SHULE ya Msingi Mwendapole Wilayani Kibaha imeomba wadau kuisaidia upatikanaji wa fedha kiasi cha shilingi milioni 80 ili kujenga uzio kukabiliana na vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa wanafunzi ikiwemo kubakwa.
Aidha mtu mmoja alihukumiwa miaka 30 jela kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wa shule hiyo huku wengine wawili kesi zao zikiendelea mahakamani kutokana na tuhuma za kubaka wanafunzi wa shule hiyo.
Hayo yalisemwa na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Rajab Chalamila wakati wa mahafali ya darasa la saba ya shule hiyo ambapo wanahitaji kiasi hicho ili kufanikisha ujenzi wa ukuta wa shule.
Kwa upande wake Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) LTD Mantawela Hamis alitoa kiasi cha shilingi 100,000 ikiwa ni mchangao wa chama hicho.
Naye Mwenyekiti wa kamati ya shule Abdulrahman Likunda alisema kuwa wamekuwa wakiihamasisha jamii kuichangia shule hiyo ili kukabiliana na changamoto mbalimbali shuleni hapo.
No comments:
Post a Comment