISABATI

KATIKA kuhakikisha wanafunzi wa shule za msingi wanapata uelewa wa somo la hisabati Mkoani Pwani Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia na Taasisi ya Elimu Tanzania kupitia program ya Shule Bora imewapatia mafunzo walimu wa somo hilo.

Akizungumza Wilayani Kisarawe baada ya ufunguzi wa mafunzo kwa viongozi wa elimu kuhusu uboreshaji ufundishaji na ujifunzaji wa umahiri wenye changamoto katika somo la hisabati Ofisa elimu Mkoani humo Sara Mlaki amesema kuwa mafunzo kwa walimu hao yatawajengea uwezo ili kupata mbinu bora za umahiri za ufundishaji wa somo la hisabati.

Aidha mafunzo hayo yameandaliwa na Ofisi ya Rais (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia pamoja na Taasisi ya Elimu Tanzania kupitia Program ya Shule Bora ambayo inatekelezwa katika mikoa tisa ya Tanzania Bara kwa Ufadhili wa Serikali ya Uingereza na kwa Usimamizi wa Cambridge Education.

Mafunzo hayo yaliendeshwa na  wawezeshaji kutoka vyuo vya Ualimu vya Tukuyu  na Mpwapwa ambapo washiriki wa  mafunzo hayo ni viongozi wa Elimu kutoka katika ngazi ya Mkoa  wakiwemo Walimu, Walimu  wakuu, Maofisa Elimu Kata, Maofisa Elimu Awali na Msingi kutoka katika Halmashauri tisa na shule teule za Wilaya ya Kisarawe.

Wednesday, September 27, 2023

SHULE SALAMA WAJADILI KUMLINDA MTOTO


WANAFUNZI 42,000 kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha watafikiwa na mpango wa Shule Salama wenye lengo la kuhakikisha wanakuwa salama kuanzia shuleni na wawapo nyumbani.

Hayo yalisemwa na Ofisa Elimu Watu Wazima anayesimamia afya Shuleni Halmashauri ya Mji Kibaha Juliana Mwakatenya wakati wa mafunzo kwa wadau wa Shule Salama kwenye Halmashauri hiyo.

Mwakatenya alisema kuwa mpango huo uyazifikia shule zote za msingi za serikali na za binafsi na umelenga kuhakikisha usalama wa mwanafunzi kuanzia shuleni na nyumbani ili kumlinda na changamoto mbalimbali ikiwemo vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa.

Kwa upande wake mratibu wa Shule Salama Halmashauri ya Mji Kibaha Japhary Kambi alisema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia wadau kuwalinda watoto ili wafikie malengo yao ambapo wadau wakijua vikwazo vinavyowakabili wanafunzi itakuwa ni rahisi kukabiliana navyo na kutoa taarifa sehemu husika ili wanaofanya vitendo hivyo wachukuliwe hatua za kisheria. 

Naye Chiku Abdul ofisa mwezeshaji wa mpango huo alisema kuwa matukio mengi ya vitendo vya ukatili yamekuwa hayaripotiwi na kufanya matukio kuongezeka kwani baadhi ya wazazi au walezi wa watoto wamekuwa wakimalizana pasipo kuyafikisha matukio hayo kwenye vyombo vya sheria.

Hatibu Omary mwenyekiti wa wasilishaji wa mada alisema kuwa wanaishukuru serikali kwa kuwapatia mafunzo ambapo waliyafanyia mkoani Morogoro na wao ndiyo wanawafundisha wadau wengine kuwa ulinzi na usalama wa mtoto ni jukumu la watu wote ndani ya jamii na kuwataka kutofumbia macho vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa watoto.


TIMU YA NYUMBU YAENDELEA NA MICHEZO YA KUJIPIMA NGUVU YATOKA SARE 1-1 NA POLISI TANZANIA

TIMU ya Soka ya Nyumbu ya Mkoani Pwani inayojiandaa na ligi daraja la Pili imetoka sare ya goli 1-1 na timu ya Polisi Tanzania kwenye mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja wa Chuo Cha Polisi Kurasini Jijini Dar es Salaam.

Nyumbu huo ni mchezo wake wa pili wa kujipima nguvu ambapo jana ilicheza na timu ya Mashujaa ya Mkoani Kigoma ambayo inashiriki ligi Kuu ya NBC Premium League ambapo pia ilitoka sare ya kufungana goli 1-1 kwenye uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya michezo hiyo kocha mkuu wa timu hiyo Rajab Gwamku amesema kuwa anafurahishwa na viwango vya wachezaji wake kupitia michezo hiyo ya kujipima nguvu waliocheza.

Gwamku amesema wataendelea kucheza michezo ya kirafiki zaidi ili kuiimarisha timu yake kabla ya kuanza kwa michezo ya ligi daraja la pili kwa kipindi itakapopangwa kuchezwa ligi hiyo.

Amewaomba Wanapwani kuiunga mkono timu yao ili iweze kufanya vyema kwenye ligi daraja la pili na kupanda daraja la kwanza huku malengo yakiwa ni kupanda ligi kuu ili kuuwakilisha vyema mkoa huo.

WAFUGAJI WILAYANI KIBAHA WABUNI MBINU YA ULINZI KULINDA MIFUGO YSO



KUFUATIA vitendo vya wizi wa mifugo kushamiri Chama cha Wafugaji Wilaya ya Kibaha mtaa wa Mwanalugali kimeweka mkakati wa kutumia ulinzi shirikishi ili kudhibiti vitendo hivyo.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na mwenyekiti wa chama hicho Haji Myaya alisema kuwa wamefikia maamuzi hayo baada ya kikao na wafugaji ambapo ndani ya wiki moja matukio matatu ya wizi yametokea

Myaya alisema kuwa changamoto ya wizi wa mifugo hasa ng'ombe umekuwa ukijitokeza mara kwa mara na kuwasababishia umaskini wafugaji na kuamua kuwa na walinzi hao.

"Tumekaa kikao na kukubaliana wanachama wote kutoa michango ya kila mwezi ili kuwalipa walinzi hao kupitia ulinzi shirikishi ili watulindie mifugo yetu na hata mali za wananchi,"alisema Myaya.

Alisema kuwa wezi hao huiba na kuwachinja ng'ombe na kisha kuchukua nyama na kwenda kuiuza sehemu zisizojulikana ambapo huacha vichwa na utumbo tu.

Naye Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa nyama na mfugaji Aidan Mchiwa alisema kuwa kwa kushirikiana na chama cha wafugaji wamekuwa wakikabiliana na wezi wa mifugo kwa kuwa na mikakati mbalimbali ya kiulinzi.

Mchiwa alisema kuwa moja ya njia ni kuhakikisha nyama inayouzwa inakuwa imethibitishwa na mganga wa mifugo kwa kugongwa muhuri wa serikali ili kuepuka kuuza nyama ya wizi.

Alisema kuwa wafugaji wanashauriwa kuwa na mawasiliano ya simu ili linapotokea tukio la wizi wanaungana kwa pamoja na kufuatilia ng'ombe ambapo juzi walifanikiwa kurudisha ngombe watano ambao waliibiwa na kupelekwa Bagamoyo na wezi kukimbia.

"Tunashirikiana vizuri na jeshi la polisi katika kudhibiti wezi na kuwashauri wafugaji kutoa taarifa mapema wizi unapotokea ili kuwafuatilia wezi kabla hawajawachinja au kuwasafirisha mbali na kwenda kuwauza,"alisema Mchiwa.

Aidha aliwataka wafugaji kuwa na mahusiano mazuri na wafanyakazi wao wa mifugo kwa kuwalipa kwa wakati ili wasiingie vishawishi na kushirikiana na wezi kuiba mifugo.

WAFUGAJI KUTUMIA WALINZI SHIRIKISHI KULINDA MIFUGO YAO

KUFUATIA vitendo vya wizi wa mifugo kushamiri Chama cha Wafugaji Wilaya ya Kibaha mtaa wa Mwanalugali kimeweka mkakati wa kutumia ulinzi shirikishi ili kudhibiti vitendo hivyo.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na mwenyekiti wa chama hicho Haji Myaya alisema kuwa wamefikia maamuzi hayo baada ya kikao na wafugaji ambapo ndani ya wiki moja matukio matatu ya wizi yametokea

Myaya alisema kuwa changamoto ya wizi wa mifugo hasa ng'ombe umekuwa ukijitokeza mara kwa mara na kuwasababishia umaskini wafugaji na kuamua kuwa na walinzi hao.

"Tumekaa kikao na kukubaliana wanachama wote kutoa michango ya kila mwezi ili kuwalipa walinzi hao kupitia ulinzi shirikishi ili watulindie mifugo yetu na hata mali za wananchi,"alisema Myaya.

Alisema kuwa wezi hao huiba na kuwachinja ng'ombe na kisha kuchukua nyama na kwenda kuiuza sehemu zisizojulikana ambapo huacha vichwa na utumbo tu.

Naye Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa nyama na mfugaji Aidan Mchiwa alisema kuwa kwa kushirikiana na chama cha wafugaji wamekuwa wakikabiliana na wezi wa mifugo kwa kuwa na mikakati mbalimbali ya kiulinzi.

Mchiwa alisema kuwa moja ya njia ni kuhakikisha nyama inayouzwa inakuwa imethibitishwa na mganga wa mifugo kwa kugongwa muhuri wa serikali ili kuepuka kuuza nyama ya wizi.

Alisema kuwa wafugaji wanashauriwa kuwa na mawasiliano ya simu ili linapotokea tukio la wizi wanaungana kwa pamoja na kufuatilia ng'ombe ambapo juzi walifanikiwa kurudisha ngombe watano ambao waliibiwa na kupelekwa Bagamoyo na wezi kukimbia.

"Tunashirikiana vizuri na jeshi la polisi katika kudhibiti wezi na kuwashauri wafugaji kutoa taarifa mapema wizi unapotokea ili kuwafuatilia wezi kabla hawajawachinja au kuwasafirisha mbali na kwenda kuwauza,"alisema Mchiwa.

Aidha aliwataka wafugaji kuwa na mahusiano mazuri na wafanyakazi wao wa mifugo kwa kuwalipa kwa wakati ili wasiingie vishawishi na kushirikiana na wezi kuiba mifugo.

Tuesday, September 26, 2023

MAOFISA ELIMU WALIMU WA HISABATI MKOANI PWANI WAPIGWA MSASA

WALIMU wanaofundisha somo la Hisabati Mkoani Pwani wametakiwa kutumia ufanisi umahiri na dhana stahiki kupitia mbinu za ufundishaji wa somo hilo ili kuongeza ufaulu.

Hayo yamesemwa Wilayani Kisarawe na Katibu Tawala (RAS) Mkoa wa Pwani Ramadhan Mchatta ambaye aliwakilishwa na Ofisa Elimu Mkoa Sara Mlaki wakati wa Mafunzo kwa viongozi wa elimu kuhusu uboreshaji ufundishaji na ujifunzaji wa umahiri wenye changamoto katika somo la hisabati kwa mkoa huo.

Mchatta amesema kuwa kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya wanafunzi kwenye somo la hisabati ambapo utafiti umebaini baadhi ya wanafunzi kufanya vibaya kwenye mitihani ikiwemo ile ya Mock Wilaya na Mkoa.

Naye mtaalamu kiongozi wa Shule Bora Vicent Katabalo ameupongeza Mkoa wa Pwani kwa kutekeleza vizuri afua mbalimbali za mradi wa Shule Bora na kutaka waendeleze jitihada ili kufikia malengo yaliyowekwa ili kuboresha ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi.

Kwa upande wake ofisa elimu mkoa wa Pwani Sara Mlaki amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuimarisha umahiri wa wa walimu na viongozi wa  Elimu  katika kutumia mbinu shirikishi za ufundishaji na ujifunzaji wa somo la Hisabati ili kuleta matokeo chanya kwa wanafunzi wote.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Ofisi ya Rais (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia pamoja na Taasisi ya Elimu Tanzania kupitia Program ya Shule Bora ambayo inatekelezwa katika mikoa tisa ya Tanzania Bara kwa Ufadhili wa Serikali ya Uingereza na kwa Usimamizi wa Cambridge Education.

Mafunzo hayo yameendeshwa na  wawezeshaji kutoka vyuo vya Ualimu vya Tukuyu  na Mpwapwa ambapo washiriki wa  mafunzo hayo ni viongozi wa Elimu kutoka katika ngazi ya Mkoa  wakiwemo Walimu, Walimu  wakuu, Maofisa Elimu Kata, Maofisa Elimu Awali na Msingi kutoka katika Halmashauri tisa na shule teule za Wilaya ya Kisarawe.

Thursday, September 21, 2023

MAAFISA,WAKAGUZI, NA ASKARI POLISI KUTOKA MAKAO MAKUU WANOLEWA NAMNA BORA YA KUSHIRIKIANA NA WANANCHI

 


Na, Benedict Mlawa wa Jeshi la Polisi

MSEMAJI wa Jeshi la Polisi Nchini,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP) David  Misime amefunga mafunzo ya siku mbili kwa Maafisa,Wakaguzi na Askari wa Polisi kutoka Makao Makuu na Mkoa wa Dodoma.

SACP Misime amewaeleza Askari hao kuwa mafunzo hayo ni mfululizo  wa mafunzo yanayotolewa kwa Askari  katika Vyuo ndani ya nchi, nje ya nchi na kazini kwa lengo la kuwabadilisha kifikra (mindset change) ili kutoa huduma bora kwa jamii.

SACP Misime amefungua mafunzo hayo Septemba 20, 2023   katika ukumbi wa Polisi Jamii Mkoa wa Dodoma Yakifanyika kwa engo la kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao ya kazi za Polisi kwa Nidhamu, Haki, Weledi na Uadilifu.

"Mkibadilika kifikra na kuhudumia wananchi kwa Nidhamu,Haki,Weledi na Uadilifu mtakuwa na uwezo wa kusimama mbele ya wananchi kifua mbele na kwa kutumia Falsafa ya Polisi,wananchi waka waamini na kuongeza imani kwa Jeshi la Polisi ili waoneshe ushirikiano katika kubaini na kuzuia uhalifu".Amesema Misime.

Pamoja na hayo, Misime amewapongeza Askari kwa kushiriki vyema katika mafunzo hayo na kazi kubwa wanayofanya huku akiwataka kwenda kuyafanyia kazi yale waliojifunza ili wananchi waweze kuona mabadiliko ya kifikra na  kiutendaji kulingana na mageuzi makubwa yanayoendelea ndani ya Jeshi la Polisi.

Awali akizungumza Mkuu wa Kitengo cha Dawati la Jinsia na watoto  kutoka  Makao  Makuu  ya Polisi Kamisheni ya Polisi Jamii  Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Faidha Suleiman amewasisitiza Askari wa Kike kuzingatia maadili, kutunza familia, kujijengea  uwezo wa kujiamini, kuwa wasafi na kuachana na vyanzo vyote vya mawazo kama vile kujiingiza katika mikopo isiyo na msingi ambayo muda mwingi huwapelekea kuwa ni watu wenye mawazo.

Hata hivyo, ACP Faidha Suleiman ambaye ni mratibu wa Dawati la Jinsia na watoto Makao makuu ya Polisi amewataka askari kuhakikisha wanafuata na  kutekeleza miradi ya Polisi Jamii katika majukumu yao ya kila siku kwani miradi hiyo inagusa kila kitengo cha Jeshi la Polisi. 

Amesisitiza katika kuzuia vitendo vya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji wa watoto katika familia zao na jamii kwa ujumla ikiwemo wao wenye kutokujifanyia ukatili. 

Naye Mkuu wa Dawati la mtandao wa Polisi wananwake (TPF Net) Makao Makuu ya Polisi Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Eva Stesheni amewataka askari kujifunza namna ya kuandika ripoti ya kazi zao ili kuleta ufanisi katika utendaji kazi  pamoja na kuwasidia katika utunzaji wa kumbukumbu za nyaraka kwa kuwa na mpango kazi ulio mzuri ilikufikia malengo sahihi , Kuwasilisha taarifa, mawazo  na kuendeleza ujuzi  hasa kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto.

Mkuu wa dawati la jinsia na watoto  mkoa wa Dodoma mkaguzi wa Polisi  Teresina  Mdendemi amewataka askari kutoa huduma bora kwa wateja wa ndani na nje  kwani kupitia utoaji wa huduma bora huweza kusaidia kurahisha utendaji kazi wa kila siku na kusaidia katika kupambana na vitendo vya kihalifu hususani unyanyasaji wa kijinsia.

"Tutambue na  kufahamu aina ya wateja  Pamoja na  hisia zao pia tuwe  na moyo wa kusamehe kwa lengo la kuimarisha mahusiano mazuri kati ya Jeshi la Polisi na Jamii  katika kupunguza vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia  na ukatili dhidi ya watoto   na vitendo vyote vya kihalifu".Amesesisitiza Mdendemi

Kwa upande wake Mkuu wa  Dawati la Jinsia  mkoa wa Pwani  Mkaguzi  Msaidizi wa Polisi  Eliezer  Hokororo  amezungumzia  Faida na athari ya afya ya akili na kusema kuwa ukiponya akili umeponya maisha yako yote maana akili ni mfumo mzima maisha ya mwanadamu. 

Hokororo amesema kwamba watu wengi wameathirika na ugonjwa wa Sonona ambao umetokana na kukosekana na ubora wa afya ya akili na   kuchangia kuharibu Fikra, Hisia na Matendo ya mtu kutokana na kutokuwa na afya bora ya akili na mara nyingine kushindwa kabisa kutatua changamoto wananzokutana nazo.

Aidha Mkuu wa Dawati la Jinsia Mkoa wa Njombe Mkaguzi msaidizi wa Polisi Wilfred Willa  aliwataka askari wa kike kutambua na kuzingatia wajibu wao kwa kuihudumia vyema Familia na jamii huku akisema mwanamke anapaswa kuwa kioo na mwenye tabia njema maana ndiye nguzo kwa jamii.


Picha na Benedict Mlawa wa Jeshi la Polisi

Tuesday, September 19, 2023

ASHIKILIWA KWA KUMWAGIA CHAI YA MOTO DADA WA KAZI

JESHI la Polisi Mkoani Pwani linamshikilia mkazi wa Kwa Mathias Wilayani Kibaha Janeth Dominick (26) kwa tuhuma za kumwagia chai ya moto sehemu mbalimbali za mwili dada wa kazi Filomena Erick (17).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi mkoani humo ACP Pius Lutumo ilisema kuwa mtuhumiwa alimuunguza dada huyo na chai aliyomwagia.

Lutumo amesema kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 14 mwaka huu majira ya saa 2:00 asubuhi ambapo  mtuhumiwa ni mwajiri wake alimuunguza maeneo ya shingoni, mkononi, kifuani na tumboni.

"Mtuhumiwa alifikia hatua hiyo kwa kumtuhumu kuiba unga, sukari na simu ya mkononi katika chumba cha mpangaji mwenzao,"amesema Lutumo.

Amesema kuwa mtuhumiwa atafikishwa kwenye mifumo ya kisheria mara upelelezi utakapokamilika kuhusiana na tukio hilo.

"Jeshi la polisi linatoa rai kwa watu wote wanaoishi na wadada wa kazi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani tukio hilo halikubaliki katika jamii na ni kinyume cha sheria,"amesema Lutumo

Sunday, September 17, 2023

MWANAFUNZI ATAKAYE ONGOZA KITAIFA DARASA LA SABA KIPS KUPATA MILIONI TANO


MKURUGENZI wa Kampuni ya Njuweni Ltd Alhaj Yusuph Mfinanga ameahidi kutoa kiasi cha shilingi milioni tano kwa mwanafunzi atakayefaulu na kuongoza kitaifa kwenye mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kutoka shule tatu zinazomilikiwa na kampuni hiyo. 

Aidha atawasomesha bure wanafunzi 20 watakaofaulu masomo ya kumaliza elimu ya msingi na kupata alama za daraja A kwa masomo yote ambapo watasoma kwenye shule za sekondari za kampuni hiyo za Vuchama Islamic Secondary School na Mangio Secondary School zilizopo Mkoani Kilimanjaro.

Mfinanga ameyasema hayo wakati wa mahafali ya shule hizo ambazo ni Kibaha Independence School (KIPS), Anex na Msangani zote zilizopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.

Amesema kuwa ametoa fursa hiyo kama motisha kwa wanafunzi wa shule hizo ili kuhamasisha wafanye vizuri kwenye mitihani yao na kuzifanya shule hizo ziwe na matokeo mazuri.

Kwa upande wake mgeni rasmi Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka amesema kuwa sekta binafsi kwenye sekta ya elimu ina mchango mkubwa sana kwani inaipunguzia serikali mzigo wa wanafunzi.

Koka amesema kuwa licha ya ujenzi wa madarasa kujengwa na serikali mara kwa mara lakini bado kuna changamoto kubwa ya upungufu wa madarasa na miundombinu mingine hivyo ushirikiano na sekta binafsi unahitajika.

Kwa upande wake meneja wa KIPS Nuru Mfinanga amesema kuwa wanashirikiana vizuri na serikali katika kukabiana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza kwenye sekta hiyo lengo likiwa ni kutoa elimu bora.

Mfinanga amesema kuwa wanaipunguzia mzigo serikali kwa kuwasomesha wanafunzi kupitia sekta binafsi na kuwataka wazazi kuwafuatilia watoto wao ili wafanye vizuri kwenye masomo yao na kuwataka walipe ada kwa wakati ili waweze kujiendesha na kutoa elimu bora.



Tuesday, September 12, 2023

*ASKARI WA TAWA WAMUOKOA MTOTO WA TEMBO ALIYETUMBUKIA SHIMONI*

 

Na Beatus Maganja, TAWA

Askari wahifadhi kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) septemba 11, 2023 walifanikiwa kumuokoa mtoto wa tembo anayekadiriwa kuwa na umri wa wiki nne (4) aliyezama katika shimo lenye matope katika Kijiji cha Kwamsanja kilichopo kata ya kibindu  halmashauri ya Chalinze jirani na Pori la Akiba Wamimbiki.

Taarifa za Mtoto huyo wa tembo aliyetelekezwa na kundi lake kutumbukia shimoni zilitolewa na raia mwema aitwaye Manase Thomas Baha mkazi wa Kijiji cha Kwamsanja na kumlazimu Kamanda wa Pori la Akiba Wamimbiki Emmanuel Lalashe kutuma timu ya askari wanne (4) walioshirikiana na askari wa Jeshi la Akiba (migambo) sita (6) kwa ajili ya zoezi zima la kumuokoa mtoto huyo wa tembo.

Akizungumza baada ya zoezi la uokoaji, Kamanda Emmanuel Lalashe aliwashukuru wananchi wanaoishi pembezoni mwa hifadhi ya Wamimbiki kwa ushirikiano wanaoutoa katika kulinda rasilimali za Nchi yetu zilizopo katika hifadhi hiyo hususan rasilimali Wanyamapori ambazo ni chachu ya shughuli za Utalii na Pato la Nchi.

Mahusiano mazuri yaliyojengwa kati ya wahifadhi wa hifadhi ya Wamimbiki na wananchi wanaoishi vijiji Jirani na hifadhi hiyo umekuwa na manufaa makubwa siku za hivi karibuni kwani wananchi wamekuwa wakitoa ushirikiano mkubwa katika shughuli za uhifadhi.

*DKT JAFO AFUNGUA MRADI WA MAJI KITUO CHA AFYA MZENGA*

Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi ofisi ya makamu wa RAIS Muungano na Mazingira Mhe Dkt Selemani Saidi Jafo amefungua Mradi wa Maji katika Kituo Cha Afya Mzenga na kuwataka wananchi kuutunza Mradi huo 12.09.2023.

Akiziungumza wakati wa kufungua Mradi huo wa Maji alisema ni wajibu wa wananchi Hao wa Mzenga kuitunza miundombinu ya Mradi ili uweze kudumu kwa Muda mrefu huku ukiwahudimia wananchi mbalimbali na wale wanaofika Katika kituo cha Afya Mzenga,

*"Ndugu wananchi nimehangaika sehemu mbalimbali kutafuta wafadhili na kuwapata Hawa ndugu zetu Afrika Relief ambao wameweza kutusaidia kutatua hii kero ya maji hapa Mzenga niwashukuru sana Hawa afrika  Relief kukubali kutujengea Mradi Huu mkubwa alisisitiza Mhe Dkt Jafo*"

Nae Meneja wa Taasisi ya Afrika Relief Kanda ya Tanzania Mohamed Gewily alishukuru kisarawe kwa kupokea msaada wa Mradi huo wa Maji huku akitaja umegarimu  Shilingi Milioni Tisa na Laki Tatu na Elfu Hamsini hivyo akatoa wito zaidi kwa Wanakisarawe hasa Mzenga kuitunza miundombinu ya Mradi ili idumu na Kuendelea Kutoa huduma kwa Muda mrefu,

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Wilaya kisarawe katika ufunguzi wa mradi wa Maji Ndg Nancy Kasamala Alisisitiza kuhifadhi miundombinu ya Mradi pamoja na Kutoa wito kwa Jamii Kuendelea kuzitumia vyema Kamati za maji za Vijiji katika kusimamia  Mradi,

*"Ndugu zangu tuliopo hapa naomba niwakushe  jambo Moja kuna bodi ya maji Vijijini Hivyo nashauri mshirikiane na Uwongozi wa kituo Cha Afya Mzenga kwa kuendesha Mradi huu ambao umejengwa hapa kituoni badala ya Kijijini alishauri Ndugu Kasamala*"

Mradi Huu wa maji katika Tarafa ya Mzenga kata ya Mzenga Kijiji Cha Mzenga umefadhiliwa na Taasisi ya Afrika Relief umegarimu  dhamani ya Milioni Tisa na Laki Tatu na Elfu Hamsini unategemea kuwahudumia watu Elfu Moja  mia Nne na Sitini na Tatu pamoja watu mbalimbali wanaofika kituo Cha Afya Mzenga,

Aidha Mradi huo pia Unategemea kwa Raia kuchangia Bei ya Maji kwa Ndoo  Moja ya  lita Ishirini kwa  Shilingi Arobaini Tu kwa Mujibu wa muongozo ili uweze kuendesha Miundombinu mbalimbali pamoja na Kukarabati.

WATOTO ZAIDI YA LAKI 4 KUPATA CHANJO YA POLIO MKOA WA SONGWE

 

Na. WAF - Songwe

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amebainisha kuwa zaidi ya watoto laki Nne wanatarajia kupata chanjo dhidi ya ugonjwa wa Polio katika Mkoa wa Songwe. 

Waziri Ummy ameyasema hayo Septemba 11, 2023 wakati akianza ziara yake ya kukagua huduma zinazotolewa katika Halmashauri ya Wilaya ya Songwe ambapo ameanza kutembelea katika Hospitali ya Wilaya hiyo, Zahanati ya Mbala pamoja na Kituo cha Afya Mbuyuni kilichopo katika Wilaya hiyo.

“Baada ya kupatikana kwa mtoto Mmoja mwenye ugonjwa wa Polio tumeamua kutoa chanjo ya ugonjwa huo ambapo kwa Mkoa wa Songwe tunatarajia kuchanja watoto takribani Laki Nne ambao wana umri chini ya Miaka Nane”. Amesema Waziri Ummy 

Amesema, Mwaka 2015 Shirika la Afya Duniani (WHO) iliitangaza Tanzania kuwa ni nchi ambayo imetokomeza ugonjwa Polio, Mwaka huu 2023 Tanzania imepata Mtoto mwenye ugonjwa huo katika Manispaa ya Sumbawanga Mkaoni Rukwa. 

“Baada ya Miaka 8 toka WHO iitangaze Tanzania kumalizika kwa ugonjwa wa Polio, Mwaka huu 2023 tumepata mtoto mmoja kutoka Mkoa wa Rukwa ambaye ana virusi vya ugonjwa wa Polio (aina ya Pili)”. Amesema Waziri Ummy 

Aidha, Waziri Ummy amesema kutokana na hatari iliyopo, Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais TAMISEMI imeamua kuendesha kampeni maalumu ya kutoa chanjo ya kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa wa Polio. 

Amesisitiza kuwa, chanjo hiyo itatolewa katika Mikoa Sita iliyopo mipakani ambayo ni Mkoa wa Songwe, Kigoma, Rukwa, Katavi, Mbeya pamoja na Kagera. 

“Mikoa Sita itafikiwa na zoezi hili na lengo ni kuwafikia zaidi ya watoto Mil. 3.5 ambao wana umri chini ya Miaka Nane kwa sababu watoto wote waliozaliwa kuanzia Mwaka 2016 walipata chanjo ya Polio ya kukinga kirusi aina ya kwanza”. Amesema Waziri Ummy 

Pia, Waziri Ummy amesema zoezi hilo la utolewaji wa chanjo litaendeshwa kwenye vituo vya kutoa huduma za Afya, mashuleni, nyumba kwa nyumba, sehemu za ibada na vilabuni.

“Wakati wa zoezi hili tutawatumia watu Watatu Watatu katika kila timu ambao watapita kama ni mashambani, mashuleni au masokoni kwa ajili ya kuwapa watoto chanjo hiyo dhidi ya ugonjwa wa Polio ili tuwakinge watoto wetu na ugonjwa huo”. Amesema Waziri Ummy

KIBITI WAKABIDHIWA VIFAA VYA MICHEZO NYERERE SUPER CUP


Picha ya matukio ya Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ikiwakirishwa na Ndugu Omary Punzi Katibu wa Taasisi hiyo wakikabidhi Tshirt na Mipira ya zawadi ya mashindano ya NYERERE SUPER CUP 2023 Kwa Mhe Kanali Joseph kolombo Mkuu wa wilaya ya Kibiti Mashindano hayo yanatarajiwa kuanza Tarehe 23.9.2023 na kutamatisha 12.10.2023 yakishirikisha Timu 12 Timu 6 kutoka Kibiti na Timu 6 kutoka Rufiji wadhamini wa mashindano ni NSSf,NBC BANK na  TANGANYIKA ORGANIC Kauli mbiu ya mashindano AMANI NA UMOJA VITAWALE MITANO TENA

Saturday, September 9, 2023

NYERERE SUPER CUP TIMU ZAKABIDHIWA VIFAA



Katika kuelekea kumbukizi ya Miaka 24 ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ikiwakirishwa na Ndugu Omary Abdull Katibu wa Taasisi hiyo Mkoa wa Pwani Leo Tarehe 9.9.2023 imekabidhi Vifaa vya michezo ya mashindano ya NYERERE SUPER CUP Jezi seti Moja na Mpira Mmoja Kwa Kila Timu, Tshirt za maandalizi ya Ufunguzi, Zawadi za Mashindano na Mpira Kwa Chama Cha Mpira Rufiji Kwa Mkuu wa wilaya ya Rufiji Mhe Meja Edward Gowele ili akabidhi Kwa Timu sita hizo zitakazoshiriki kwa upande wa Rufiji 1. NGORONGO 2.UTETE,3.MGOMBA, 4.MUHORO 5.UMWE na 6.MKONGO yatakayoshirikisha Wilaya Mbili KIBITI na RUFIJI yatanza kutimua vumbi kuanzia tarehe 23.9.2023 na kutamatika 12.10.2023 Wadhamini wa mashindano hayo NBC bank, NSSF, TANGANYIKA ORGANIC na UNGA AFYA LISHE kauli mbiu ya Mashindano UMOJA NA AMANI VITAWALE MITANO TENA

MTANZANIA ALICE GYUNDA AOMBA APIGIWE KURA MRS/MISS AFRICA UK 2023




MSHIRIKI wa shindano la Miss/Mrs Africa UK 2023 kutoka Tanania Alice Gyunda amesema kuwa endapo atafanikiwa kushinda taji hilo atajenga studio kwenye baadhi ya shule a msingi a Jijini Dar es Salaam ili kuzalisha vipaji vingi vya waimbaji waweze kuitangaa nchi kupitia muziki.

Aidha alisema kuwa ndoto yake nyingine ni kusaidia jamii ya watu wenye ulemavu hususani wanawake na watoto ili waweze kupata haki zao za msingi ili nao waweze kufikia malengo waliojiwekea katika maisha yao.

Gyunda ambaye ni mwalimu na mwimbaji akizungumza kwa njia ya simu kutokea nchini Uingereza anakoishi alisema kuwa endapo Watanania watampigia kura kwa wingi atakuwa na uwezo wa kushinda kwani hadi sasa bado yuko kwenye nafasi nzuri ya kufanya vema.

“Namewaomba Watanzania wanipigie kura ili nishinde ambapo vigezo ni kuonyesha utashi jinsi unavyo ongea na watu na namna unavyofanya mambo yako uwe mtu mwenye ushawishi na nikiwa mshindi nitakuwa balozi wa Kiswahili duniani na malengo yangu kuacha alama kwenye jamii kwa kusaidia watu wasiojiweza huko nyumbani japo niko mbali,”alisema Gyunda.

Alisema kuwa endapo atashinda atahakikisha anajenga studio kwenye baadhi ya shule za Msingi Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya wanafunzi ambao wana vipaji lakini hawana uwezo wa kurekodi itakuwa bure bure au kama kutakuwa na malipo yatakuwa ni madogo sana kwani muziki Tanzania uko chini sana licha ya kuwa na vipaji vingi kwani wengi hawawezi kurekodi kutokana na gharama kuwa kubwa.

“Nia ni kuinua muziki ambapo tutawekea kwa wanafunzi na vijana ambao wana vipaji vikubwa lakini kutokana na mazingira magumu ya uwezo wanashindwa kutimiza ndoto zao na wakipatikana vijana wenye vipaji wataenda kwenye matamasha ya American Good Talent au UK Good Talent ambapo vijana wa nchi za Uganda na Kenya huwa wanakwenda kwenye matamasha hayo ambapo atashirikiana na serikali ili nao washiriki wakirudi wawe chachu kwa wengine,”alisema Gyunda.

Aliongeza kuwa aliingia kwenye shindano hilo baada ya kuona tangazo na walipewa maswali 10 kuchujwa ambapo walikuwa 30 wakachujwa tena wakabaki 20 wakachujwa na kubaki 15 na baadaye mchujo mwingine ulifanyika na kubaki 13 ambapo wanatoka nchi za Afrika na Asia na kuwaomba Watanania wampigie kura ambapo hadi wakati anaongea alikuwa ameshapigiwa kura 1,800 kupitia https://africaukpageants.co.uk/poll/mrs-miss-africa-finalist-2023/

MTANZANIA ALICE GYUNDA AOMBA APIGIWE KURA MRS/MISS AFRICA UK 2023

MSHIRIKI wa shindano la Miss/Mrs Africa UK 2023 kutoka Tanania Alice Gyunda amesema kuwa endapo atafanikiwa kushinda taji hilo atajenga studio kwenye baadhi ya shule a msingi a Jijini Dar es Salaam ili kuzalisha vipaji vingi vya waimbaji waweze kuitangaa nchi kupitia muziki.

Aidha alisema kuwa ndoto yake nyingine ni kusaidia jamii ya watu wenye ulemavu hususani wanawake na watoto ili waweze kupata haki zao za msingi ili nao waweze kufikia malengo waliojiwekea katika maisha yao.

Gyunda ambaye ni mwalimu na mwimbaji akizungumza kwa njia ya simu kutokea nchini Uingereza anakoishi alisema kuwa endapo Watanania watampigia kura kwa wingi atakuwa na uwezo wa kushinda kwani hadi sasa bado yuko kwenye nafasi nzuri ya kufanya vema.

“Namewaomba Watanzania wanipigie kura ili nishinde ambapo vigezo ni kuonyesha utashi jinsi unavyo ongea na watu na namna unavyofanya mambo yako uwe mtu mwenye ushawishi na nikiwa mshindi nitakuwa balozi wa Kiswahili duniani na malengo yangu kuacha alama kwenye jamii kwa kusaidia watu wasiojiweza huko nyumbani japo niko mbali,”alisema Gyunda.

Alisema kuwa endapo atashinda atahakikisha anajenga studio kwenye baadhi ya shule za Msingi Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya wanafunzi ambao wana vipaji lakini hawana uwezo wa kurekodi itakuwa bure bure au kama kutakuwa na malipo yatakuwa ni madogo sana kwani muziki Tanzania uko chini sana licha ya kuwa na vipaji vingi kwani wengi hawawezi kurekodi kutokana na gharama kuwa kubwa.

“Nia ni kuinua muziki ambapo tutawekea kwa wanafunzi na vijana ambao wana vipaji vikubwa lakini kutokana na mazingira magumu ya uwezo wanashindwa kutimiza ndoto zao na wakipatikana vijana wenye vipaji wataenda kwenye matamasha ya American Good Talent au UK Good Talent ambapo vijana wa nchi za Uganda na Kenya huwa wanakwenda kwenye matamasha hayo ambapo atashirikiana na serikali ili nao washiriki wakirudi wawe chachu kwa wengine,”alisema Gyunda.

Aliongeza kuwa aliingia kwenye shindano hilo baada ya kuona tangazo na walipewa maswali 10 kuchujwa ambapo walikuwa 30 wakachujwa tena wakabaki 20 wakachujwa na kubaki 15 na baadaye mchujo mwingine ulifanyika na kubaki 13 ambapo wanatoka nchi za Afrika na Asia na kuwaomba Watanania wampigie kura ambapo hadi wakati anaongea alikuwa ameshapigiwa kura 1,800 kupitia https://africaukpageants.co.uk/poll/mrs-miss-africa-finalist-2023/

Friday, September 8, 2023

WAFANYABIASHARA WATAKA UBORESHWAJI WA HUDUMA SOKONI HAPO


WAFANYABIASHARA wa soko la Uhindini Wilaya ya Chunya wameomba uboreshwaji wa huduma  zikiwemo za miundombinu ya barabara maji na umeme ili waweze kutoa huduma kwa ubora kwa wateja wao.

Hayo yamebainishwa na wafanyabiashara wa wilaya hiyo wakati wa mkutano wa wafanyabiashara ulioongozwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania Bw. Hamis Livembe September 7 wenye lengo la kupokea changamoto kero na maoni ya biashara ili kupatiwa ufumbuzi.

Mmoja wa wafanyabiashara wilayani hapo Qeen Mwasakela  amesema kuwa changamoto ya umeme ina takribani miaka 10 tangu soko hilo kuanzishwa na kuiomba serikali kutatua kero hiyo.

Naye katibu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Mkoa wa Tanga Ismail Masoud amewataka wafanyabiashara kueleza changamoto kwa mamlaka husika bila ya kuogopa ili zipatiwe ufumbuzi.

Katika hatua nyingine Masoud amewataka  wafanyabiashara hao kutoungana na baadhi ya maofisa wa mamlaka mbalimbali ambao wanahujumu mipango ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hasan ya ukusanyaji wa mapato.

Amesema kuwa wasikubali kudanganywa kuwa watapunguziwa au kufutiwa kodi kwa kutakiwa kutoa rushwa ambapo mamlaka zinazohusika zikifuatilia hujikuta akiwa na deni kubwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania Bw. Hamis  Livembe amesema kuwa ukosefu wa huduma bora za msingi za kibiashara zinasababisha kushuka kwa biashara na ulipaji kodi kutofanyika vizuri na  atahakikisha changamoto hizo zinafikishwa kwenye mamlaka husika ili kupatiwa ufumbuzi.

WATAKA HATUA ZAIDI KUONGEZA MATUMIZI YA GESI

IMEELEZWA kuwa matumizi ya nishati ya gesi kwa ajili ya kupikia ni asilimia moja tu huku matumizi ya kuni na mkaa ikiwa ni asilimia 98.9 hapa nchini huku ikihitajika hatua za makusudi za kuzuia matumizi hayo ya miti ili kupunguza athari kubwa za kimazingira.

Aidha serikali imeombwa kuweka bei ya juu ya
upatikanaji wa vibali vya ukataji wa miti ili kupunguza matumizi ya mkaa na kuhamasisha matumizi ya gesi majumbani.

Hayo yamesemwa Jijini Dar es Salaam na ofisa Mahusiano wa kampuni ya Taifa Gesi Ambwene Mwakalinga alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali waliotembelea eneo la ujazaji wa gesi ya (LPG) kwenye ghala lililopo Kigamboni.

Mwakalinga amesema kuwa matumizi ya kuni na mkaa ni makubwa sana hivyo kuna haja ya serikali kuweka jitihada za makusudi za kukabiliana na hali hiyo ili kusitokee mabadiliko ya Tabianchi ambayo yanasababisha athari ikiwemo ukosefu wa mvua na uharibifu wa mazingira.

Naye meneja wa ghala hilo la Kigamboni Juma Masese amesema kuwa Taifa Gesi ndiyo kampuni ya hifadhi kubwa ya gesi hapa nchini ambayo inamilikiwa na mzawa ambapo kwa sasa inahifadhi ujazo wa metriki tani 7,400 ambapo inatarajia kuwa kampuni ya kwanza Afrika kwa kuwa na hifadhi kubwa ya nishati hiyo ambayo huletwa na meli kutoka nchi zinazozalisha gesi duniani.

Kwa upande wake ofisa usalama wa kampuni hiyo Albert Bungayela amesema kuwa wanatoa elimu kwa mawakala ili nao watoe elimu kwa watumiaji kuwa makini katika matumizi ili kuepuka madhara yatokanayo na matumizi mabaya ya gesi.


Thursday, September 7, 2023

JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA WACHARUKA MKOANI MBEYA

 



WAFANYABIASHARA mkoani Mbeya waiomba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Mbeya kufanya marekebisho ya baadhi ya mifumo na Sheria za Kodi zinachochea rushwa .


Hayo yamesemwa na wafanyabiashara wa mkoani hapo wakati wa kupokea kero, maoni na changamoto za wafanyabiashara katika mkutano uliofanyika eneo la soko jipya la Mwanjelwa chini ya Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe.

Wamesema kuwa TRA mkoani hapo imekuwa ikitumia mifumo hiyo kama chanzo cha mapato binafsi na si kuwasaidia kukuza biashara  za wafanyabiashara hao.

Aidha wameitaka serikali kutambua kuwa uchumi wa Watanzania wengi unajengwa kupitia biashara hivyo wanaiomba serikali ipunguze ututiri wa kodi .

Awali Mwenyekiti wa  Jumuiya wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe amesema kuwa moja ya sababu ya kufanya ziara mkoani hapo ni kukusanya changamoto , kero na maoni ili kuyatafutia ufumbuzi kwa mamlaka husika.

Livembe amesema kuwa zipo changamoto zinazowakumba wafanyabiashara hivyo kama kiongozi wa Jumuiya ya wafanyabiashara atahakikisha kero  zote zimetafutiwa ufumbuzi.

Naye katibu wa Jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania Abdall Salim amesema kuwa wafanyabiashara wote Tanzania wanatakiwa kuungana kwa pamoja ili kukomboa biashara zao hivyo wanapaswa kujisajili na Jumuiya hiyo.

Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania ni Taasisi inayosimamiwa na wafanyabiashara wenyewe wenye lengo la kuhakikisha wanatatua changamoto za kibiashara.

Wednesday, September 6, 2023

JAMII YAFUNDISHWA USAWA WA KIJINSIA KULETA MAENDELEO JUMUISHI


HALMASHAURI ya Mji Kibaha imedhamiria kuhakikisha inafikia asilimia 50 ya usawa wa kijinsia ili kuleta maendeleo jumuishi kwa wananchi.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na ofisa maendeleo ya jamii kitengo cha jinsia wa Halmashauri ya Mji Kibaha Maria Nkangali wakati wa mafunzo kwa watu maarufu kwenye jamii kupitia mradi wa uongozi wa wanawake na haki za kiuchumi (WLER).

Nkangali alisema kuwa hadi sasa wamefikia asilimia 20 kwenye mradi huo wa miaka mitano kuanzia 2021 hadi 2026 ambapo hadi sasa wako kwenye kata tatu za Visiga, Mkuza na Pangani.

"Lengo la mradi huu ni kuwa na usawa wa kijinsia kwenye masuala mbalimbali ikiwemo uongozi, uchumi, umiliki wa ardhi na kupata huduma za kijamii,"alisema Nkangali.

Kwa upande wake wakili wa serikali kutoka Halmashauri ya Mji Kibaha Elizabeth Lukumay  alisema kuwa baadhi ya ndoa zinakuwa ni batili kutokana na kutofuata taratibu za kisheria hivyo inapotokea zinavunjika mwanamke na watoto wanakosa haki.

Naye mwenyekiti wa wazee kata ya Mkuza Anangisye Mwakapande alisema kuwa changamoto za ndoa na ardhi ni kubwa sana kutokana na kutokuwa usawa wa kijinsia.



Tuesday, September 5, 2023

MBUNGE MUHARAMI MKENGE AKUTANA NA NAIBU WAZIRI MKUU DK DOTTO BITEKO NA WAZIRI MSTAAFU WA MALIASILI WA KENYA NAJIB BALALA

MBUNGE wa Jimbo la Bagamoyo Muharami Shabani Mkenge, Leo tarehe 5 mwezi wa 9 alipata  wasaa wa kuwa na mazungumzo na Naibu waziri mkuu na waziri wa Nishati  Mhe Dotto Biteko,  pamoja na waziri wa maliasili mstaafu wa Kenya Mhe Najib Balala  ofisini kwa Naibu  waziri  mkuu 

Wakijadili uwekezaji  katika sekta ya chumvi, pamoja na upatikanaji wa umeme wa uhakika katika Jimbo la Bagamoyo.

IMETOLEWA NA OFISI YA MBUNGE JIMBO LA BAGAMOYO🇹🇿

WAFANYABIASHARA WA PEMBEJEO NJOMBE WAMSHUKURU RAIS KWA RUZUKU YA MBOLEA

Na Mwandishi Wetu, Makambako

WAFANYABIASHARA wa pembejeo Soko Kuu la Mji wa Makambako, mkoani Njombe, wamemshukuru na kumpongeza Rais Samia kwa kuweka ruzuku ya mbolea iliyorahisisha shughuli za kilimo na upatikanaji mazao ya kutosha kwa wakulima mkoani humo.

Wizara ya Kilimo mwaka 2023/24, kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), inaendelea kuratibu upatikanaji wa mbolea nchini  kutoa ruzuku kwa wakulima hadi mwaka 2025/26 ili kuongeza matumizi ya mbolea kutoka kilo 19 hadi kilo 50 kwa hekta, kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza upatikanaji wa mazao.

Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Pembejeo za Kilimo mkoani Njombe, Abdusalim Mangoma alitoa pongezi hizo kwa niaba ya wenzake wakati akizungumza kwenye mkutano wa viongozi wa Jumuiya ya Wafanyabishara Tanzania (JWT), katika ofisi za jumuiya hiyo zilizopo Mji Mdogo wa Makambako.

Vìongozi hao wakiongozwa na Mwenyekiti wake Hamis Luvembe, wanafanya ziara ya kutembelea wafanyabishara wa mikoa ya Njombe, Mbeya na Songwe kwa ajili ya kusikiliza kero zinazowakabili ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu na kusajili wanachama  wake.

 Sanga alisema hatua ya serikali kutoa ruzuku ya mbolea kwa wakulima imeonesha matokeo chanya kwenye uzalishaji mazao katika mkoa huo.

"Wakulima sasa wananunua mbolea kwa utaratibu maalum, tofauti na awali hawakuwa wanaunua mbolea kwa sababu bei zilikuwa siyo rafiki kwao hivyo kushindwa kupata mazao ya kutosha," alisema.

Naye Katibu wa wafanyabiashara hao, Mhema Wakala, alisema mfumo wa usajili wakulima umesaidia kutambulika maeneo walipo na mashamba yao.

"Hii imetusaidia wasambazaji wa mbolea kuwatambua wakulima na kuwafikia kwa urahisi hadi waliopo vijijini," alisema Wakala.

Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Njombe na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Sifael Msigala, alisema wafanyabiashara wa mikoa hiyo wanatekeleza majukumu yao kikamilifu kutokana na kupata ushirikiano mkubwa kutoka kwa viongozi wa serikali ikiwamo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Katibu wa JWT, Abdallah Salim, aliwasihi wafanyabishara kutekeleza vyema majukumu yao kwa kufuata taratibu na kanuni za serikali kwa sababu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anasikiliza na kuzifanyia kazi kero zinazowakabili.

"Endeleeni kufanyabiashara huku mkitembea kifua mbele kwa sababu Rais Dkt. Samia tunaendelea kumfikishia kero zenu na kuzifanyia ufumbuzi, lengo ni wafanyabishara kuwa na ustawi kwenye taifa latu," alisema.

Naye Katibu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa JWT, Ismail Masoud,  alisema Rais Dkt. Samia ni kiongozi wa mfano kwa sababu amegusa moja kwa moja matatizo ya wafanyabiashara nchini.

Kwa mujibu wa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, akizungumza Agosti 8, 2023 kwenye kilele cha Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane, jijini Mbeya, alisema eneo la uzalishaji kabla ya ruzuku ya mbolea lilikuwa ekari 10,440,000  mwaka 2021/2022 hadi kufikia hekta 11,137,874.

Aidha, matumizi ya mbolea yameongezeka kutoka hekta 363,599 mwaka 2021/22 hadi tani 580,529 5085,590 mwaka 2022/23

Uzalishaji wa chakula umeongezeka kutoka tani. 17,148,290 mwaka 2021/22 hadi tani 20,42,014 mwaka 2022/23 sawa na ongezeko la tani 3,000,000.

Aidha, mbolea zitakazohusika kwenye ruzuku ni mbolea za kupandia na kukuzia ambapo DAP kwaajili ya kupandia na Urea kwaajili ya kukuzia ambazo ni takribani asilimia 50 ya matumizi ya mbolea nchini.

Mbolea za kupandia na kukuzia za aina zingine zinahusika kwenye ruzuku kulingana na mahitaji ya soko.

Monday, September 4, 2023

WAHAMIAJI HARAMU WAKAMATWA

 

JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani limewakamata wahamiaji haramu watatu toka nchi mbalimbali kwa kuingia nchini bila ya kibali.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kaimu kamanda wa polisi mkoani Pwani ACP Muhudhwari Msuya imesema kuwa watuhumiwa hao wamekabidhiwa Uhamiaji kwa hatua za kisheria.

Msuya amesema kuwa watuhumiwa hao ni kutoka nchi za Ethiopia mmoja, Kenya mmoja na Uganda mmoja.

Amesema kwenye matukio mengine jeshi hilo limekamata jumla ya Pikipiki 111 za aina mbalimbali Haoujue 23, Boxer 30, Fekon 10, SanLg 16, Sinray 1, Kinglion, Senke 01, bajaji 4 na Tvs 23 mali zidhaniwazo kuwa za wizi na watuhumiwa 97 walikamatwa.

Pia kwenye matukio mengine jeshi limefanikiwa kukamata Bhangi viroba 7, Puli 60, Kete 791 na Mbegu za Bangi kilogramu 5, Mirungi Kilogramu 5, Bunda 3 za mirungi ambapo umla ya watuhumiwa 114 wamekamatwa katika makosa hayo.


POLISI PWANI WAKAMATA WATUHUMIWA NYAMA YA SWALA NA MAGAMBA 11 YA KAKAKUONA

JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na askari wa wanyama pori limefanikiwa kukamata watubuhumiwa 14 wakiwa na nyama ya swala na magamba 11 ya mnyama Kakakuona.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani humo ACP Muhudhwari Msuya amesema kuwa baadhi ya watuhumiwa walifikishwa mahakamani.

Msuya amesema kuwa kukamatwa watuhumiwa hao 14 ni mafanikio ya jeshi hilo ambapo kati ya hao watuhumiwa watatu wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Amesema kuwa watu watatu wamehukumiwa vifungo tofuati kutokana na kukutwa na makosa ya ubakaji na ulawiti.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Salim Issa ambaye amehukumiwa kifungo cha maisha baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kulawiti mwingine ni Albino Anthony amehukumiwa kifungo cha miaka 30 baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kubaka.

"Mazoea Salum amehukumiwa kifungo cha miaka 30 baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kubaka huku Hamisi Idd amehukumiwa kifungo cha miaka 20 baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kupatikana na nyara za Serikali,"amesema Msuya.

Aidha amesema kuwa Yusuph Athuman naye  amehukumiwa kifungo cha maisha baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kupatikana na nyara za Serikali.

"Katika kipindi cha mwezi Agosti jumla ya kesi zilizoshinda mahakamani zilikuwa 75 zikiwemo hizo za watuhumiwa ambao walihukumiwa jela maisha na wengine jela miaka 30 kwa kosa la kulawiti na kubaka watuhumiwa waliotiwa hatiani katika mahakama za Mkoa wa Pwani na kwenda jela kwa baadhi ya kesi,"amesema Msuya.

JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA WATEMBELEA VIONGOZI NJOMBE

Picha ikiwaonesha Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania Abdalla Salim wakisalimiana na Katibu  wa Wafanyabiashara Makambako  Mkoani Njombe Edison Gadau Leo September 4,2023.

UONGOZI JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA WAINGIA MKOANI NJOMBE

Picha ikimuonesha Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania Abdalla Salim akiwa anasaini Kitabu Cha  wageni Katika Ofisi ya Jumuiya ya Wafanyabiashara Makambako mkoani Njombe Leo September 4,2023.

MWENYEKITI JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA AKUTANA NA UONGOZI MKOA WA NJOMBE

Picha ikimuonesha Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe akizungumza na Uongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Makambako Mkoani Njombe kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Jumuiya Leo September 4, 2023.

MWENYEKITI (JWT) TAIFA MKOANI NJOMBE

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe akiwa anasaini Kitabu Cha Wageni Katika Ofisi ya Jumuiya ya Wafanyabiashara Makambako Mkoani Njombe Leo September 4,2023.

MWENYEKITI JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA ATUA MKOANI NJOMBE

Mwenyekiti wa Jumuiya Wafanyabiashara Tanzania  Hamis Livembe akiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara Makambako Mkoani Njombe Sifaeli Msigala Leo September 4, 2023.

MWENYEKITI JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA ATUA MKOANI NJOMBE

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe akiwa anasaini Kitabu Cha Wageni Katika Ofisi ya Jumuiya ya Wafanyabiashara Makambako Mkoani Njombe Leo September 4,2023.

MWENYEKITI JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA AKIWA MKOANI NJOMBE

 

Mwenyekiti wa Jumuiya Wafanyabiashara Tanzania  Hamis Livembe akiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara Makambako Mkoani Njombe   Sifaeli Msigala Leo September 4, 2023.

MWENYEKITI (JWT) TAIFA ATEMBELEA MKOA WA NJOMBE

Mwenyekiti wa Jumuiya Wafanyabiashara Tanzania  Hamis Livembe akiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyabiashara Makambako Mkoani Njombe   Sifaeli Msigala Leo Septemba 4, 2023.

MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA AKUTANA NA UONGOZI MKOA WA IRINGA

 

Picha ikimuonesha Mwenyekiti wa jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe akizungumza na uongozi wa jumuiya ya Makambako mkoani Iringa kuhusu utekelezaji wa majukumu ya jumuiya leo Septemba 4, 2023.

Sunday, September 3, 2023

REHEMA KAWAMBWA ATEULIWA UJUMBE SOKA LA WANAWAKE COREFA

 

REHEMA KAWAMBWA ameteuliwa kushika nafasi ya ujumbe kamati tendaji ya chama cha mpira wa miguu mkoa wa pwani(corefa) kuwakilisha soka la wanawake ya muda kusubiri uchaguzi baada ya mjumbe aliyekuwa anashika nafasi hiyo Faraja Makale  kujiuzulu.

MKE WA MBUNGE KIBAHA MJINI MLEZI CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA PWANI

MKE wa mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Selina Koka amekubali kuwa mlezi wa Chama Cha Waandishi Wa Habari Wanawake mkoani Pwani, ambapo ameahidi kuwabeba ili kutimiza malengo yao.

Akizungumza na wanachama wa Chama hicho ,ambao alikutana nao kwa mara ya kwanza baada ya kukubali ombi hilo, alieleza waandishi ni kama makundi mengine katika jamii ambayo yanahitaji kujiinua kupitia miradi mbalimbali, biashara na kupitia shughuli zao .

Selina alisema anawaunga mkono waandishi wa habari,na atahakikisha wanajiinua katika Chama chao kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

"Nimekubali Kuwa mlezi wenu nachosisitiza ni Umoja, Mshikamano ,msiniangushe, naamini tutafanya mengi ,"Simamieni katiba yenu,shirikianeni katika mambo ya Chama na ya kijamii ,saidianeni na mjiepushe na kukwazana ,kila mmoja aondoe tofauti zake kwa mwenzake na mtafika"alishauri Selina.

Vilevile Selina anawaomba kujiwekea malengo kwa juhudi na mikakati madhubuti, na kwa dhana hiyo ameambatana na Ujumbe kutoka Taasisi ya kifedha ya Azania , ili kuwaunganisha kuweka akiba kwa manufaa Yao.

Nae Neema Masanja na Nuru Athuman maofisa kutoka Taasisi ya kifedha ya Azania Tawi la Tegeta walieleza,ni bank ambayo haina makato ya kumuumiza mtanzania wala mwanamke.

Nuru alifafanua, ni wakati wa akinamama kunufaika na ujio wa akaunti na mkopo mahsusi kwa wanawake ya MWANAMKE HODARI ambapo,riba yake ni nafuu asilimia moja kwa mwezi na haina makato na unafungua akaunti bure.

Awali Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi Wa Habari Wanawake mkoani Pwani, Mwamvua Mwinyi, alimshukuru Mama Koka kwa kukubali ombi hilo la Ulezi.

Alieleza kwamba, Chama hicho ,kimeanza rasmi Michakato ya kuwa chama kamili 2013, kina viongozi wanne,wanachama 15 ,kwa miaka mitano kilisimama kwa muda kujiweka sawa na sasa kimekuja kivingine.

"Ongezeko la vitendo vya ukatili kwa watoto ikiwemo kubakwa ,kulawitiwa, mimba za utotoni pamoja na baadhi yao kunyimwa haki ya Elimu ,linaonekana kuwa kubwa, tumekuwa tukishuhudia baadhi ya watoto wakinyimwa haki zao za msingi na wengine kulawitiwa ama kubakwa huku mijibaba iliyohusika kutuhumiwa kutenda vitendo hivyo ikiona ni jambo la kawaida suala ambalo linatakiwa kulipiga vita kwa nguvu zote,pasipo kulifumbia macho hata kidogo " 

Mwamvua anaeleza,masuala hayo ndio yaliyowagusa na kuwashawishi kuanzisha chama ili kuweza kushirikiana na jamii,dawati la jinsia,ustawi wa jamii kwa lengo la kutimiza adhma ya kutokomeza vitendo hivyo.


Saturday, September 2, 2023

WAKAGUZI WA POLISI PWANI WATAKIWA KUWA WATII

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina Msaidizi wa Polisi Pius Lutumo, amefunga mafunzo ya kuwajengea uwezo wakaguzi wa Polisi toka Wilaya zote na vikosi vyake kwa awamu ya pili huku akiwataka wakaguzi hao kuwa na UTII na kwenda kufanya kazi kulingana na viapo vyao, mafunzo hayo ya muda wa miezi miwili yamefungwa Leo katika viwanja vya Polisi Mkoa wa Pwani ambapo Kamanda Lutumo ameelza hategemei kuona Mkaguzi aliyehitimu Leo hii kufanya kazi kinyume na viapo vyao kwenye kuwahudumia wananchi

WATANZANIA WAASWA KUENZI VILIVYOACHWA NA WAASISI WA TAIFA

Katibu wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ndugu Omary Abdull Punzi katika Mahafali ya 22 ya Shule ya msingi Kambarage wilaya Kibaha Mkoani Pwani amewambia wazazi,walimu wanafunzi na wageni waliohudhuria mahafali kulinda vitu vyao vikiwemo vilivyoachwa na waasisi wa Taifa letu.

Punzi amesema kuwa wananchi wanawajibu wa kulinda vya kwao na kufanya matendo yaliyo kuwa mema waliorithishwa na wazee pamoja na kuunga nuhudi za Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amesema kuwa wanapaswa kuwekeza katika idara ya Elimu na maeneo mingine sambamba na hilo aliwaeleza Falsafa mbili za kuwa mzalendo za TA TE TI TO TU na ile ya SA SE SI SO SU Falsafa hizi zinapendwa sana kuzungumzwa na Mheshimiwa Paul Petro Kimiti Mwenyekiti wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Taifa Mhe Kimiti alishika nafasi mbalimbali serikalini.

Katika Mahafali hiyo Mgeni Rasmi alikuwa Ndugu Festo Issingo Meneja wa benki ya NMB Mkoa wa Pwani alichangia madawati 100 baada ya kuambiwa kuna uhaba wa madawati.

Kwa Upande wa Mkuu wa shule ya Msingi KAMBARAGE alimshukuru Katibu wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani na Meneja wa benki ya NMB Mkoa wa Pwani. 

Kwa niaba ya wazazi na walimu walimpendekeza ndugu Omary Abdull Punzi Katibu wa Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwa mlezi wa Shule ya Kambarage Nyerere kwa kuwasaidia mawazo ili kufanikisha malengo yao.

Friday, September 1, 2023

WADAU WAOMBWA KUCHANGIA UZIO KUNUSURU WANAFUNZI KUBAKWA

SHULE ya Msingi Mwendapole Wilayani Kibaha imeomba wadau kuisaidia upatikanaji wa fedha kiasi cha shilingi milioni 80 ili kujenga uzio kukabiliana na vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa wanafunzi ikiwemo kubakwa.

Aidha mtu mmoja alihukumiwa miaka 30 jela kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wa shule hiyo huku wengine wawili kesi zao zikiendelea mahakamani kutokana na tuhuma za kubaka wanafunzi wa shule hiyo.

Hayo yalisemwa na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Rajab Chalamila wakati wa mahafali ya darasa la saba ya shule hiyo ambapo wanahitaji kiasi hicho ili kufanikisha ujenzi wa ukuta wa shule.

Kwa upande wake Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) LTD Mantawela Hamis alitoa kiasi cha shilingi 100,000 ikiwa ni mchangao wa chama hicho.

Naye Mwenyekiti wa kamati ya shule Abdulrahman Likunda alisema kuwa wamekuwa wakiihamasisha jamii kuichangia shule hiyo ili kukabiliana na changamoto mbalimbali shuleni hapo.